Haya ndiyo mambo ya ajabu niliyowahi kuona na kushuhudia kwa macho yangu, sitoyasahau katika maisha yangu

Haya ndiyo mambo ya ajabu niliyowahi kuona na kushuhudia kwa macho yangu, sitoyasahau katika maisha yangu

Aliponea hospital?
Yes, hiyo ilikuwa ni miaka 15 iliyopita na mwaka 2018 alipata tatizo lingine linalofanana kama hilo

Hilo tatizo lilikuwa kama ni ukichaa, watu wakasema amelogwa, mume wake ikabidi ampeleke kwa kanisani aombewe.

Baadaye zikarudi taarifa mchungaji kapigwa na kiti cha plastic halafu kuna uharibifu aliufanya. Ikabidi uongozi wa kanisa umfunge kwenye chumba ambacho yuko pele yake.

Halafu mikono wakaifunga kwenye bomba la chuma, sisi tunaenda kumuona tunakuta ile kamba imemchuna mikono mpaka damu kwasababu alikuwa anahangaika kujitoa kwenye ile kamba.

Niliingiwa na hasira kwa jinsi nilivyomuona Sister ila nilijizuia ikabidi niombe kumchukua Sister kumpeleka hospitali.

Huko alikutwa na Malaria ya kichwa akapewa dripu za kutosha akaandikiwa na dawa

Ambapo mpaka saizi bado yupo kwenye dose ya hizo dawa
 
Yes, hiyo ilikuwa ni miaka 15 iliyopita na mwaka 2018 alipata tatizo lingine linalofanana kama hilo

Hilo tatizo lilikuwa kama ni ukichaa, watu wakasema amelogwa, bwana yake ikabidi ampeleke kwa kanisani aombewe.

Baadaye zikarudi taarifa mchungaji kapigwa na kiti cha plastic halafu kuna uharibifu aliufanya. Ikabidi uongozi wa kanisa umfunge kwenye chumba ambacho yuko pele yake.

Halafu mikono wakaifunga kwenye bomba la chuma, sisi tunaenda kumuona tunakuta ile kamba imemchuna mikono mpaka damu kwasababu alikuwa anahangaika kujitoa kwenye ile kamba.

Niliingiwa na hasira kwa jinsi nilivyomuona Sister ila nilijizuia ikabidi niombe kumchukua Sister kumpeleka hospitali.

Huko alikutwa na Malaria ya kichwa akapewa dripu za kutosha akaandikiwa na dawa

Ambapo mpaka saizi bado yupo kwenye dose ya hizo dawa
Is she alright?
Ina maana mpaka mda huu dada hajapona? maisha haya acheni tu
 
Sister yangu alishawahi kutana na hili tatizo (anaona vitu ambavyo havipo)

Mnaweza mkawa naye pamoja afu ghafla akaanza kupiga kelele kuwa "niache, niache" huku akijificha kama ishara ya mtu anayetaka kumchukua bila ridhaa yake.

Anakuwa serious analia na kulia na sometimes katika purukushani unakuta mpaka anaji jeruhi, anasema watu anaowaona wanatisha wana meno marefu na nywele nyingi wanamuambia twende nyumbani

Mara adai kutokewa na watu waliokufa wakisema "twende ambapo tupo sisi"

Makuzi yetu ya kiafrika na uduni wa elimu ulifanya watu wakubali majibu yasio sahihi kuwa ni ushirikina kwa kuyaamini macho na ubongo wetu.

Lakini tulipoenda kwa Doctor ambaye ni mbobezi kwenye maswala ya mental health alitusaidia na sasa hilo tatizo halipo tena

Sayansi inasema muda wote haupaswi kuyaamini macho, masikio na ubongo wako

They can play fool sometimes

Kweli mzee
 
Is she alright?
Ina maana mpaka mda huu dada hajapona? maisha haya acheni tu
Tatizo lililomuanza miaka 15 iliyopita alipona completely

2018 aliugua Malaria ambayo ilipanda kichwani na kumfanya awe kama chizi.

