Hata huko hospital nako tunabet tu binafsi shangazi yangu aliwahi kupelekwa hospital ya kanisa inaitwa NAMBAYA wakampima hana ugonjwa wakampeleka hospital ya wilaya ya masasi (mkomaindo) kumpima hana homa yeyote ila mtu yupo hoi,pale tukaanza kugawanyika mwingine anadai twende kwa mganga kwasababu hospital hauonekani ugonjwa ila baada ya majadiliano ya muda mrefu tukaamua tumpeleke hospitalin ndanda ile tumemfikisha baada ya kupimwa kumbe ni kisukari tu
Ukiona hospital inakwambia tumepima hatujaona ugonjwa tambua hiyo hospital haina vipimo vyote na haina wataalamu wa kusoma vipimo vyote.
Muhimbili yenyewe kuna vifaa vya baadhi vipimo haina. Ndio maana watu wanaenda nje ya nchi kutibiwa.
Wabongo wakiambiwa tumepima ugonjwa hauonekani wanakimbilia kwa waganga ama manabii huku wanasahau wameambiwa ugonjwa hauonekani sababu vipimo vya kupima huo ugonjwa hakuna kwenye hiyo hospital