Hawa Nitarejea wa Diamond yupo hoi kitandani, anaomba msaada wa kusaidiwa

Ningekuwa nimemhukumu, nisingemuombea hata hiyo huruma ya Mungu. Ninge'conclude kwa kusema hafai kusaidiwa ova.
Ila badala yake sijashawishi mtu alimsaidie, ila mimi sitaweza kumsaidia kwa hata 100 mbovu na kumwachia Mungu
Una hakika gani kama hiyo huruma uliyo omba kwa Mungu ime work out?
Je ww ni msafi kiasi kwamba una waombea watu wengine huruma kwa Mungu?
 
Tanzania ukisikia MTU anaomba msaada ujue alikua celebrity ( wengi wao),nadhani sasa waanzishe foundation yao mapema waende NHIF
 
Una hakika gani kama hiyo huruma uliyo omba kwa Mungu ime work out?
Je ww ni msafi kiasi kwamba una waombea watu wengine huruma kwa Mungu?

usitake nitoke kwenye mada. Mi si msafi ila mara zote nikiomba Mungu huwa anajibu na ninaimani hata kwa hili amesikia na atajibu vile apandavyo.
 
Tumewachoka kwanini wanaotembeza bakuli kila kikicha wanakuwa hao hao,wacha wapambane na hali zao wenyewe.
 
Hawa wapuuzi hawastahilo huruma, huu ni wakati wa kila mtu kupambana na hali yake, pesa za kubwia unga kama nyoka angelipia bima ya NHIF saa hizi asingetuletea huu upuuzi wake.
Tena hii tabia ikome.
Omba Mungu akupe mwisho mwema.
Ww hujui hatma yako itakuwaje.
Weka maneno ya akiba.
 


Hawa wa 'Diamond' msanii wa Bongo fleva aliyeimba na msanii maarufu Diamond Platnumz wimbo wa Nitarejea kwasasa anahitaji msaada wa hali na mali kutokana na hali yeke ya kaifya kwa sasa,Akihojiwa na kipindi cha Shelawadu Hawa akiwa nyumbani na mama yake alionekana akiwa katika maumivu makali sana huku akionekana akiwa na tumbo kubwa sana na alipohojiwa na mtangazaji w akipindi hicho alisema amaekuwa akipata matibabu yake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa kutolewa maji kila yanapojaa na hakuna lingine zaidi ya hilo na alipohojiwa zaidi alisema kuwa ameambiwa ini lake ni kubwa na halifanyi kazi vizuri hivyo atakuwa anatolewa maji tu ingawa anasema kuwa aliuliza kama kuna tiba nyingine akaambiwa ni kubadili ini na kuweka ini lingine lakini kwasasa huduma hiyo haitolewi Muhimbili labda mpaka mwakani.

Nadhani wengi wamesaidiwa na wadau au serikali kwa sababu sauti zao zilisikika na wenye mamlaka mfano mzuri ni Wastara sasa na huyu ni msanii na mtanzania ambaye naye anahitaji msaada wa hali na mali hasa msaada wa tiba na inavyoonekana kwasasa ni tiba ya ini au kubadili ini yaan Liver transplant kazi ambayo haifanyiki Tanzania mpaka huko nje ya nchi.
Nadhani wadau wanaohusika ni muhimu sasa kuangalia jinsi ya kumsaidia huyu dada ambaye anaangamia taratibu huku akiona kama sasa mwisho wa maisha yake umefika kama kuna uwezekana wa kufanya jambo kwa binti huyu basi tufanye sasa ili kuokoa maisha yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…