Haya ndiyo mambo ya ajabu niliyowahi kuona na kushuhudia kwa macho yangu, sitoyasahau katika maisha yangu

Haya ndiyo mambo ya ajabu niliyowahi kuona na kushuhudia kwa macho yangu, sitoyasahau katika maisha yangu

(9) NILIWAHI KUWA KWENYE MAHUSIANO NA BINTI MMOJA NILIYEMUOTA KWENYE NDOTO KABLA YAKUKUTANA NAE.

hii dunia Ina maajabu na kila mwanaadamu ana maajabu yake au uwezo aliopewa na mungu, hizi stori ninazo Shea hapa jukwaani ni Mambo yaliyonitokea na yanayoendelea kunitokea katika maisha maana bado naishi.

Ipo hivi, miaka minne iliyopita nilikua napiga mishe za kufundisha ujasiriamali sehemu mbalimbali.

Siku moja nililala nikaota njozi moja nipo maeneo ya relini sehemu ambayo sijafika kabla nikiwa pale relini nimekaa Mara alitokea binti mmoja alikua amesuka nywele msuko wa twende kilioni, mfupi wastani na ni maji ya kunde, ndoto ilinionesha Yule binti alitabasamu na Mimi nilivutiwa naye ndipo nilipoamua kumuita akanisogelea nikaanza kuzungumza nae nilimuambia maneno mawili tu nakupenda nahitaji uwe mpenzi wangu

Yule binti alicheka sana nilimsogelea nikamshika mkono alinyamaza kucheka akaanza kuona aibu na ndipo nilishituka katika hiyo ndoto.

UHALISIA KATIKA MAISHA YAKAWAIDA.

baada ya Kama wiki kupita nilisafiri kwenda Kijiji kimoja kinachoitwa idodi, nilifikia gest moja pale center kutokana na uchovu siku hiyo sikutoka kwenda sehemu yoyote.

Kesho yake nilitoka kwenda kutembea nakuangalia mazingira lakini katika pitapita nilijikuta nimetokea maeneo ya relini nilisogea mpaka kwenye reli lakini nilipokua nimesimama Mara gafla nilimuona binti wa dizaini ile ile niliyemuona kwenye ndoto takiribani wiki moja iliyopita.

Akili yangu ilikumbuka mpaka maneno niliyozungumza nilistaajabika sana nikajisemea kimoyomoyo hebu ngoja nijaribu kuzungumza Kama nilivyozungumza kwenye ndoto.

Nilimuita Yule binti akaja mpaka maeneo niliyokuwa nimesimama pale relini baada ya salamu sikutaka kuzungumza mengi nilimwambia Mimi nakupenda nahitaji uwe mpenzi wangu.

Alicheka sana Kisha nilimsogelea Kama nilivyofanya kwenye ndoto, aliponiona nipo karibu alinyamaza nakuanza kuona aibu, kumbuka ndoto iliishia hapo

Pale pale nilimwambia nipe namba yako ya simu alininipa na Kisha tukawa tuna wasiliana mwisho wa siku akawa mpenzi wangu kabisa.

Kwa upande wangu nilikua najiuliza sana juu ya huyo binti, maana mazingira tuliyokutana ni mazingira Yale yale, na usukaji wake ni ule ule tofauti ni mavazi tu maana wa kwenye ndoto alijifunga lubega lakini wa kiuhalisia alivaa mavazi ya kawaida tu.

Mwanzo nilikua namuhofia hata kulala nae nilihisi anaweza akawa ni jini lakini nilipomzoea niliona kawaida tu, nilitembea nae sana na hakuna baya lililonitokea.
 
