Haya Kombe la Dunia hilo linakuja tuanze sasa kugawana Timu za Kushabikia mapema

Haya Kombe la Dunia hilo linakuja tuanze sasa kugawana Timu za Kushabikia mapema

Mkuu, tatizo wewe unadhani labda kila mtu ni lazima ashabikie timu kubwa.

Unabaki mdomo wazi kisa nini?

Mimi naishabikia kwa mapenzi kutoka moyoni na siyo kufuatana mkumbo km nyie kila mtu Germany Germany Germany...

Sawa Baba yameisha!
 
Mkuu, kuishabikia timu hakuhusiani kabisa na kujua mpira. Ushabiki unaendana na mapenzi na hisia kutoka moyoni.

Uchambuzi wa soka ndiyo unaendana na ujuzi/elimu ya soka.

Shikamoo Mkuu.
 

Wewe lazima tu utakuwa unajua Mpira halafu pia umeucheza vile vile. Mpaka sasa bado namuwazia na simpatii Picha huyu Member aliyenitajia Saudi Arabia. Yaani Mwarabu aache Kujivisha Mabomu ya Kujilipua acheze / asakate mpira kweli? Kama kuna Timu ambayo natabiri mapema itarudi Kwao na Zawadi la Kapu la Magoli / Mabao ya Kufungwa huko Urusi katika Fainali za Kombe la dunia basi ni Saudi Arabia. Halafu wako katika Kundi baya sana lenye Timu zenye roho mbaya tupu katika Kandanda.
 
Una uhakika kabisa kwamba Bange / Bangi uliyoivuta leo ilikuwa sahihi kwa matumizi kamili ya Mwanadamu Mkuu?
Yeah... Simba wananyakua UCL... piga ua. Liverpool lazima wakamate kombe la dunia.... Barca wanakamata EURO na Mabwe guys wanakamata VPL...

Mi ntakuwa natibu maumivu ya watakaokuwa wanaumia na matokeo
 
mi nashabikia spain......ila pia nashabikia saudi arabia naomba tu ipite kwe makundi na iran apite kwe kundi lake wakutane itakua bonge la burudani dadeki
 
TIMU ZA KIAFRIKA AMBAZO KUTOKANA NA MAKUNDI WALIYOMO BASI NINA UHAKIKA KWA ASILIMIA 100% KUWA ZITATOLEWA KATIKA HATUA YA MAKUNDI NI:

1) NIGERIA
2) TUNISIA
3) MOROCCO


TIMU ZA KIAFRIKA AMBAZO ZIKIKAZA KIDOGO TU KALINGANA NA MAKUNDI WALIYOMO BASI WATATOBOA NI:

1) EGYPT
2) SENEGAL


Mimi Ni Mshabiki Wa ENGLAND Lakini Sitegemei Hata Kuvuka Robo Fainali.

But ingawa Ninazichukia GERMANY na BRAZIL ukweli utabakia kuwa Ndiyo Timu Pekee Hizi Zenye Nafasi Kubwa Ya Kuchukua Ubingwa.

Na ARGENTINA kama Kawa Wataingia RUSSIA wakiamini Kuwa na MESSI Ndiyo Kushinda Kila Kitu hatimae Watajikutia Wanarudi Kwao Kila Mtu Kwa Ndege Yake.

Ukweli Usiofichika HITLER Kwenye Soka Katuachia Kizazi Chenye Roho Mbaya Kama Yeye.
 
Form One hadi Form Four nilikuwa Mchezaji wa Kutumainiwa kabisa wa Timu ya Shule hapo nchi jirani tu ambako UKIMWI ulizinduliwa rasmi na Hayati Philemon Lutaya na nilicheza hadi katika Mashindano ya Shule makubwa huku mnayaita UMISETA na nilikuwa nikicheza sana nafasi za Beki wa Kulia au Kushoto ila nilipofika Kidato cha Tano kwenda cha Sita kutokana na aina ya Shule niliyokuwepo tulibahatika kuwa na Kocha wa Kizungu ambaye pia alikuwa ni Mwalimu wetu na alinibadilisha kutoka Kucheza nafasi ya Beki wa Kulia na Kushoto na sasa akanitengeneza hadi nikawa nacheza Kiungo cha chini ( yaani namba Sita ) na nakumbuka wakati huo nilikuwa nawaiga sana Marafiki zangu wachezaji mahiri wa Kibongo wakati huo Selemani Matola ' Veron ' na Waziri Mahadhi ' Mendieta ' uchezaji wao na nilitokea Kukubalika mno na Wanafunzi wenzangu hadi na Raia waliokuwa wakiniona nikicheza na nakumbuka hata katika hizo Shule zote nilikuwa napendwa na Mademu kwakuwa nilikuwa ' nakichafua / nakipiga ' sana dimbani Mkuu.

Niliachana na Mpira rasmi baada ya kumaliza Kidato cha Sita na kutingwa zaidi na ratiba zingine za Kitaaluma japo hata wakati nilipokuwa Chuo Kikuu nilijaribu Kucheza lakini sikuweza tena kuwa vizuri kama enzi zangu kwakuwa Mpira wangu mwingi nilipokuwa Chuoni nilikuwa nauchezea sana Gesti / Loji huku Waamuzi / Marefarii wakiwa ni Wahudumu wa hizo Nyumba za Kulala Wageni nilizokuwa nikiingia.

Kwa sasa huwa nikipata muda najaribu kucheza kidogo pale Leaders Club na akina Bakari Malima ' Jembe Ulaya ', Ally Yusuph ' Tigana ', Mtwa Kihwelo ' Dally Kimoko ' na Omary Kapilima ' Caminero ' au pande za Tanganyika Packers Kawe na akina Omary Mkuku, Kudra Omary na Benito John ila siko ' active ' kivile kwakuwa Kasi ya Vyuma Kukaza Kimasha sasa imeongezeka hivyo ' Mbichwa ' wangu muda wote unawaza nitawezaje kuielewa Kasi na hii Falsafa ya Maisha ya Rais JPM.

Ni hayo tu Mkuu.
Kweli wewe uliwahi kukipiga, sisi wengine ukituletea kwenye mguu utangonga katika ugoko kisha utapiga katika kidevu habari itaishia hapo, wazazi walituzuia kucheza michezo ya kipuuzi, walisema ''mpira utakufikisha wapi?''.
 
Mtu yoyote anayeshabikia England hajui kabisa Mpira. Samahani kama nitakuwa nimekuudhi / nimekukwaza kwa hili Mkuu.
Mkuu, swali lilikuwa kuchagua timu tunazoshabikia, au timu tunazohisi zitafanya vizuri?
 
Back
Top Bottom