Hayati Baba Wa Taifa amewahi kusema kuwa Hatuna mjomba wa kuja kutujengea nchi yetu

Hayati Baba Wa Taifa amewahi kusema kuwa Hatuna mjomba wa kuja kutujengea nchi yetu

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu napenda niwaambie kuwa Tanzania itajengwa na sisi wenyewe watanzania, Hatuna mtu atakuja kutujengea nchi yetu, Katika kufikia ndoto ya Tanzania tuitakayo na kuwa Kama ulaya Ni lazima tufahamu kuwa Kuna kipindi Cha mpito.

Lazima tupitie maumivu Kama walivyo pitia mataifa ya ulaya .walitozana Sana kodi, Tozo na ushuru kufikia hapo walipo, walijifunga mikanda, walijinyima ndio wakazijenga nchi zao

Hata sisi katika kuijenga nchi yetu hakuna njia fupi ya kutufikisha waliko fika wenzetu kimaendeleo, tusidanganywe na mtu kuwa tutaendelea pasipo kuwajibika kulipia na kugharamia miradi yetu, lazima tuighalamie na kuwa na uchungu wa kuilinda miradi yetu kwa kutambua kuwa tukiharibu tutaijenga wenyewe tena,

Uzuri wa serikali hii imekuwa na uwazi mkubwa katika matumizi yake, kwani hamuvioni vituo vya Afya, zahanati,shule na hata Barabara zilizojengwa kwa tozo na Kodi zetu, mnataka fedha zitoke wapi tusipochangishana mifukoni mwetu, mnataka kila siku tukakope tu, Ni lini tutaijenga wenyewe nchi yetu. hapana

Ni Sasa wakati wa watanzania Kuendelea kuijenga nchi yetu na kusimamia kile tukijengacho kwa mikono yetu

Hatuwezi tukawajazia madeni ya kulipa kizazi kijacho badala ya kukipa nafasi ya kujenga nacho maisha na mstakabari wake, lazima tujitwishe mzigo wetu wenyewe, Tumuunge mkono mh Rais katika kuijenga nchi hii, Tuwe wa kwanza kuilinda miradi yetu kwa uchungu.

Tuwawajibishe tutakao ona wanapalamia pesa zetu tunazotaka kujengea nchi yetu

Rais wetu anauchungu mkubwa na nchi hii na Tuendelee kumwamini, penye kurekebisha atarekebisha na panapohitaji kuangalia upya Sheria iliyosainiwa atafanya hivyo, Mh Rais wetu Ni msikivu Sana na Mwenye huruma Sana ,hivyo nchi ipo mikono salama, Kama una ushauri wa chanzo kingine zaidi Cha mapato wewe toa na ujumbe utafika kwa mh Rais na ataupokea na kufanyia kazi Kama unafaa maana mh Rais Ni msikivu sana
 
Chanzo mingine lipo hapo mjengoni Dodoma yaani azuie posho za binge na awakate Kodi kwenye mishahara Yao. Pia yeye mwenyewe apunguze msururu wa magari wakati wa ziara zake na ikimpendeza aache kununulia viongozi wenzake magari ya anasa.
Na yeye rais akatwe Kodi kwenye mshahara wake na akiwaachisha wateule wake kazi waliopwe mafao TU na nauli za kwenda kwao! Na la muhimu ni hili:-
Asitishe tozo zote kwani ni wizi mtupu.
 
Awamu hii tuna viongozi waoga ,wanatakiwa kutoka hadharani na kutetea maamuzi yao.

Shida wanakaa kimya watu wanajilalamikia weeee wakati ni mambo madogo tuu haya.

Maendeleo sio lelemama.
 
Awamu hii tuna viongozi waoga ,wanatakiwa kutoka hadharani na kutetea maamuzi yao.

Shida wanakaa kimya watu wanajilalamikia weeee wakati ni mambo madogo tuu haya.

Maendeleo sio lelemama.
Kabisa mkuu inatakiwa watoke waelezee hasa wenye dhamana katika wizara husika walioaminiwa na mh Rais Wetu, wasitake kumuangusha mh Rais wetu, Naomba wawe wepesi katika kutoa ufafanuzi wa jambo lolote linalokuwa linaleta mtafaruku ili kuziba mianya ya upotoshaji inayokuwa inafanywa na baadhi ya watu wasio wazalendo

Watu wanajuwa namna Rais wetu anavyofanya kazi vizuri na kuwa muwazi kwa kila hatua apigayo na kwa maamuzi ayachukuayo, Ni darasa kwa viongozi wengine kuiga katika utendaji kazi wa mh Rais kwa kuwa na uharaka na wepesi wa kutoa na kufafanua Taarifa zinazokuwa hazijaeleweka au zinazokuwa zinapotoshwa na baadhi ya watu,

Tuna Imani na mh Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan na tunamatumaini Naye makubwa Sana katika kuijenga nchi yetu, Amejidhihirisha waziwazi kuwa yeye Ni mtumishi wetu na anatutumikia watanzania kwa uaminifu na upendo mkubwa sana
 
Pamoja na hayo;
1.Serikali idhibiti uvujaji wa fedha za umma
2.Ofisi za umma zibane matumizi
3.Kila raia wa Tanzania, mwenye mshahara akatwe kodi ya PAYE
4.Hao wabunge 19 wasiokuwa na chama wafukuzwe(japo sio permanent solution).
 
