Basi ilikuwa mikopo mizur Sanaa maana waarabu hawa kopeshi pesa Kwa ribaJiwe alikopa nchi za kiarabu mfano Kuwait fund, Morocco, UAE, n.k
Hakupenda kwenda kukopa nchi zinazokazia utawala bora maana alikuwa dikteta
Magufuli hakutaka mikopo ya kudhalikisha utu wetu( hMikopo ya biashara au benki binafsi hata Putin akitaka Kukopa Marekani atapewa maana ina riba kubwa na mda mfupi wa marejesho..
Ila concessional loans hupewi na Wala ile mikopo yenye sura ya msaada kama wa covid hupewi
Mkuu sang'udi, Kama uwezo upo ni sahihi kabisa, na sina tatizo kupata kiongozi mwenye uthubutu wa kiwango hicho na kwa hilo 👏👏👍👍 kwa JPM(RIP)Mkuu,
Siyo kwamba hatuna uwezo wa kupambana na matatizo yetu.
Magufuli ametuonesha kwa vitendo inawezekana kabisa kujenga nchi kwa kodi zetu wenyewe, na mikopo michache sana.
Ukumbuke pia hilo deni la karibu Trillion 30 linahusisha na madeni yaliyoiva ya nyuma ambayo amepambana sana kuyalipa.
Ametufundisha inawezekana kabisa kuendesha nchi vizuri bila misaada ya mabeberu na tukapata maendeleo.
Sote tu mashahidi wa hili, na namba hazidanganyi. Si dhambi kufanya kwa kasi kubwa kama uwezo upo.
"Mabeberu" watu wanao kimbilia ili neno wana nia moja tu, kulinda legacy. Kote ume ongea point ila umeharibu vyote kwa hapoMkuu,
Siyo kwamba hatuna uwezo wa kupambana na matatizo yetu.
Magufuli ametuonesha kwa vitendo inawezekana kabisa kujenga nchi kwa kodi zetu wenyewe, na mikopo michache sana.
Ukumbuke pia hilo deni la karibu Trillion 30 linahusisha na madeni yaliyoiva ya nyuma ambayo amepambana sana kuyalipa.
Ametufundisha inawezekana kabisa kuendesha nchi vizuri bila misaada ya mabeberu na tukapata maendeleo.
Sote tu mashahidi wa hili, na namba hazidanganyi. Si dhambi kufanya kwa kasi kubwa kama uwezo upo.
Bank gani ambayo Inakopesha bila ribaMagufuli alikuwa anakopa zaidi pesa kutoka benki za kibiashara ambapo riba huwa kubwa na huko hawana tatizo na mkopaji, maana ni suala la kibiashara na sio kisiasa.
Kawaulize alikokopa, mtu ametia hasara halafu mnambeba na bachelor zenu, bure kabisa!Hebu tueleze hizo riba ni asilimia ngapi
Sasa si ndio wanakukopesha vizuri, tena kibiashara, ukiwakorofisha haupati mikopo ya bila riba, wapate kukumiliki vizuri.Leo 10:15pm 07/05/2022
Kabla ya Rais Magufuli kuingia madarakani Mwaka 2015,Tanzania ilikuwa katika uchumi wa chini,ukiwa katika uchumi wa chini kabisa,sera ya taifa na lengo linapaswa kuwa kuelekea uchumi wa kati wa ngazi ya chini,hii ni hatua moja kutoka katika uchumi wa chini,adhma na ndoto ya Rais John Pombe Magufuli ilikuwa kuipeleka Tanzania uchumi wa kati,Benki ya Dunia hutazama pato la taifa kwa mfano kupitia jumla ya utajiri wa rasilimali zetu zote,Ujenzi wa miundo mbinu itayokuja kuiingizia Taifa fedha za kigeni kutokana na shughuli mbalimbali zitakazotokana na miundo mbinu hiyo na utajiri wa kifedha kugawanya na idadi ya watu wa Tanzania,
Kwa calculation zake Rais Magufuli iliwezekana,ndoto ya Rais Magufuli ilikuwa ni kuingia Uchumi wa kati,sasa ataingia vipi,Mambo mawili akataka kuyatimiza ambayo ndio yatakuwa kichocheo cha kuiingiza Tanzania katika uchumi wa kati,Mambo hayo ni Umeme wa Uhakika kutoka Bwawa la Julius Nyerere,Rufiji na Uchumi wa Viwanda,hivi viwili kwa calculation zake vingeweza kutufikisha kwenye kundi la Nchi zenye Uchumi wa Kipato cha Kati (MIC),kwa hakika aliwaza vyema na alitimiza ndoto hiyo,ili kufanikisha hilo Rais Magufuli alihimiza mambo yafuatayo,
•Ujenzi wa Viwanda nchini Tanzania,viwanda vinahitaji malighafi (kilimo, mifugo, uvuvi, madini, nk);.
