Hayati Magufuli aliwezaje kukopa kwa Wazungu ikiwa aliharibu uhusiano na nchi za Ulaya?

Hayati Magufuli aliwezaje kukopa kwa Wazungu ikiwa aliharibu uhusiano na nchi za Ulaya?

mikopo ya kibiashara SWISS CREDIT walishawahi chukua mkopo wa usd milion 500 ndani ya muda mfupi walipe usd milllions 900
 
Mikopo ya biashara au benki binafsi hata Putin akitaka Kukopa Marekani atapewa maana ina riba kubwa na mda mfupi wa marejesho..

Ila concessional loans hupewi na Wala ile mikopo yenye sura ya msaada kama wa covid hupewi
Magufuli hakutaka mikopo ya kudhalikisha utu wetu( h
Kuwatambua mashoga nk,) full stop
 
Huo muda ulitumia kuandaa huu utopolo ungetumia kutafiti kidogo tu ungeona

1652011976176.png
 
  • Thanks
Reactions: Qwy
Mkuu,
Siyo kwamba hatuna uwezo wa kupambana na matatizo yetu.

Magufuli ametuonesha kwa vitendo inawezekana kabisa kujenga nchi kwa kodi zetu wenyewe, na mikopo michache sana.

Ukumbuke pia hilo deni la karibu Trillion 30 linahusisha na madeni yaliyoiva ya nyuma ambayo amepambana sana kuyalipa.

Ametufundisha inawezekana kabisa kuendesha nchi vizuri bila misaada ya mabeberu na tukapata maendeleo.

Sote tu mashahidi wa hili, na namba hazidanganyi. Si dhambi kufanya kwa kasi kubwa kama uwezo upo.
Mkuu sang'udi, Kama uwezo upo ni sahihi kabisa, na sina tatizo kupata kiongozi mwenye uthubutu wa kiwango hicho na kwa hilo 👏👏👍👍 kwa JPM(RIP)

Nitaandika kwa urefu ila tafadhali kama hutojali soma ili uelewe hoja yangu.

Pamoja na hayo aliyofanya, biashara hazikupaswa zifungwe, account za wafanyabiashara hazikupaswa zifungwe, mishahara kwa kiasi fulani ilipaswa iongezwe, huduma za uuzaji mazao hazikupaswa kuondolewa kwa wafanya biashara na kufanya ni state business na mengine mengi.

Nasema hivi kwasababu hivi ndivyo vitu vinavyomwezesha raia wa kawaida kufanya maendeleo binafsi na kurithisha vizazi vya mbele wakati yeye akiendelea kupokea pension ya uraisi na kushuhudia vizazi vyake vikifurahia urithi alioacha na akiendelea kupokea sifa za treni na ndege alizoacha.

NITAKUPA MFANO HAI WA MAMBO YALIYOTOKEA CHINI YA SERIKALI YA JPM:

Wote tunajua sheria zetu wakati mwingine huwa zinakuwa na mapungufu ya kuzitekeleza, mfano sheria za kuwataka wenye kampuni za consultancy wajisajili na VAT na waandae mahesabu bila kujali uwezo wa mtaji.

Kama mtu ana kakampuni kake ka sheria, kameajiri watu 5, sheria inamtaka aandae mahesabu kila mwaka na ajiunge VAT. Gharama ya kuandaa mahesabu si chini ya Tsh 500,000 mpaka 1,000,000 nje ya gharama za uhasibu, gharama ya kufile VAT si chini ya 50,000 mpaka 100,000 kila mwezi.

Sasa huyu mwenye kakampuni hakuwa akifile hesabu za mwisho kwa kutokujua au kwa kupuuza kwa sababu ya gharama za ukaguzi na uhasibu, na akawa anaenda kufanya makadirio kila mwaka kisha analipa kodi anaendelea na biashara kama presumptive tax payers wanavyofanya ilihali yeye ni corporate.

Sasa serikali kwa sababu ina marejesho ya mkopo wa reli ikatumia sheria ya kutokupeleka hesabu TRA ya adhabu ya Tsh 225,000 kila mwezi, na ikatumia sheria ya kutoa assessment kukadiria kodi ambayo huenda ingepatikana kwa kufanya examination of books of accounts.

Ikachukua % ya turnover ya miaka 5 ikaiita profit ikacharge penalty na interest kila mwezi ikapata makisio ya kodi ikajumlisha na zile 225,000 kila mwezi za miaka 5 na kumtaka mfanya biashara alipe plus interest each month for 5 years na kuzuia akaunti yake ya biashara huenda yenye pesa za wateja ikimlazimisha kodi ilipwe, mfanyabiashara akashindwa, biashara ikafungwa. Ukumbuke kwa huo mfumo uliotumika inaweza kuja hata kodi ya M40-M50, pesa ambayo mfanya biashara huyo hajawahi kuota kuishika kwa pamoja.

Kisheria raisi alikuwa sahihi na atakuwa alipata rejesho, ila katika uhalisia aliwanyima raia wake haki ya kufanya maendeleo binafsi kwa kuchukua mishahara yao huenda ya miaka 10 mbele ambayo wangelipwa kama angetumia busara na hako kakampuni kakaendelea kuwepo.

Sawa atapeleka rejesho ila, wale watu 5 ambao mshahara wao ameuchukua? Watoto wao mbeleni itakuwa vipi watakapokuta baba zao walilipia treni ila hawana pa kulala?

Sasa ukute baba anahako kakampuni na mama ni mwajiriwa kwenye kahoteli kalikokuwa kanategemea vikao vya wafanyakazi wa serikali vilivyopigwa marafuku kufanyika kwenye mahoteli hako kahoteli kakafungwa huku mzee wao akiwa anacheti cha darasa la saba akaondolewa kazini akiwa na miaka 57.
 
Mkuu,
Siyo kwamba hatuna uwezo wa kupambana na matatizo yetu.

Magufuli ametuonesha kwa vitendo inawezekana kabisa kujenga nchi kwa kodi zetu wenyewe, na mikopo michache sana.

Ukumbuke pia hilo deni la karibu Trillion 30 linahusisha na madeni yaliyoiva ya nyuma ambayo amepambana sana kuyalipa.

Ametufundisha inawezekana kabisa kuendesha nchi vizuri bila misaada ya mabeberu na tukapata maendeleo.

Sote tu mashahidi wa hili, na namba hazidanganyi. Si dhambi kufanya kwa kasi kubwa kama uwezo upo.
"Mabeberu" watu wanao kimbilia ili neno wana nia moja tu, kulinda legacy. Kote ume ongea point ila umeharibu vyote kwa hapo
 
Magufuli alikuwa anakopa zaidi pesa kutoka benki za kibiashara ambapo riba huwa kubwa na huko hawana tatizo na mkopaji, maana ni suala la kibiashara na sio kisiasa.
Bank gani ambayo Inakopesha bila riba
 
Leo 10:15pm 07/05/2022

Kabla ya Rais Magufuli kuingia madarakani Mwaka 2015,Tanzania ilikuwa katika uchumi wa chini,ukiwa katika uchumi wa chini kabisa,sera ya taifa na lengo linapaswa kuwa kuelekea uchumi wa kati wa ngazi ya chini,hii ni hatua moja kutoka katika uchumi wa chini,adhma na ndoto ya Rais John Pombe Magufuli ilikuwa kuipeleka Tanzania uchumi wa kati,Benki ya Dunia hutazama pato la taifa kwa mfano kupitia jumla ya utajiri wa rasilimali zetu zote,Ujenzi wa miundo mbinu itayokuja kuiingizia Taifa fedha za kigeni kutokana na shughuli mbalimbali zitakazotokana na miundo mbinu hiyo na utajiri wa kifedha kugawanya na idadi ya watu wa Tanzania,

Kwa calculation zake Rais Magufuli iliwezekana,ndoto ya Rais Magufuli ilikuwa ni kuingia Uchumi wa kati,sasa ataingia vipi,Mambo mawili akataka kuyatimiza ambayo ndio yatakuwa kichocheo cha kuiingiza Tanzania katika uchumi wa kati,Mambo hayo ni Umeme wa Uhakika kutoka Bwawa la Julius Nyerere,Rufiji na Uchumi wa Viwanda,hivi viwili kwa calculation zake vingeweza kutufikisha kwenye kundi la Nchi zenye Uchumi wa Kipato cha Kati (MIC),kwa hakika aliwaza vyema na alitimiza ndoto hiyo,ili kufanikisha hilo Rais Magufuli alihimiza mambo yafuatayo,

•Ujenzi wa Viwanda nchini Tanzania,viwanda vinahitaji malighafi (kilimo, mifugo, uvuvi, madini, nk);.
• Ujenzi wa bwawa la Umeme la Rufiji litalozalisha megawatts 2,115 ikiwa sasa hivi tunatumia megawatts 1,500 Ili Sekta hizo zizalishe malighafi za kutosheleza mahitaji ya matumizi ya ndani tunahitaji Umeme wa uhakika kutoka Bwawa la Julius Nyerere kule Rufiji,viwanda, na mauzo ya nje ya nchi, lazima kuwepo miundo mbinu bora na imara (usafiri ardhini, majini na angani, maji, nishati).
• Kumudu uendeshaji na ukarabati (Operations & Maintenance) wa miundo mbinu hiyo, kunahitaji rasilimaliwatu wenye uwezo na ujuzi;
• Kupata rasilimaliwatu wa aina hiyo kunahitajika Uzalendo kwa Taifa la Tanzania,huduma bora za jamii (elimu na afya),hii kwa ujumla ilimfanya Rais Magufuli kuanza kuijenga upya Tanzania,laiti Mungu angempa maisha marefu basi watoto na wajukuu wetu wangefaidi matunda ya utekelezwaji wa ndoto za Rais Magufuli.

-Ndoto ya Rais Magufuli kuipeleka Tanzania uchumi wa kati iliwachukiza wazungu na vibaraka wao.

Nimeona nukuu kutoka kwa Wassira ikisema "Magufuli alisema hatuhitaji mikopo tunajenga kwa kutumia fedha zetu, Tanzania ni tajiri lakini yeye ndiye aliyekopa sana kuliko Marais wote,alikopa mikopo yenye riba kubwa kwa kificho kutekeleza ujenzi,deni la Taifa limepanda sana ndani ya miaka 6 ya Uongozi wake" sasa niulize swali, Serikali ya CCM ya Awamu ya tano,iliyoongozwa na Rais Magufuli,ambayo haikuwa na mahusiano mazuri na nchi zote za Ulaya iliwezaje kukopa kwa Serikali za Ulaya ambazo haina mahusiano nazo mazuri!?

-Vibaraka walivyokwenda Ulaya kuzuia mikopo isije Tanzania,kimbilio la Rais Magufuli likawa Benki ya Maendeleo ya Afrika,AFDB.

Benki ya Afrika ndio ilikuwa kimbilio la Rais Magufuli,na hata mtendaji wake Mkuu alifika Chato,kuhani msiba wa rafiki yake,AfDB wamekuwa wakitoa fedha kwenye sekta za maji, nishati na nyinginezo nchini Tanzania na wameridhishwa na utekelezaji wa mradi wa maji wa Jiji la Arusha mara baada ya kutembelea Matenki ya Maji ya Themi Hills, Ofisi ya Kanda ya AUWSA-Moshono, Kituo cha kusukuma Maji Namba 4 na Tenki la Maji la Seedfarm lenye ujazo wa lita milioni 10 mkoani Arusha,sasa wanaojua madeni ya awamu ya tano watuambie alikopa kiasi gani hapo Benki ya Afrika? na hicho alichokikopa ndio hicho wanachotuambia kikubwa!?

Vyama vya upinzani nchini Tanzania na wanaharakati wa haki za binadamu hapa nchini Tanzania na wa kimataifa walikuwa wakiweka shinikizo la kutotolewa mikopo kwa Tanzania hadi pale Tanzania itakaporuhusu wanafunzi wanaopata ujauzito waruhusiwe kuendelea na mfumo rasmi wa elimu,kiongozi wa chama upinzani cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe aliwahi kusema kuwa Benki ya Dunia haitakiwi kuikopesha Tanzania dola milioni 500 za elimu kabla ya mabadiliko ya kisera kufanyika.Kwa mujibu wa nyaraka za Benki ya Dunia, pamoja na mambo mengine, mkopo huu ulikusudiwa kwenda kusaidia upatikanaji wa elimu bora na kwa urahisi kwa wanafunzi waliokuwa wanarudi shule baada ya kuwa wamepata ujauzito. Lakini mradi huu wa elimu ulikuwa ni kupitia elimu mbadala na si katika mfumo rasmi.

Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt Akinumwi Adesina,alifika mara kwa mara nchini Tanzania na alimpongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kazi kubwa aliyokuwaanaifanya kuimarisha uchumi wa Tanzania na alijadiliana mambo kadhaa na Rais Magufuli yakiwemo namna benki hiyo ilivyosaidia juhudi za maendeleo za Tanzania tangu mwaka 1971 na inavyoendelea kusaidia katika ufadhili wa miradi mbalimbali ya maendeleo,nikimnukuu katika moja ya mahojiano yake alisema
"Yote kwa yote nimemhakikishia Rais Magufuli kuwa AfDB itamuunga mkono katika mipango yake na maono yake ili tuweze kuisaidia Tanzania kukua zaidi, nimefurahi kuzungumza na Mhe. Rais na naona Tanzania ipo katika njia sahihi," alisema Dkt Adesina kwa mujibu wa taarifa hiyo ya ikulu wakati wa Awamu ya tano,AfDB ilifadhili miradi ya maendeleo yenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 3.457 (sawa na Shilingi Trilioni 7.78 Tanzania) zikiwemo fedha za miradi 25 zilizotolewa kuanzia mwezi Novemba, 2017 yenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 1.986 (Shilingi Trilioni 4.47 Kitanzania).

Nimalizie kwa kuishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB) kwa kutoa mikopo kwa Serikali ya Tanzania kusaidia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati iliyobuni ajira kwa Watanzania wengi na iliyotarajiwa kubuni ajira nyingi kwa Watanzania mara tu Bwawa la Julius Nyerere,Rufiji litakapoisha,ilitarajiwa tani zaidi ya laki tano za mpunga na mazao mengine kuzalishwa pembeni ya Bwawa la Umeme la Julius Nyerere pale Rufiji na tungeweza kuuza mchele (export) nje ya nchi na kuliingizia Taifa fedha za kigeni na hivyo kukuza thamani ya shilingi ya Tanzania,hivi ni kati ya vitu ambavyo viliivutia Benki ya dunia kuitangaza Tanzania kama taifa lenye kipato cha kati mnamo mwezi Julai 2020.

Mbali na uongozi thabiti wa rais Magufuli katika kudhibiti matumizi ya fedha na kukabiliana na ufujaji wake,taifa la Tanzania lilitarajiwa kuimarika kiviwanda hali ya kwamba lina karibia viwanda 60 tangu lilipojipatia Uhuru, huku uongozi wa rais Magufuli ukifanikiwa kuanzisha zaidi ya viwanda elfu nane katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake,hivi sasa nchini Tanzania tunaunganisha matinga humu nchini,tunaunganisha mabasi na kuzalisha nondo ,mabati na kadhalika,kufikia tar 01/07/2020 siku ya Jumatano,Benki ya Dunia,iliiorodhesha Tanzania katika orodha ya nchi za uchumi wa kipato cha kati,kabla ya lengo ya dira ya Taifa kuiingiza Tanzania katika uchumi wa kati mwaka 2025.

Nikiishia hapa, Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854

-Bachelor of Business Administration in International Business.

-Master of Leadership and Management.

Recent Publication;-
-Assessment on the Effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
Sasa si ndio wanakukopesha vizuri, tena kibiashara, ukiwakorofisha haupati mikopo ya bila riba, wapate kukumiliki vizuri.

Hujaona Magufuli alibana kwenye dhahabu mwishowe mwenyewe akaachia. Unafikiri kwanini?

H
 
Magufuli tutamkumbuka
Bwawa la umeme
Rel tren ya mwendokasi
Ikulu dodoma
Stand kuu kila mkoa
Masoko kila mkoa
Hospital kubwa kila mkoa
Fryover ubungo na tazara
Fryover zingine 4 zinajengwa
Idara za maji ziko vizuri

Naasingeuliwa vyote hivyo vingesha kamilika na angetuletea manufaa mengine

R.I.P JPM
 
Mkuu sang'udi, Kama uwezo upo ni sahihi kabisa, na sina tatizo kupata kiongozi mwenye uthubutu wa kiwango hicho na kwa hilo 👏👏👍👍 kwa JPM(RIP)

Nitaandika kwa urefu ila tafadhali kama hutojali soma ili uelewe hoja yangu.

Pamoja na hayo aliyofanya, biashara hazikupaswa zifungwe, account za wafanyabiashara hazikupaswa zifungwe, mishahara kwa kiasi fulani ilipaswa iongezwe, huduma za uuzaji mazao hazikupaswa kuondolewa kwa wafanya biashara na kufanya ni state business na mengine mengi.