Ndugu zangu napenda niwaambie kuwa Tanzania itajengwa na sisi wenyewe watanzania, Hatuna mtu atakuja kutujengea nchi yetu, Katika kufikia ndoto ya Tanzania tuitakayo na kuwa Kama ulaya Ni lazima tufahamu kuwa Kuna kipindi Cha mpito.

Lazima tupitie maumivu Kama walivyo pitia mataifa ya ulaya .walitozana Sana kodi, Tozo na ushuru kufikia hapo walipo, walijifunga mikanda, walijinyima ndio wakazijenga nchi zao

Hata sisi katika kuijenga nchi yetu hakuna njia fupi ya kutufikisha waliko fika wenzetu kimaendeleo, tusidanganywe na mtu kuwa tutaendelea pasipo kuwajibika kulipia na kugharamia miradi yetu, lazima tuighalamie na kuwa na uchungu wa kuilinda miradi yetu kwa kutambua kuwa tukiharibu tutaijenga wenyewe tena,

Uzuri wa serikali hii imekuwa na uwazi mkubwa katika matumizi yake, kwani hamuvioni vituo vya Afya, zahanati,shule na hata Barabara zilizojengwa kwa tozo na Kodi zetu, mnataka fedha zitoke wapi tusipochangishana mifukoni mwetu, mnataka kila siku tukakope tu, Ni lini tutaijenga wenyewe nchi yetu. hapana

Ni Sasa wakati wa watanzania Kuendelea kuijenga nchi yetu na kusimamia kile tukijengacho kwa mikono yetu

Hatuwezi tukawajazia madeni ya kulipa kizazi kijacho badala ya kukipa nafasi ya kujenga nacho maisha na mstakabari wake, lazima tujitwishe mzigo wetu wenyewe, Tumuunge mkono mh Rais katika kuijenga nchi hii, Tuwe wa kwanza kuilinda miradi yetu kwa uchungu.

Tuwawajibishe tutakao ona wanapalamia pesa zetu tunazotaka kujengea nchi yetu

Rais wetu anauchungu mkubwa na nchi hii na Tuendelee kumwamini, penye kurekebisha atarekebisha na panapohitaji kuangalia upya Sheria iliyosainiwa atafanya hivyo, Mh Rais wetu Ni msikivu Sana na Mwenye huruma Sana ,hivyo nchi ipo mikono salama, Kama una ushauri wa chanzo kingine zaidi Cha mapato wewe toa na ujumbe utafika kwa mh Rais na ataupokea na kufanyia kazi Kama unafaa maana mh Rais Ni msikivu sana
Duh!

Andiko la ajabu sana hili!

Kichwa habari kingine, habari inayozungumziwa nyingine!

Huyu Rais unayemzungumzia hapa, "anaamini tuna wajomba," na kweli tunao, wengine wapo Oman watakaokuja kutuletea maendeleo.

Nikueleze wazi hapa; kwa mwendo tunaokwenda nao sasa Tanzania haitakuwa na tofauti yoyote na nchi kama Haiti.
Kuna aina hiyo ya mataifa, ambayo daima yatakuwa ni mataifa duni hata ufanye nini.
Mbaya zaidi, hata ule msisimko wa wananchi kujitutumua kuondoka kwenye rindi la umaskini ndio nao unadidimia. Sasa unategemea nchi kuwa na maendeleo kwa vipi, kama hata wananchi wanahimizwa kuwategemea wawekezaji waje kuleta maendeleo!

Huo msemo wa Mwalimu uliouweka katika kichwa cha mada yako ni wazi hukuuelewa; na mbaya zaidi hata uliyoeleza ndani ya mada hayana uhusiano wowote na aliyosema Mwalimu Nyerere. Umependa tu kunakili hayo maneno ili kupotosha maana nzima ya lengo la hayo maneno.

Bure Kabisa!
 
Duh!

Andiko la ajabu sana hili!

Kichwa habari kingine, habari inayozungumziwa nyingine!

Huyu Rais unayemzungumzia hapa, "anaamini tuna wajomba," na kweli tunao, wengine wapo Oman watakaokuja kutuletea maendeleo.

Nikueleze wazi hapa; kwa mwendo tunaokwenda nao sasa Tanzania haitakuwa na tofauti yoyote na nchi kama Haiti.
Kuna aina hiyo ya mataifa, ambayo daima yatakuwa ni mataifa duni hata ufanye nini.
Mbaya zaidi, hata ule msisimko wa wananchi kujitutumua kuondoka kwenye rindi la umaskini ndio nao unadidimia. Sasa unategemea nchi kuwa na maendeleo kwa vipi, kama hata wananchi wanahimizwa kuwategemea wawekezaji waje kuleta maendeleo!

