Hayati Dkt. John Magufuli alikuwa na Unique Style of Leadership

Hayati Dkt. John Magufuli alikuwa na Unique Style of Leadership

Magufuli ana mengi mazuri aliyotuachia ikiwemo:
  • Mapambano ya rushwa na ufisadi,
  • Ulinzi wa rasilimali,
  • Nidhamu serikalini na
  • Dhana ya Kujitegemea ambavyo ni lazima vienziwe
Pia kuna mengine mapungufu lakini hayo hapo juu imetuweka kwenye mstari mnyoofu
Nikweli ila one man army ni ngumu kutoboa, Taasisi ndiyo mfumo mzuri.....spirit ya kujitegemea Yes,Serikalini kulikuwa bado hakuna nidhamu bado bila Rushwa hupati huduma,ulinzi wa rasilimali bado aliwaamini walikuwa wanapiga tu fresh, akiambiwa anadhani ni majungu tu bila kujua ile imani aliyowapa inawapa kiburi cha kuiba
FB_IMG_1617000073596.jpg
 
Mjue adui wa mwafrika ni mwafrika mwenyewe
Mzee wa watu mmepinga majungu mengi sana licha ya shida yake kubwa ilikuwa ni kuisogeza nchi pazuri zaidi
Lakini kwa kuwa wengi ni wapenda vya kunyonga basi mkaona anawabania na badala yake mkaona wazungu ndio ndugu zenu
Hata enzi za mkoloni wazungu walitumia watu kama nyie kutumiza agenda zao
Mnaitwaga puppet ...mfano halisi ni Tundu lissu msomi aliyetanguliza njaa
 
Legacy ya JPM itadumu sana, so far tangu kuzaliwa Tanganyika Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere ndo na Hayati John Pombe Joseph Magufuli ndo maraisi pekee ambao watakumbukwa sana katika historia ya nchi hii. Pamoja na sababu nyingi ikiwemo kutetea wanyonge na kuataka Tanzania isonge mbele kimaendeleo kwa kuhakikisha rasilimali inanufaisha watu wote. Ni mtu ambaye amekuwa akijichanganya na watu wa kila aina.

Pamoja kuwa Rais bado yeye na familia yake wamekuwa wakiishi maisha ya kawaida sana pasipo kujiinua, pamoja na mapungufu machanche ya kujiiinua kama personality badala ya kuimarisha taasisi kwa kipindi kifupi amekuwa taaa na mwanga kwa alipotufikisha. Aliweza kutoa majibu ya hapo kwa hapo kulingana na shida za wananchi. Kwake mabo ya machakato na process haikuwa na nafasi katika utawala wake.

Rest in peace Hard Rock, chuma imara, Mungu akulaze mahala pema panapostahili peponi kulingana na matendo yako.
Tanzania iliingia kwenye hovyo hovyo na nilikuwa nimechoka mno kuona bado miaka mingine mitano, Mungu si Athmani.
 
Hatimaye Mama Samia Suluhu Hassan ameanza kwa style ileile ya Magu, tumbua mama, lete heshima, ngoa visiki, toa machaka ya wapigaji,
Tunakungalia kwa siku 100 mama, shikamoo mazaaaaa
Acha nijibu salamu kwa niaba yake,"Marhaba!!!".
 
Legacy ya JPM itadumu sana, so far tangu kuzaliwa Tanganyika Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere ndo na Hayati John Pombe Joseph Magufuli ndo maraisi pekee ambao watakumbukwa sana katika historia ya nchi hii. Pamoja na sababu nyingi ikiwemo kutetea wanyonge na kuataka Tanzania isonge mbele kimaendeleo kwa kuhakikisha rasilimali inanufaisha watu wote. Ni mtu ambaye amekuwa akijichanganya na watu wa kila aina.

Pamoja kuwa Rais bado yeye na familia yake wamekuwa wakiishi maisha ya kawaida sana pasipo kujiinua, pamoja na mapungufu machanche ya kujiiinua kama personality badala ya kuimarisha taasisi kwa kipindi kifupi amekuwa taaa na mwanga kwa alipotufikisha. Aliweza kutoa majibu ya hapo kwa hapo kulingana na shida za wananchi. Kwake mabo ya machakato na process haikuwa na nafasi katika utawala wake.