• Ujenzi wa bwawa la Umeme la Rufiji litalozalisha megawatts 2,115 ikiwa sasa hivi tunatumia megawatts 1,500 Ili Sekta hizo zizalishe malighafi za kutosheleza mahitaji ya matumizi ya ndani tunahitaji Umeme wa uhakika kutoka Bwawa la Julius Nyerere kule Rufiji,viwanda, na mauzo ya nje ya nchi, lazima kuwepo miundo mbinu bora na imara (usafiri ardhini, majini na angani, maji, nishati).
• Kumudu uendeshaji na ukarabati (Operations & Maintenance) wa miundo mbinu hiyo, kunahitaji rasilimaliwatu wenye uwezo na ujuzi;
• Kupata rasilimaliwatu wa aina hiyo kunahitajika Uzalendo kwa Taifa la Tanzania,huduma bora za jamii (elimu na afya),hii kwa ujumla ilimfanya Rais Magufuli kuanza kuijenga upya Tanzania,laiti Mungu angempa maisha marefu basi watoto na wajukuu wetu wangefaidi matunda ya utekelezwaji wa ndoto za Rais Magufuli.
-Ndoto ya Rais Magufuli kuipeleka Tanzania uchumi wa kati iliwachukiza wazungu na vibaraka wao.
Nimeona nukuu kutoka kwa Wassira ikisema "Magufuli alisema hatuhitaji mikopo tunajenga kwa kutumia fedha zetu, Tanzania ni tajiri lakini yeye ndiye aliyekopa sana kuliko Marais wote,alikopa mikopo yenye riba kubwa kwa kificho kutekeleza ujenzi,deni la Taifa limepanda sana ndani ya miaka 6 ya Uongozi wake" sasa niulize swali, Serikali ya CCM ya Awamu ya tano,iliyoongozwa na Rais Magufuli,ambayo haikuwa na mahusiano mazuri na nchi zote za Ulaya iliwezaje kukopa kwa Serikali za Ulaya ambazo haina mahusiano nazo mazuri!?
-Vibaraka walivyokwenda Ulaya kuzuia mikopo isije Tanzania,kimbilio la Rais Magufuli likawa Benki ya Maendeleo ya Afrika,AFDB.
Benki ya Afrika ndio ilikuwa kimbilio la Rais Magufuli,na hata mtendaji wake Mkuu alifika Chato,kuhani msiba wa rafiki yake,AfDB wamekuwa wakitoa fedha kwenye sekta za maji, nishati na nyinginezo nchini Tanzania na wameridhishwa na utekelezaji wa mradi wa maji wa Jiji la Arusha mara baada ya kutembelea Matenki ya Maji ya Themi Hills, Ofisi ya Kanda ya AUWSA-Moshono, Kituo cha kusukuma Maji Namba 4 na Tenki la Maji la Seedfarm lenye ujazo wa lita milioni 10 mkoani Arusha,sasa wanaojua madeni ya awamu ya tano watuambie alikopa kiasi gani hapo Benki ya Afrika? na hicho alichokikopa ndio hicho wanachotuambia kikubwa!?
Vyama vya upinzani nchini Tanzania na wanaharakati wa haki za binadamu hapa nchini Tanzania na wa kimataifa walikuwa wakiweka shinikizo la kutotolewa mikopo kwa Tanzania hadi pale Tanzania itakaporuhusu wanafunzi wanaopata ujauzito waruhusiwe kuendelea na mfumo rasmi wa elimu,kiongozi wa chama upinzani cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe aliwahi kusema kuwa Benki ya Dunia haitakiwi kuikopesha Tanzania dola milioni 500 za elimu kabla ya mabadiliko ya kisera kufanyika.Kwa mujibu wa nyaraka za Benki ya Dunia, pamoja na mambo mengine, mkopo huu ulikusudiwa kwenda kusaidia upatikanaji wa elimu bora na kwa urahisi kwa wanafunzi waliokuwa wanarudi shule baada ya kuwa wamepata ujauzito. Lakini mradi huu wa elimu ulikuwa ni kupitia elimu mbadala na si katika mfumo rasmi.
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt Akinumwi Adesina,alifika mara kwa mara nchini Tanzania na alimpongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kazi kubwa aliyokuwaanaifanya kuimarisha uchumi wa Tanzania na alijadiliana mambo kadhaa na Rais Magufuli yakiwemo namna benki hiyo ilivyosaidia juhudi za maendeleo za Tanzania tangu mwaka 1971 na inavyoendelea kusaidia katika ufadhili wa miradi mbalimbali ya maendeleo,nikimnukuu katika moja ya mahojiano yake alisema
"Yote kwa yote nimemhakikishia Rais Magufuli kuwa AfDB itamuunga mkono katika mipango yake na maono yake ili tuweze kuisaidia Tanzania kukua zaidi, nimefurahi kuzungumza na Mhe. Rais na naona Tanzania ipo katika njia sahihi," alisema Dkt Adesina kwa mujibu wa taarifa hiyo ya ikulu wakati wa Awamu ya tano,AfDB ilifadhili miradi ya maendeleo yenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 3.457 (sawa na Shilingi Trilioni 7.78 Tanzania) zikiwemo fedha za miradi 25 zilizotolewa kuanzia mwezi Novemba, 2017 yenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 1.986 (Shilingi Trilioni 4.47 Kitanzania).
Nimalizie kwa kuishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB) kwa kutoa mikopo kwa Serikali ya Tanzania kusaidia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati iliyobuni ajira kwa Watanzania wengi na iliyotarajiwa kubuni ajira nyingi kwa Watanzania mara tu Bwawa la Julius Nyerere,Rufiji litakapoisha,ilitarajiwa tani zaidi ya laki tano za mpunga na mazao mengine kuzalishwa pembeni ya Bwawa la Umeme la Julius Nyerere pale Rufiji na tungeweza kuuza mchele (export) nje ya nchi na kuliingizia Taifa fedha za kigeni na hivyo kukuza thamani ya shilingi ya Tanzania,hivi ni kati ya vitu ambavyo viliivutia Benki ya dunia kuitangaza Tanzania kama taifa lenye kipato cha kati mnamo mwezi Julai 2020.
Mbali na uongozi thabiti wa rais Magufuli katika kudhibiti matumizi ya fedha na kukabiliana na ufujaji wake,taifa la Tanzania lilitarajiwa kuimarika kiviwanda hali ya kwamba lina karibia viwanda 60 tangu lilipojipatia Uhuru, huku uongozi wa rais Magufuli ukifanikiwa kuanzisha zaidi ya viwanda elfu nane katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake,hivi sasa nchini Tanzania tunaunganisha matinga humu nchini,tunaunganisha mabasi na kuzalisha nondo ,mabati na kadhalika,kufikia tar 01/07/2020 siku ya Jumatano,Benki ya Dunia,iliiorodhesha Tanzania katika orodha ya nchi za uchumi wa kipato cha kati,kabla ya lengo ya dira ya Taifa kuiingiza Tanzania katika uchumi wa kati mwaka 2025.
Nikiishia hapa, Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854
-Bachelor of Business Administration in International Business.
-Master of Leadership and Management.
Recent Publication;-
-Assessment on the Effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
Ninakupata sana mkuu.Mkuu sang'udi, Kama uwezo upo ni sahihi kabisa, na sina tatizo kupata kiongozi mwenye uthubutu wa kiwango hicho na kwa hilo 👏👏👍👍 kwa JPM(RIP)
Nitaandika kwa urefu ila tafadhali kama hutojali soma ili uelewe hoja yangu.
Pamoja na hayo aliyofanya, biashara hazikupaswa zifungwe, account za wafanyabiashara hazikupaswa zifungwe, mishahara kwa kiasi fulani ilipaswa iongezwe, huduma za uuzaji mazao hazikupaswa kuondolewa kwa wafanya biashara na kufanya ni state business na mengine mengi.
Nasema hivi kwasababu hivi ndivyo vitu vinavyomwezesha raia wa kawaida kufanya maendeleo binafsi na kurithisha vizazi vya mbele wakati yeye akiendelea kupokea pension ya uraisi na kushuhudia vizazi vyake vikifurahia urithi alioacha na akiendelea kupokea sifa za treni na ndege alizoacha.
NITAKUPA MFANO HAI WA MAMBO YALIYOTOKEA CHINI YA SERIKALI YA JPM:
Wote tunajua sheria zetu wakati mwingine huwa zinakuwa na mapungufu ya kuzitekeleza, mfano sheria za kuwataka wenye kampuni za consultancy wajisajili na VAT na waandae mahesabu bila kujali uwezo wa mtaji.
Kama mtu ana kakampuni kake ka sheria, kameajiri watu 5, sheria inamtaka aandae mahesabu kila mwaka na ajiunge VAT. Gharama ya kuandaa mahesabu si chini ya Tsh 500,000 mpaka 1,000,000 nje ya gharama za uhasibu, gharama ya kufile VAT si chini ya 50,000 mpaka 100,000 kila mwezi.
Sasa huyu mwenye kakampuni hakuwa akifile hesabu za mwisho kwa kutokujua au kwa kupuuza kwa sababu ya gharama za ukaguzi na uhasibu, na akawa anaenda kufanya makadirio kila mwaka kisha analipa kodi anaendelea na biashara kama presumptive tax payers wanavyofanya ilihali yeye ni corporate.
Sasa serikali kwa sababu ina marejesho ya mkopo wa reli ikatumia sheria ya kutokupeleka hesabu TRA ya adhabu ya Tsh 225,000 kila mwezi, na ikatumia sheria ya kutoa assessment kukadiria kodi ambayo huenda ingepatikana kwa kufanya examination of books of accounts.
Ikachukua % ya turnover ya miaka 5 ikaiita profit ikacharge penalty na interest kila mwezi ikapata makisio ya kodi ikajumlisha na zile 225,000 kila mwezi za miaka 5 na kumtaka mfanya biashara alipe plus interest each month for 5 years na kuzuia akaunti yake ya biashara huenda yenye pesa za wateja ikimlazimisha kodi ilipwe, mfanyabiashara akashindwa, biashara ikafungwa. Ukumbuke kwa huo mfumo uliotumika inaweza kuja hata kodi ya M40-M50, pesa ambayo mfanya biashara huyo hajawahi kuota kuishika kwa pamoja.
Kisheria raisi alikuwa sahihi na atakuwa alipata rejesho, ila katika uhalisia aliwanyima raia wake haki ya kufanya maendeleo binafsi kwa kuchukua mishahara yao huenda ya miaka 10 mbele ambayo wangelipwa kama angetumia busara na hako kakampuni kakaendelea kuwepo.
Sawa atapeleka rejesho ila, wale watu 5 ambao mshahara wao ameuchukua? Watoto wao mbeleni itakuwa vipi watakapokuta baba zao walilipia treni ila hawana pa kulala?
