Haya masuala mawili naomba jibu, Mwalimu kamaliza kazi yake, sisi tukoje?

Haya masuala mawili naomba jibu, Mwalimu kamaliza kazi yake, sisi tukoje?

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
Mwalimu ndiye alianzisha mbio za Mwenge nchini, nia ikiwa kuenneza upendo na umoja kati ya Mwatanzania.

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, 1958 wakati akihutubia kikao cha 35 cha Umoja wa Mataifa na kuyarudia tarehe 22 Oktoba, 1959 wakati akihutubia Baraza la Kutunga Sheria la Tanganyika (LEGCO) alisema.

“Sisi watu wa Tanganyika, tunataka kuwasha Mwenge na kuuweka juu ya Mlima kilimanjaro, umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini pale ambapo hakuna matumaini, upendo pale ambapo pamejaa chuki na heshima palipo na dharau”

Maneno haya hata baada ya miongo ni mazito na yanatia tumaini kwa yeyote anayeyasikiliza. Na ndiyo maana tunayaenzi kivitendo hadi leo, tunaenzi fikra zilizo njema za Mwalimu.

Mwalimu Nyerere alizaliwa 13th April 1922, na kufariki 14th October 1999.
Tukio la msiba wa baba wa Taifa nalo lilikuwa kubwa sana kwa nchi hii na sina nia ya kurudia kueleza umuhimu wake.

Sasa leo nimeona hata katika magazeti watu wanatumiana HAPPY NYERERE DAY!

Maoni yangu ni kama ifuatavyo:

1. Kuzima Mwenge ni shughuli nzito na mahsusi kwa makusudi yaliyotarajiwa. Sielewi kwa nini imechanganywa na siku kama hii ya kumkumbuka Mwalimu Nyerere.

2. HAPPY NYERERE DAY iwe siku ya KUZALIWA Mwalimu Nyerere na sio siku ya kumbukumbu ya msiba wa kitaifa.
Tarehe ya 14 October 1999 ni simu ya REMEMBRANCE ya Mwalimu.

Hatuwezi kuwa na Happy Nyerere Day siku ya kumbukumbu ya msiba mzito uliotupata wa Mwalimu.

Wadau naomba tujimwage maoni maana kuchanganya hivi vitu, vizazi vijavyo havitatuelewa.

Nawasilisha!
 
Kuzima mwenge wa uhuru na sherehe za Mwalimi Nyerere ni sherehe vitatu tofauti.
1. Mwenge wa Uhuru
2. Mwalimu kuzaliwa
3. Kumbukumbu kifo cha Mwalimu
 
Hakuna sababu ya msingi mpaka Leo hii 2022 kuendelea kukimbiza taa inayo toa moshi [ mwenge ] kwa bajeti ya gharama kubwa isiyo kuwa na faida yoyote ile kwa taifa letu.

Ujinga ni gonjwa baya sana liki komaa utengeneza kitu kinacho itwa upumbavu, taifa letu hili lina ujinga ulio komaa.
 
Hakuna sababu ya msingi mpaka Leo hii 2022 kuendelea kukimbiza taa inayo toa moshi [ mwenge ] kwa bajeti ya gharama kubwa isiyo kuwa na faida yoyote ile kwa taifa letu.

: Ujinga ni gonjwa baya sana liki komaa utengeneza kitu kinacho itwa upumbavu, taifa letu hili lina ujinga ulio komaa.
Kama huelewi kwa nini Mwenge unakimbizwa unakaribishwa kwenda Afghanistani.

Halafu kimbelembele chako tu, hata mafuta huchangii!
 
Wanazi wa CCM walikurupuka. Na jamaa hawajielewi ma hawaambiliki, na kukosolewa au kurekebishwa sio sehemu yao ya maisha.
 
Hakuna sababu ya msingi mpaka Leo hii 2022 kuendelea kukimbiza taa inayo toa moshi [ mwenge ] kwa bajeti ya gharama kubwa isiyo kuwa na faida yoyote ile kwa taifa letu.

: Ujinga ni gonjwa baya sana liki komaa utengeneza kitu kinacho itwa upumbavu, taifa letu hili lina ujinga ulio komaa.
Mwenge ni uchawi, Mwenge ni laana, Mwenge ni uzinzi, mwenge ni ulevi, mwenge ni ibada ya shetani
 
Hakuna sababu ya msingi mpaka Leo hii 2022 kuendelea kukimbiza taa inayo toa moshi [ mwenge ] kwa bajeti ya gharama kubwa isiyo kuwa na faida yoyote ile kwa taifa letu.

: Ujinga ni gonjwa baya sana liki komaa utengeneza kitu kinacho itwa upumbavu, taifa letu hili lina ujinga ulio komaa.
Nyie vijana ndio mnayea kwenye vigae vya vyungu ambavyo mama zenu walipikia mlipokuwa mnakuzwa.
 
