Elungata
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 40,205
- 33,287
Yale maji yanauzwagwa bei juu sana,, wateja wakubwa ni waganga,, sasa wamama wanapoenda kwa waganga kutafuta dawa ya kuwashika waume zao, hupewa hayo maji kwenye kichupa kidogo kama cha ppf ya sindano,Mimi natoa Mikasa ambayo nimekutana nayo na nimeshuhudia kwa macho yangu Kama Kuna mtu anaona kuwa hizi ni stori za kutunga basi shauri yake.
Lakini haya ninayoyazungumza Kuna lakujifunza ndani yake hii dunia ni pana sana nitaendelea kutoa au kushea nilivyoviona katika huu ulimwengu .
Kama Kuna mtu pia yalishawahi kumtokea makubwa zaidi ya haya pia asisite kushea ili tuendeleee kupanua ubongo.
(9) SITOSAHAU NILIVYOKUNJANA MASHATI NA WAOSHA MAITI NDANI YA CHUMBA CHA MAITI.
Hii ilitokea mkoa wa pwani, nilipo mrudisha babu yangu mzaa mama nyumbani kutoka hospital aliuugua kwa muda mrefu tulimuuguza sana mwisho wa siku alikata roho.
Pale mtoto wa kiume nilikua nipo Mimi ndiyo mjukuu mkubwa wengine walikua bado hawajafika kutoka mjini, Sasa ilibidi tuanze kushughulika na mazishi.
Msiba ni wakiislam, maana babu kwenye uhai wake alikua ni muislam nakumbuka alifariki alfajir mpaka saa kumi na mbili hivi saa moja moja nilikwenda kutoa taarifa msikitini.
Naam mchakato ulianza walikuja wazee wa makamo watatu wao kazi yao nikuosha maiti nilielewana nao nikawalipa waanze kazi yao yakuosha pamoja na maandalizi ya ushonaji wa sanda.
Utaratibu uliendelea, maiti ya mzee iliwekwa juu ya kitanda Cha kamba, Hilo zoezi lilikua linafanyika ndani ila chini yakitanda palichimbwa shimo ili Yale maji ya maiti au fuo yamwagigikie chini.
Zoezi lilifanyika Kama utaratibu ulivyo na Mimi sikua mbali nilikua karibu sana na waosha maiti kuhakikisha zoezi linakwenda sawiya.
Sasa basi zoezi lilifanyika Kama lilivyopangwa cha ajabu walipokua wanamuosha mzee pale chini ya shimo walitegesha chombo Kama kibeseni hivi ili kukinga maji ya maiti.
Hilo nililiona lakini sikutaka kuuliza maana wao ndiyo wataalam, ikanibidi niwe mpole kwenye sehemu Kama huwezi kuleta ujuaji na ukiangalia ni wazee wa makamo.
Baada yakukamilisha zoezi lao, waliianda maiti vizuri wakafukia pale chini ya kitanda lakini maji waliyokua wanayakinga waliyaweka kwenye kidumu Cha lita na mengine waliyafukia vizuri kabisa.
Mimi muda huo nilikua nawaangalia nakuwatafakari hawa maji wanataka kupeleka wapi??
Nilijiuliza sana lakini nilijisemea moyoni itafahamika tu.
Walipomaliza shuguli zao, si ndiyo walitaka kutoka nje na Yale maji.
Mimi niliwazuia mlangoni, niliwauliza mnapeleka wapi hayo maji??
Mmoja akajibu tunakwenda kuyaombea, niliwaambia hakitoki kitu hapa toka lini maji ya maiti yakaombewa??
Mzee mwingine alidakia nakusema kijana usijitafutie matatizo tunaomba utupishe tupite!
Kabla sijajibu mzee mmoja alinikunja shati, na Mimi niliona liawalo na liwe tukaanza kukabana ndani ya chumba Cha maiti na nje Kuna watu bahati nzuri kile chumba tulichokuwemo tulikua tumejifungia ndani.
Baada ya hizo purukushani ndiyo mzee mmoja akawaambia wenzake jamani hili la leo lishakua gumu tumuachie hayo maji.
Waliyaacha huku wananikata jicho na waliniambia siku nyingine ukipatwa na matatizo hapa kwenye familia yenu hatuji hata kwa dawa.
Na Mimi niliwaambia sawa.
........................................................................
KWA NINI NILIZUIA YALE MAJI YA MAITI??
nilijua kabisa hawa Kama siyo waganga basi watakua washirikina na Kama siyo washirikina basi watakua wanayataka Yale maji wakayauze.
Nirudi nyuma kidogo Kuna wakati fulani nilikua morogoro masikani tumekaa na washikaji tukipiga stori za hapa na pale.
Alitokea dalali mmoja alituambia kuwa Kuna dili la pesa na dili Hilo Kuna mganga anataka maji ya maiti akafanye Mambo yake lakini dalali hakusema kuwa ni Mambo gani .
Tulicheka nakumpuuza mana hiyo dili ilikuwa ya Moto kwa vijana Kama sisi pale tusingethubutu kabisa kuanza kutafuta maji ya maiti.
Kutoka na mfano Kama huo nilijifunza kuwa maji ya maiti ni dili sana yanatafutwa na waganga kila kukicha au washirikina na kwenda kufanyia Mambo yao huko wanayoyajua.
Ndiyo maana nilikua mkalisana nakufikia hatua kukunjana mashati na wale wazee ndani ya chumba Cha maiti,
Hapa Kuna funzo ni muhimu sana Kama umepatwa na msiba na mtu wako wakaribu basi kuwa karibu sana maana Kuna Mambo ya ajabu hutokea pale msibani anaweza akalifanya hata ndugu yako wakaribu.
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
So mama anapewa maelezo ya kuchanganya kwa chakula cha mume, akila tu basi anakuwa kama kondoo, hafurukuti kama maiti mbele ya mkewe,, 🤷