Hayati Dkt. Magufuli alishindwa kupambana na ufisadi, alikuwa mkali tu

Hayati Dkt. Magufuli alishindwa kupambana na ufisadi, alikuwa mkali tu

Hata mi nilishangaa tunaambiwa na meko kuwa wizi umekomeshwa lakini mtaani hali mbaya sana, wakati wa kikwete wizi ulikuwepo escro, epa e.t.c lakini mtaani mambo yalikuwa shwari mtaani , kumbe awamu hii walikomba mpaka za mtaani tukabaki kula magunia.
Richmond, APTL sijui,MKURABITA[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mtu mmoja aliamua aweke mabilioni ndani Kama sehemu ya mavuno yake ya wavuja jasho, Hapo no mzunguko wa pesa mtaani mabilioni yamepotea alafu anazidi kukamua watu kitaa hii ni hatari kwa Taifa
 
Chadema Ninyi hamna jema lolote Nyie mmelifanyia nini taifa hili? Mliapata ridhaa ya kuongoza Majiji mlifanya nini?

Kipindi cha jakaya mliponda hivi hivi tena mkasema Anatakiwa Rais Mkali Adhibiti wizi rushwa na Ufisadi kaja Magufuli Mnageuza tena nakuanza kuponda.

Mwingine Mchungaji msigwa kwenye Msiba kalamba Matapishi Yake zitto kabwe naye kalamba matapishi yake.


Wacheni unafiki wenu. Kila kitu mnajifanya mnajua mkipewa nchi hata robo ya Laliyofanya Magufuli Hamtaweza kufanya. Kama mmeshindwa hata kujenga Ofc za chama mtaweza kuongoza nchi? Nchi sio kijiwe cha kahawa.
Wewee wacha porojo zako. Bandarini zimeibwa au hazijaibwa? Madege yenu hayajalitia taifa hasara?

Wapumbavu wachache ninyi mnaoliibia taifa mkimdanganya Rais na kumsifia. Mmemaliza pesa za umma mnadanganya Watanzania
 
Kwangu mimi magufuli alikuwa siyo fisadi na pia alikuwa hapendi ufisadi. Ila alikuwa na udhaifu ambao wengi waliutumia kujinufaisha. Magufuli alikuwa hapendi mawazo mbadala. Alikuwa anapenda watu wa ''ndiyo baba'' na watu wa kumsifia. Matokeo yake ''wajanja'' walitumia hii loophole kupewa uteuzi ili wapige. Hii ni cha mtoto. Mtu kama Makonda, Kigwangala, na wote waliokuwa wanasifia kama wanamsifu Mungu wamepiga fedha ndefu sana. Kingine alikuwa hatengenezi system bali alikuwa anafanya one man show. Tanzania ni kubwa hangeweza kudhibiti kila mtu yeye peke yake. Na mabaya zaidi aliua upinzani ambao ndiyo ungeweza kusema vitu kama hivi.

Mkuu maana hasa ya ufisadi ni kwenda kinyume cha maadili, taratibu, kanuni, na sheria ili kutimiza maslahi binafsi.

Kwa mfano, kujichotea fedha bila kufuata mipango iliyoidhinishwa na Bunge na kukiuka taratibu za manunuzi ili utekeleze miradi kama kujenga kiwanja cha ndege cha kimataifa kijijini kwako, kununua ndege kwa cash, nk. Halafu kuzuia ukaguzi usifanyike wala habari za utekelezaji zisiyolewe ndio ufisadi wenyewe huo.
 
Kuna mambo ambayo binadamu sisi wasahaulifu sana. Wale walamba miguu waliojua kumpaka mzee mafuta kwa mgongo wa chupa walijawa unafki na hawa ndio waliokua wakimwibia na kumdanganya. Sitaki kulisema hili sana nakazia pia alivyosema Mtani wangu James Ile Millya.

Kama kweli hayati Rais Magufuli aliweza kupambana na ufisadi haya mabilioni ya bandarini hayakuibwa akiwa mzima? Haya mabilioni ambayo inasemekana kuna tatizo BoT si ndio wasimamizi ni wale wale aliowaweka yeye? Waliiba vipi wakati wao ndio waliokua wakiimba kua mzee anapambana na mafisadi na waliompinga pia mafisadi?

Mabilioni yaliyochotwa bandarini na tetesi zilizopo BOT inakosemekana kuna shida huko, huu ni mwanzo tu. Vipi kuhusu pesa zinazotolewa kujenga SGR na STIGLERS kule? Vipi mamlaka ziingine kama TANAPA na TRA hawaibi kweli?

Nilichogundua huenda awamu hii ufisadi ulikua mkubwa kuliko awamu zilizopita na ilikua ngumu watu kujulikana maana walilala kwenye kumsifia mzee ili asiwastukie. TAKUKURU wachape kazi hii nchi bado inapigwa sana na Rais wetu Mama Samia asimame imara.
Hapana. Ni mapema Sana kusema Kuna ufisadi.

Auditor siku zote huwa anaandika tu upotevu pale asipopata documents kwa wakati.

Nenda taratibu kutoa tuhuma ambazo hata wewe mwenyewe unamashaka nazo.

Subiri uchunguzi kwanza.
 
Kuna mambo ambayo binadamu sisi wasahaulifu sana. Wale walamba miguu waliojua kumpaka mzee mafuta kwa mgongo wa chupa walijawa unafki na hawa ndio waliokua wakimwibia na kumdanganya. Sitaki kulisema hili sana nakazia pia alivyosema Mtani wangu James Ile Millya.

Kama kweli hayati Rais Magufuli aliweza kupambana na ufisadi haya mabilioni ya bandarini hayakuibwa akiwa mzima? Haya mabilioni ambayo inasemekana kuna tatizo BoT si ndio wasimamizi ni wale wale aliowaweka yeye? Waliiba vipi wakati wao ndio waliokua wakiimba kua mzee anapambana na mafisadi na waliompinga pia mafisadi?

Mabilioni yaliyochotwa bandarini na tetesi zilizopo BOT inakosemekana kuna shida huko, huu ni mwanzo tu. Vipi kuhusu pesa zinazotolewa kujenga SGR na STIGLERS kule? Vipi mamlaka ziingine kama TANAPA na TRA hawaibi kweli?

Nilichogundua huenda awamu hii ufisadi ulikua mkubwa kuliko awamu zilizopita na ilikua ngumu watu kujulikana maana walilala kwenye kumsifia mzee ili asiwastukie. TAKUKURU wachape kazi hii nchi bado inapigwa sana na Rais wetu Mama Samia asimame imara.

Mbwa Mkali na asiyeng'ata hana Faida.
 
Back
Top Bottom