nteze john lungu
JF-Expert Member
- Jul 20, 2018
- 214
- 200
Duuu inasikitisha sana kwa mchezaji aliyecheza kwa kiwango chake kuishia kunywa gongoMarehemu alikuwa ' anasubiri ' kwa Kipenzi changu Patrick Betwell ' Buba ' Mmasai ' Kamarada ' wangu. Huyo Betwell alikuwa anaujua mpira hadi wengi tulikuwa tunashangaa na kujiuliza ni kwanini hakutaka kwenda Ulaya kwani asingekosa Timu. Hivi sasa yupo zake tu Mkoani Ruvuma ( Songea ) anavuna Mahindi na kushinda tu kunywa Gongo japo makazi yake mengine ni Mkoani Morogoro. Kuna wakati ' Rafiki ' yangu mmoja aliniambia alimuona ' Vibanda ' vya Gongo pale eneo la ' Manzese ' Mkoani Morogoro jirani na Uwanja ule wa Sabasaba akiwa ' kalewa ' chakari na Gongo niliumia, nilihuzunika na kusikitika sana ' Kamarada '.