Haya anayofanya Freeman Mbowe ni unafiki mkubwa kuwahi kutokea. Angefanya Zitto Kabwe wa ACT moto ungewaka

Haya anayofanya Freeman Mbowe ni unafiki mkubwa kuwahi kutokea. Angefanya Zitto Kabwe wa ACT moto ungewaka

Kwakweli nimechoka na siasa za bongo.

Miezi michache iliyopita Zitto Kabwe alikuwa anashambuliwa Kila Kona kwa sababu ya ruzuku. Wakamwita msaliti na matusi chungu nzima. Leo Chadema chini ya Freeman Mbowe wamechukua ruzuku na wamekausha kimyaaa. Unafiki!

Miezi michache iliyopita walimshambulia Zitto kila kona kwa kukubali kufanya kazi ya pamoja katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakamwita mnafiki akayaoga matusi mazito kabisa. Leo mgeni rasmi kwenye mkutano mkuu wa BAWACHA ni Rais Samia. Duu, huu ndio upinzani wetu.

Joe Biden wa democratic anakuwa mgeni rasmi wa mkutano mkuu wa Republican. Haijawahi tokea ni Chadema tu ndio utayaona haya maajabu. Wanachukua pesa wanasahau na malengo makuu ya upinzani.

Hongera Zitto Kabwe sasa tumewajua wanafiki halisi wa mageuzi ya Tanzania.
Chadema walipokandamizwa na awamu ya 5 wote tulikuwa kimya tukiwaacha wateseke peke yao.

Leo wameridhiana na awamu ya 6 tunawalaumu kwamba ni wasaliti na kupinga hata wao kupokea ruzuku ambayo wameipokea baada ya matokeo mazuri ya maridhiano.

Hii ndio maana ya unafiki.
 
Wewe ni maiti umekufa alafu umeoza unanuka! Uko tayari kushabikia upumbavu wowote kikubwa kulinda chadema na maslahi Yako huna lolote
Unajua wanachadema wangapi walifungwa kwa kesi za uongo kipindi cha jiwe? Unajua wangapi wametoka? na wangapi bado wako magelezani.? Hujui njinsi mbowe anavyopambania.
 
Naona mnajiongelesha kwa kupokezana. Ukweli ni kwamba CHADEMA imeamua kuwapiga chenga ya mwili wanafiki. Wakati Tundu Lissu analimwa risasi mlimcheka na kumdhihaki, Mbowe mkamwita gaidi na ikawa dhambi kuwa mwanachama wa CHADEMA. Leo nashangaa wanaoumia na maridhiano ya chadema na Serikali ni Hawa wanafiki walioikebehi CHADEMA kipindi Cha mateso.
 
Back
Top Bottom