Haya ni makosa watu huyafanya na kuwagharimu kwenye ngumi za Mtaani (Street Fights)

Haya ni makosa watu huyafanya na kuwagharimu kwenye ngumi za Mtaani (Street Fights)

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Pengine unaweza kujiona upo salama kwa kudhani ngumi za mtaani ni kwa wapiga debe, bodaboda, au watu wa tabaka fulani tu. Ukweli ni kwamba, mtu yeyote anaweza kujikuta kwenye hali hii, tulichotofautiana ni viwango tu, Unaweza ukawa unajenga nyumba yako mmepishana kauli na fundi kiasi cha kutwangana, Makazini mnaweza kupishana kauli mkapigana, Jela ni kawaida sana kupigana lasivyo unakuwa target, Hata watu wazima huwa kuna kuoneana kuna muda itabidi ujitetee, n.k.

Ni bora zaidi kuzuia pambano pigana ikiwa hakuna mbadala​

Ulimi ni moja ya kiungo makini sana katika kuepusha ugomvi, neno dogo kama samahani mkuu linaweza epusha mengi, jaribu kusuluhisha mzozo kidiplomasia au kwa kuondoka eneo hilo. Kupigana inapaswa kuwa chaguo la mwisho kabisa. Kupigana kunaweza kusababisha madhara makubwa kama vile majeraha makubwa, kuua mtu kwa bahati mbaya na visasi vya kikatili. Aidha, kunaweza kuwa na athari kubwa za kisheria kama kufungwa jela.

Kufikiri Kuna Sheria​

Ni kosa kuingia kwenye mapambano ya mtaani ukidhani kuna sheria za kufuatwa. Hii sio boxing, hakuna mwamuzi, hakuna muda wa kupumzika, na mara nyingi, hakuna huruma. Kufikiri kwamba mpinzani wako atafuata kanuni ni kosa kubwa. Mapambano ya mtaani mara nyingi hayana heshima, na ni muhimu kuelewa kuwa usalama wako unapaswa kuwa kipaumbele.


Kutokukimbia Kisu au Silaha inapotolewa​

Kuna mikoa kama Arusha ugomvi huambatana na visu hawawezi kuzichapa kavu, Unapoona kisu kwenye pambano, jambo bora zaidi unaloweza kufanya ni kukimbia, Kiburi cha kuendelea kupigana kwa hofu ya kuonekana muoga waweza poteza uhai wako. Mapambano dhidi ya mtu mwenye silaha ni hatari sana na mara nyingi huishia kwa madhara makubwa. Kisu hakihitaji nguvu nyingi ili kusababisha majeraha mabaya, na kukabiliana nacho kunaweza kuwa kosa la maisha.


Kutohifadhi Nguvu​

Watu wengi hutumia nguvu zote kwa mpigo ndani ya zile sekunde 30 za mwanzo, matokeo yake huchoka haraka kwa kutumia nguvu nyingi mwanzoni mwa pambano, Hii ni advantage kubwa kwa mtu unaepigana nae alietunza nguvu atakudonoa sana ukiwa huna nguvu, Ni vema kutumia nguvu kwa sekunde 10 za mwanzo ukiona adui bado anastahimili ni muda wa kujitafakari kutunza nguvu zako.. Ni muhimu kugawa nguvu zako ili usiwe rahisi kushindwa.


Kujitamba na Kuongea Maneno mengi (Kupiga Bla Bla)​

Ni pambano la kimwili sio kuchambana kwa mdomo, Usiongee sana kabla ya pambano, Anza kuongea ukiingia kwenye pambano na dalili zinaonesha unammudu, Kuchimba mkwara au kujigamba kuhusu kile utakachofanya huchochea hasira za mpinzani na kumpa nafasi ya kujipanga jinsi ya kukushushia kipigo. Kimya na umakini ni silaha bora za akili wakati wa mapambano ya mtaani.


Kujaribu Kuiga Mapigo ya Kwenye Filamu​

Mapambano ya kwenye filamu ni ya kubuni na mara nyingi hayahusiani na hali halisi. Kujaribu kuruka au kufanya miondoko ya kushangaza kama unavyoona kwenye filamu kunaweza kukuweka kwenye hatari zaidi. Badala yake, elewa hali halisi na tumia mbinu za msingi.


Kufikiri Kuzuia / Kublock ngumi ni Rahisi Kama Kwenye Game​

Katika hali halisi, kuzuia ngumi sio rahisi. Badala ya kujaribu kuzuia ngumi zote, ni bora zaidi kurudi nyuma au kuendelea kumshambulia mpinzani. Kuwaza kuwa unaweza kuzuia kila ngumi kama kwenye game ni kosa litakalo kugharimu.


Kutoshusha Kidevu Chini​

Kidevu kilichoinuliwa huacha uso wazi na rahisi kushambuliwa kwa uppercuts na vifuti. Kuweka kidevu chini ni mbinu ya msingi ambayo inapunguza hatari ya kupata pigo kubwa kwenye uso. Hakikisha unalinda kichwa chako vizuri.


Kuacha baada ya Kumwangusha Mpinzani​

Baada ya kumwangusha mpinzani, usidhani pambano limeisha na kugeuza mgongo kuondoka. Wengi wao huweza kusimama tena na kuendeleza shambulizi. Hakikisha unadhibiti hali na kuwa tayari iwapo atajaribu kushambulia tena. Usimpe nafasi ya kukushambulia unapogeuka.

Kumsukuma Mtu Baada ya Kusukumwa​

Kusukuma hakutatatua chochote. Ikiwa umesukumwa, jibu kwa ngumi badala ya kurudisha msukumo. Hii inakupa nafasi ya kujilinda na kushinda pambano kabla mpinzani hajapata nguvu ya kushambulia tena.

Kupigana na Mtu Mwenye Mwili Mkubwa au Mrefu​

Kupigana na mtu mwenye nguvu nyingi, mwili mkubwa, au mrefu ni hatari zaidi. Watu hawa mara nyingi wana faida ya kimwili inayoweza kukuangamiza kwa urahisi. Badala ya kupigana, tafuta njia ya kuzuia au kujiepusha kabisa.


Kutaka kuendelea Kulinda Heshima baada ya kushushiwa kipigo​

Kutaka kuendelea kupigana kwa sababu ya kiburi au kujaribu kuokoa heshima mara nyingi hupelekea madhara makubwa. Ikiwa umeona hali ni mbaya umeshushiwa kipigo hevi ni bora zaidi kukubali kushindwa au kutoroka. Hakuna aibu katika kuokoa maisha yako.

Kurudia Mbinu Zisizozaa Matunda​

Ikiwa mbinu fulani haifanyi kazi kwa mpinzani, kuendelea kujaribu hakuwezi kubadilisha matokeo. Badala yake, kuwa mbunifu na badilisha mkakati wako. Kurudia makosa yale yale kunaongeza tu nafasi ya kushindwa.
 
" Kumsumkuma mtu baada ya kusukumwa"
..................
" Ikiwa umesukumwa jibu kwa ngumi, usijibu kwa msukumo".😁😁😁 SIO RAHISI KIHIVYO MKUU.


Mkuu kusema ni rahisi kuliko kutenda. Ngumi sio sawa na mpira wa miguu kwamba useme ukizidiwa utampasia mwenzako.


Uzi wako ni sahihi kabisa kama unaongea na watu wangumi na sio wenzangu na Mimi ambae anaingia kwenye pambano la ngumi huku kimoyomoyo akiomba Mungu afanye muujiza atokee mtu wa kuamua.

Kikubwa kuliko vyote ambacho umekisahau ni kuhusu saikolojia ya watu kwenye ngumi.

Unajua kwanini mtu huwa anasukuma baada ya kusukumwa? Do u know the psychology behind?


Ni kwamba wote wana ogopana? Anaeanza kusukuma anaogopa na anae rudisha msukumo anaogopa pia.

Wanasukumana kwa ajili ya kubuy time waje watu wagombelezee au kujaribu kugather courage ya kurusha ngumi kwa mara ya kwanza.

Kupigana sio jambo rahisi kama ambavyo mtoa mada unajaribu kuiweka
 
20240822_072134.jpg
 
"Kujitamba kwa kuongea maneno mengi ".


Hii ni mbinu ya kisaikolojia kuua ari ya mpinzani wako na KUMTISHA.

Kwa mfano napigana na mtu huku nikisema " Nakuchinja leo wewe Mse## Nakuua leo. Nakupasua macho n.k.

