Haya ndiyo maandamano ya ovyo kuwahi kutokea katika nchi yetu. Hata wanaoandamana hawajui kwanini wanaandamana!

Haya ndiyo maandamano ya ovyo kuwahi kutokea katika nchi yetu. Hata wanaoandamana hawajui kwanini wanaandamana!

Hebu weka ile aerial picture aliyopost tulia insta... Mimi siwezi natumia kitochi
Screenshot_20240220-184228.jpg

Hii hapa mkuu mbeya imeitika sanaaa
 
Haina tofauti na wanachama wengi wa CCM ambao wanaburuzwa kwenda kupiga kura na hawajui kwa nini wanachagua chama kinacholikwamisha Taifa kimaendeleo..

Wachache ndani ya CCM ndo wanafaidika
CCM wanaonufaika hawazidi elf 5 wengine wote wanasindikiza pekee
 
Mmesha waswagwa dar, Mwanza na Mbeya, kwenye hub muhimu zote, na hali haikuwa nzuri ilivyotegemewa, sasa uongozi mnategemea kuziswaga nyumbu pande zipi, nadhani mwende DODOMA/ARUSHA/MOSHI, sasa,Ndizo point zilizobaki.
 
Ukitaka soma, ukitaka acha lakini ukweli ni kwamba haya maandamano ya Freeman na washirika wake ni ya hovyo na sijawahi kushuhudia.

Wanaojua kwa nini wanaandamana ni freemani na washirika wake, lakini waandamanaji hawajui kitu chochote!

Hawajui kwa nini wanatembezwa kwenye jua Kali mchana kutwa, hawajui na nawaonea huruma kwakuwa hawajui.

Wakina Freeman wakimaliza maandano jioni ya Leo watakuwa hotelini wakila minofu ya kuku na kushushia john walker pamoja na k vant! Wenzangu na Mimi watakuwa Ituha, Isyesye, Ilemi na Ilolo wakitafuna numbu na kulala fofofo.

Wenzao yaani ile big 8 hawako pale kupoteza muda, wapo kazini na jioni posho inaenda kwa familia zao, nyinyi walala hoi mnaowasindikiza mpaka uwanjani wakabwabwaje Kisha wasema pipooz na nyinyi kwa njaa Kali mtaitikia poweeer.

Mnaonekana malofa! Watanzania tuamke, Tusiwe madaraja au mirija ya kuwaburudisha watu.

Kwa nini hatubadiliki? Wakienda ujerumani wakirudi hawasemi walichovuna kule! Chadema walipewa magari na pesa nyingi na wadau mbalimbali ,yakaishia kusikojulikana big 8 hawajawahi kusema popote.

Chadema hawana mpango wa kuwa watawala ila wanatumia siasa kama kazi na mtaji wao ni sisi manamba tunaovaa kombati na kuingia mabarabarani bila sababu! Tugutuke.
Kwa mbowe hii ni faida maana akienda ujerumani na kujiita chama cha upinzani anapewa grant ya kuendeleza democrasia

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Mmesha waswagwa dar, Mwanza na Mbeya, kwenye hub muhimu zote, na hali haikuwa nzuri ilivyotegemewa, sasa uongozi mnategemea kuziswaga nyumbu pande zipi, nadhani mwende DODOMA/ARUSHA/MOSHI, sasa,Ndizo point zilizobaki.
Wanaandanmana hadi na vibaka wale wanaoona maandamano ni furusa maana wanaweza kudokoa chochote kitu

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom