Haya ndiyo mambo ya ajabu niliyowahi kuona na kushuhudia kwa macho yangu, sitoyasahau katika maisha yangu

Haya ndiyo mambo ya ajabu niliyowahi kuona na kushuhudia kwa macho yangu, sitoyasahau katika maisha yangu

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
10,587
Reaction score
13,425
Dunia Ina Mambo mengi sana na ni rahisi sana kupinga au kubisha Kama hayo Mambo ya ajabu hujayashuhudia na pia ni Bora uwe unasimuliwa tu na usije kukutana nayo maana unaweza ukadhurika ama ukawa hai.

Naam leo nimepata muda nikaona ni Bora nishee haya machache niliyokutana nayo katika huu ulimwengu,


(1) sitosahau nilipokutana na mtu mrefu asiyekuwa na mwisho inasadikika ni jini

Yapata mishale ya saa saba usiku, niliwasha pikipiki yangu kutoka Kambarage kuelekea Matanda kwa wale wenyeji wa Shinyanga wanayaelewa haya maeneo.

Nilikuwa nafanya kazi ya ulinzi kitengo Cha supervising na kupiga patrol kuwaausha walinzi usiku kwa hiyo mishale ya saa saba , saa sita ,saa nane mpaka saa tisa ndyo ilikuWa mida yangu kwenda kuwapatrol walinzi ili kazi za watu ziwe salama.

Nakumbuka nilitoka nyumbani vizuri pale Kambarage nikafika mitaa ya ofisi ya mkuu wa wilaya ili nishike barabara ya kuingia Tanesco Matanda.

Nikawa nakaribia kupita geti la ofisi ya mkuu wa wilaya, Mara gafla nikaona mtu amevaa nguo nyekundu akiwa amesimama katikati ya barabara ninapoelekea Mimi,

Kiukweli haikunishitua nikaendelea kusogea maana ile njia huwa napita sana, nilishawahi kukuta watu wanaogeshana usiku wa manane, Mara watu wanavunja Nazi kwa hiyo nilijua tu huyo aliyevaa nguo nyekundu ni mtu Kama wale ninaowaonaga.

Sasa nilipokuwa naendelea kumkaribia cha ajabu alikuwa anazidi kuwa mrefu na njiani hataki kutoka ilinibidi nipunguze spidi huku nikishusha gia za pikipiki mpaka namba moja hapo nilikuwa nishamkaribia kwa ukaribu na alikuwa ni mrefu kichwa hakionekani hana mwisho.

Sikuamini nilichokiona na ndiyo ilikuwa ni Mara yangu ya kwanza kukutana na kitu kama kile, niliamua kuzima taa na kuziwasha, kitendo cha kuzima nakuwasha tu, lile dubwana lilipotea kama upepo sikuliona tena akili yangu ilibadilika nilikimbiza pikipiki kama mwendawazimu kurudi nyumbani maana sikuendelea na Safari yangu, siku iliyofuata niliumwa sana nililala ndani bila kutoka kwa muda wa siku tano.


(2) NILIUA NYOKA WA MTU, MWENYE NYOKA ALINIFUATA AKAANZA KUNIDAI NYOKA WAKE.

Miaka ya nyuma nilikuwa nafanya kazi katika kiwanda kimoja cha chai huko Iringa kwa majina sitotaja, siku hiyo ilikuwa ni siku ya usafi tulikuwa tunasafisha maeneo ya kiwanda maana siku ya usafi wa mitambo na mazingira kwa ujumla uzalishaji husimama.

Mimi nilikuwa nafyeka majani, lile eneo tulipangiwa wawili lakini mwenzangu kwa muda ule alienda kunywa chai atakaporudi na mimi niende tulipeana zamu.

Kipindi nafyeka gafla nikaona nyoka mwezi anakuja upande wangu, ni mrefu mwembamba, Mimi binafsi nyoka nawajua ni moja Kati ya nyoka wenye sumu kali.

Sikutaka kushangaa ikanibidi nimuue, nilimkata na kwanja tenganisha kichwa na kiwiliwili akafa.

Mara punde alikuja mmoja wa maafisa wakubwa pale kiwandani akihema kama mtu aliye na presha, alinifokea na machozi yakimtoka alisema "kwanini umeua nafsi yangu"

"Huyu ndiyo ananifanya niishi hapa"

Nilishikwa na butwaa sana, maana yule alikuwa ni boss mkubwa nilibaki najiuliza huyu boss na manyoka wapi na wapi.

Na hakuishia hapo aliendelea kunitishia amani akidai nyoka wake arudi na ule ndiyo ilikuwa ni ulinzi wake.

Mimi nilipoona hivyo nikajua kabisa hii ni serious sana nilimuomba msamaha sana nikamwambia sikujua.

Hakika like kitendo cha mtu kusema nimeua nafsi yake kilinistaajabisha sana.


(3) SITOSAHAU NILIPOMKUTA MMASAI AKIONGEA NA CHUNGU NA CHUNGU KILIMJIBU.

Hii nimeshuhudia kwa macho yangu mpaka niliona Kama ninaota, nakumbuka tulikuwa kwenye mitihani ya darasa la saba tena ulikuwa ni muda wa mapumnziko.

Nilikwenda kutafuta darasa moja ambalo lilikuwa lipo mbali na yale tuliyokuwa tunafanyia mtihani nikiwa na lengo la kwenda kupumnzika nitulize akili yangu kidogo.

Nilipokuwa nakaribia kwenye hilo darasa nilianza kusikia sauti ndipo nilipoamua kuchungulia, nikamuona mwanafunzi mwenzangu mmasai, tuliyekuwa nae darasa moja na yeye alikuwa nafanya mtihani wakuhitimu darasa la saba.

Kilichonishangaza alikuwa ameweka chungu pembezoni kabisa ya darasa juu ya dawati kile chungu kilikuwa kinawaka Moto.

Sasa kipindi naendelea kuchungulia alikuwa anaongea peke yake kwa lugha ya kimasai huku akiwa amekunja mikono yake na amenyenyekea kweli mbele ya hicho chungu,

Alipomaliza kuzungumza kile chungu kilimjibu kwa sauti ya kike, kilizungumza kwa lugha ya kimasai pia, niliogopa sana kile kitendo niliinama chini nikasota kwa hatua kama tano hivi nikakimbia sana kuondoka kwenye hilo eneo.

Muda wa mtihani ulipofika masai nae akaja kupiga pepa, tulivyomaliza mitihani sikumuona yule jamaa mpaka sasa ila siku hiyo sikuwa na amani na nilimuogopa sana.


(4)NILISHUHUDIA MAMA WA KISUKUMA AKIIMBA NYIMBO NZURI NA KUMTOA NYOKA TOKA MAFICHONI.

Ukistaajabu ya Musa basi utayaona ya Firauni na wanasema tembea uone mengi na ujifunze.

Nikiwa bwana mdogo nilikwenda kumtembelea shangazi Shinyanga Kijijini baada yakufunga shule.

Siku hiyo nakumbuka ilikuwa ni mchana mishale ya saa 8 mchana tulikuwa tumekaa karibu na mlango tunakula chakula cha mchana.

Mara gafla alipita panya buku kwa spidi ya ajabu sana bila kujali chochote yule panya aliingia ndani maana mlango ulikuwa wazi.

Kabla hatujamaliza kumshangaa panya buku gafla tukashitushwa na bonge la nyoka jeusiii na lenyewe likazama ndani, kumbe lilikuwa linafukuzia kitoweo chake panya buku.

Na sisi baada ya kuona nyoka tukaruka wote kila mtu na njia yake maana wote tulikuwa watoto, tuakaanza kupiga makelele nyoka nyoka nyoka!!

Jirani alikuwepo mama mmoja wa kisukuma alikuja na akatuambia acheni makelele, alimchungulia dirishani Yule nyoka alimuona kajificha kwenye mtungi alituambia nipeni rungu halafu mkae huku.

Alikaa pembezoni na ule mlango alioingilia nyoka, alianza kuimba nyimbo ya kisukuma kwa sauti nzuri sana huku ameshikilia rungu

Aliimba kama dakika tano hivi kisha akatuambia chungulieni hapo dirishani kipindi naimba akikaribia mlangoni mniambie

Kweli yule mama aliendelea kuimba na kadri anavyoimba nyoka alikuwa anasogea taratibu taratibu.

Kilichonishangaza kingine ni pale mama alipokuwa anaacha kuimba na nyoka nae anasimama mpaka yule mama alipoendelea kuimba nyoka nae aliendelea na Safari mpaka alipokuwa amekaa yule mama.

Na ndipo ukawa mwisho wa maisha yake yule nyoka baada ya kukutana na rungu zito alipomkaribia yule mama wa kisukuma.

Nitaendelea kushea kumbukumbu zingine na kama unakumbukumbu za kushea ruksa kushea ili tusome maajabu ya dunia.
 
Hii ni simulizi yatatu ikionyeshakanda ya ziwainaongoza kwa ulozi,simulizi moja ni toka kwa umughaka,y pili simkumbuki jina ila inaitwa babu yangu kama rafiki yangu na wewe hii
Mambo ya dunia hakika yanashangaza.
 
Ujuzi kama huu tunaupiga vita kwa kusema ni uchawi ila kumbe ukute ni nguvu chanya ambazo tungezikubali na kuziboresha zingeweza kutatua changamoto zetu za kila siku.

Hizi dini zimetudumaza akili hadi tumeacha mambo yetu mazuri kwa kuyakashfu. Kama hizi nguvu tukizikubali, tukaziendeleza na kuzienzi tutakuwa sehemu salama kuliko hizi dini zinazokubali za mashoga.
 
Dunia Ina Mambo mengi sana na ni rahisi sana kupinga au kubisha Kama hayo Mambo ya ajabu hujayashuhudia na pia ni Bora uwe unasimuliwa tu na usije kukutana nayo maana unaweza ukadhurika ama ukawa hai.

Naam leo nimepata muda nikaona ni Bora nishee haya machache niliyokutana nayo katika huu ulimwengu,

(1) sitosahau nilipokutana na mtu mrefu asiyekuwa na mwisho inasadikika ni jini

Yapata mishale ya saa saba usiku, niliwasha pikipiki yangu kutoka kambarage kuelekea matanda kwa wale wenyeji wa shinyanga wanayaelewa haya maeneo.

Nilikua nafanya kazi ya ulinzi kitengo Cha supervising na kupiga patrol kuwaamusha walinzi usiku kwa hiyo mishale ya saa saba , saa sita ,saa nane mpaka saa tisa ndyo ilikua mida yangu kwenda kuwapatrol walinzi ili kazi za watu ziwe salama.

Nakumbuka nilitoka nyumbani vizuri pale kambarage nikafika mitaa ya ofisi ya mkuu wa wilaya ili nishike barabara ya kuingia tanesco matanda.

Nikawa nakatibia kupita geti la ofisi ya mkuu wa wilaya, Mara gafla nikaona mtu amevaa nguo nyekundu akiwa amesimama katikati ya barabara ninapoelekea Mimi,

Kiukweli haikunishitua nikaendelea kusogea maana ile njia huwa napita sana, nilishawahi kukuta watu wanaogeshana usiku wa manane, Mara watu wanavunja Nazi kwa hiyo nilijua tu huyo aliyevaa nguo nyekundu ni mtu Kama wale ninao waonaga.

Sasa nilipokuwa naendelea kumkalibia Cha ajabu alikua anazidi kuwa mrefu na njiani hataki kutoka ilinibidi nipunguze spidi huku nikishusha gia za pikipiki mpaka namba moja hapo nilikua nishmkaribia kwa ukaribu na alikua ni mrefu kichwa hakionekani Hana mwisho.

Sikuamini nilichokiona na ndiyo ilikua ni Mara yangu ya kwanza kukutana na kitu Kama kile, niliamua kuzima taa na kuziwasha, kitendo Cha kuzima nakuwasha tu, lile dubwana lilipotea Kama upepo sikuliona Tena akili yangu ilibadilika nilikimbiza pikipiki Kama mwenda wazimu kurudi nyumbani maana sikuendelea na Safari yangu, siku iliyofuata niliumwa sana nililala ndani bila kutoka kwa muda wa siku tano.


(2) NILIUA NYOKA WA MTU, MWENYE NYOKA ALINIFUATA AKAANZA KUNIDAI NYOKA WAKE.

Miaka ya nyuma nilikua nafanya kazi katika kiwanda kimoja Cha chai huko iringa kwa majina sitotaja, siku hiyo ilikuwa ni siku ya usafi tulikua tunasafisha maeneo yakiwanda maana siku ya usafi wa mitambo na mazingira kwa ujumla uzalishaji husimama.

Mimi nilikua nafyeka majani, lile eneo tulipangiwa wawili lakini mwenzangu kwa muda ule alienda kunywa chai atakaporudi na mimi niende tulipeana zamuu.

Kipindi nafyeka gafla nikaona nyoka mwezi anakuja upande wangu, ni mrefu mwembamba, Mimi binafsi nyoka nawajua ni moja Kati ya nyoka wenye sumu kali.

Sikutaka kushangaa ikanibidi nimuue, nilimkata na kwanja tenganisha kichwa na kiwiliwili akafa.

Mara punde alikuja mmmoja wa maafsa wakubwa pale kiwandani akihema Kama mtu aliyepresha, alinifokea na machozi yakimtoka alisema "kwa nini umeua nafsi yangu"

"Huyu ndiyo ananifanya niishi hapa"


Nilishikwa na butwaa sana, maana Yule alikuwa ni boss mkubwa nilibaki najiuliza huyu boss na manyoka wapi na wapi.

Nahakuishia hapo aliendelea kunitishia amani akidai nyoka wake arudi na ule ndiyo ilikua ni ulinzi wake.

Mimi nilipoona hivyo nikajua kabisa hii ni serious sana nilimuomba msamaha sana nikamwambia sikujua.

Hakika like kitendo Cha mtu kusema nimeua nafsi yake kilinistaajabisha sana.

(3) SITOSAHAU NILIPOMKUTA MMASAI AKIONGEA NA CHUNGU NA CHUNGU KILIMJIBU.

Hii nimeshuhudia kwa macho yangu mpaka niliona Kama ninaota, nakumbuka tulikua kwenye mitihani ya darasa la saba Tena ulikua ni muda wa mapumnziko.

Nilikwenda kutafuta darasa moja ambalo lilikua lipo mbali na Yale tuliyokua tunafanyia mtihani nikiwa na lengo la kwenda kupumnzika nitulize akili yangu kidogo.

Nilipokuwa nakaribia kwenye Hilo darasa nilianza kusikia sauti ndipo nilipoamua kuchungulia, nikamuona mwanafunzi mwenzangu mmasai, tuliyekuwa nae darasa moja na yeye alikua nafanya mtihani wakuhitimu darasa la saba.

Kilichonishangaza alikua ameweka chungu pembezoni kabisa ya darasa juu ya dawati kile chungu kilikua kinawaka Moto.

Sasa kipindi naendelea kuchungulia alikua anaongea peke yake kwa lugha ya kimasai huku akiwa amekunja mikono yake na amenyenyekea kweli mbele ya hicho chungu,

Alipomaliza kuzungumza kile chungu kilimjibu kwa sauti ya kike, kilizungumza kwa lugha yakimasai pia, niliogopa sana kile kitendo niliinama chini nikasota kwa hatua kama tano hivi nikakimbia sana kuondoka kwenye Hilo eneo.

Muda wa mtihani ulipofika masai nae akajakupiga pepa, tulivyomaliza mitihani sikumuona Yule jamaa mpaka sasa ila siku hiyo sikua na amani na nilimuogopa sana.

(4)NILISHUHUDIA MAMA WAKISUKUMA AKIIMBA NYIMBO NZURI NAKUMTOA NYOKA TOKA MAFICHONI.

Ukistaajabu ya musa basi utayaona ya firauni na wanasema tembea uone mengi na ujifunze.

Nikiwa bwana mdogo nilikwenda kumtembelea shangazi shinyanga kijijini baada yakufunga shule.

Sikuhiyo nakumbuka ilikua ni mchana mishale ya saa 8 mchana tulikua tumekaa karibu na mlango tunakula chakula Cha mchana.

Mara gafla alipita panya buku kwa spidi ya ajabu sana bila kujali chochote Yule panya aaliingia ndani maana mlango ulikua wazi.

Kabla hatujamaliza kumshangaa panya buku gafla tukashitushwa na bonge la nyoka jeusiii na lenyewe likazama ndani, kumbe lilikua linafukuzia kitoeo chake panya buku.

Na sisi baada yakuona nyoka tukaruka wote kila mtu na njia yake maana wote tulikua watoto, tuakaanza kupiga makelele nyoka nyoka nyoka!!

Jirani alikuwepo mama mmoja wakisukuma alikuja na akatuambia acheni makelele, alimchungulia dirishani Yule nyoka alimuona kajificha kwenye mtungi alituambia nipeni rungu halafu mkae huku.

Alikaa pembezoni na ule mlango alioingilia nyoka, alianza kuimba nyimbo yakisukuma kwa sauti nzuri sana huku ameshikilia rungu,

Aliimba Kama dakika tano hivi Kisha akatuambia chungulieni hapo dirishani kipindi naimba akikaribia mlangoni mniambie

Kweli Yule mama aliendelea kuimba na kadri anavyoimba nyoka alikua anasogea taratibu taratibu.

Kilichonishangaza kingine ni pale mama alipokua anacha kuimba na nyoka nae anasimama mpaka Yule mama alipoendelea kuimba nyoka nae aliendelea na Safari mpaka alipokuwa amekaa Yule mama.

Na ndipo ukawa mwisho wa maisha yake Yule nyoka baada ya kukutana na rungu zito alipomkaribia Yule mama wakisukuma.

Nitaendelea kushea kumbukumbu zingine na Kama unakumbukumbu zakushea ruksa kushea ili tusome maajabu ya dunia.
Unaukakika huvuti bangi mkuu?
 
Sister yangu alishawahi kutana na hili tatizo (anaona vitu ambavyo havipo)

Mnaweza mkawa naye pamoja afu ghafla akaanza kupiga kelele kuwa "niache, niache" huku akijificha kama ishara ya mtu anayetaka kumchukua bila ridhaa yake.

Anakuwa serious analia na kulia na sometimes katika purukushani unakuta mpaka anaji jeruhi, anasema watu anaowaona wanatisha wana meno marefu na nywele nyingi wanamuambia twende nyumbani

Mara adai kutokewa na watu waliokufa wakisema "twende ambapo tupo sisi"

Makuzi yetu ya kiafrika na uduni wa elimu ulifanya watu wakubali majibu yasio sahihi kuwa ni ushirikina kwa kuyaamini macho na ubongo wetu.

Lakini tulipoenda kwa Doctor ambaye ni mbobezi kwenye maswala ya mental health alitusaidia na sasa hilo tatizo halipo tena

Sayansi inasema muda wote haupaswi kuyaamini macho, masikio na ubongo wako

They can play fool sometimes
 
Sister yangu alishawahi kutana na hili tatizo (anaona vitu ambavyo havipo)

Mnaweza mkawa naye pamoja afu ghafla akaanza kupiga kelele kuwa "niache, niache" huku akijificha kama ishara ya mtu anayetaka kumchukua bila ridhaa yake.

Anakuwa serious analia na kulia na sometimes katika purukushani unakuta mpaka anaji jeruhi, anasema watu anaowaona wanatisha wana meno marefu na nywele nyingi wanamuambia twende nyumbani

Mara adai kutokewa na watu waliokufa wakisema "twende ambapo tupo sisi"

Makuzi yetu ya kiafrika na uduni wa elimu ulifanya watu wakubali majibu yasio sahihi kuwa ni ushirikina kwa kuyaamini macho na ubongo wetu.

Lakini tulipoenda kwa Doctor ambaye ni mbobezi kwenye maswala ya mental health alitusaidia na sasa hilo tatizo halipo tena

Sayansi inasema muda wote haupaswi kuyaamini macho, masikio na ubongo wako

They can play fool sometimes
Aliponea hospital?
 
Back
Top Bottom