Habari zenu ndugu zangu. Baada ya salam, ningependa niende kwenye mada husika kwa kutumia mifano hai iliyopita.
Katika historia ya nchi yetu toka tapate uhuru mpaka leo, hakuna kipindi kilichokuwa na changamoto za kiusalama kama kipindi cha miaka ya 1989 hadi 1993. Hiki ndio kipindi ambacho nchi ilishuhudia vikundi mbali mbali vya kihalifu kama vile COMANDO YOSSO, RED SOLDIER (red sonja) SIAFU FAMILY, WATOTO WA SHETANI nk.
Kati ya hayo makundi mimi nililijua zaidi kundi la "COMMANDO YOSSO" hili kundi lilikuwa ni kundi hatari kati ya makundi yote yaliokuwepo wakati huo. Kundi hili lilianzishwa na lilikuwa na masikani yake huko Mburahati, ambapo vijana wa kundi hilo walikuwa ni wenyeji wa maeneo hayo ya Mburahati, Kigogo, Mabibo, Manzese, na baadhi ya vijana kutoka maeneo ya Tandale na Kagera mikoroshini pia walikuwemo. Kiongozi mkuu wa kundi hilo alikuwa ni baba yangu mdogo kwa jina alikuwa anaitwa Kuveta R.I.P. Bila shaka wazee, vijana, na watu mbali mbali wa maeneo hayo miaka hiyo walikuwa wanamfahamu aidha kwa kumuona au kumsikia.
Baba yangu mdogo huyo hakuwa katili kivile, ila ukiingia kwenye 18 zake hauwezi kubaki salama. Kwenye 18 zake yeye hakujali wewe ni askari, muhuni mwenzake au nani. Mara nyingi alikuwa na machale kiasi kwamba akikaa maskani akiwaambia tuondokeni basi watakaopuuza baada ya dakika mbili jela itawahusu, japo sometimes na yeye polisi walikuwa wanamuotea, pia alijaaliwa uwezo wa kupambana na adui yeyote.
Alikuwa kaenda hewani, mwili jumba hasa kwa upande wa kifua na mikono, miguu iliyo imarika. Utotoni alijifunza michezo hatari ya ngumi na karate maeneo mbali mbali, swala la kuvunja tofali kwa ngumi au kichwa lilikuwa la kawaida kwake. Kwahiyo alikuwa fit na aliogopeka kweli kweli, maana hata kukamatwa kwake, alikuwa anamatwa na lundo la askari tena wenye silaha za moto.
Hakuna jela ya Tanzania ambayo hakuwahi kufungwa, na kote alipokwenda wababe mkwara walimpa heshima yake, na alikuwa mpaka na tandiko lake. Nasikia kuna bongo movie washawahi kucheza sinema yake (japo sijaiona kutokana na kuishi nje ya Tz muda mrefu).
Tukiachana na yeye pia kulikuwa na baadhi ya watemi wengine wa chini yake kina Domokeka, Kaboka mchizi, Chura dume, na wengine wengi wa makundi hayo ambao nimewasahau majina yao. Pia kulikuwa na vikundi vya michiriku ambavyo navyo vilikuwa vikifuga wahuni mbali mbali jijini. Yani hicho ndio kilikuwa kipindi hatari kwa utumiaji wa madawa ya kulevya, ulevi usiokuwa na kipimo, wizi wa usiku na mchana kweupe.
Ilifikia kipindi kukiwa na mnanda karibu yenu basi msicheze mbali na milango au madirisha yenu, au kundi la wahuni linaweza kumteka mwanamk mbele ya mumewe likaenda kufanya mambo yao na wakimaliza wanamuacha arudi kwao nk.
Watu walikatwa mapanga hovyo bila sababu, makundi haya yalimiliki silaha za moto, na za jadi kama vile bunduki, mapanga, shoka nk. Yani hicho ndio kilikuwa kipindi kibaya cha umwagaji damu jijini Dar es salaam na Tanzania kwa ujumla. Raisi Mwinyi alipoona hali ya usalama nchini inazidi kuwa mbaya ikabidi amteuwe mh Augustino .L. Mrema kuwa waziri wa mambo ya ndani.
Mrema alipoteuliwa akaapa kuyatokomeza makundi hayo kwa kuandaa oparation maalumu ya polisi, wakishirikiana na sungu sungu ambao yeye (Mrema) ndo muasisi. Basi bwana shughuli ikaanza huku Mrema mwenyew akiwa mstari wa mbele katika oparation ile.
Kwa vile serikali ilishirikisha sungu sungu ambao ni wananchi wa maeneo mbali mbali ya jiji, basi ilikuwa rahisi kuwatambua kimya kimya wahusika wa makundi yale pamoja na wahalifu wengine. Ikawa wakijua nyumba fulani kuna kijana muhalifu wazee wa kazi askari wakishirikiana na sungu sungu wanakuja usiku wanagonga mlango askari wanaingia, wanamchomoa waliemfuata wanaondoka nae. Kama wewe ni mzazi au ndugu, basi asubuhi utaletea taarifa na mjumbe kuwa uende sehemu fulani ukachukue mzoga wako uuzike.
Oparation hii haikushia kwenye nyumba tu bali mpaka kwenye maskani zao walifuatwa na kuangamizwa huko huko. Nakumbuka bamdogo Kuveta aliuwawa siku ya tatu tu akiwa ametoka jela. Akiwa ameenda kulala kwa demu wake, siku hiyo ghafla usiku walivamiwa na kundi la watu zaidi ya 50 wakiwemo askari wenye silaha na sungu sungu wenye mapanga na kuanza kumshambulia.
Maiti yake tulikuta ikiwa na majeraha makubwa kwenye maungio ya mikono yake, kifuani na kichwani. Tulipomuuliza demu wake akasema alipata yale majeraha ya mikononi baada ya kupambana na askari mwenye silaha, ambapo sungu sungu waliona angefanikiwa kumpokonya askari ile bunduki basi ingekuwa hatari kwa uhai wao, so suluhisho likawa ni kuikata mikono yake kwa mapanga japo hiyo haikumfanya aache kupambana, ndipo wakaamia kichwani na kifuani so kutokana na kuvuja sana kwa damu akaishiwa nguvu akaanguka na kufariki.
Pia yule demu wake walimjeruhi baadhi ya sehemu za mwili wake, ila hawakumuua. Baada ya mauaji hayo ya wahalifu mbali mbali, wizi ukapungua kama sio ukaisha kbs jijini Dar es salaam. Vikundi vya michiriko (minanda) navyo vikaanza kusambaratika, amani ikarejea.
Watu wakaanza kuishi kama Saudia Arabia ambapo mida ya sala inafika, watu wanaenda kusali huku wakiwa wameacha biashara zao wazi kabisa. Sasa inashangaza sasa hivi vipanya road vyenye umri wa miaka 14, 15 hadi 18 vinafunga mtaa wa wanaume wenye umri mkubwa na kuchukua kila kitu ndani ya majumba yao.
Kwanini ile oparation maalumu ya Mrema isirudie kuwamaliza mbwa hao. Au polisi kwanini wasishirikane na wananchi (sungu sungu) kwa style ile ile waliyotumia wenzao kumaliza ushenzi huo unaoendelea kwa kasi jijini na nchini kwa ujumla? Watanzania tuiombe serikali irudishe OPARATION MREMA, huu uhalifu utaisha mara moja.