Ameen
Mpenda Yesu.
Basi na tuendelee kupata barak za bwana katika uombaji
HAYA EE MOYO WANGU.
1.Haya ee moyo wangu, imba kwa furaha
Umwimbie muumbaji, mbingu na dunia
Atukuzwaye pote umsifu na wewe
Kwa nguvu zako zoote umri wako wote
2.Mungu wake Yakobo ndiye Mungu wetu.
Ukimchagua yeye, una fungu jema.
Unacho ktu chema, umepata mali.
Moyo utakung'aa, shida zitakwisha.
3.Ni mwenye nguvu nyingi, hana amshindaye.
Kwa hekima, aumba, vyote ni vya ajabu.
Misitu na mabonde, milima na mashamba.
Vilivyo baharini, wanyma porini
4.Ana mizungu mingi, kuponya wanawe,
Anawapa riziki, hata siku za njaa.
Wenye chakula haba, wanenepa miili
Hata waliofungwa, anawafungua.
5.Mashangilio yote, hayamtoshi yeye.
Ni mwema peke yake, nami ni vumbi tu
Ananihurumia, kwa kuwa ni wake.
Kwa hiyo nalikuza jina lake pote