Haya ni Machotara ya Kipemba wanaocheza Ulaya

Nadhani Itakuwa ulikua ama miaka hiyo ulikua hujazaliwa au unanyonya, aka uku nyumba Tuu, waulize waliwahi kusafiri miaka hiyo tena ulitakiwa ufanye utafiti Kabla ya kuandika.
Nilisafiri mimi mwenyewe 1991 na nilienda kuchukua visa ubalozini! Sikudandia maroli ya kabichi ndugu
 
Kwanza niseme Sanahani Kama nitakua nimekukwaza, lkn hii lugha saivi sana Mjini Na humu jf imejaa, ni rahisi kueleweka.

Na kutupiwa ndizi mm bado sijafikia huko
.
mkuu wewe ni muungwana na mstaarabu...hivyo usichukuliwe na wengi!1 wewe weka personality yako kama wewe mwenyewe.
Ukitumia lufudhi njema pia utaeleweka... Moreover hao wachezaji wanajitangaza ka wa Africa wa TANZANIA!! nilishasoma katika mageazeti ya UK !!
ubarikiwe.
 
Mitanzania ndo kazi iliyobakia nayo tu. Kuwahusisha watu na nchi zao. Ujinga wa miaka yote kama kipindi kile mikenya inafurahia obama ana asili ya kwao. So wat? Ni ujinga tu unaowasumbua watu.
 
Mkuu labla kije kizazi kingine tofauti na chetu hapo bongo bhana hata kama una kipaji kitauliwa tu kwa fitna Hasheem Thabit yupo wapi? Samatta tu tumebaki nae

Jambazi hebu sema kweli Hasheem Thabit katiliwa fitna Na Nani? Huyo HT alikuwa babu kubwa alivyo kuwa Ucon(university of Connecticut) akachaguliwa Na 3 dunia nzima kuwa mchezaji bora wa mpira wa vikapo huko USA Lakini yeye Mwenyewe kajitilia fifta.
Kuna kitu kinaitwa (wajibu wa Kibinafsi) ukiwa Na kipaji unafanya zaidi kuongeza kipaji ulichonacho.Sio kulaumu watu kwa uzembe.
Ukisifiwa ongeza juhudi Na ujiepushe Na mambo mabaya Na kufanya mambo mazuri.
Hata urogwe vipi,utiwe fitna vipi wewe hugeuki nyuma.Samatta hakuwa Na bahati ya HT Lakini mcheki Leo anadunda hiyo initwa Wajibu wa Kibinafsi
 
Rashford sio mpemba wala hana asili ya pemba, Rashford Kazaliwa Manchester na kakulia hapo hapo, wewe umekwenda kusoma joke's za Eddo kumwembe ukazibeba jumla jumla bila kujua anafanya joke's,
 
Rashford sio mpemba wala hana asili ya pemba, Rashford Kazaliwa Manchester na kakulia hapo hapo, wewe umekwenda kusoma joke's za Eddo kumwembe ukazibeba jumla jumla bila kujua anafanya joke's,
Hawa ndio wale viazi wameanza kutumia social medi juzi juzi, sasa kila kitu anachokikuta yeye anameza hajui jokes wala nini.. Edo akisema kitu basi yeye kameza .. Na hapokei ushauri.
 
Imebidi nije kutoa ushuhuda kwa hili,nimeishi Zanzibar miaka kibao nikifanya kazi huko. Mimi sikufika Pemba lakini Ugunja kila familia, narudia kila familia au ukoo utakuta mmoja ama wanafamilia wawili wako Ulaya ama Uarabuni,mwezi mtukufu wa ramadhani unapokalibia ndipo hao jamaa walioko Ulaya na Uarabuni hutuma mahitaji kwa ndugu zao ikiwemo pesa na nguo kwa wingi sana na ndiyo sababu utakuta Wazanzibar wanatembelea gari za bei mbaya huku wakiwa hawana chanzo cha kipato tofauti na kuuza kahawa,kashata na bofulo. Ndugu mimi naamini unachokisema hapa kina ukweli flani ila amini kuna watu jamii forum ni wapuuzi sana kwa sababu tayari wameshaigiza ubaguzi kwenu Wapemba tofauti na ulivyoposti. Nakumbuka mimi kuna Wazanzibar wengi sana wako Australia walikimbia 2001 kwa kisingizio cha machafuko ya siasa kule Pemba na walikuwa wanachukua picha tu za nyumba ikiwa imechomwa moto na wanakwea pipa huko Mombasa Kenya. Narudia tena kama kuna watu wanaongoza kuwa nchi za ng'ambo hapa Tanzania basi ni Wazanzibar. Mwisho nawakumbisha wakati mtangazaji wa BBC akiwafanyia interview watanzania wanaoishi Uingereza (wakifanya kazi ya saloon) kwa kuwahudumia huduma ya kunyoa wachezaji wa Leicester City wengi wao walikuwa na asili ya Mombasa/Coastal area includes Zanzibar. South huku kuna wasukuma waliingia kwa gia ya wakimbizi wa Sudan Kusini lkn ukweli ni wenyeji wa Maswa Shinyanga (Hivyo Zuma anaamini ana raia wa Sudani kumbe wasukuma kama ulivyosema Wapemba kujiandikisha ni Wasomali). Mwisho nyie mnaobishi kuna kitu nilijifunza, Watanzania bara wengi wao hawapendi kwenda Zanzibar kufanya kazi tofauti na watu wa kanda ya Ziwa (kihistoria) ambao wengi huzamia huko kwenda kulima na kazi zingine ngumu kama kulisha ng'ombe japo kwa sasa wamepunguza sana. Hivyo hawafahamu lolote kuhusu Zanzibar. Kuna supplier mmoja hapo Breeze Beach Club Bwejuu Zanzibar anaitwa Omary na rafiki yake Ame,ndugu zao wako na wameoa Australia tangu 2002 na wanatuma tu misaada mbalimbali. Hivyo naamini ulichoandika kina ukweli sana hata mimi huku South kama nikizaa siwezi kuhangaika kumpatia uraia wa Tanzania mtoto wangu labda kama Magufuli atabaki miaka 50 madarakani maana analeta matumaini japo ya muda mrefu nikiwa nishajifia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…