Darasa la 6 nilitoka kukesha msibani asubuhi sana,wakati narudi asubuhi sana pembeni ya kaburi la yule marehemu nilimuona baba mrefu sana ana kanzu nyeupe sana na kofia ndefu kama kindoo ya barakashia.Nilipiga jicho Mara moja nikakimbia nyumbani na kugonga mlango.Hayo madude yapo wadau
[emoji16] ila nimecheka sana
 
(9) NILIWAHI KUWA KWENYE MAHUSIANO NA BINTI MMOJA NILIYEMUOTA KWENYE NDOTO KABLA YAKUKUTANA NAE.

hii dunia Ina maajabu na kila mwanaadamu ana maajabu yake au uwezo aliopewa na mungu, hizi stori ninazo Shea hapa jukwaani ni Mambo yaliyonitokea na yanayoendelea kunitokea katika maisha maana bado naishi.

Ipo hivi, miaka minne iliyopita nilikua napiga mishe za kufundisha ujasiriamali sehemu mbalimbali.

Siku moja nililala nikaota njozi moja nipo maeneo ya relini sehemu ambayo sijafika kabla nikiwa pale relini nimekaa Mara alitokea binti mmoja alikua amesuka nywele msuko wa twende kilioni, mfupi wastani na ni maji ya kunde, ndoto ilinionesha Yule binti alitabasamu na Mimi nilivutiwa naye ndipo nilipoamua kumuita akanisogelea nikaanza kuzungumza nae nilimuambia maneno mawili tu nakupenda nahitaji uwe mpenzi wangu

Yule binti alicheka sana nilimsogelea nikamshika mkono alinyamaza kucheka akaanza kuona aibu na ndipo nilishituka katika hiyo ndoto.

UHALISIA KATIKA MAISHA YAKAWAIDA.

baada ya Kama wiki kupita nilisafiri kwenda Kijiji kimoja kinachoitwa idodi, nilifikia gest moja pale center kutokana na uchovu siku hiyo sikutoka kwenda sehemu yoyote.

Kesho yake nilitoka kwenda kutembea nakuangalia mazingira lakini katika pitapita nilijikuta nimetokea maeneo ya relini nilisogea mpaka kwenye reli lakini nilipokua nimesimama Mara gafla nilimuona binti wa dizaini ile ile niliyemuona kwenye ndoto takiribani wiki moja iliyopita.

Akili yangu ilikumbuka mpaka maneno niliyozungumza nilistaajabika sana nikajisemea kimoyomoyo hebu ngoja nijaribu kuzungumza Kama nilivyozungumza kwenye ndoto.

Nilimuita Yule binti akaja mpaka maeneo niliyokuwa nimesimama pale relini baada ya salamu sikutaka kuzungumza mengi nilimwambia Mimi nakupenda nahitaji uwe mpenzi wangu.

Alicheka sana Kisha nilimsogelea Kama nilivyofanya kwenye ndoto, aliponiona nipo karibu alinyamaza nakuanza kuona aibu, kumbuka ndoto iliishia hapo

Pale pale nilimwambia nipe namba yako ya simu alininipa na Kisha tukawa tuna wasiliana mwisho wa siku akawa mpenzi wangu kabisa.

Kwa upande wangu nilikua najiuliza sana juu ya huyo binti, maana mazingira tuliyokutana ni mazingira Yale yale, na usukaji wake ni ule ule tofauti ni mavazi tu maana wa kwenye ndoto alijifunga lubega lakini wa kiuhalisia alivaa mavazi ya kawaida tu.

Mwanzo nilikua namuhofia hata kulala nae nilihisi anaweza akawa ni jini lakini nilipomzoea niliona kawaida tu, nilitembea nae sana na hakuna baya lililonitokea.
Aisee
 
Hii ni simulizi yatatu ikionyeshakanda ya ziwainaongoza kwa ulozi, simulizi moja ni toka kwa umughaka ya pili simkumbuki jina ila inaitwa babu yangu kama rafiki yangu na wewe hii
 
Dunia Ina Mambo mengi sana na ni rahisi sana kupinga au kubisha Kama hayo Mambo ya ajabu hujayashuhudia na pia ni Bora uwe unasimuliwa tu na usije kukutana nayo maana unaweza ukadhurika ama ukawa hai.

Naam leo nimepata muda nikaona ni Bora nishee haya machache niliyokutana nayo katika huu ulimwengu,


(1) sitosahau nilipokutana na mtu mrefu asiyekuwa na mwisho inasadikika ni jini

Yapata mishale ya saa saba usiku, niliwasha pikipiki yangu kutoka Kambarage kuelekea Matanda kwa wale wenyeji wa Shinyanga wanayaelewa haya maeneo.

Nilikuwa nafanya kazi ya ulinzi kitengo Cha supervising na kupiga patrol kuwaausha walinzi usiku kwa hiyo mishale ya saa saba , saa sita ,saa nane mpaka saa tisa ndyo ilikuWa mida yangu kwenda kuwapatrol walinzi ili kazi za watu ziwe salama.

Nakumbuka nilitoka nyumbani vizuri pale Kambarage nikafika mitaa ya ofisi ya mkuu wa wilaya ili nishike barabara ya kuingia Tanesco Matanda.

Nikawa nakaribia kupita geti la ofisi ya mkuu wa wilaya, Mara gafla nikaona mtu amevaa nguo nyekundu akiwa amesimama katikati ya barabara ninapoelekea Mimi,

Kiukweli haikunishitua nikaendelea kusogea maana ile njia huwa napita sana, nilishawahi kukuta watu wanaogeshana usiku wa manane, Mara watu wanavunja Nazi kwa hiyo nilijua tu huyo aliyevaa nguo nyekundu ni mtu Kama wale ninaowaonaga.

Sasa nilipokuwa naendelea kumkaribia cha ajabu alikuwa anazidi kuwa mrefu na njiani hataki kutoka ilinibidi nipunguze spidi huku nikishusha gia za pikipiki mpaka namba moja hapo nilikuwa nishamkaribia kwa ukaribu na alikuwa ni mrefu kichwa hakionekani hana mwisho.

Sikuamini nilichokiona na ndiyo ilikuwa ni Mara yangu ya kwanza kukutana na kitu kama kile, niliamua kuzima taa na kuziwasha, kitendo cha kuzima nakuwasha tu, lile dubwana lilipotea kama upepo sikuliona tena akili yangu ilibadilika nilikimbiza pikipiki kama mwendawazimu kurudi nyumbani maana sikuendelea na Safari yangu, siku iliyofuata niliumwa sana nililala ndani bila kutoka kwa muda wa siku tano.


(2) NILIUA NYOKA WA MTU, MWENYE NYOKA ALINIFUATA AKAANZA KUNIDAI NYOKA WAKE.

Miaka ya nyuma nilikuwa nafanya kazi katika kiwanda kimoja cha chai huko Iringa kwa majina sitotaja, siku hiyo ilikuwa ni siku ya usafi tulikuwa tunasafisha maeneo ya kiwanda maana siku ya usafi wa mitambo na mazingira kwa ujumla uzalishaji husimama.

Mimi nilikuwa nafyeka majani, lile eneo tulipangiwa wawili lakini mwenzangu kwa muda ule alienda kunywa chai atakaporudi na mimi niende tulipeana zamu.

Kipindi nafyeka gafla nikaona nyoka mwezi anakuja upande wangu, ni mrefu mwembamba, Mimi binafsi nyoka nawajua ni moja Kati ya nyoka wenye sumu kali.

Sikutaka kushangaa ikanibidi nimuue, nilimkata na kwanja tenganisha kichwa na kiwiliwili akafa.

Mara punde alikuja mmoja wa maafisa wakubwa pale kiwandani akihema kama mtu aliye na presha, alinifokea na machozi yakimtoka alisema "kwanini umeua nafsi yangu"

"Huyu ndiyo ananifanya niishi hapa"

Nilishikwa na butwaa sana, maana yule alikuwa ni boss mkubwa nilibaki najiuliza huyu boss na manyoka wapi na wapi.

Na hakuishia hapo aliendelea kunitishia amani akidai nyoka wake arudi na ule ndiyo ilikuwa ni ulinzi wake.