Inaweza KUMTISHA mpinzani wako
Ni kwa maeneo kama kanda ya Pwani maneno hutumika zaidi kwenye ugomvi, Bondia kama Mandonga ni mfano

Kwengine utameza ngumi wakati unaongea na mapengo
 
Ni kwa maeneo kama kanda ya Pwani wanakopenda kutumia zaidi mdomo, Niliwahi kuona kuna mashindano ya kuchambana.

Kwengine utameza ngumi wakati unaongea na mapengo
Inategemea:

1.unaepigana nae . Kama unapigana na muoga wa kupigana utamshinda.


2. Itategemeana na matendo unayo yafanya wakati unatamka hayo maneno kama unatamka maneno tupu yes itakuwa hivyo unavyo sema wewe lakini kama unaongea huku unafanya vitendo utapata matokeo. Nimekupiga roba nakupiga vifuti vya puani huku nakwambia nakuua kwanini isiwe na impact...?

Usiwasharau watu wa pwani mkuu siku moja utakuja kupinda shayo.

Hata Mwakinyo na Dullah Mbabe ni watoto wa pwani pia mkuu.

Usikariri
 
Inategemea:

1.unaepigana nae . Kama unapigana na muoga wa kupigana utamshinda.


2. Itategemeana na matendo unayo yafanya wakati unatamka hayo maneno kama unatamka maneno tupu yes itakuwa hivyo unavyo sema wewe lakini kama unaongea huku unafanya vitendo utapata matokeo. Nimekupiga roba nakupiga vifuti vya puani huku nakwambia nakuua kwanini isiwe na impact...?

Usiwasharau watu wa pwani mkuu siku moja utakuja kupinda shayo.

Hata Mwakinyo na Dullah Mbabe ni watoto wa pwani pia mkuu.

Usikariri
Na MANDONGA pia .
 
Inategemea:

1.unaepigana nae . Kama unapigana na muoga wa kupigana utamshinda.


2. Itategemeana na matendo unayo yafanya wakati unatamka hayo maneno kama unatamka maneno tupu yes itakuwa hivyo unavyo sema wewe lakini kama unaongea huku unafanya vitendo utapata matokeo. Nimekupiga roba nakupiga vifuti vya puani huku nakwambia nakuua kwanini isiwe na impact...?

Usiwasharau watu wa pwani mkuu siku moja utakuja kupinda shayo.

Hata Mwakinyo na Dullah Mbabe ni watoto wa pwani pia mkuu.

Usikariri
Suala ni kuongea sana kabla ya pambano a,k,a

Mkishaanza kupigana ukiwa na possession nzuri mananeo yana advantage kubwa kumdhoofisha mpinzani.
 
Kuna siku maeneo ya job kuna mwamba alikuwa anampa kisago na watu wameuchuna tu
Nikaona sio fair ngoja nikaawamulie
Jamaa akamuache Yule mpenzi akanivaa Mimi Ile kunishika Tu nikajua MH tayari nishauvaa msala manake alikuwa mbavu alafu amepanda
Raia nao wanasogea sio kuamulia Bali kutengeneza uwanja dah nikaona no way out hapa ni kupambana Tu
Kilichotokea SASA......
 
Asante kwa SoMo zuri hasa kwasisi wababe uchwara wa mtaa .

Mimi najitahidi kuongeza pumzi ya kukimbia lakini pia najaza kamkono kangu ,alafu mdomo mkwara mwingi kiasi kwamba Kama hunijui ukakuta nampiga mtu biti basi utasema jamaa anaua .

Ila kubwa kuliko najitahidi kuwa na mbio shitukizi yaani kikubwa sahau kupambana na Mimi dakika kumi na tano alafu naona utanizidi maguvu lazima nile winga

Ila sipigani sehemu nisiyoona Kuna ukaribu na mawe ili hata njia za kula winga zikifungwa basi nihamie kwenye mandazi ya Mungu
 
Kuna siku maeneo ya job kuna mwamba alikuwa anampa kisago na watu wameuchuna tu
Nikaona sio fair ngoja nikaawamulie
Jamaa akamuache Yule mpenzi akanivaa Mimi Ile kunishika Tu nikajua MH tayari nishauvaa msala manake alikuwa mbavu alafu amepanda
Raia nao wanasogea sio kuamulia Bali kutengeneza uwanja dah nikaona no way out hapa ni kupambana Tu
Kilichotokea SASA......
Watu wanasogea sio kuamulia ila kutengeneza uwanja 🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom