Haya bei hizo kwa wale wasafiri wa ATCL

Basi mororooo, mapanga shaaaaaaa!
160,000 one way, two way 320,000/-. Au kuna punguzo? Watabaki kupanda wale wale. Na ATCL ina madeni ya Nyuma. Kila senti itaenda kulipa deni. Mpaka 2025 madeni yatakuwa bado hayajaisha. Atakuja Rais mwingine atapuyanga na yake.
 
Go and return za ndege haziko hivyo mkuu, ikiwa one way ni 160,000, kwenda na kurudi inaweza kuwa 270,000
 
TUNAOMBA NA WEE UWE MTU WA KWANZA KUPANDA PIA NA ULIPE HIYO NAULI

OVA
Uchumi wa Kati tutaufikia, Usafiri wa muda mfupi kwenda mwanza na Arusha unafanya biashara na kurudi Dar siku hiyo hiyo.

Hapa kazi tu .

 
Mleta mada ni kile kikundi cha "wanapropaganda" wa Lumumba mitandaoni,wakiongozwa na Chriss Lukosi kule Fb.
Hii wamekaa tu watu na kuitengeneza,haina ukweli wowote.Mpaka sasa bado ndege mpya hazijanyanyuka...Hata system mpya ya booking online ipo off...Lazima wezi wa tiketi waliwe vichwa kwanza.

Sasa hizi Propaganda za Wakudadavuwa zinaweza ama kulipaisha shirika au kuliuwa.Maana mtu akiona bei hii hapa,akienda akakuta ipo juu zaidi atasema ATCL ni wahuni,mitandaoni bei hii,uhalisia ni bei hii.Matokeo yake manapoteza abiria kijinga jinga sbb ya Propaganda za Lumumba.

Mmeshaleta ndege,nyie kaeni pembeni na siasa zenu.Tuachieni ndege zifanye kazi.Kama kutekeleza ahadi mshatekeleza,haina haja ya "siasa" huku kwingine.Bei zitaendana na soko,sio siasa za kufurahisha watu halafu ATCL irudi ilikotokea.Mshindwe na mlegeee!!Mnataka tena kuliuwa shirika letu na siasa zenu za kibwege.
 
Mbona nauli ni kama ya PW? Labda taaifa hii haina ukweli!!
 
Dogo kwa hiyo hadi kuwe na online booking system?...unatawaliwa na chuki,hasira....sasa hapo kilichokuudhi nini?
 
Kuanzia saivi wanitegemee waweke na ya Mbeya.


[emoji817]
 
Kila kitu negative,bavicha mnaumwa na nini?
 
Dogo kwa hiyo hadi kuwe na online booking system?...unatawaliwa na chuki,hasira....sasa hapo kilichokuudhi nini?
Nitawaliwe na chuki ya nini?Mimi niko huru...ninapongeza na kukosoa panapostahili...
Kinachoniudhi na watu kama wewe kuingiza "siasa" kwenye biashara.Ndege zimeshakuja,acheni kanuni za biashara zifuate mkondo wake.Watu wameshaamini kuwa ndege zimeshuka na sio siasa tena bali ni uhalisia kuwa ndege zimefika.

Sisi tumeamini,tumefurani na tumeziona...Siwezi kuwa na chuki kwa ndege nilizozipigia debe na kutukanwa kutwa kucha,ila nakuwa na "chuki" na watu kama wewe wanaoongea kitu ambacho hakipo na hakijawekwa.Sio lazima upige siasa kila mahali.Wewe subiri utapata bei.

Halafu tuheshimiane kuniita "dogo"...Mi sio dogo aseee!!Tafadhali sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…