Maana hadi wodi za machizi amekaa

Alipotibiwa alipewa na dawa ambazo alikuwa anameza vidonge 20 kwa siku

Na sharti alilopewa ni kuwa asi-skip dose hata siku moja kwani kufanya hivyo kunaweza sababisha ugonjwa umrudie tena.

At that time alikuwa anakunywa dawa ila yupo vizuri kila kitu kipo katika utimamu wake, hicho ndio kilichomfanya aanze kuona uvivu kunywa dawa.

Kwa hiyo baada ya ku skip dose ni kweli ugonjwa ulimrudia tena, na ndio hapo akaanza upya na saizi kaanza kupunguziwa idadi ya vidonge naskia anameza vitatu kwa siku badala ya 20 kama ilivyokuwa zamani.
 
Sister yangu alishawahi kutana na hili tatizo (anaona vitu ambavyo havipo)

Mnaweza mkawa naye pamoja afu ghafla akaanza kupiga kelele kuwa "niache, niache" huku akijificha kama ishara ya mtu anayetaka kumchukua bila ridhaa yake.

Anakuwa serious analia na kulia na sometimes katika purukushani unakuta mpaka anaji jeruhi, anasema watu anaowaona wanatisha wana meno marefu na nywele nyingi wanamuambia twende nyumbani

Mara adai kutokewa na watu waliokufa wakisema "twende ambapo tupo sisi"

Makuzi yetu ya kiafrika na uduni wa elimu ulifanya watu wakubali majibu yasio sahihi kuwa ni ushirikina kwa kuyaamini macho na ubongo wetu.

Lakini tulipoenda kwa Doctor ambaye ni mbobezi kwenye maswala ya mental health alitusaidia na sasa hilo tatizo halipo tena

Sayansi inasema muda wote haupaswi kuyaamini macho, masikio na ubongo wako

They can play fool sometimes
Ni kweli, huyu jamaa alikua na wenge zake tu 😂😂
 
Sister yangu alishawahi kutana na hili tatizo (anaona vitu ambavyo havipo)

Mnaweza mkawa naye pamoja afu ghafla akaanza kupiga kelele kuwa "niache, niache" huku akijificha kama ishara ya mtu anayetaka kumchukua bila ridhaa yake.

Anakuwa serious analia na kulia na sometimes katika purukushani unakuta mpaka anaji jeruhi, anasema watu anaowaona wanatisha wana meno marefu na nywele nyingi wanamuambia twende nyumbani

Mara adai kutokewa na watu waliokufa wakisema "twende ambapo tupo sisi"

Makuzi yetu ya kiafrika na uduni wa elimu ulifanya watu wakubali majibu yasio sahihi kuwa ni ushirikina kwa kuyaamini macho na ubongo wetu.

Lakini tulipoenda kwa Doctor ambaye ni mbobezi kwenye maswala ya mental health alitusaidia na sasa hilo tatizo halipo tena

Sayansi inasema muda wote haupaswi kuyaamini macho, masikio na ubongo wako

They can play fool sometimes
Upo sahihi kwa maoni yako.
 
Yes, hiyo ilikuwa ni miaka 15 iliyopita na mwaka 2018 alipata tatizo lingine linalofanana kama hilo

Hilo tatizo lilikuwa kama ni ukichaa, watu wakasema amelogwa, mume wake ikabidi ampeleke kwa kanisani aombewe.

Baadaye zikarudi taarifa mchungaji kapigwa na kiti cha plastic halafu kuna uharibifu aliufanya. Ikabidi uongozi wa kanisa umfunge kwenye chumba ambacho yuko pele yake.

Halafu mikono wakaifunga kwenye bomba la chuma, sisi tunaenda kumuona tunakuta ile kamba imemchuna mikono mpaka damu kwasababu alikuwa anahangaika kujitoa kwenye ile kamba.

Niliingiwa na hasira kwa jinsi nilivyomuona Sister ila nilijizuia ikabidi niombe kumchukua Sister kumpeleka hospitali.

Huko alikutwa na Malaria ya kichwa akapewa dripu za kutosha akaandikiwa na dawa

Ambapo mpaka saizi bado yupo kwenye dose ya hizo dawa
Pole mkuu
 
Bibi kadhihirisha kuwa na sauti ya kumtoa nyoka pangoni.

Ila dunia ina mengi mno.
 
Sister yangu alishawahi kutana na hili tatizo (anaona vitu ambavyo havipo)

Mnaweza mkawa naye pamoja afu ghafla akaanza kupiga kelele kuwa "niache, niache" huku akijificha kama ishara ya mtu anayetaka kumchukua bila ridhaa yake.

Anakuwa serious analia na kulia na sometimes katika purukushani unakuta mpaka anaji jeruhi, anasema watu anaowaona wanatisha wana meno marefu na nywele nyingi wanamuambia twende nyumbani

Mara adai kutokewa na watu waliokufa wakisema "twende ambapo tupo sisi"

Makuzi yetu ya kiafrika na uduni wa elimu ulifanya watu wakubali majibu yasio sahihi kuwa ni ushirikina kwa kuyaamini macho na ubongo wetu.

Lakini tulipoenda kwa Doctor ambaye ni mbobezi kwenye maswala ya mental health alitusaidia na sasa hilo tatizo halipo tena

Sayansi inasema muda wote haupaswi kuyaamini macho, masikio na ubongo wako

They can play fool sometimes
Ngoja nitakuletea na shuhuda yangu tulipompeleka brother kwa madaktari bingwa wakamfanyia vipimo nakusema hakuna anacho umwa.

Lakini yeye kila inapofika usiku kucha analia vibaya mno nakudai kuwa anachomwa chomwa sindano analia vibaya mno hakuna anayelala.

Tukampeleka hospital akalazwa hali ilikua ni ile ile, mwanzo walizani ni mgonjwa wa akili mchana hakuwa na shida ila ilipofika usiku alianza kulia sana huku akijikunja kunja nakudai kuwa anachomwa sindano zinazompa maumivu makali.

Alikuja dokta mmoja pale alimtazama sana nakusema jamani vipimo vyetu havioni ugonjwa wa namna yoyote jaribuni njia mbadala labda inaweza kutatua tatizo.

Kesho yake asubuhi wazeee walimpeleka wanapopajua wao alikaa kwa muda wa siku tano na walitoa majibu yakua kaacha kulia na kuchomwa chomwa hakuna hasikii Tena kiufupi Hilo tatizo lilikwisha na broo alirudi katika famililia yake nakuendelea na harakati zake.

Hiyo nilishuhudia kwa macho yangu pasipo kusimuliwa na mtu yoyote kuwa madaktari walishindwa kung'amua tatizo na wakatoa ushauri kuwa apelekwe katika tiba mbadala.
 
Dunia Ina Mambo mengi sana na ni rahisi sana kupinga au kubisha Kama hayo Mambo ya ajabu hujayashuhudia na pia ni Bora uwe unasimuliwa tu na usije kukutana nayo maana unaweza ukadhurika ama ukawa hai.

Naam leo nimepata muda nikaona ni Bora nishee haya machache niliyokutana nayo katika huu ulimwengu,


(1) sitosahau nilipokutana na mtu mrefu asiyekuwa na mwisho inasadikika ni jini

Yapata mishale ya saa saba usiku, niliwasha pikipiki yangu kutoka Kambarage kuelekea Matanda kwa wale wenyeji wa Shinyanga wanayaelewa haya maeneo.

Nilikuwa nafanya kazi ya ulinzi kitengo Cha supervising na kupiga patrol kuwaausha walinzi usiku kwa hiyo mishale ya saa saba , saa sita ,saa nane mpaka saa tisa ndyo ilikuWa mida yangu kwenda kuwapatrol walinzi ili kazi za watu ziwe salama.