Sasa ukute baba anahako kakampuni na mama ni mwajiriwa kwenye kahoteli kalikokuwa kanategemea vikao vya wafanyakazi wa serikali vilivyopigwa marafuku kufanyika kwenye mahoteli hako kahoteli kakafungwa huku mzee wao akiwa anacheti cha darasa la saba akaondolewa kazini akiwa na miaka 57.
Safari ya Canada ivi nilini mama yetuHoja nzito sana!
Magufuli hajawahi kwenda kubembea Dubai ila huyu mmh!
Hapa tulipofikia inatosha kukubaliana na kushikana mikono. 🤝Ninakupata sana mkuu.
Biashara hazijaanza kufungwa wakati wa JPM pekee, hata sasa kuna biashara nyingi tu zinafungwa kwa sababu mbalimbali ikiwemo makadirio yasiyokuwa ya busara kwa walipa kodi.
Ninafikiri tatizo halikuwa kwa Magufuli zaidi ila watendaji wake, japo anawajibika kama mkuu wa taasisi. Hata hivyo ni wakati huu tulishuhudia TRA ikifanya kazi iliyotukuka na yenye manufaa kwa taifa arguably kuliko wakati wowote ule.
Ninakubali, kunapokuwa na overhaul ya taasisi ya ukubwa huo kuna baadhi ya watu wanakuwa vulnerable kuathirika kwa irregularities zinazojitokeza.
Ninafikiri hizi zinabaki kama changamoto ambazo pengine hakuzi-address ipasavyo hasa kwa kuwa na ile attitude ya wafanyabiashara hukwepa kodi.
Kuhusu vyeti vya kughushi ninaamini alifanya kazi nzuri sana. Hatuwezi kuwa taifa lenye "watalaamu" wasiokidhi vigezo. Hawa walikuwa moja ya sababu za kuwa na malfunctioning institutions nyingi ambazo hazikuwa na afya kwa taifa letu.
Ninafikiri hizi ni gaps ambazo wenzake wanapaswa kuzi-address.
Ulitaka maanisha our?RiP ower John Pombe Magufuli
Nenda kaulize Benki Kuu ya TanzaniaKatika hizo ulizotaja ni ipi samia hajakopa mpakasasa?
Hivi unajuwa kuwa USA walitaka kununua mafuta Venezuela mwezi Machi kwa Nicholas Maduro?Unamaanisha mrusi anaweza kumkopa mmarekani katika Hali ya sasa? Au Ukraine akamkopa urusi?
HISTORIA KIDOGO:Siasa ina play role hata kwenye biashara.
Mfano nchi kama korea kaskazini , Iran au Russia zote zina matatizo kiuchumi kutokana na aina ya siasa wanazofanya.
Ni benki chache sana duniani zitafanya biashara na let say North Korea au Iran.
Sasa kama kweli Magufuli alikua hapatani na West kwa kiasi hicho wasingempa fedha.
Naomba uniwie radhi kukuita goigoi wa kifikira... tumekuwa nchi huru more than 50 years lakini hatukuwahi kuja na mradi wenye kutoa suluhisho la kudumu la shida ya umeme.Hapana.
Bank za biashara zinalenga faida, si siasa.
Kuhusu alichokuwa anafanya na hiyo mikopo anastahili pongezi kwa sababu miradi ya maendeleo ipo na tunaiona, LAKINI kwa gharama gani?
Wote tunajenga nchi moja, tunastahili heshima na kuwekwa wazi juu ya nini tunagharamikia ili tupate maendeleo.
Hakukuwa na ulazima tumalize ujenzi wa Tanzania katika awamu ya 5, tunafanya pale tunapoweza kwa uaminifu na tunatoa nafasi kwa wengine kufanya sehemu yao.
Sasa tunajenga reli ya kisasa kwa gharama ya kuchukua pesa ya mfanyabiashara kutoka akaunti yake ya bank ili ulipe mkopo wa biashara wa kujenga reli wenye riba kubwa? Mfanya biashara mwenyewe unakuta pesa na yeye alikopa, au ni za wateja wanasubiri huduma. Haikuwa sahihi.