Hatma ya mradi Stiegler’s Gorge: Hatakama hatukubaliana kiitikadi, tukubaliane katika Ushauri wa kitaalam

Hatma ya mradi Stiegler’s Gorge: Hatakama hatukubaliana kiitikadi, tukubaliane katika Ushauri wa kitaalam

..tunahitaji umeme wa maji lakini siyo kwa style na utaratibu huu aliotumia bwana mkubwa.

..kwanza, mradi wa stieglers ni mkubwa sana, unatumia fedha nyingi, na muda mrefu kukamilika.

..pili, ni mradi ambao unatugombanisha na marafiki na wadau wetu wa maendeleo.

..kwa maoni yangu, serikali ilipaswa kujenga miradi ya ukubwa wa kati. Na miradi hiyo ijengwe ktk vyanzo ambavyo havina migogoro na wafadhili wetu.

..advantage ya hatua hiyo ingekuwa kuingiza umeme kwa awamu bila kusuburi muda mrefu kama tunavyofanya kwenye mradi wa stieglers. Pia tusingekuwa na ugomvi na marafiki na wafadhili wetu. Zaidi tungekuwa na fedha za kugharamia miradi mingine muhimu kama viwanda, kilimo cha umwagiliaji, etc etc.

..Stieglers inatumia fedha nyingi, na imesababisha miradi mingine muhimu ikose fedha. Waswahili wana msemo kuwa " tumeweka mayai yote ktk kikapu kimoja ."
Nchi yetu ,mradi wetu,fedha zetu , halafu tugombane na washirika wa maendeleo?,huo ni ukoloni wa wazi kabisa.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha mtu mwenye mikosi anawezaje kufika mbali hivyo kwenye career yake? Amepitaje huko koote mpaka kuwa Top Boss? I mean from zero to hero? Mimi nafikiri wewe ndiyo mikosi imekuandama na kukukwamisha kufika popote katika maisha yako na umebakiza chuki na wivu tu kama Wamarangu wenzako, ...
Mbona mwenye mikosi yuko wazi na hata wewe mwenyewe wamjua?? Wewe ndege zako unazifungia uwani inakwenda kuwapa tenda majirani zako kama sio mikosi inamuandama ni nini?? Au ulifikiri hakupenda kupeperusha twiga wake??

Yuko anajaribu kuoga na maji ya chumvi ziwani kutwa mara tatu labda yaweza kutowesha mikosi.

Mkuu ukibarikiwa umebarikiwa na ukilaaniwa umelaaniwa. Kila mtu utamuona ni adui. Kila siku kulialia eti anahujumiwa na mabeberu hadi kwenye corona wakati ni janga la kidunia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanajamvi heshima sana kwenu hasa kipindi hiki ambacho Covid 19 inatesa ulimwengu.

Nimsifu pia Mheshimiwa Yerico kwa andiko lake zuri linalofikirisha ingawa pia limejaa mashaka kibao,na hoja nyingi zikiwa zimewekwa nakshi pengine kumfurahisha msomaji au kumzubaisha asifikiri nje ya box.

Awamu ya 4 chini ya Mheshimiwa Kikwete ulianzishwa mradi mkubwa wa ujenzi wa bomba la gasi kutoka Kusini hadi Dar es Saalam.WaTanzania wengi walihoji kwanini bomba lijengwe kwa gharama kubwa wakati tungeweza kujenga mitambo ya umeme huko Mtwara.Jambo hili lilifinyangwa finyangwa pasipo majibu ya kuridhisha.Badala yake ubabe ukatumika na bomba likajengwa kwa matumani makubwa na maneno mazuri kwamba tatizo la umeme lingekwisha kabisa na lingekuwa historia.

Baada ya ujenzi wa bomba la gesi kukamilika ghafla tumehamia Striegler's Gorge huku tukisahaulishwa kimkakati na ghilba za kijasusi eti sasa mradi huu ndio ukombozi wetu ?.Najiuliza hivi bomba la gesi tumelitumia kwa kusafirisha gesi kwa asilimia ngapi hadi leo hii !.

Miradi yote hii inatafuna budget kubwa sana na hivyo kusababisha miradi mingine kuwekwa kando au kuachwa kabisa.Hii si dalili nzuri hata kidogo,tunaweza kujikuta tunatumia fedha nyingi katika miradi ambayo itakwamisha maendeleo ya taifa kwasababu tayari ipo miradi mingine ambao ilitarajiwa ingeongezewa nguvu kidogo na kuweza kutuletea tija na faida kubwa kwa taifa.Tatizo hapa ni kuweka akili za watanzania wote chini ya mtu mmoja au kikundi kidogo sana ambacho kinaangazia maslahi ya kisiasa ya muda fupi tu.

Angalia manunuzi ya ndege leo jiulize tumeingiza kiasi gani na tumetumia kiasi gani.Leo tunashuhudia shehena ya minofu ya sangara ikisafirishwa na Rwandair kwanini Air Tanzania haifanyi kazi hiyo wakati ndege zipo ?.Huo ujasusi mbona siuoni katika mambo madogo kama haya ambayo hata form four lever angeweza kufikiri vyema na kutoa maamuzi mazuri.
 
Wataliwekea maji?

Leo sudan kagoma
Ewe jasusi uchwara Ethiopia wanajengewa bwawa lao na Waitaliano halafu wangekuja kutujengea sisi?!

Ewe jasusi uchwara unayelima bamia Mbutu unawezaje kujua sehemu Ujerumani walipoweka majasusi wake duniani?

Ewe jasusi uchwara intelegensia yako inasemaje kuhusu kushindwa kwa bomba la gesi kutuletea umeme wa kutosha kama tulivyoahidiwa?
 
Huwezi kushinda kwenye soko la dunia kama competitive advantage yako iko chini.
Hichi kisingizio cha mazingira mbona kwao wao wanajenga?
Tatizo letu tuna midomo sana . Ethiopia walipokuwa wanajenga walikaa kimya. Wananchi wao walichanga kupitia government bonds.
Sisi tuliitangazia dunia vita. Hilo ndo kosa letu.
Wazo zuri la maendeleo kwa taifa ila ulimi umetujengea maadui!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio watanzania, sema midomo ya CHADEMA na Zitto Kabwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bunge la Ujerumani liliweka azimo kuitaka serikali ya nchi hiyo kuzuia ujenzi wa mradi huo wa Rufiji na badala yake serikali ya Ujerumani isaidie kujenga vinu vya gesi kwaajili ya nishati ya umeme. Kwakuangazia jambo hili watu wengi wanaweza kujiuliza, itakuwaje nchi ya Ujerumani iingilie masuala ya ndani ya Tanzania? Mifumo ya kijasusi iko hivi, kwamjibu wa Nyaraka za idara ya ujasusi ya nchini Lithium (Anual report 2016) inaonyesha kuwa Ujerumani pekee ina majasusi 11 wa ngazi za juu ndani ya UNESCO, na kwa nadharia hiyo, Ujerumani ikitaka kuzuia miradi yoyote yenye uharibifu wa mazingira inatumia msukumo wa UNESCO.
Hivi kuwa na world heritage sites kunawasaidia nini mnaowaita mabeberu? Hivi mradi ukijengwa watapata hasara gani mpaka washupae usijengwe? Nielimishe...
 
Mimi sio nabii, lakini angalau nikisema jambo nakuwa nimeona kijacho mbeleni, Naomba nikukumbushe jambo muhimu ambalo niliandika 13 March 2019 katika makala hii chini,

Katika makala hii nilianza kwakusema, "Vita vya Kiuchumi Tanzania chini ya mradi mtambuka wa maporomoko ya Rufiji, siasa ya Mazingira duniani na muundo na mienendo ya Shirika la Elimu, Sayansi na Udhibiti wa Mazingira duniani (UNESCO), vinanipa sababu ya kuiponeza TISS katika ulimbe huu wa vita vya kiuchumi.

Bonde la Rufiji liko kwenye urithi wa dunia kwamjibu wa Shirika la Uhifadhi wa Mazingira (UNESCO), Na hivyo ulinzi wa bonde hili ni kwa sheria za kidunia sio kwa sheria za Tanzania, hapa ndipo ambapo nataka kusifu idara za ujasusi na kumsifu Rais Magufuli kwa kuishinda dunia dhidi ya misimano na sera za mashirika haya ya kidunia ambayo Mwalimu yalimshinda, Mwinyi yalimshinda, Mkapa yakamshinda, Kikwete yakamshinda

Kwa wiki kadhaa nimekuwa nikipitia nyaraka za kijasusi za mashirika na taasisi mbalimbali ulimwenguni (Realiised docs), nimejiridhisha kuwa vita nikubwa kuliko wengi wanavyofikiri, na ikiwa mradi wa umeme bonde la Rufiji utafanikiwa, basi TISS itaingia kwenye historia ya mashirika bora kabisa ulimwenguni kwa counter intelligence hii. Palipo na uthubutu lazima tupongeze,

Awali mradi huu wa Umeme wa Stiegler's Gorge Ethiopia walikubali kujenga, lakini hakuna maelezo kama waliishia wapi ama walishindwa tenda. Zikawepo taarifa za Waturuki kuwa watajenga, nazo zikaishia hewani. Kisha tukashuhudia Arabb Contractors wa Misri wakisaini mikataba ya ujenzi. Bado ujenzi rasmi haijaanza, lakini hatua tu ya kuthubutu kusaini mkataba ni hatua kubwa inayostahili kupongezwa.

