Hayati Magufuli alifanikiwa kutengeneza kundi lililomuamini na kumtii mithili ya wafia Dini

Hayati Magufuli alifanikiwa kutengeneza kundi lililomuamini na kumtii mithili ya wafia Dini

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
FB_IMG_1652379712226.jpg

Huu ulikuwa uwezo wa kipekee sana Sijapata kuona ! Inafahamika kwamba Viongozi karibu wote wa ccm wanatengeneza Makundi, lakini Mara zote viongozi hao hutengeneza makundi ya kampeni, yaani wanatengeneza wapambe wa kufanya kampeni, kwamba angalau pamoja na kuiba kura, angalau viongozi wa ccm waliopita waliunda hata timu ya kushawishi wananchi ili wawachague.

Dr Magufuli aliunda kikundi cha hiyari cha "kumuabudu" nasema cha hiyari maana sikuwahi kuona watu wakilazimishwa kujiunga nacho, hiki kikundi hakikuwa cha Kampeni, maana Magufuli hakuwahi kuamini katika demokrasia, hili kundi lilikuwa kama zile Praise team za makanisa, ni kulinda imani kufa na kupona, kwamba chochote atakachokifanya hata kama kilikuwa hatari kwa nchi, kama kuvunja kienyeji mikataba na wawekezaji wa kimataifa, jambo ambalo ni hatari lakini kikundi hiki kilishangilia kufa na kupona.

Kilikuwepo hata kikundi cha kutukana Wazee, wastaafu na Wanasiasa wa vyama vyote ikiwemo CCM, hakuna yoyote aliyepingana na Magufuli hata kwenye mambo ya msingi ambaye hakushambuliwa na kikundi hiki, mmemsahau Musiba na yale Magazeti yake yaliyodaiwa kuchapishwa na Usalama wa Taifa?

Inasemekana Magufuli alipenda sana kusifiwa, kwahiyo jamii inatambua wako waliokuwa wanamsifia na kujikuta wakiingizwa kwenye praise team na kuteuliwa.

Sasa mshangao wangu ni huu, Mtu huyu ambaye hakuwa na ushawishi wowote Majukwaani aliwezaje kutengeneza kikundi cha kumuabudu na kumtii mithili ya Machifu wa enzi za Ujima?
 
Kuna mambo yanafurahisha sana kwenye siasa!!

Hivi unaanzaje kumsema Mwamba yule kuwa hakuwa na ushawishi wowote majukwaani!?

Labda nikusaidie tu. Kuelekea uchaguzi wa 2025 tutajua kama Magufuli hakuwa na ushawishi wowote kwa Watanzania kama unavyotaka kutuaminisha hapa. labda ungesema Magufuli hakuwa mwanasiasa mzuri bali alikuwa Rais anayejituma, kufanya kazi kwa bidii na aliipenda nchi yake. Huenda alikuwa na madhaifu yake lakini yule mzee tuacheni unafiki alikuwa anapiga kazi. Na hadi vizazi na vizazi atabaki kwenye historia.

Sasa nyie mnaojiita wana demokrasia shangilieni sasa kwani sasahv hakuna rushwa, maisha ya wananchi yamekuwa mazuri, demokrasia imeleta watalii nchini, kodi na tozo hakuna tena, umeme na maji vinapatikana kwa wingi, deni la taifa limepungua na pia demokrasia imeimarisha uwajibikaji kwa mawaziri na watumishi wa serikali. Sasa hivi ukienda maofisini watu wanachapa kazi.

Ama kweli demokrasia imefungua nchi. Ripoti ya CAG inafanyiwa kazi kwani demokrasia imesababisha wala Rushwa wachukuliwe hatua za haraka. Machinga wanafanya biashara kwa uhuru. Nani kama Wapinzani walioleta maridhiano?

Magufuli kwakweli aende zake in Peace!
 
Nchi ilizizima Kwa furaha alipokufa watu mabaa yalifunguliwa upyaaaaa na yaliyobakiza wanywaji wawili kufumba na kufumbua kukawa na wateja kama wote Arusha mbeya dar acha kabisa Arusha ngombe na mbuzi walichakaa!
 
Hapana bali kulikuwa na kundi la wanafki, wenye kujali maslahi yao binafsi na waliokuwa wanamuogopa. Hata alipokosea wengi walinyamaza bila kusema wakiacha mambo mengine yanaharibika.

Ni rafiki yake mmoja tu walikuwa wameshibana ndio ambaye alikuwa na uwezo wa kumwambia hapa umefanya sivyo hapa umekosea, alikuwa ni rafiki yake Al Haj Mussa Iyombe
 
1. Kwanza unatakiwa utambue Magu hakuwa mwanasiasa ndio maana hakufanya kwa propaganda. He walked the talk.

2. Magu alifanya vitu vilivyoonekana hata na mtoto mdogo. Hata bosi wako Mbowe alipata kusema alikuwa na uthubutu wa ajabu kuliko kawaida. Tafuta hiyo clip.

3. Mara nyingi mtu anayeleta mafanikio hujikuta na watu wanaomuamini na kupenda kufanya nae kazi. Sababu wanaopenda kweli bado wapo wengi tu.

4. Kupenda kusifiwa ni hulka ya mwanadamu. Hata Samia wanaomjua wameamua kumtengenezea verae ya mana anaupiga mwingi nae hudemka kutwa na hiyo verse.

Mbowe pia ukimueleza ukweli atakuambia sumu haijaribiwi kwa kuonja, anataka umsifie tu mwenyekiti tuvushee.
 
Hiyo ndio Kiongozi

Kiongozi asipoyumba hata ajapo kufa atakuwa anaishi

Ndio hao akina Martin Luther
Magufuli alikuwa dikteta. Madikteta wote duniani sifa yao ni kuwa na watu wa kuwatukuza na kuwasifu. Ndiyo maana alifanikiwa. Namfananisha Magufuli na Chavez. Wote walikuwa populist waliodhani wanasaidia nchi zao kumbe wanaziletea majanga makubwa.

Kama Chavez alivyofia madarakani Magufuli naye alifia madarakani. Tofauti ndogo kati ya hawa wawili ni kuwa Chavez alikuwa na mrithi anaeendeleza ujinga wake. Magufuli alikuwa bado hajaanda mrithi wa kueendeleza udikteta wake
 
Back
Top Bottom