Hatma ya Muungano Tanganyika na Zanzibar

Hatma ya Muungano Tanganyika na Zanzibar

aleesha

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
798
Reaction score
1,178
Kesho ni siku ambayo, kesi ya Madai ya Uhalali wa Muungano iliyofunguliwa na Wazanzibari wapatao 40,000 itasikilizwa. Waswahili wana maneno yao wanasema "Bora kua na adui alieelimika utanufaika, kuliko kua na Swahib mjinga".

Msemo huu unaakisi hasa dhana ya Uswahib wa Zanzibar na Tanganyika kupitia Muungano huu ambao uliundwa tarehe 26 April 1964.

Hata hivyo, ni muhimu baada ya miaka kadhaa iliyopita ya Muungano, leo tukaangalia khatma ya Muungano wetu, hasa kwa kuzingatia kua, kesho tarehe 8 March 2018 kesi ya Muungano itasikilizwa ndani ya Mahakama ya Afrika Mashariki - Arusha.

Ni vyema sasa tukaonyeshana njia ya eidha, kama Wazanzibari wanazo sababu na ishara za kushinda kesi hiyo au laah?

Mapema miaka ya 1960 kabla ya Uhuru wa nchi za Afrika Mashariki kupatikana, kuliibuka vuguvugu la kuundwa Shirikisho la Afika Mashariki (East African Federation - EAF). Katika Shirikisho hilo, nchi ambazo zilitarajiwa kuunda Shirikisho hilo zilikua ni Kenya, Uganda, Tanganyika na Zanzibar.

Marehemu Mwalimu J.K Nyerere alitangaza kua, endapo nchi hizo zote zingepata kua huru kwa pamoja angeghairisha adhma yake ya kupigania Uhuru wa Tanganyika ili kuunda Shirikisho hilo la Afrika Mashariki. Hata hivyo, hilo halikufanyika.

Miezi minne kabla ya Zanzibar kupata Uhuru wake wa tarehe 10 December 1963, Washirika hao wa Afrika Mashariki walimtuma Marehem Tom Mboya kutoka Kenya kuja kuiuliza Serikali ya Zanzibar, kama iko tayari kuanza majadiliano kuhusu kujiunga na Shirikisho hilo (EAF) na Zanzibar ikakubali.

Hata hivyo, mara baada ya Mapinduzi ya Zanzibar kutokea, Raisi J.K Nyerere pasi na kushauriana na wenzake aliamua kulifuta wazo hilo la kuundwa kwa Shirikisho la Afrika Mashariki na badala yake akaunda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na hapo ikawa ndio mwanzo wa kile kinachoitwa "Kero za Muungano".

Inasemakana kua, chanzo cha Mwalimu J.K Nyerere kulifuta wazo hilo pasi na kushauriana na wenzake ni kwamba, Kenya na Uganda walikua wakisita kujiunga katika Shirikisho hilo kutokana na kua na mashaka/hofu na nia ya Mwalimu J.K Nyerere ambapo, hadithi ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar imethibitisha ukweli wa hofu yao hiyo.

Pamoja na Mwalimu J.K Nyerere kutumia fursa ya hali ya ulinzi mkali Zanzibar haraka baada ya Mapinduzi, Mwalimu J.K Nyerere pia alitishia kuwaondosha askari wake wapatao 300 aliowatuma kumlinda Raisi Abeid A. Karume, endapo Raisi Karume angelilipinga wazo la Muungano lililotolewa na Mwalimu J.K Nyerere.

Hata Baraza la Mapinduzi ambalo ndicho kilichokua chombo pekee cha utendaji na cha kutunga sheria halikufahamu kuhusu wazo la kuwepo kwa Muungano, mpaka siku mbili kabla ya kutangazwa mnamo tarehe 26 April 1964, siku mia moja baada ya Mapinduzi.

Hivyo, hoja ya kwanza ya Wazanzibari katika kesi hiyo kama ilivyo, ni Uhalali wa Muungano, hasa kwa kuzingatia kua, kwanza Raisi Karume aliingizwa katika Muungano huu kwa ushawisho usiofaa (Vitisho) ambapo, licha ya hayo niliyoyaeleza juu, Raisi Karume pia alidanganywa na kuaminishwa kwamba alikua anasaini mkataba wa Shirikisho la nchi mbili huru zenye mamlaka sawa. Udanganyifu huo ulifanywa baada ya aliekua Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kulazimishwa kundoka katika shughuli hiyo ya utiaji saini.

Pili; Kifungu cha (viii) cha Mkataba wa Muungano ambacho ndio hati ya kuzaliwa kwa Muungano, kimesema kua, Mkataba huo ulipaswa kuridhiwa na Bunge na Baraza la Mapinduzi. Wakati vifungu hivyo vikiridhiwa kwa upande wa Tanganyika na kuhalalishwa kupitia Gazeti la Serikali la Tanganyika, hakuna makubaliano yaliyofikiwa kwa upande wa Zanzibar, kwa kua hakuna Sheria iliyopitishwa na Baraza la Mapinduzi ili kuidhinisha kama walivyoidhinisha Tanganyika na hakuna taarifa yoyote iliyotolewa katika Gazeti la Serikali ya Zanzibar.

Tatu; Jina rasmi la Muungano katika Mkataba wa Muungano lilikua ni "Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar". Miezi sita baadae, kwa mara ya pili, Mwalimu J.K Nyerere bila ya kushauriana na mwenzake, aliamua kubadili jina hilo kutoka jina lililokua ndani ya Mkataba wa Muungano na kua "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" ambalo lilipitishwa rasmi na Bunge la Tanganyika lakini halikupitishwa na Baraza la Mapinduzi. Huu ulikua ukiukwaji mwengine wa wazi wa Mkataba wa Muungano.

Nne; Mkataba wa Muungano Vifungu (vii(b) vimeeleza wazi kua, Bunge litakutana ndani ya mwaka mmoja kutengeneza Katiba ya kudumu, lakini mwisho wa mwaka wa kwanza, Mwalimu J.K Nyerere kwa mara ya tatu pasi na kushauriana na yoyote, aliamua kughairisha kupitishwa kwa Katiba ya kudumu kwa miaka 13 hadi mwaka 1977 baada ya mauaji ya Raisi Karume na kuunganishwa kwa Vyama vya TANU na AFROSHIRAZI na kua Chama kimoja (CCM). Hapo ndipo pakapitishwa Katiba ya sasa tena bila ya kushauriana na Wazanzibari.

Hivyo, licha ya hoja hizi nne kutoa ishara ya namna gani Wazanzibari wanavyoweza kushinda kesi hiyo au laah! Swala la Muungano pia limekua na ukakasi mkubwa ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano hasa baada ya mfumo wenyewe wa Muungano kushindwa kujieleza kama ni mfumo wa Muungano wa nchi moja au Shirikisho. "Although it's 22 years of the Union, the natural and content of the Union has presented considerable confusion both in Tanzania and abroad. It is not clarified wether the Union is a federation or unitary state".

Pia; Swala la Mambo ya Muungano (Union Matters) ni swala ambalo limekua likiibua mjadala mkubwa. Wachambuzi wanadai kua, ndani ya Mkataba wa Muungano, mambo yaliyokubaliwa kama ni mambo ya Muungano ni 11 tu, lakini idadi ya mambo hayo yamekua yakiongezeka mara mbili zaidi baada ya miaka 50 ya Muungano na kupelekea Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kudhoofika siku hadi siku.

Swala la kuondoshwa kwa nafasi ya Raisi wa Zanzibar kua Makamo wa raisi wa Tanzania kinyemela ni sawala jengine linalotoa taaswira mbovu ya adhma ya Tanganyika dhidi ya Zanzibar.

Swala la Raisi wa Muungano kuchaguliwa kwa kura nyingi za Tanganyika bila ya mahitaji ya kura chache za Zanzibar kama vile Wazanzibari hawana sauti ama hawahusiki na Muungano huu, pia linaonyesha jinsi Muungano huu inavyokosa uhalali zaidi.

Chini ya kifungu cha 98 cha Sheria ya Umoja wa Mataifa (UN), Sheria yoyote iliyotungwa juu ya jambo lolote la Muungano inapitishwa na zaidi ya nusu ya kura/wajumbe (Simple Majority). Hivyo, Bunge ambalo idadi yake ya Wabunge kutoka Zanzibar haizidi asilimia 20% haihitaji ushahidi zaidi kuthibitisha kua Muungano huu ni Muungano wa kilaghai.

Haya na mengine mengi, ndio mambo ambayo Wazanzibari wanapaswa kuyajua wanapoenda kuamua khatma ya Muungano wao, hasa katika kipindi hichi ambacho kesi yao ya madai ya Muungano imeshafunguliwa na inaanza kusikilizwa.
 
Kila kiongozi huapa kuulinda muungano kwa nguvu zote, hii inamaanisha kuwa kuna jambo nyuma ya pazia. Kama halipo kwanini itumike nguvu kubwa kiasi hicho na vitisho kwa wanaohoji na kuijadili muungano? Tusubiri kitakacho amriwa maana kwauelewa wangu rais huyu hawezi kukubali muungano umfie mikononi.
 
Huo Muungano una wenyewe wana nguvu kubwa kuliko -:
Serikali ya Muungano.
Serikali ya Mapinduzi.

Je tumesahau baada ya Mwl.Nyerere Kustaafu uraisi Wabunge machachali wakati wa chama kimmoja G45,bunge kwa kauli mmoja lilipitisha kuundwa kwa serikali tatu,LAKINI akatokea ghafla Raisi Mstaafu Mwl Nyerere kuja na nguvu zisizo kwenye katiba :

Kauwa hoja iliopitishwa na Bunge.
Kamungoa Waziri Mkuu Malecela
Kamuadabisha Horice Kolimba na kuwatungia kitabu.
Lakini hata baada ya kufariki Mwl Nyerere:

Tume ya Warioba iliotaka serikali tatu iliangushwa.

Katiba mpya iliyeyuka kiajabu licha ya kutumia gharama kubwa
Jumbe alietaka serikali tatu aliendelea kukaa kifungo baridi hadi kufariki kwake.

Mwenye Funguo za Muungano anayeweza kuuwa au kukubali marekebisho sio mwingine bali ni Marekani,na Uingereza.

Tukitaka kumaliza tatizo lipeleke UNO kwa VETO members walijadili
 
Kila kiongozi huapa kuulinda muungano kwa nguvu zote, hii inamaanisha kuwa kuna jambo nyuma ya pazia. Kama halipo kwanini itumike nguvu kubwa kiasi hicho na vitisho kwa wanaohoji na kuijadili muungano? Tusubiri kitakacho amriwa maana kwauelewa wangu rais huyu hawezi kukubali muungano umfie mikononi.


NA KANISA KATOLIKI NDIO LIMEKUJA NA HAYA

Kardinali Pengo: Muungano si bahati nasibu



Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amewataka waamini na wananchi kwa ujumla kutambua kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar si jambo la bahati nasibu.


Kardinali Pengo ameyasema hayo ofisini kwake hivi karibuni alipoitisha vyombo vya habari vya Kanisa Katoliki kuzungumzia pamoja na mambo mengine ongezeko la Parokia mpya jimboni kwake pamoja na mabadiliko kwa Maparoko na Maparoko Wasaidizi katika baadhi ya Parokia jimboni humo.