Huo msemo wa Mwalimu uliouweka katika kichwa cha mada yako ni wazi hukuuelewa; na mbaya zaidi hata uliyoeleza ndani ya mada hayana uhusiano wowote na aliyosema Mwalimu Nyerere. Umependa tu kunakili hayo maneno ili kupotosha maana nzima ya lengo la hayo maneno.

Bure Kabisa!
Kodi na Tozo hutaki ziwepo halafu hapo hapo unataka maendeleo, hayo maendeleo unataka Nani ayalete, unataka Nani avuje jasho kwa ajili yetu sisi, unataka Nani abebe maumivu yetu ili sisi tuishi kwa starehe, unataka Nani abebe wajibu wetu, tuijenge nchi yetu kwa kuchangia kidogo kidogo toka katika vipato vyetu tulivyo navyo,
 
Kodi na Tozo hutaki ziwepo halafu hapo hapo unataka maendeleo, hayo maendeleo unataka Nani ayalete, unataka Nani avuje jasho kwa ajili yetu sisi, unataka Nani abebe maumivu yetu ili sisi tuishi kwa starehe, unataka Nani abebe wajibu wetu, tuijenge nchi yetu kwa kuchangia kidogo kidogo toka katika vipato vyetu tulivyo navyo,
Nikiangalia unavyoandika ni wazi wewe ni mwepesi sana. Kazi yako hapa ni kuwa "chawa" huna lingine lolote.

Hivi vi-'tozo' unavyovivimbishia tumbo, wewe unadhani ndivyo vitakavyokuletea maendeleo? Kwanza hii ni michango tu ya wapigaji, na kuwalipa watu kama wewe mnaoshinda hapa mkivimbisha mishipa ili muonekane kwa hao mnaowasifia mnafanya kazi mnayotumwa.

Yaani wewe ulikwenda shule ili utokee kuwa mtu aliyejitoa akili kiasi hiki?

Hovyo kabisa.

Lakini sina budi nijilaumu mwenyewe kwa kujihusisha katika kuchangia kwenye mada mbovu kama hii. Mada kama hizi huwa napita tu!
 
Ndugu zangu napenda niwaambie kuwa Tanzania itajengwa na sisi wenyewe watanzania, Hatuna mtu atakuja kutujengea nchi yetu, Katika kufikia ndoto ya Tanzania tuitakayo na kuwa Kama ulaya Ni lazima tufahamu kuwa Kuna kipindi Cha mpito.

Lazima tupitie maumivu Kama walivyo pitia mataifa ya ulaya .walitozana Sana kodi, Tozo na ushuru kufikia hapo walipo, walijifunga mikanda, walijinyima ndio wakazijenga nchi zao

Hata sisi katika kuijenga nchi yetu hakuna njia fupi ya kutufikisha waliko fika wenzetu kimaendeleo, tusidanganywe na mtu kuwa tutaendelea pasipo kuwajibika kulipia na kugharamia miradi yetu, lazima tuighalamie na kuwa na uchungu wa kuilinda miradi yetu kwa kutambua kuwa tukiharibu tutaijenga wenyewe tena,

Uzuri wa serikali hii imekuwa na uwazi mkubwa katika matumizi yake, kwani hamuvioni vituo vya Afya, zahanati,shule na hata Barabara zilizojengwa kwa tozo na Kodi zetu, mnataka fedha zitoke wapi tusipochangishana mifukoni mwetu, mnataka kila siku tukakope tu, Ni lini tutaijenga wenyewe nchi yetu. hapana

Ni Sasa wakati wa watanzania Kuendelea kuijenga nchi yetu na kusimamia kile tukijengacho kwa mikono yetu

Hatuwezi tukawajazia madeni ya kulipa kizazi kijacho badala ya kukipa nafasi ya kujenga nacho maisha na mstakabari wake, lazima tujitwishe mzigo wetu wenyewe, Tumuunge mkono mh Rais katika kuijenga nchi hii, Tuwe wa kwanza kuilinda miradi yetu kwa uchungu.

Tuwawajibishe tutakao ona wanapalamia pesa zetu tunazotaka kujengea nchi yetu

Rais wetu anauchungu mkubwa na nchi hii na Tuendelee kumwamini, penye kurekebisha atarekebisha na panapohitaji kuangalia upya Sheria iliyosainiwa atafanya hivyo, Mh Rais wetu Ni msikivu Sana na Mwenye huruma Sana ,hivyo nchi ipo mikono salama, Kama una ushauri wa chanzo kingine zaidi Cha mapato wewe toa na ujumbe utafika kwa mh Rais na ataupokea na kufanyia kazi Kama unafaa maana mh Rais Ni msikivu sana
Mjomba Peter 😀😀😀😬😎 sterling wa royo tuwa..
 
Back
Top Bottom