Rest in peace Hard Rock, chuma imara, Mungu akulaze mahala pema panapostahili peponi kulingana na matendo yako.
Ukweli mkuu huyu Baba atakumbukwa vizazi na vizazi historia itasimulia. Mambo ya swala fulani lipo kwenye mchakto, mara tuunde kamati ya uchunguzi hakutaka kuyasikia kabisa yaaani alimaliza papo kwa papo jibu lake lilikuwa kama digital watch yaani yes or no. Hizi ni sifa za watu wenye IQ kubwa. Hakupenda kucheleweshwa wala kukwamishwa daaah! tazimiss sana hotuba za Rais wangu JPM. sikuwahi choka kumsikiliza akiwa anhutubia maana hakutaka kuandikiwa hotuba alizungumza real fact.
 
Sisi kama watu wa Kaskazini Hatuna cha Kumkumbuka Rais Magufuli
 
Style ya leadership ya:

1.Kuondoka duniani wakati hahitajiki.

2.Kuteka wapinzani wake kama akina Azory Gwanda.

3.Kutesa wapinzani wake.

4.Kuua wapinzani wake na wakosoaji wake kama akina Ben saanane na kuwapiga wapinzani wake risasi kama ilivyokuwa kwa Tindu Lissu.

5.Kuua vyombo vya habari.

6.Kuua uhuru wa kujieleza.

7.Kuiba kura.

8.Kuua biashara za watu kupitia sera mbovu za uchumi.

9.Kudanganya katika takwimu za uchumi wa nchi.

10.Kuweka mihimili yote mitatu mfukoni mwake.

11.Kuua uchumi wa nchi kupitia sheria mbovu za uwekezaji.

12.Kuua watu kwa Corona kupitia leadership negligence.

13.Kuhakikisha kuwa akina Ben Saanane na Azory Gwanda walikipata cha mtema kuni.

14.Ukabila kwa kuhamishia rasilimali nyingi za nchi Chato na kujaza wasukuma serikalini.

15 Ukanda kwa kupeleka SGR mwanza wakati siyo economic strategic zone.

16.Ubaguzi wa rangi kwa kuwakandia wanawake weusi.

17.Kugandamiza demokrasia kwa kukataza vyama vya upinzani kufanya siasa wakati CCM kufanya siasa ni ruksa.

18.Kunyanyasa malaika-watoto wa kike wasirudi shule wakipata mimba.

19.Ufisadi wa kutisha kwa kufanya miradi mikubwa bila budget kupita bungeni.

20.Wizi wa kutisha wa mali ya uma kupitia Mayanga constructions LTD.

21.Kubambikizia kesi za kuhujumu uchumi wapinzani wake nchi nzima

22.Kugushi report ya CAG ya hasara za mabilion za ndege za TTCL.
 
Safi, unajua sana.
Alichofanikiwa zaidi ni kutengeneza mfumo wa kusiwa yeye tu! Magazeti, redio na TV vilipigwa pini ili kumsifu yeye! Angeruhusu na madhaifu yake yatangazwe na yabainishwe kwa raia sidhani kama ungetuandikia pambio kama hili! R.I.P JPM ulifanya yako kama walivyofanya watangulizi wako
 
Kwa nini asingepeleka mswaada bungeni avifute vyama vingi kama alivyopeleka wa kuhamishia ATCL Ikulu isifanyiwe ukaguzi bila ridhaa yake?
Wapinzani ndio wajuaji na dawa ya wajuaji na wasaliti ni kuwa eliminate tu [emoji16] he did a wonderful job ambayo inastahili pongezi. Huwezi kuwa unafundisha halafu wanafunzi wapumbavu wanapiga makelele huko backbenchaz
 
Sasa mbona unasema aliweka nidhamu serikalini!
Sasa kwani hata wewe kipindi unaruka ukuta wa shule form 2 pale ulikuwa ukiuruka mbele ya mwalimu wenu wa Nidhamu?
 
Kwa nini asingepeleka mswaada bungeni avifute vyama vingi kama alivyopeleka wa kuhamishia ATCL Ikulu isifanyiwe ukaguzi bila ridhaa yake?
Halafu akishavifuta mseme mmenyang'anywa demokrasia?
 
Back
Top Bottom