Asemema suala la Muungano linapaswa kuchukuliwa kwa uzito wa pekee kwa kila Mtanzania hasa waamini Wakatoliki na kwamba kila mwamini anapaswa kutambua kuwa amepewa jukumu na Mwenyezi Mungu kulinda na kuombea Muungano huo.
 
Hivi mkoa unaweza shitaki mahakama ya jumuiya ya afrika mashariki kuomba kujitenga? Tanzania ni mwanachama wa jumuiya .Zanzibar ni kama mkoa tu hauna nguvu kisheria kujitambulisha kama nchi mahakama za kimataifa.Walioshtaki wanapoteza muda.Pia muungano uliliridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi wao ni kina nani? Huwezi tengua kitu kilichoridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi ambao ndio wawakilishi halali na kisheria wa wananchi.Huwezi kusanya sahihi za vibaka na wanga elfu 40 vijiweni eti wanataka muungano uvunjike.Muungano haukufanywa vijiweni
 
Hivi mkoa unaweza shitaki mahakama ya jumuiya ya afrika mashariki kuomba kujitenga? Tanzania ni mwanachama wa jumuiya .Zanzibar ni kama mkoa tu hauna nguvu kisheria kujitambulisha kama nchi mahakama za kimataifa.Walioshtaki wanapoteza muda.Pia muungano uliliridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi wao ni kina nani? Huwezi tengua kitu kilichoridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi ambao ndio wawakilishi halali na kisheria wa wananchi.Huwezi kusanya sahihi za vibaka na wanga elfu 40 vijiweni eti wanataka muungano uvunjike.Muungano haukufanywa vijiweni
Mkuu naomba ninukuu maneno yako mazuri, haya maneno ni sahihi kabisa na kiongozi wa zanzibar ni mkuu wa mkoa aliyepewa jina la raisi
 
Hivi mkoa unaweza shitaki mahakama ya jumuiya ya afrika mashariki kuomba kujitenga? Tanzania ni mwanachama wa jumuiya .Zanzibar ni kama mkoa tu hauna nguvu kisheria kujitambulisha kama nchi mahakama za kimataifa.Walioshtaki wanapoteza muda.Pia muungano uliliridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi wao ni kina nani? Huwezi tengua kitu kilichoridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi ambao ndio wawakilishi halali na kisheria wa wananchi.Huwezi kusanya sahihi za vibaka na wanga elfu 40 vijiweni eti wanataka muungano uvunjike.Muungano haukufanywa vijiweni


Huu si muungano ni uvamizi uliopewa jina la muungano.Tanganyika chini ya Laanatullahi Nyerere iliivamia Zanzibar na kumkamata Waziri Mkuu wake Muhammed Shamte Mpemba aliyechaguliwa na wananchi pamoja na mawaziri wake na kuwafunga katika magereza ya Tanganyika bila kuwafikisha mahakamani kabla hata huo uitwao Muungano haujafikiriwa.
 
Huu si muungano ni uvamizi uliopewa jina la muungano.Tanganyika chini ya Laanatullahi Nyerere iliivamia Zanzibar na kumkamata Waziri Mkuu wake Muhammed Shamte Mpemba aliyechaguliwa na wananchi pamoja na mawaziri wake na kuwafunga katika magereza ya Tanganyika bila kuwafikisha mahakamani kabla hata huo uitwao Muungano haujafikiriwa.
muungano uliridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi utauitaje uvamizi?
 
