Hayati Dkt. Magufuli alishindwa kupambana na ufisadi, alikuwa mkali tu

Hayati Dkt. Magufuli alishindwa kupambana na ufisadi, alikuwa mkali tu

Prof Koboko

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2020
Posts
350
Reaction score
2,550
Kuna mambo ambayo binadamu sisi wasahaulifu sana. Wale walamba miguu waliojua kumpaka mzee mafuta kwa mgongo wa chupa walijawa unafki na hawa ndio waliokua wakimwibia na kumdanganya. Sitaki kulisema hili sana nakazia pia alivyosema Mtani wangu James Ile Millya.

Kama kweli hayati Rais Magufuli aliweza kupambana na ufisadi haya mabilioni ya bandarini hayakuibwa akiwa mzima? Haya mabilioni ambayo inasemekana kuna tatizo BoT si ndio wasimamizi ni wale wale aliowaweka yeye? Waliiba vipi wakati wao ndio waliokua wakiimba kua mzee anapambana na mafisadi na waliompinga pia mafisadi?

Mabilioni yaliyochotwa bandarini na tetesi zilizopo BOT inakosemekana kuna shida huko, huu ni mwanzo tu. Vipi kuhusu pesa zinazotolewa kujenga SGR na STIGLERS kule? Vipi mamlaka ziingine kama TANAPA na TRA hawaibi kweli?

Nilichogundua huenda awamu hii ufisadi ulikua mkubwa kuliko awamu zilizopita na ilikua ngumu watu kujulikana maana walilala kwenye kumsifia mzee ili asiwastukie. TAKUKURU wachape kazi hii nchi bado inapigwa sana na Rais wetu Mama Samia asimame imara.
 
Alishindwa au alikuwa sehemu ya ufisadi? Kama ndege kanunua bila idhini yabunge, SGR, Stiglers, nk una semaje hakuwa sehemu ya ufisadi?

Ukiona kiongozi ana zuia uhuru wa habari, huyo ni ukoma. JPM alikuwa namna hiyo. Mungu amuweke anapi stahili.
 
Vp mkuu wewe ungegewa kitengo usingepiga?

Ova
 
Kuna wajinga huko TBC utawakuta wanamsifia.
Karudisha nidhamu kazini.

Mtu mwenye nidhamu anaweza kuficha hadi milion mia4 ndani!!

Hovyo kabisa.
Una uhakika na unachokisema. Au ni akili za kwenye mtandao?
 
Waimba mapambio na washangiliaji wameumbuka.
 
Hata mi nilishangaa tunaambiwa na meko kuwa wizi umekomeshwa lakini mtaani hali mbaya sana, wakati wa kikwete wizi ulikuwepo escro, epa e.t.c lakini mtaani mambo yalikuwa shwari mtaani , kumbe awamu hii walikomba mpaka za mtaani tukabaki kula magunia.
 
Back
Top Bottom