Haya mambo ya kumwagiana maji wakati wa 'Birthday' mtakuja muue mtu

Kuna wengine wanakumwagia maji machafu aseee hii inakera sanaaa
Mimi iliwahi nitokea siku hiyo nimepigilia pamba mwisho wa sanduku yaani nimetokelezea juu mpaka chini
Banaaa wee mara maji chwaaaaa…… kwanzia kwenye nywele mpka miguuni yaaani nilichukia but sikua na namna
Hii stlye sio kabisa watu waziachie hukohuko boarding kwao chaaaaa
 
Pole sana Next time nitakupeleka Ibiza kusherekea birthday sidhani nao kama wana tabia kama hizi ,teh teh
 
Mimi mtu akinimwagia maji na uzee huu namjeruhi na kitu chenye ncha kali....kudadeki....ishakuwa nongwa sasa....
 
Hahaha huwa wanaandaa na nguo za kubadilisha?

Imagine unamwagiwa maji ofisini.
 
The reason I celebrate birthdays privately... I hate surprises... Siku ntakayomwagiwa maji atakaenimwagia hana bahati maana ntamdunda
 
ujinga waswahili kwa kuiga balaa,soon watapakazana mavi.walianza na kupakazana keki usoni
 
Mkuu...
Bora unge sema tu wazi, nini kimejiri baada ya mtu mzima kumwagiwa maji😕
 
Hii kitu mimi mwenyewe sipendi birthday yenyewe sikumbuki ni lini nimesherekea
Dah!! Kumbe tupo wengi.
Mara nyingi hukumbuka leo siku yangu ya kuzaliwa nikiwa tayari nipo kitandani naitafuta siku nyingine, kile kitendo cha kufikiria mihangaiko ya siku nzima, ndio baadae hukumbuka...ah! Kumbe leo siku yangu ya kuzaliwa!!, tayari siku inakuwa imeisha.
Wakati mwingine hupita wima hata sikumbuki, wacha kusheherekea.
Baada ya kuoa limekuwa jukumu la wife kunikumbusha, mie nasema na hela tu.
Dah! Maisha haya!!, wacha tu.
 
Tupo wengi mkuu ,kuna mda mtu unasahau kula achilia mbali kukumbuka siku ya kuzaliwa ,Mara nyingi mama ndio hunikumbusha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…