Hivi mkoa unaweza shitaki mahakama ya jumuiya ya afrika mashariki kuomba kujitenga? Tanzania ni mwanachama wa jumuiya .Zanzibar ni kama mkoa tu hauna nguvu kisheria kujitambulisha kama nchi mahakama za kimataifa.Walioshtaki wanapoteza muda.Pia muungano uliliridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi wao ni kina nani? Huwezi tengua kitu kilichoridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi ambao ndio wawakilishi halali na kisheria wa wananchi.Huwezi kusanya sahihi za vibaka na wanga elfu 40 vijiweni eti wanataka muungano uvunjike.Muungano haukufanywa vijiweni
Unazungumza kama upo haja kabla ya muungano ilikuwa nchiyenye madaraka kamili ndio sababu kunaneno muungano wa nchi 2 sasa iwe nakubwa kama chumba chako cha kulala lakini ninchi
 
Hivi mkoa unaweza shitaki mahakama ya jumuiya ya afrika mashariki kuomba kujitenga? Tanzania ni mwanachama wa jumuiya .Zanzibar ni kama mkoa tu hauna nguvu kisheria kujitambulisha kama nchi mahakama za kimataifa.Walioshtaki wanapoteza muda.Pia muungano uliliridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi wao ni kina nani? Huwezi tengua kitu kilichoridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi ambao ndio wawakilishi halali na kisheria wa wananchi.Huwezi kusanya sahihi za vibaka na wanga elfu 40 vijiweni eti wanataka muungano uvunjike.Muungano haukufanywa vijiweni
hahahah wanyamwezi bwana, mnaforce tu vichogo
 
This man is a son of Devil
emoji48.png
himself!
muungano uliridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi utauitaje uvamizi?



Uliridhiwa baada Waziri Mkuu wake Muhammed Shamte Mpemba aliyechaguliwa na wananchi pamoja na mawaziri wake kukamatwa na kufungwa katika jela za Tanganyika bila kuwafikisha mahakamani kabla hata huo uitwao Muungano haujafikiriwa?? Watu wako magerezani January huo unaoitwa muungano ulianza 26 April
 
Serikali tatu bado siyo muwaarobaini. Tuache uvyama. Sera ya CDM ya Majimbo na kuwa na Serikali Kuu itatuimarisha sisi na Wenzetu.
 
Hivi mkoa unaweza shitaki mahakama ya jumuiya ya afrika mashariki kuomba kujitenga? Tanzania ni mwanachama wa jumuiya .Zanzibar ni kama mkoa tu hauna nguvu kisheria kujitambulisha kama nchi mahakama za kimataifa.Walioshtaki wanapoteza muda.Pia muungano uliliridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi wao ni kina nani? Huwezi tengua kitu kilichoridhiwa na bunge na baraza la wawakilishi ambao ndio wawakilishi halali na kisheria wa wananchi.Huwezi kusanya sahihi za vibaka na wanga elfu 40 vijiweni eti wanataka muungano uvunjike.Muungano haukufanywa vijiweni
Ndio maana wameparidhaa ya kusikilizwa na hiyo mahakama
 
Mtafuteni mwandishi wa makala ndugu Joseph Mihangwa anaijua Zanzibar kuliko hata kina shen na Maalim Seif.

Huu muungano wetu kwa mujibu wa viongozi wa ccm ni "Muungano wa kipekee"
 
Imefikia wakati sasa kwa wazanzibar kuudai huru wao ulio mezwa na watanganyika kwenye koti la muungano.
 
NA KANISA KATOLIKI NDIO LIMEKUJA NA HAYA

Kardinali Pengo: Muungano si bahati nasibu



Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amewataka waamini na wananchi kwa ujumla kutambua kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar si jambo la bahati nasibu.


Kardinali Pengo ameyasema hayo ofisini kwake hivi karibuni alipoitisha vyombo vya habari vya Kanisa Katoliki kuzungumzia pamoja na mambo mengine ongezeko la Parokia mpya jimboni kwake pamoja na mabadiliko kwa Maparoko na Maparoko Wasaidizi katika baadhi ya Parokia jimboni humo.

Asemema suala la Muungano linapaswa kuchukuliwa kwa uzito wa pekee kwa kila Mtanzania hasa waamini Wakatoliki na kwamba kila mwamini anapaswa kutambua kuwa amepewa jukumu na Mwenyezi Mungu kulinda na kuombea Muungano huo.
Pengo auombee muungano peke yake asitupe kazi wakatoliki wote nchi nzima.
 
