Hawa na hili pekee ndiyo litakalo muokoa Rais wa TFF Malinzi vinginevyo imekula Kwake

Aliyeamini kuwa Malinzi angetoka kwa dhamana ni mpuuzee,sasa kesi ya kutakatisha hela ina dhamana?
 
Hii ina maana kuwa akitunisha msuli atakosa vyote...urais TFF na maisha huru ya uraiani.......

Habari ndiyo hiyo Mkuu. Bado tu nalia na wale Wajumbe Wanne ( 4 ) kwa kuwataka ' waachane ' na kutaka ' kumbeba ' Malinzi na Malinzi mwenyewe kupitia Wakili wake Aloyce Komba aseme tu kuwa ' amejitoa ' katika Kinyang'anyiro cha Uchaguzi Mkuu wa TFF otherwise watamponza na atajiponza.

Yangu macho!
 
Yaani jamaa ni kinganganizi. Si, akubali tu yaishe aachane na huo uenyekiti!!
 
Swala siyo system ila tu kuwa waliigeuza TFF kama duka lao, kila kinachoiingia wanaamishia kwenye matumba yao.
Wamevuna walichopanda.
Soka la Tz linashindwa kukua kisa watu walioko tFF wanakula tu ela, kueendeleza soka letu kwao sio agenda.
Agenda yao ni kupiga tu utafikiri hizo ela ni za kwao.
Uongozi wote wa TFF ulipaswa uondoke, upishe wengine.
 
Malinzi anataka kumwaga mboga ,kwamba anataka akiondoka TFF huku Tz iwe imefungiwa na Fifa , hivyo anafanya vurugu za makusudi
nasi tutawaambia vijana huko keko wanoe vikojoleo vyao wamkomoe
 
Duh..!! Soka letu ndiyo limefikia hapa! Tutasubiri sana.
 
Aliyeamini kuwa Malinzi angetoka kwa dhamana ni mpuuzee,sasa kesi ya kutakatisha hela ina dhamana?
Hivi kutakatisha hela ni kama ya Ndama Mutoto ya ng'onbe!!? Mhh..
 
Reactions: SDG
Hii ina maana kuwa akitunisha msuli atakosa vyote...urais TFF na maisha huru ya uraiani.......
Tatizo la malinzi anaamini kuwa, kwa vile masuala ya soka kutokana na katiba ya FIFA... Mambo ya soka hayatakuwi kuingiliwa na serikali. Sasa jamaa akajiona kuwa yeye ni untouchable! na maovu yake yote akawa ameyaficha chini ya TFF iliyo chini ya FIFA! Hajui kuwa Serp Blatter na genge lake walichomolewa moja baada ya mwingine na FBI... Mimi nadhani ifike wakati FIFA itoe hicho kipengele cha kufugia majizi waache serikali husika zifanye uchunguzi kama Kuna ulazima!
 
kwakua naye alikuwa RAIS akadhan ana Kinga ya kutoshtakiwa vyeo vya urais havijawah kumuacha mtu salama
1.Rais wa FIFA
2.Rais wa Gabon
3.Rais wa TFF
4.Rais wa SOUTH KOREA
5.Rais wa SIMBA
6.Rais wa Tunisia
 
Ni kweli Mashirikisho mengi ya soka yamejaa ubadhilifu kwa kuwa wanaona kuwa mkono wa serikali husika ya nchi ni ngumu kuwashtaki.
Alichosahau Malinzi ni kuwa TFF haifanyi shughuli zake hewani.
 
Fifa wala haijazuia wabadhirifu na wezi au watakatishaji fedha wasishitakiwe na kupewa adhabu. Bali imekataza serikali zisiingilie mambo ya kiutendaji ya kiuongozi au ya kikanuni za kimchezo kuingiliwa na serikali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…