Nakumbuka nilitoka nyumbani vizuri pale Kambarage nikafika mitaa ya ofisi ya mkuu wa wilaya ili nishike barabara ya kuingia Tanesco Matanda.

Nikawa nakaribia kupita geti la ofisi ya mkuu wa wilaya, Mara gafla nikaona mtu amevaa nguo nyekundu akiwa amesimama katikati ya barabara ninapoelekea Mimi,

Kiukweli haikunishitua nikaendelea kusogea maana ile njia huwa napita sana, nilishawahi kukuta watu wanaogeshana usiku wa manane, Mara watu wanavunja Nazi kwa hiyo nilijua tu huyo aliyevaa nguo nyekundu ni mtu Kama wale ninaowaonaga.

Sasa nilipokuwa naendelea kumkaribia cha ajabu alikuwa anazidi kuwa mrefu na njiani hataki kutoka ilinibidi nipunguze spidi huku nikishusha gia za pikipiki mpaka namba moja hapo nilikuwa nishamkaribia kwa ukaribu na alikuwa ni mrefu kichwa hakionekani hana mwisho.

Sikuamini nilichokiona na ndiyo ilikuwa ni Mara yangu ya kwanza kukutana na kitu kama kile, niliamua kuzima taa na kuziwasha, kitendo cha kuzima nakuwasha tu, lile dubwana lilipotea kama upepo sikuliona tena akili yangu ilibadilika nilikimbiza pikipiki kama mwendawazimu kurudi nyumbani maana sikuendelea na Safari yangu, siku iliyofuata niliumwa sana nililala ndani bila kutoka kwa muda wa siku tano.


(2) NILIUA NYOKA WA MTU, MWENYE NYOKA ALINIFUATA AKAANZA KUNIDAI NYOKA WAKE.

Miaka ya nyuma nilikuwa nafanya kazi katika kiwanda kimoja cha chai huko Iringa kwa majina sitotaja, siku hiyo ilikuwa ni siku ya usafi tulikuwa tunasafisha maeneo ya kiwanda maana siku ya usafi wa mitambo na mazingira kwa ujumla uzalishaji husimama.

Mimi nilikuwa nafyeka majani, lile eneo tulipangiwa wawili lakini mwenzangu kwa muda ule alienda kunywa chai atakaporudi na mimi niende tulipeana zamu.

Kipindi nafyeka gafla nikaona nyoka mwezi anakuja upande wangu, ni mrefu mwembamba, Mimi binafsi nyoka nawajua ni moja Kati ya nyoka wenye sumu kali.

Sikutaka kushangaa ikanibidi nimuue, nilimkata na kwanja tenganisha kichwa na kiwiliwili akafa.

Mara punde alikuja mmoja wa maafisa wakubwa pale kiwandani akihema kama mtu aliye na presha, alinifokea na machozi yakimtoka alisema "kwanini umeua nafsi yangu"

"Huyu ndiyo ananifanya niishi hapa"

Nilishikwa na butwaa sana, maana yule alikuwa ni boss mkubwa nilibaki najiuliza huyu boss na manyoka wapi na wapi.

Na hakuishia hapo aliendelea kunitishia amani akidai nyoka wake arudi na ule ndiyo ilikuwa ni ulinzi wake.

Mimi nilipoona hivyo nikajua kabisa hii ni serious sana nilimuomba msamaha sana nikamwambia sikujua.

Hakika like kitendo cha mtu kusema nimeua nafsi yake kilinistaajabisha sana.


(3) SITOSAHAU NILIPOMKUTA MMASAI AKIONGEA NA CHUNGU NA CHUNGU KILIMJIBU.

Hii nimeshuhudia kwa macho yangu mpaka niliona Kama ninaota, nakumbuka tulikuwa kwenye mitihani ya darasa la saba tena ulikuwa ni muda wa mapumnziko.