Ukweli mchungu ambao Mzee Nyerere aliona lakini alikataa kuukiri ni kwamba siku ambayo Zanzibar inatoka kwenye huu Muungano kutakuwa na machafuko makubwa sana huko Zanzibar. Lakini baada ya muda Zanzibar itatulia na kuwa taifa moja tajiri sana Afrika ya Mashariki, siyo tajiri kwa kubahatisha bali tajiri haswaaa na kitakuwa ndicho kitovu kikubwa cha dini ya Uislamu kusini mwa jangwa la sahara. Itafika kipindi hata kama tunaweza kuwawekea vikwazo vya kiuchumi wao wanaweza kuishi vizuri kabisa bila bughudha ya Tanganyika.

Kardinali Pengo na baadhi ya viongozi wa dini wanaujua sana huu ukweli,
Mzee Nyerere alilijua hili ndiyo maana "akasema ukiwaacha Wazanzibari watapewa mapesa mengi kutoa kwa waarabu"
Ukikaa na Wazanzibari utakuja kugundua mbali na tofuati zao, wana kitu cha ziada ambacho sisi Watanganyika hatuna kabisa: Kwenya maslahi mapana ya Zanzibar CUF na CCM visiwani wote huwa na sauti moja.

NB: Kimkakati Zanzibar kutoka kwenye Muungano kunaweza kuwanufaisha sana kwasababu eno lao limekaa vizuri sana kijographia. Hasa hasa ukiangalia Maritime Silk Road inapita hapo baada ya Kutoka The Strait of Malacca kwa upande wa Bahari ya Pasifiki na Suez Canal ukiwa umetoka Ulaya. Kama wataamua kutanua bandari yao basi wanaweza kujihakikishia kuwa na soko kubwa sana la biashara za kimataifa kama ilivyo Dubai. Pia inaweza kuwapunguzia sana kutegemea Tanganyika kwasababu bidhaa zao wanaweza kuzipata kutoka Asia, Ulaya, Uarabuni na Mombasa (Haya yatafanyika kama watapata viongozi wenye akili na upeo mkubwa wa kufikiri bila kutumiwa kama vibaraka wa Tanganyika ili kuwagawanya Wazanzibar kama ilivyo sasa hivi)

Tanganyika wakiacha siasa za kidini na kibaguzi basi wanaweza kuitumia Zanzibar kama moja ya kitega uchumi kikubwa,
Pia Zanzibar inaweza ikaongezewa uhuru (Commercial Autonomy) kwenya masuala ya kibiashara kama Bandari na Kodi ili kuutenga mfumo wa kodi wa Muungano ili kuweza kutengeneza soko la kimtaifa ambapo wafanya biashara wa Tanganyika na Zanzibar wanaweza kupata bidhaa nyingi kwa bei ndogo kutoka Ulaya, Asia ya Mbali na Ghuba ya Uajemi. Haya yanawezekana kama tu, tutaamua kukaa kama Taifa na kuweka siasa na udini pembeni......ZANZIBAR INAWEZA KUUINGIZIA MUUNGANO PESA NYINGI SANA....

LONG LIVE THE UNION.............
THE FUTURE IS VERY BRIGHT FOR BOTH TANGANYIKA AND ZANZIBAR!
 
.
Miezi minne kabla ya Zanzibar kupata Uhuru wake wa tarehe 10 December 1963 Washirika hao wa Afrika Mashariki walimtuma Marehem Tom Mboya kutoka Kenya kuja kuiuliza Serikali ya Zanzibar, kama iko tayari kuanza majadiliano kuhusu kujiunga na Shirikisho hilo (EAF) na Zanzibar ikakubali.
.
Kwa maana hiyo ile january 12/1964 ilikuwa uhuru upi tena! Tanganyika wapeni Wazanzibari uhuru wao.
 
Back
Top Bottom