Hatua ya kwanza ya mafanikio ni kuondoka nyumbani

Hatua ya kwanza ya mafanikio ni kuondoka nyumbani

Acha uongo unasema elimu ya Tanzania haimjengi mtu kuwa na mawazo ya kujiajiri,una takwimu za kutuonyesha graduates wangapi wameshindwa kujiajiri,kujiajiri kunategemea na kujifikirisha kwa mtu kama mkichwa wako umelala ndio hivo utakaa tu nyumbani kusubiri kuajiriwa.

Tusisingizie elimu tuvilaumu vichwa vyetu vilivyolala,wapo watu wengi tu wamejiajiri baada ya kumaliza chuo sasa na hawa wamesoma elimu gani kama sio hii hii tunayoisoma wote
Nini lengo la kwenda shule?..
 
Ebu fanya maisha yako ya kwao waachie wenyewe [emoji124][emoji124][emoji124]

Sent from my SM-G928F using JamiiForums mobile app
Hahah mkuu humu kuna watoto wa kiume wapo kama dada zao...yani mtoto wa kiume over18 alafu kwao masikini bado anafagilia kukaa kwa wazazi na hana mchango wowote kama anasubiri kuolewa nayeye au wazazi wake wataishi milele...
 
Hakuna cha aibu kukaa kwenu mkuu, mbaya ni kuwa tegemezi wa kila kitu. Kuna ambao wamekimbia kwao kwenda kupanga na bado wanategemea kulipiwa chakula na pango na ndugu au wazazi wao.
Kwenu unaweza kukaa kama una nafasi kubwa pia, ila kama unavyosema usiwe tegemezi kabisa pengine wewe unaweza kujipa majukumu kadhaa ukawa unahudumia baadhi ya vitu ili kupunguza mzigo kwa mzee wako pia.
Kuna watu nimeona mpaka wameoa wakiwa kwao ili mradi hawachangamani na wazazi wao nyumba moja yaani anaishi chumba cha nnje na mke wake na anajitegemea kula kitu na wazazi wake anawasaidia baadhi ya mambo pia.
 
Kwenu unaweza kukaa kama una nafasi kubwa pia, ila kama unavyosema usiwe tegemezi kabisa pengine wewe unaweza kujipa majukumu kadhaa ukawa unahudumia baadhi ya vitu ili kupunguza mzigo kwa mzee wako pia.
Kuna watu nimeona mpaka wameoa wakiwa kwao ili mradi hawachangamani na wazazi wao nyumba moja yaani anaishi chumba cha nnje na mke wake na anajitegemea kula kitu na wazazi wake anawasaidia baadhi ya mambo pia.
Mkuu kukaa nyumbani umri kuanzia 25+ ..ni uzembe huo
 
Hi wana Jf,
Nimejaribu kuchunguza hasa hizo nchi zetu za Africa hususani (East Africa) limekuwa ni jambo la kawaida kukuta kijana ana miaka takribani 30 na bado anaishi kwa wazazi wake bila aibu anasubiri ugali wa shikamoo.
Hili jambo ukiliangalia kwa mapana utagundua linasababishwa na vitu Vingi..

Mfano mfumo wetu wa elimu nao unachangia kwa sababu elimu mtu anayopata mpaka chuo kikuu haimjengi muhusika katika kuwa na mawazo ya kujiajiri . Tatizo linakuja pale mtu kamaliza chuo alafu kakosa kazi ..utashangaa mtu anakaa nyumbani mpaka anaoa/kuolewa akiwa nyumbani.

Lakini upande wa pili hata kama mtu hajasoma pia bado utakuta anaishi nyumbani kwa wazazi akiwa na umri mkubwa..mi nadhani pia sisi wa Africa uvivu unatupeleka pabaya.

Tumezoea kukaa vijiweni muda mwingi tukijadili mambo yasiyo na msingi na tumekuwa watu wa kutojali muda kabisa... Wala hatuna ratiba ..

Yangu ni hayo tuu kama kuna mwingine mwenye mawazo tofauti na mimi anaweza akaongeza au kunipinga kwa hoja lakini...
Nawasilisha
Unaondoka nyumbani ukiwa na nini?Mtaji,bidhaa?Ufafanuzi tafadhali.
 
Hi wana Jf,
Nimejaribu kuchunguza hasa hizo nchi zetu za Africa hususani (East Africa) limekuwa ni jambo la kawaida kukuta kijana ana miaka takribani 30 na bado anaishi kwa wazazi wake bila aibu anasubiri ugali wa shikamoo.
Hili jambo ukiliangalia kwa mapana utagundua linasababishwa na vitu Vingi..