Mimi nilipoona hivyo nikajua kabisa hii ni serious sana nilimuomba msamaha sana nikamwambia sikujua.

Hakika like kitendo cha mtu kusema nimeua nafsi yake kilinistaajabisha sana.


(3) SITOSAHAU NILIPOMKUTA MMASAI AKIONGEA NA CHUNGU NA CHUNGU KILIMJIBU.

Hii nimeshuhudia kwa macho yangu mpaka niliona Kama ninaota, nakumbuka tulikuwa kwenye mitihani ya darasa la saba tena ulikuwa ni muda wa mapumnziko.

Nilikwenda kutafuta darasa moja ambalo lilikuwa lipo mbali na yale tuliyokuwa tunafanyia mtihani nikiwa na lengo la kwenda kupumnzika nitulize akili yangu kidogo.

Nilipokuwa nakaribia kwenye hilo darasa nilianza kusikia sauti ndipo nilipoamua kuchungulia, nikamuona mwanafunzi mwenzangu mmasai, tuliyekuwa nae darasa moja na yeye alikuwa nafanya mtihani wakuhitimu darasa la saba.

Kilichonishangaza alikuwa ameweka chungu pembezoni kabisa ya darasa juu ya dawati kile chungu kilikuwa kinawaka Moto.

Sasa kipindi naendelea kuchungulia alikuwa anaongea peke yake kwa lugha ya kimasai huku akiwa amekunja mikono yake na amenyenyekea kweli mbele ya hicho chungu,

Alipomaliza kuzungumza kile chungu kilimjibu kwa sauti ya kike, kilizungumza kwa lugha ya kimasai pia, niliogopa sana kile kitendo niliinama chini nikasota kwa hatua kama tano hivi nikakimbia sana kuondoka kwenye hilo eneo.

Muda wa mtihani ulipofika masai nae akaja kupiga pepa, tulivyomaliza mitihani sikumuona yule jamaa mpaka sasa ila siku hiyo sikuwa na amani na nilimuogopa sana.


(4)NILISHUHUDIA MAMA WA KISUKUMA AKIIMBA NYIMBO NZURI NA KUMTOA NYOKA TOKA MAFICHONI.

Ukistaajabu ya Musa basi utayaona ya Firauni na wanasema tembea uone mengi na ujifunze.

Nikiwa bwana mdogo nilikwenda kumtembelea shangazi Shinyanga Kijijini baada yakufunga shule.

Siku hiyo nakumbuka ilikuwa ni mchana mishale ya saa 8 mchana tulikuwa tumekaa karibu na mlango tunakula chakula cha mchana.

Mara gafla alipita panya buku kwa spidi ya ajabu sana bila kujali chochote yule panya aliingia ndani maana mlango ulikuwa wazi.

Kabla hatujamaliza kumshangaa panya buku gafla tukashitushwa na bonge la nyoka jeusiii na lenyewe likazama ndani, kumbe lilikuwa linafukuzia kitoweo chake panya buku.

Na sisi baada ya kuona nyoka tukaruka wote kila mtu na njia yake maana wote tulikuwa watoto, tuakaanza kupiga makelele nyoka nyoka nyoka!!

Jirani alikuwepo mama mmoja wa kisukuma alikuja na akatuambia acheni makelele, alimchungulia dirishani Yule nyoka alimuona kajificha kwenye mtungi alituambia nipeni rungu halafu mkae huku.

Alikaa pembezoni na ule mlango alioingilia nyoka, alianza kuimba nyimbo ya kisukuma kwa sauti nzuri sana huku ameshikilia rungu

Aliimba kama dakika tano hivi kisha akatuambia chungulieni hapo dirishani kipindi naimba akikaribia mlangoni mniambie

Kweli yule mama aliendelea kuimba na kadri anavyoimba nyoka alikuwa anasogea taratibu taratibu.

Kilichonishangaza kingine ni pale mama alipokuwa anaacha kuimba na nyoka nae anasimama mpaka yule mama alipoendelea kuimba nyoka nae aliendelea na Safari mpaka alipokuwa amekaa yule mama.

Na ndipo ukawa mwisho wa maisha yake yule nyoka baada ya kukutana na rungu zito alipomkaribia yule mama wa kisukuma.

Nitaendelea kushea kumbukumbu zingine na kama unakumbukumbu za kushea ruksa kushea ili tusome maajabu ya dunia.
Mambo ya kuogofya haya
 
Dunia Ina Mambo mengi sana na ni rahisi sana kupinga au kubisha Kama hayo Mambo ya ajabu hujayashuhudia na pia ni Bora uwe unasimuliwa tu na usije kukutana nayo maana unaweza ukadhurika ama ukawa hai.

Naam leo nimepata muda nikaona ni Bora nishee haya machache niliyokutana nayo katika huu ulimwengu,


(1) sitosahau nilipokutana na mtu mrefu asiyekuwa na mwisho inasadikika ni jini

Yapata mishale ya saa saba usiku, niliwasha pikipiki yangu kutoka Kambarage kuelekea Matanda kwa wale wenyeji wa Shinyanga wanayaelewa haya maeneo.

Nilikuwa nafanya kazi ya ulinzi kitengo Cha supervising na kupiga patrol kuwaausha walinzi usiku kwa hiyo mishale ya saa saba , saa sita ,saa nane mpaka saa tisa ndyo ilikuWa mida yangu kwenda kuwapatrol walinzi ili kazi za watu ziwe salama.

Nakumbuka nilitoka nyumbani vizuri pale Kambarage nikafika mitaa ya ofisi ya mkuu wa wilaya ili nishike barabara ya kuingia Tanesco Matanda.

Nikawa nakaribia kupita geti la ofisi ya mkuu wa wilaya, Mara gafla nikaona mtu amevaa nguo nyekundu akiwa amesimama katikati ya barabara ninapoelekea Mimi,

Kiukweli haikunishitua nikaendelea kusogea maana ile njia huwa napita sana, nilishawahi kukuta watu wanaogeshana usiku wa manane, Mara watu wanavunja Nazi kwa hiyo nilijua tu huyo aliyevaa nguo nyekundu ni mtu Kama wale ninaowaonaga.

Sasa nilipokuwa naendelea kumkaribia cha ajabu alikuwa anazidi kuwa mrefu na njiani hataki kutoka ilinibidi nipunguze spidi huku nikishusha gia za pikipiki mpaka namba moja hapo nilikuwa nishamkaribia kwa ukaribu na alikuwa ni mrefu kichwa hakionekani hana mwisho.

Sikuamini nilichokiona na ndiyo ilikuwa ni Mara yangu ya kwanza kukutana na kitu kama kile, niliamua kuzima taa na kuziwasha, kitendo cha kuzima nakuwasha tu, lile dubwana lilipotea kama upepo sikuliona tena akili yangu ilibadilika nilikimbiza pikipiki kama mwendawazimu kurudi nyumbani maana sikuendelea na Safari yangu, siku iliyofuata niliumwa sana nililala ndani bila kutoka kwa muda wa siku tano.


(2) NILIUA NYOKA WA MTU, MWENYE NYOKA ALINIFUATA AKAANZA KUNIDAI NYOKA WAKE.

Miaka ya nyuma nilikuwa nafanya kazi katika kiwanda kimoja cha chai huko Iringa kwa majina sitotaja, siku hiyo ilikuwa ni siku ya usafi tulikuwa tunasafisha maeneo ya kiwanda maana siku ya usafi wa mitambo na mazingira kwa ujumla uzalishaji husimama.

Mimi nilikuwa nafyeka majani, lile eneo tulipangiwa wawili lakini mwenzangu kwa muda ule alienda kunywa chai atakaporudi na mimi niende tulipeana zamu.

Kipindi nafyeka gafla nikaona nyoka mwezi anakuja upande wangu, ni mrefu mwembamba, Mimi binafsi nyoka nawajua ni moja Kati ya nyoka wenye sumu kali.

Sikutaka kushangaa ikanibidi nimuue, nilimkata na kwanja tenganisha kichwa na kiwiliwili akafa.

Mara punde alikuja mmoja wa maafisa wakubwa pale kiwandani akihema kama mtu aliye na presha, alinifokea na machozi yakimtoka alisema "kwanini umeua nafsi yangu"

"Huyu ndiyo ananifanya niishi hapa"

Nilishikwa na butwaa sana, maana yule alikuwa ni boss mkubwa nilibaki najiuliza huyu boss na manyoka wapi na wapi.

Na hakuishia hapo aliendelea kunitishia amani akidai nyoka wake arudi na ule ndiyo ilikuwa ni ulinzi wake.

Mimi nilipoona hivyo nikajua kabisa hii ni serious sana nilimuomba msamaha sana nikamwambia sikujua.

Hakika like kitendo cha mtu kusema nimeua nafsi yake kilinistaajabisha sana.


(3) SITOSAHAU NILIPOMKUTA MMASAI AKIONGEA NA CHUNGU NA CHUNGU KILIMJIBU.

Hii nimeshuhudia kwa macho yangu mpaka niliona Kama ninaota, nakumbuka tulikuwa kwenye mitihani ya darasa la saba tena ulikuwa ni muda wa mapumnziko.

Nilikwenda kutafuta darasa moja ambalo lilikuwa lipo mbali na yale tuliyokuwa tunafanyia mtihani nikiwa na lengo la kwenda kupumnzika nitulize akili yangu kidogo.

Nilipokuwa nakaribia kwenye hilo darasa nilianza kusikia sauti ndipo nilipoamua kuchungulia, nikamuona mwanafunzi mwenzangu mmasai, tuliyekuwa nae darasa moja na yeye alikuwa nafanya mtihani wakuhitimu darasa la saba.

Kilichonishangaza alikuwa ameweka chungu pembezoni kabisa ya darasa juu ya dawati kile chungu kilikuwa kinawaka Moto.

Sasa kipindi naendelea kuchungulia alikuwa anaongea peke yake kwa lugha ya kimasai huku akiwa amekunja mikono yake na amenyenyekea kweli mbele ya hicho chungu,

Alipomaliza kuzungumza kile chungu kilimjibu kwa sauti ya kike, kilizungumza kwa lugha ya kimasai pia, niliogopa sana kile kitendo niliinama chini nikasota kwa hatua kama tano hivi nikakimbia sana kuondoka kwenye hilo eneo.

Muda wa mtihani ulipofika masai nae akaja kupiga pepa, tulivyomaliza mitihani sikumuona yule jamaa mpaka sasa ila siku hiyo sikuwa na amani na nilimuogopa sana.


(4)NILISHUHUDIA MAMA WA KISUKUMA AKIIMBA NYIMBO NZURI NA KUMTOA NYOKA TOKA MAFICHONI.

Ukistaajabu ya Musa basi utayaona ya Firauni na wanasema tembea uone mengi na ujifunze.

Nikiwa bwana mdogo nilikwenda kumtembelea shangazi Shinyanga Kijijini baada yakufunga shule.

Siku hiyo nakumbuka ilikuwa ni mchana mishale ya saa 8 mchana tulikuwa tumekaa karibu na mlango tunakula chakula cha mchana.

Mara gafla alipita panya buku kwa spidi ya ajabu sana bila kujali chochote yule panya aliingia ndani maana mlango ulikuwa wazi.

Kabla hatujamaliza kumshangaa panya buku gafla tukashitushwa na bonge la nyoka jeusiii na lenyewe likazama ndani, kumbe lilikuwa linafukuzia kitoweo chake panya buku.

Na sisi baada ya kuona nyoka tukaruka wote kila mtu na njia yake maana wote tulikuwa watoto, tuakaanza kupiga makelele nyoka nyoka nyoka!!

Jirani alikuwepo mama mmoja wa kisukuma alikuja na akatuambia acheni makelele, alimchungulia dirishani Yule nyoka alimuona kajificha kwenye mtungi alituambia nipeni rungu halafu mkae huku.

Alikaa pembezoni na ule mlango alioingilia nyoka, alianza kuimba nyimbo ya kisukuma kwa sauti nzuri sana huku ameshikilia rungu

Aliimba kama dakika tano hivi kisha akatuambia chungulieni hapo dirishani kipindi naimba akikaribia mlangoni mniambie

Kweli yule mama aliendelea kuimba na kadri anavyoimba nyoka alikuwa anasogea taratibu taratibu.

Kilichonishangaza kingine ni pale mama alipokuwa anaacha kuimba na nyoka nae anasimama mpaka yule mama alipoendelea kuimba nyoka nae aliendelea na Safari mpaka alipokuwa amekaa yule mama.

Na ndipo ukawa mwisho wa maisha yake yule nyoka baada ya kukutana na rungu zito alipomkaribia yule mama wa kisukuma.

Nitaendelea kushea kumbukumbu zingine na kama unakumbukumbu za kushea ruksa kushea ili tusome maajabu ya dunia.
Dza
 
kuna visa viwili vinamuhusu mtu mmoja ambaye alikua mchungaji kanisa moja la TAG lipo jirani na nyumbani kwetu.

kisa cha kwanza nimesimuliwa na Mama yangu. akasema kipindi me nikiwa mtoto mdogo bado nanyonya nikiwa nimelala kitandani mida ya jioni. anaingia chumba akakuta kuna nyoka mkuubwa kitandani upande wa miguuni. alichofanya hakuniacha akanikwapua then akatoka mbio. baba hakuwepo bahati kulikuwa na mgeni mzee mmoja pale home amelala. yule mgeni akamuua yule nyoka, then akatenganisha kichwa na kiwili wili. akachimba mashimo mawili shambani kwenye mahindi then kichwa shimo lake na kiwili wili shimo lake. kesho asubuh na mapema yule mchungaji wa kanisa akaja, akawa anauliza vipi kuna nyoka mmemuona? mama akahisi labda na yule mchungaji alikuwa amemuona nyoka, akamfukuza nyoka akakimbia akaja upande wa home. mama akasema ndio jana tulimuua nyoka.

Pastor. mlivomuua ikawaje?
mama. tulifukia.
pastor. wapi?
mama. shambani
pastor. twende ukanioneshe.

mama akashangaa ila akaamua ngoja aende. akampeleka shamban akamuonesha. pastor akaomba jembe then akafukua. akatoa kichwa kwenye shimo lake, then akaja akafukia kwenye shimo la kiwili wili. ikaisha hiyO na maswali mengi kwa mama.


kisa cha pili nilipokua shule ya msingi kuna ndege mmoja alikuja kwenye lile kanisa la pastor. yule ndege alikua anakaa mule kanisani 24/7. hatoki nje. sisi daily tulikua tunacheza ktk uwanja wa kanisa na kanisa lilikua lina madirisha yana flem za nondo hakukuwa na vioo. so sisi tukawa tunampiga mawe kupitia dirishan lkn hatoki. alikuwa anahama kenchi moja kwenda jingine lkn hatoki. alikaa mle karibu wiki 2 ndo hatukumuona tena. na aina ile ya ndege me sijawahi kuiona mpaka leo. kwetu ni kijijini na tulikua tunawinda, so nmeona ndege wengi lkn aina ile sijawah ona.

Fast foward miaka Mingi baadae yule pastor alikuja kufariki kifo cha ghafla tuu kilichoacha maswali mengi.
Huyo mchungaji alikuwa anaishi wapi
 
Nakuona MCHAWII unajaribu kupoteza lengo [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Sasa hapo mchawi ni nani kati yake anaekataa upo na wewe unaoupigia chapuo kuwa uchawi upo 😁😁 hapo mchawi unaonekana ni wewe jomba
 
Back
Top Bottom