Nasema hivi kwasababu hivi ndivyo vitu vinavyomwezesha raia wa kawaida kufanya maendeleo binafsi na kurithisha vizazi vya mbele wakati yeye akiendelea kupokea pension ya uraisi na kushuhudia vizazi vyake vikifurahia urithi alioacha na akiendelea kupokea sifa za treni na ndege alizoacha.

NITAKUPA MFANO HAI WA MAMBO YALIYOTOKEA CHINI YA SERIKALI YA JPM:

Wote tunajua sheria zetu wakati mwingine huwa zinakuwa na mapungufu ya kuzitekeleza, mfano sheria za kuwataka wenye kampuni za consultancy wajisajili na VAT na waandae mahesabu bila kujali uwezo wa mtaji.

Kama mtu ana kakampuni kake ka sheria, kameajiri watu 5, sheria inamtaka aandae mahesabu kila mwaka na ajiunge VAT. Gharama ya kuandaa mahesabu si chini ya Tsh 500,000 mpaka 1,000,000 nje ya gharama za uhasibu, gharama ya kufile VAT si chini ya 50,000 mpaka 100,000 kila mwezi.

Sasa huyu mwenye kakampuni hakuwa akifile hesabu za mwisho kwa kutokujua au kwa kupuuza kwa sababu ya gharama za ukaguzi na uhasibu, na akawa anaenda kufanya makadirio kila mwaka kisha analipa kodi anaendelea na biashara kama presumptive tax payers wanavyofanya ilihali yeye ni corporate.

Sasa serikali kwa sababu ina marejesho ya mkopo wa reli ikatumia sheria ya kutokupeleka hesabu TRA ya adhabu ya Tsh 225,000 kila mwezi, na ikatumia sheria ya kutoa assessment kukadiria kodi ambayo huenda ingepatikana kwa kufanya examination of books of accounts.

Ikachukua % ya turnover ya miaka 5 ikaiita profit ikacharge penalty na interest kila mwezi ikapata makisio ya kodi ikajumlisha na zile 225,000 kila mwezi za miaka 5 na kumtaka mfanya biashara alipe plus interest each month for 5 years na kuzuia akaunti yake ya biashara huenda yenye pesa za wateja ikimlazimisha kodi ilipwe, mfanyabiashara akashindwa, biashara ikafungwa. Ukumbuke kwa huo mfumo uliotumika inaweza kuja hata kodi ya M40-M50, pesa ambayo mfanya biashara huyo hajawahi kuota kuishika kwa pamoja.

Kisheria raisi alikuwa sahihi na atakuwa alipata rejesho, ila katika uhalisia aliwanyima raia wake haki ya kufanya maendeleo binafsi kwa kuchukua mishahara yao huenda ya miaka 10 mbele ambayo wangelipwa kama angetumia busara na hako kakampuni kakaendelea kuwepo.

Sawa atapeleka rejesho ila, wale watu 5 ambao mshahara wao ameuchukua? Watoto wao mbeleni itakuwa vipi watakapokuta baba zao walilipia treni ila hawana pa kulala?

Sasa ukute baba anahako kakampuni na mama ni mwajiriwa kwenye kahoteli kalikokuwa kanategemea vikao vya wafanyakazi wa serikali vilivyopigwa marafuku kufanyika kwenye mahoteli hako kahoteli kakafungwa huku mzee wao akiwa anacheti cha darasa la saba akaondolewa kazini akiwa na miaka 57.
Ninakupata sana mkuu.

Biashara hazijaanza kufungwa wakati wa JPM pekee, hata sasa kuna biashara nyingi tu zinafungwa kwa sababu mbalimbali ikiwemo makadirio yasiyokuwa ya busara kwa walipa kodi.

Ninafikiri tatizo halikuwa kwa Magufuli zaidi ila watendaji wake, japo anawajibika kama mkuu wa taasisi. Hata hivyo ni wakati huu tulishuhudia TRA ikifanya kazi iliyotukuka na yenye manufaa kwa taifa arguably kuliko wakati wowote ule.

Ninakubali, kunapokuwa na overhaul ya taasisi ya ukubwa huo kuna baadhi ya watu wanakuwa vulnerable kuathirika kwa irregularities zinazojitokeza.

Ninafikiri hizi zinabaki kama changamoto ambazo pengine hakuzi-address ipasavyo hasa kwa kuwa na ile attitude ya wafanyabiashara hukwepa kodi.

Kuhusu vyeti vya kughushi ninaamini alifanya kazi nzuri sana. Hatuwezi kuwa taifa lenye "watalaamu" wasiokidhi vigezo. Hawa walikuwa moja ya sababu za kuwa na malfunctioning institutions nyingi ambazo hazikuwa na afya kwa taifa letu.

Ninafikiri hizi ni gaps ambazo wenzake wanapaswa kuzi-address.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Ninakupata sana mkuu.

Biashara hazijaanza kufungwa wakati wa JPM pekee, hata sasa kuna biashara nyingi tu zinafungwa kwa sababu mbalimbali ikiwemo makadirio yasiyokuwa ya busara kwa walipa kodi.

Ninafikiri tatizo halikuwa kwa Magufuli zaidi ila watendaji wake, japo anawajibika kama mkuu wa taasisi. Hata hivyo ni wakati huu tulishuhudia TRA ikifanya kazi iliyotukuka na yenye manufaa kwa taifa arguably kuliko wakati wowote ule.

Ninakubali, kunapokuwa na overhaul ya taasisi ya ukubwa huo kuna baadhi ya watu wanakuwa vulnerable kuathirika kwa irregularities zinazojitokeza.

Ninafikiri hizi zinabaki kama changamoto ambazo pengine hakuzi-address ipasavyo hasa kwa kuwa na ile attitude ya wafanyabiashara hukwepa kodi.

Kuhusu vyeti vya kughushi ninaamini alifanya kazi nzuri sana. Hatuwezi kuwa taifa lenye "watalaamu" wasiokidhi vigezo. Hawa walikuwa moja ya sababu za kuwa na malfunctioning institutions nyingi ambazo hazikuwa na afya kwa taifa letu.

Ninafikiri hizi ni gaps ambazo wenzake wanapaswa kuzi-address.
Hapa tulipofikia inatosha kukubaliana na kushikana mikono. 🤝
 
Unamaanisha mrusi anaweza kumkopa mmarekani katika Hali ya sasa? Au Ukraine akamkopa urusi?
Hivi unajuwa kuwa USA walitaka kununua mafuta Venezuela mwezi Machi kwa Nicholas Maduro?
 
Siasa ina play role hata kwenye biashara.

Mfano nchi kama korea kaskazini , Iran au Russia zote zina matatizo kiuchumi kutokana na aina ya siasa wanazofanya.

Ni benki chache sana duniani zitafanya biashara na let say North Korea au Iran.

Sasa kama kweli Magufuli alikua hapatani na West kwa kiasi hicho wasingempa fedha.
HISTORIA KIDOGO:

Kabla halijazuka shinikizo la kumtaka ajiuzulu mwaka 2011, aliyekuwa Waziri mkuu wa Italy - Silvio Berlusconi aliwahi kumtusi aliyekuwa 'Chancellor' wa Ujerumani kipindi hicho, Bibi Angela Merkel (Tusi linahusu makalio ya bibi Angela). Likatokea anguko la kiuchumi, ambapo hali ya Italy ikawa mbaya kiasi cha kuhitaji msaada - na taifa ambalo lilikuwa linatazamwa sana kuweza kuiokoa Italy ni Ujerumani. Wakati huo Silvio alikuwa hana mahusiano mazuri na Angela, walikuwa hawawezi kutazamana uso kwa uso; lakini ilipofika wakati wa Ujerumani kuisaidia Italy - Angela hakusita kwenda kuonana na Silvio akiongoza jopo la akina Sarkozy na wengineo; na bila shaka wakampa Silvio ofa ya Mkopo.

Lakini, nyuma ya huo mkopo kulikuwa na agenda ya siri - ambayo ilikuwa ni kumg'oa Silvio madarakani! Wenyewe wanasema ilikuwa ni "The kiss of death" kwa Silvio - kwasababu angekubali kupokea ule mkopo, ingekuwa ni kwisha habari yake, na angekataa kupokea mkopo pia - kwisha habari yake!! Kuna maelezo deep kidogo kwanini ilikuwa hivyo.

