Haya ya kufanyiwa kazi haraka Simba SC kabla ya kuanza Ligi Kuu na michuano ya CAF

Haya ya kufanyiwa kazi haraka Simba SC kabla ya kuanza Ligi Kuu na michuano ya CAF

Simba ni timu mbovu na dhaifu kuanzia kocha mkuu wachezaji na viongozi hawana mbinu bora kwasasa mtauana bure tu. Hii inaitwa kidhungu Rise and Fall theory, Simba ilifika Peak sasa inashuka mashabiki wa Simba muwe wapole this is Yanga moment!! Tulieni sindano na dawa viingie vizuri tuwapasue kila mechi mpaka mkiri kuwa "Mayele hakuna beki wa kumkaba Tanzania "

msisahau asiyekubali kushindwa si mshindani! !!@
 
Kesho Geita anakufa 3
1-Beno
2-kapombe
3-Zimbwe
4-Onyango
5-Outtara
6-mkude
7-Sakho
8-kanoute
9-Dejan
10-Chama
11-Okrah
 
Kapombe ni versatile toka muda mrefu hivyo hakukuwa na kutengeneza chochote pale
Sijajua unabisha au unakubali. Kitendo cha kocha kuona kuwa timu yangu ina mapungufu fulani na mchezaji wangu fulani nikimuhamisha nikampa haya majukumu mapya na akayaweza basi huyo kocha ni mtaalamu hasa. Na kutengenezwa sijui wewe umetafsiri vipi kwa upeo wako. Kwangu mimi kutengenezwa maana yake ni kumpa mchezaji majukumu mapya uwanjani halafu unamjaribu kwenye viwanja vya mazoezi au mechi za kirafiki huku unampa maelekezo mbali mbali ni kwa namna gani wewe kocha unataka acheze ili akupe kile ambacho kinashindikana kwa "regular players" wa kila siku wa hiyo nafasi. Na ndicho kitu alikifanya Lentchantre kwa Kapombe. Kwa wanaomjua Kapombe muda mrefu ni "regular player" kwa nafasi ya beki wa pembeni au beki wa kati. Lakini Lentchantre alienda mbali zaidi kumtengeneza acheze namba 6 na wakati mwingine namba 8 ili apte matokeo anayoyahitaji kama kocha.
 
Banda
Bocco
Mzamiru
Nyoni
Mkude
Kakolanya
Mhilu
Hawawezi tufikisha popote pale
 
Kwanza mimi napingana na hoja zako zote.

1. Unasema kocha abadilike kwa kufungwa mechi moja tu na Yanga ? Si kweli Zoran aliaproach vizuri sana mechi ya Yanga first half na asingefanya mabadiliko kwenye second half wakati kikosi chake kilicheza vizuri kipindi cha kwanza.
Subs zake alifanya kwa nia njema kabisa ya kwenda kutunza mpira kwa kumuingiza Okwa na Okra alichokosea ni kumtoa Chama akamuacha Sakho, alitakiwa kumtoa Sakho amuache Chama.

2. Unasema Simba wanahitaji DM simba DM wanao zaidi ya watatu kikosini na wote wana quality kuliko timu yoyote ya ligi kuu. Akpan, Kanoute, Mkude na Mzamiru.

3. Unasema Simba wanahitaji replacement ya Prime Kanoute lini Kanoute alikuwa kwenye Prime yake ?

4. Mnataka mashabiki waachie ngazi kwa lipi? Kufungwa na Yanga mechi mbili mfululizo ? Are you serious shabiki wa namna hiyo ni shabiki maandazi and probably ni shabiki mamluki.

5. Anyway umesuggest Simba wamsajili DM wamwache nani waende wakamchukue nani ?
Hapo kwa Akpan ndipo namlaumu kocha, naamini Akpan anaweza kucheza vizuri zaidi ya Mkude akiaminiwa na kupewa nafasi, kama kocha anampa nafasi mzungu wake anayeharibu kila siku, kwanini hampi Akpan tumuone?

Naamini muda unavyokwenda atamzoea Akpan na kuuona ubora wake.
 
Goli la kwanza la Mayele ndiyo kosa la DM ila goli la pili lilikuwa kosa la timu nzima.

Hakuna aliyetrace back kwa strikers kumsumbua Dikson Job,

Kwenye midfield hakuna aliyefanya zone marking.

Defenders hakuna aliyenusa hatari ya mpira ule na kufanya interception in fact the whole team was in shambles.
Hapa ajabu naona wengine wanamlaumu mpaka Inonga kama vile yeye ndie chanzo cha yale magoli tuliyofungwa..
 
Back
Top Bottom