#COVID19 Hayati Magufuli alitia sumu masuala ya chanjo, Serikali nywesheni maziwa

#COVID19 Hayati Magufuli alitia sumu masuala ya chanjo, Serikali nywesheni maziwa

Magufuli nikiboko alipata mpaka wafuasi wazungu wakamuunga mkono hachanjwi mtu hapa [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] yule mwamba yule alikuwa nusu mungu yule
 
Alikuwa mshamba sana. Chanjo za surua, pepopunda, ndui n.k tumechanjwa hao wazungu walishindwa kuweka hizo sumu zao?
Madawa karibu yote tunaagiza nje, kwa nini wasiweke hizo sumu? Nguo pia?

vyakula, mfano ngano , mafuta, kumbe inatoka Ukraine, si wangeweka hizo sumu?

Ila ana wafuasi wengi waliomuamini,

Na wewe kwa fikra zako unadhani kichwa chako kipo sawa na hizo chanjo zako za surua?!
 
Hayati Magufuli kwa ushamba wake na kukosa exposure alijikuta anachafua hali ya hewa kuhusu chanjo. Alikuwa na imani duni kuhusu masuala ya chanjo.

Hali hiyo imechangia sana wananchi wamekuwa wakipuuza chanjo kwa imani potofu. Wananchi wengi wanaamini chanjo ni mpango wa kibeberu kuwaangamiza waafrika.

Serikali ya mama ina kazi ya kufanya kuondoa sumu aliyotia Magufuli
Mkemia mpinga chanjo
 
Chanjo zinapunguza uwezekano wa kuugua ugonjwa mkali, kulazwa hospitali au ICU na kufa
Naam, umepita mule mule kwenye mistari ya propaganda za corona.

Ni kama vile huwa mnaimba chorus za hip hop.

Ongezea na hii:

CHANJO ZINAPUNGUZA UWEZEKANO WA KUJAMBA SANA KUNAKOPELEKEA KULAZWA SIPITALI KUTOKANA NA KUPANUKA HAJA KUBWA.

VILE VILE CHANJO ZINAZUIA KIFO, HIVYO UTAISHI MILELE KWA RAHA MUSTAREHE.

 
Ni uchumi upi ambao haukudidimia ?
Usiwe kama huna Qooma bana, Magufuli ametuacha vizuri kuliko huyu delilah aliyekuja kuvuruga utaratibu na kuturudisha miaka 8 nyuma.

Mtu hana vision wala mission alizoachiwa kuziendeleza kakwama anasikiliza matapeli tu. Wamemfanya zuzu bila yeye kuelewa akishinda angani watu wanachota tu hela na kuseti mikataba ya kinyonyaji.

Wanaandaa miswaada ya kutukamua kama swala la tozo wanamfix tu yani hajielewi hovyo kabisa. Nchi haiwezi songa mbele kwa kukomalia kukopa na kuendekeza matanuzi.
 
Hayati Magufuli kwa ushamba wake na kukosa exposure alijikuta anachafua hali ya hewa kuhusu chanjo. Alikuwa na imani duni kuhusu masuala ya chanjo.
Heheheee! Naona mmeanza tena!

Hali hiyo imechangia sana wananchi wamekuwa wakipuuza chanjo kwa imani potofu. Wananchi wengi wanaamini chanjo ni mpango wa kibeberu kuwaangamiza waafrika.
Kwani si wana uhuru wa kuamini watakacho? Unataka serikali iwaamulie mpaka wananchi namna ya kufikiri?
Halafu watu kama wewe mlikuwa mnapiga kelele mpewe uhuru? Ili muwe madikteta kwa wasiokubaliana nanyi?

Serikali ya mama ina kazi ya kufanya kuondoa sumu aliyotia Magufuli
Mzee Magufuli hakumwaga sumu yoyote. Watanzania sio wagonjwa wa akili, na serikali ya Rais Samia ina kazi ya kuwaletea maendeleo wananchi sio kuanza kugombana nao kwa vitu vya kijinga kama hivi.

Yaani watu wanahitaji maji, huduma za kujifungua, na mambo kadha wa kadha muhimu wewe unamchosha rais wa nchi na useless rants?

Gombea basi 2025 upige lockdown nchi nzima na kumarisha JW wachanje kila mtanzania kwa nguvu halafu uridhike dikteta wewe!
 
Jiwe hukumu yake itakuwa ni ya kwanza kwa watenda maovu mbele ya Mungu
kwani wewe ni personal assistant wa mungu wako huyo feki?
Mungu hashauriwi na maamuzi yake hayaathiriwi na mahaba au chuki za wanadamu.
Ana utaratibu wake na kwa utaratibu huo atamhukumu Rais Magufuli, wewe, mimi na kila mwanadamu.
Halafu usijidai sana as if unajua umebakiza muda kiasi gani. Duniani tunapita tu hapa!
 
Hayati Magufuli kwa ushamba wake na kukosa exposure alijikuta anachafua hali ya hewa kuhusu chanjo. Alikuwa na imani duni kuhusu masuala ya chanjo.

Hali hiyo imechangia sana wananchi wamekuwa wakipuuza chanjo kwa imani potofu. Wananchi wengi wanaamini chanjo ni mpango wa kibeberu kuwaangamiza waafrika.

Serikali ya mama ina kazi ya kufanya kuondoa sumu aliyotia Magufuli
Yaani unashindanan na marehemu na bado anakupiga mweleka! Kwa habari ya uongo wa corona na chanjo watanzania hatuwezi kudanganywa na yeyote! Walisema tutaokota miili barabarani haikutokea na haitatokea! Watanzania tuko salama sana mikononi mwa Mungu!
 
Mpaka Sasa countrywise coverage ya Chanjo ya UVIKO -19 haifiki hata 20 percent lakini husikii Tena story za UVIKO. Hata walioitengeneza UVIKO nao wameachana nayo just kama JPM alivyofanya. Tatizo la JPM alikua mbele ya viongozi wengi kifkra juu ya uelekeo sahihi wa kuchukua katika mapambano dhidi ya UVIKO .
 
Hayati Magufuli kwa ushamba wake na kukosa exposure alijikuta anachafua hali ya hewa kuhusu chanjo. Alikuwa na imani duni kuhusu masuala ya chanjo.

Hali hiyo imechangia sana wananchi wamekuwa wakipuuza chanjo kwa imani potofu. Wananchi wengi wanaamini chanjo ni mpango wa kibeberu kuwaangamiza waafrika.

Serikali ya mama ina kazi ya kufanya kuondoa sumu aliyotia Magufuli
Moja ya sifa ya kiongozi kukubalika na watu wake ni kuwaambia jiwe mkate na wakakubali mkate [emoji3][emoji3] ila ukiona kiongozi akisema mkate ni mkate na bado watu wakabaki Wana amini ni jiwe ....aisee uwazie Sana ushawishi wake Kuna big??????
 
Jiwe hukumu yake itakuwa ni ya kwanza kwa watenda maovu mbele ya Mungu
Afadhali yeye hukumu yake "itakuwa" (future tense), yule jamaa anayeshikishwa ukuta kule ubeberuni yeye amekwisha kuhukumiwa tayari. Siku akikata kamba ni kwenda motoni straight forward.
 
Back
Top Bottom