Mwenge ni uchawi, Mwenge ni laana, Mwenge ni uzinzi, mwenge ni ulevi, mwenge ni ibada ya shetani
Ukilitazama lile shimo la choo chenu cha shimo kule kijijini kwenu, wewe unaona harufu tu, lakini ndio linalokusanya uharo na uchafu wenu wote pale nyumbani kwenu.

Ujaliwe hekima ya kulielewa hilo.
 
Ukilitazama lile shimo la choo chenu cha shimo kule kijijini kwenu, wewe unaona harufu tu, lakini ndio linalokusanya uharo na uchafu wenu wote pale nyumbani kwenu.
Ujaliwe hekima ya kulielewa hilo.
Kwahiyo unataka kusema na mimi nianze kuabudu kibatari?
 
Mwenge ni uchawi, Mwenge ni laana, Mwenge ni uzinzi, mwenge ni ulevi, mwenge ni ibada ya shetani
Naunga mkono hoja. Haiwezekani watu wazima na akili zao wazunguke na mshumaa nchi nzima wakiuabudu na kuutukuza eti ndio umetuletea uhuru na unatuletea maendeleo.
 
Wadau naomba tujimwage maoni maana kuchanganya hivi vitu, vizazi vijavyo havitatuelewa.
Naungana nawe mkuu 'Jidu', kwa haya uliyoandika hapa; lakini ningependa kukukumbusha wewe na wasomaji wa mada yako, kwamba siku zimekwenda sana.

Tanzania ya leo siyo Tanzania ya Mwalimu Nyerere tena. Leo hii, sana sana ni kutumia tu jina lake ili mahitaji yetu yafanikiwe.

Hatuna tena ile 'commitment' iliyokuwepo nyakati zile katika mambo yaliyonuiwa kufanywa. Leo hii tunapiga tu midomo, basi mradi mahitaji yetu yanatimizwa.

Lakini naomba usinielewe vibaya, sisemi kwamba hatuyatamani mengi aliyosimamia Mwalimu, hapana. Kuyataka na kuwa na moyo na uwezo wa kuyafanya na kuyaishi ndio hatunavyo.

Ndiyo maana tunafanya kila njia tuonekane tunaenzi, lakini zaidi ya kuenzi hakuna kitu tukifanyacho kwa sababu ya madhaifu makubwa tuliyo nayo, na kukosa uwezo wa kushawishi kama aliokuwa nao Mwalimu.
 
Naungana nawe mkuu 'Jidu', kwa haya uliyoandika hapa; lakini ningependa kukukumbusha wewe na wasomaji wa mada yako, kwamba siku zimekwenda sana.

Tanzania ya leo siyo Tanzania ya Mwalimu Nyerere tena. Leo hii, sana sana ni kutumia tu jina lake ili mahitaji yetu yafanikiwe.

Hatuna tena ile 'commitment' iliyokuwepo nyakati zile katika mambo yaliyonuiwa kufanywa. Leo hii tunapiga tu midomo, basi mradi mahitaji yetu yanatimizwa.

Lakini naomba usinielewe vibaya, sisemi kwamba hatuyatamani mengi aliyosimamia Mwalimu, hapana. Kuyataka na kuwa na moyo na uwezo wa kuyafanya na kuyaishi ndio hatunavyo.

Ndiyo maana tunafanya kila njia tuonekane tunaenzi, lakini zaidi ya kuenzi hakuna kitu tukifanyacho kwa sababu ya madhaifu makubwa tuliyo nayo, na kukosa uwezo wa kushawishi kama aliokuwa nao Mwalimu.
Nakubaliana na wewe mkuu kwa hiyo observation
Wanasiasa wanatumia tu jina la Mwalimu kwa covenience yao, lakini moyoni hawafanyi kile ambacho Mwalimu angefanya.

Kweli nyakati zimesonga, lakini hii ya kulundika pamoja legacy ya Mwalimu na mbio za mwenge ndiyo naona dalili za kumrelegate Mwalimu into obscurity.
 
Kweli nyakati zimesonga, lakini hii ya kulundika pamoja legacy ya Mwalimu na mbio za mwenge ndiyo naona dalili za kumrelegate Mwalimu into obscurity.
Aaah! Hata wafanye nini, kum"'relegate Mwalimu into obscurity'", hilo haliwezekani kabisa. Hakuna kiongozi wa leo aliye na uwezo wa kufanya hivyo. Wote wataendelea hivyo hivyo kuwa wanamtumia tu kivyao ili wakubalike kwa wananchi.

Lakini hakuna hata mmoja anayeweza kusogelea ''caliber' ya uongozi wa Mwalimu Nyerere.
 
Back
Top Bottom