Mfano mfumo wetu wa elimu nao unachangia kwa sababu elimu mtu anayopata mpaka chuo kikuu haimjengi muhusika katika kuwa na mawazo ya kujiajiri . Tatizo linakuja pale mtu kamaliza chuo alafu kakosa kazi ..utashangaa mtu anakaa nyumbani mpaka anaoa/kuolewa akiwa nyumbani.

Lakini upande wa pili hata kama mtu hajasoma pia bado utakuta anaishi nyumbani kwa wazazi akiwa na umri mkubwa..mi nadhani pia sisi wa Africa uvivu unatupeleka pabaya.

Tumezoea kukaa vijiweni muda mwingi tukijadili mambo yasiyo na msingi na tumekuwa watu wa kutojali muda kabisa... Wala hatuna ratiba ..

Yangu ni hayo tuu kama kuna mwingine mwenye mawazo tofauti na mimi anaweza akaongeza au kunipinga kwa hoja lakini...
Nawasilisha
Na Hakuna kitu unatufanya
 
Nimefarijika sana kuona Mada nlioianzisha ...2016 ..Leo ikipewa platform katika page kubwa ya jamii forum ..huko mjini fb wataijadili

Real recognize real [emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
Screenshot_20210704-100102.jpg
 
Kwenu unaweza kukaa kama una nafasi kubwa pia, ila kama unavyosema usiwe tegemezi kabisa pengine wewe unaweza kujipa majukumu kadhaa ukawa unahudumia baadhi ya vitu ili kupunguza mzigo kwa mzee wako pia.
Kuna watu nimeona mpaka wameoa wakiwa kwao ili mradi hawachangamani na wazazi wao nyumba moja yaani anaishi chumba cha nnje na mke wake na anajitegemea kula kitu na wazazi wake anawasaidia baadhi ya mambo pia.
Mkuu ukiwa unajitambua sio mbaya sana ..Ila sisi wa Africa tunajuana tulivyo ...ndo maana nkasema kwa Africa Bora kuondoka nyumbani
 
Mi siondoki home,takufa njaa bure!kwani dhambi kukaa kwa wazazi?na nina miaka 36 sasa
Hapo mkuu unakwama sio vizuri maana ukikaa sana nyumbani na akili inakuwa haichangamki (passive) maana inajua chakula kipo tu but ukiwa away from home akili inakuwa active kutafuta ili wewe ule pamoja na familia yako
 
kibongo bongo ni heri kutoka home ukaenda kujitafutia maisha hasa pale unapoona hali ya home hairuhusu na wewe ni mkubwa.
kwa wasio wabongo wakiona home mambo safi hakuna kuondoka ni kubanana hapohapo kurithi utajiri na mtoto akitaka kusepa wazazi wanamkataza wanamtengenezea mazingira ya kuwa mrithi wao...
shida ya huku kwetu unakuta familia ina watoto 8 au zaidi, mtoto wa kwanza kamaliza chuo kikuu mdogo wake wa mwisho hata chekechea hajaanza, so kuendelea kukaa home ni kubana tu nafasi kwanza unajishtukia mwenyewe.
Thanks for that I agree with you
 
Mada imenikuta nimeweka mgongo kwny godoro macho kwa dari, natafakari nawaza mbali.. npo mji wa watu takribani 6 months najitegemea kwa heka ya TAESA, kijana niliemaliza chuo mwaka jana na mtaa hausomi.. 26 ndio age yangu lakn natafakar sijui nirudishe mpira kwa kipa😅
 
Ni bora kuanza kujitegemea ukiwa nyumbani kwa wazazi vijana wengi walioondoka home asilimia kubwa bado ramani hazisomi
 
Mkuu kukaa nyumbani umri kuanzia 25+ ..ni uzembe huo
Napingana na wewe. Mimi nimekaa home mpaka naoa nikiwa na umri wa miaka 30+ Baada ya kuoa nikahama nyumbani nikahamia kwenye nyumba niliyojenga na ninayoishi mpaka leo. Sikuona kwa nini nitoe pesa kulipa kodi badala ya kuipeleka kwenye ujenzi wa nyumba yangu mwenyewe.
Tatizo la vijana wengi ni kuwa na mienendo ambayo inakua vigumu kuishi na wazazi (ulevi, umalaya, u-popo, n.k). Kama unaishi kistaarabu, unachangia pesa ya matumizi nyumbani, utapewa heshima zote na hakuna atakayetamani uondoke.
 
Back
Top Bottom