Nilikwenda kutafuta darasa moja ambalo lilikuwa lipo mbali na yale tuliyokuwa tunafanyia mtihani nikiwa na lengo la kwenda kupumnzika nitulize akili yangu kidogo.

Nilipokuwa nakaribia kwenye hilo darasa nilianza kusikia sauti ndipo nilipoamua kuchungulia, nikamuona mwanafunzi mwenzangu mmasai, tuliyekuwa nae darasa moja na yeye alikuwa nafanya mtihani wakuhitimu darasa la saba.

Kilichonishangaza alikuwa ameweka chungu pembezoni kabisa ya darasa juu ya dawati kile chungu kilikuwa kinawaka Moto.

Sasa kipindi naendelea kuchungulia alikuwa anaongea peke yake kwa lugha ya kimasai huku akiwa amekunja mikono yake na amenyenyekea kweli mbele ya hicho chungu,

Alipomaliza kuzungumza kile chungu kilimjibu kwa sauti ya kike, kilizungumza kwa lugha ya kimasai pia, niliogopa sana kile kitendo niliinama chini nikasota kwa hatua kama tano hivi nikakimbia sana kuondoka kwenye hilo eneo.

Muda wa mtihani ulipofika masai nae akaja kupiga pepa, tulivyomaliza mitihani sikumuona yule jamaa mpaka sasa ila siku hiyo sikuwa na amani na nilimuogopa sana.


(4)NILISHUHUDIA MAMA WA KISUKUMA AKIIMBA NYIMBO NZURI NA KUMTOA NYOKA TOKA MAFICHONI.

Ukistaajabu ya Musa basi utayaona ya Firauni na wanasema tembea uone mengi na ujifunze.

Nikiwa bwana mdogo nilikwenda kumtembelea shangazi Shinyanga Kijijini baada yakufunga shule.

Siku hiyo nakumbuka ilikuwa ni mchana mishale ya saa 8 mchana tulikuwa tumekaa karibu na mlango tunakula chakula cha mchana.

Mara gafla alipita panya buku kwa spidi ya ajabu sana bila kujali chochote yule panya aliingia ndani maana mlango ulikuwa wazi.

Kabla hatujamaliza kumshangaa panya buku gafla tukashitushwa na bonge la nyoka jeusiii na lenyewe likazama ndani, kumbe lilikuwa linafukuzia kitoweo chake panya buku.

Na sisi baada ya kuona nyoka tukaruka wote kila mtu na njia yake maana wote tulikuwa watoto, tuakaanza kupiga makelele nyoka nyoka nyoka!!

Jirani alikuwepo mama mmoja wa kisukuma alikuja na akatuambia acheni makelele, alimchungulia dirishani Yule nyoka alimuona kajificha kwenye mtungi alituambia nipeni rungu halafu mkae huku.

Alikaa pembezoni na ule mlango alioingilia nyoka, alianza kuimba nyimbo ya kisukuma kwa sauti nzuri sana huku ameshikilia rungu

Aliimba kama dakika tano hivi kisha akatuambia chungulieni hapo dirishani kipindi naimba akikaribia mlangoni mniambie

Kweli yule mama aliendelea kuimba na kadri anavyoimba nyoka alikuwa anasogea taratibu taratibu.

Kilichonishangaza kingine ni pale mama alipokuwa anaacha kuimba na nyoka nae anasimama mpaka yule mama alipoendelea kuimba nyoka nae aliendelea na Safari mpaka alipokuwa amekaa yule mama.

Na ndipo ukawa mwisho wa maisha yake yule nyoka baada ya kukutana na rungu zito alipomkaribia yule mama wa kisukuma.

Nitaendelea kushea kumbukumbu zingine na kama unakumbukumbu za kushea ruksa kushea ili tusome maajabu ya dunia.
Tajiri anadai nyoka wake 😅😅😅
 
Back
Top Bottom