Pointi yangu ni kwamba, haya mataifa makubwa siku zote yanatanguliza maslahi na malengo yao kwanza. Kwahiyo, hata kama wewe ni adui yao, kama huo mkopo au msaada au makubaliano au chochote kile watakachokifanya kwako au kwa kushirikiana na wewe kinawasaidia wao kutimiza malengo yao... kwanini wasifanye?

"Keep your friends close and your enemies closer"
 
Hapana.
Bank za biashara zinalenga faida, si siasa.

Kuhusu alichokuwa anafanya na hiyo mikopo anastahili pongezi kwa sababu miradi ya maendeleo ipo na tunaiona, LAKINI kwa gharama gani?

Wote tunajenga nchi moja, tunastahili heshima na kuwekwa wazi juu ya nini tunagharamikia ili tupate maendeleo.

Hakukuwa na ulazima tumalize ujenzi wa Tanzania katika awamu ya 5, tunafanya pale tunapoweza kwa uaminifu na tunatoa nafasi kwa wengine kufanya sehemu yao.

Sasa tunajenga reli ya kisasa kwa gharama ya kuchukua pesa ya mfanyabiashara kutoka akaunti yake ya bank ili ulipe mkopo wa biashara wa kujenga reli wenye riba kubwa? Mfanya biashara mwenyewe unakuta pesa na yeye alikopa, au ni za wateja wanasubiri huduma. Haikuwa sahihi.
Naomba uniwie radhi kukuita goigoi wa kifikira... tumekuwa nchi huru more than 50 years lakini hatukuwahi kuja na mradi wenye kutoa suluhisho la kudumu la shida ya umeme.

Suluhisho la kudumu la usafiri wa anga kwa mfano leo kuna Royal Tour ya Mama Samia ili iweze ku mature usafiri wa anga utakuwa na mchango mkubwa sana.

Ili tuendeshe nchi kwa kutoa unafuu kwa raia, na ushindani wa soko lazima tuwe na low cost in production and distribution chain hapo bado tunaongelea usafiri wa kila aina kuanzia land, railway include SGR, usafiri wa njia za majini, barabara nk ambao ndio ilikuwa miradi ya kimkakati....

Kuanzisha viwanda ili kuongeza thamani ya malighafi zetu, kukuza kilimo ikiwemo uanzishaji wa kilimo cha mpunga pembezoni mwa mradi wa JNHPP ambapo kungepatikana ziada ya kuuza nje na ukiangalia miradi yote ya kimkakati mpaka sasa ikiweza kusimamiwa vyema itatuingizia fedha za kutosha... ikiwa ni pamojama kipata rejesho la mikopo nk. Itazalisha ajira na kupandisha pato la mmoja mmoja (GDP )
Ntaenda mpaka uanzishaji au ukuzaji wa Burigi kwa kufanya wild animal transfer kwa jamii ambazo hazikuwepo kwenye mazingira ya awali lakini mfanano wa mazingira na tabia nchi unafanana kwa wamwanya hamishiwa kuishi... mikopo hiyo hata kwa akili za kawaida unaona kabisa ilikuwa na uwezo wa kujilipa... maana mbali na kutatua changamoto za muda mrefu bado ilikuwa inaingiza fedha toka ndani na nje inazaa ajira.. hapo hatujagusa miradi mikubwa ya maji safi na maji taka.... hatujagusa miradi ya kiudhibiti kama mizani nk... swali ambalo ulitakiwa kujiuliza kabla je? tungeacha kipi na tufanye kipi ambacho sio kipaumbele.
 
Usichokijua ni kuwa ugomvi sio chanzo cha kunyimwa mkopo.

Mkopo unapewa sababu una masharti yanayokaa kwenye maandishi.

Wazungu hufanya kazi au mikataba yenye "interest " kwao bila kuangalia ugomvi.

US na China ni rivals ila iPhone iko designed China na inakua assembled California.

Ni biashara nyingi tu wanafanya hata US anazo bidhaa zake za kuuza China tu kwa Africa hamuwezi kumudu.

Hili linaenda sambamba na quality na geography ya eneo husika , nishawahi kuona bus za Yutong pale Haifa sio Yutong za aina hiyo zipo bongo.

Nchi nyingi zina ugomvi na Israel ila Haifa lipo eneo lina majengo ya KIA, Hyundai, Toyota , Nissan ,Suzuki , Ford na kadhalika.

Whites only work on interest basis.
 
Back
Top Bottom