Bunge la Ujerumani liliweka azimo kuitaka serikali ya nchi hiyo kuzuia ujenzi wa mradi huo wa Rufiji na badala yake serikali ya Ujerumani isaidie kujenga vinu vya gesi kwaajili ya nishati ya umeme. Kwakuangazia jambo hili watu wengi wanaweza kujiuliza, itakuwaje nchi ya Ujerumani iingilie masuala ya ndani ya Tanzania? Mifumo ya kijasusi iko hivi, kwamjibu wa Nyaraka za idara ya ujasusi ya nchini Lithium (Anual report 2016) inaonyesha kuwa Ujerumani pekee ina majasusi 11 wa ngazi za juu ndani ya UNESCO, na kwa nadharia hiyo, Ujerumani ikitaka kuzuia miradi yoyote yenye uharibifu wa mazingira inatumia msukumo wa UNESCO.

Kinachoweza kutokea ni kuwa UNESCO inaweza kuiandikia barua ya katazo nchi husika kwamba pale ni sehemu ya Urithi wa Dunia (World Heritage site.) na hairuhuriwi kupajenga. Na wanaonya kuwa ukiwa mbishi na ukaendelea kujenga utakuwa black listed. Na kampuni inayopata tenda ya kujenga nayo inapewa barua na kuonywa kuwa itakuwa black listed na Bank Account zako zitakamatwa. Kwakufanya hivyo wanashinikiza kampuni zijitoe katika mradi husika.

Majasusi hawa wamefanya hivyo kuidhibiti Iran, enzi za Reza Khan kwakutumia mashirika haya ya kidunia , ambayo mengi ni mashirika ya kijasusi. Pia nchi za Panama zimewahi kukumbana na nguvu ya mashirika haya.

Kwa namna yoyote naipongeza Serikali kwa ujasiri huu wa kufunga masikio na kelele za kidunia na kuamua kuanzisha mradi huu uliokwamba tangu miaka ya 60+. Hii ni hatua kubwa sana na ninaamini itaacha legacy kubwa sana kwa rais Magufuli na kwa vyombo vya ujasusi nchini ikiwa utafanikiwa, ingawa hakuna nchi au kikundi kilichowahi kushindana na mashirika haya ya kidunia na kikashinda, zaidi ya hapo labda ziwe ni siasa za kura. Bado naamini tumethubutu pakubwa sana, na katika ndoto tutashinda". Makala iliishia hapo.

Sasa mwaka mmoja na baadaa ya makala hii, Kampuni iliyokuwa ikijenga mradi huo imeandika taarifa hii ambayo inajumuisha ndani yake katazo la UNESCO. Isome hapa kwa lugha ya kitumwa....>>> ElSewedy Electric Co - Council on Ethics

Unaweza kujipa nafasi ya kusoma kwa undani zaidi kitabu cha Ujasusi kujua nama Ujasusi dhidi ya Ujasusi unavyofanya kazi na mifano hai toka katika viunga vya dunia ya ujasusi.

Nunua Kitabu kwa Ofa ya Mwezi Mtukufu na #Corona kwa 25,000 tu popote ulipo. Badala ya bei halisi ya 80,000/=

Nunua kwa Mpesa na Tigopesa 0715865544/ 0755865544 (Yericko Nyerere) kisha tuma majina yako na mahali ulipo.

Kwa Dar kitabu kitaletwa ulipo bure. Nje ya Dar nauli ni 8,000/=
Tunapaswa kutii mikataba tuliyoingia. Leo hii rais akija na mapendekezo ya kujenga jiji kubwa ndani ya Serengeti dunia haiwezi kukaa kimya. Selous game reserve ni urithi wa dunia na tunalazimika kuulinda. Inashangaza kwamba tunaharibu urithi huu wakati ni wetu tulipaswa kuulinda sio kuuharibu, aibu sana.
 
Hahaha mtu mwenye mikosi anawezaje kufika mbali hivyo kwenye career yake? Amepitaje huko koote mpaka kuwa Top Boss? I mean from zero to hero? Mimi nafikiri wewe ndiyo mikosi imekuandama na kukukwamisha kufika popote katika maisha yako na umebakiza chuki na wivu tu kama Wamarangu wenzako, ...
Nyie mnamuunga mkono jiwe kwasababu uelewa wenu wa mambo ni finyu sana kama wa kwake. Ona kila kitu afanyacho kipo hovyo na hayo yanadhihirika wazi kila kukicha na nchi inaabika sana kwasasa.
 
Nyie mnamuunga mkono jiwe kwasababu uelewa wenu wa mambo ni finyu sana kama wa kwake. Ona kila kitu afanyacho kipo hovyo na hayo yanadhihirika wazi kila kukicha na nchi inaabika sana kwasasa.


Mti utupiwao mawe, Tanzania is rising na ndio maana majirani wote wana wivu na chuki tu, ...
 
Back
Top Bottom