Hayati Magufuli angejaliwa subira hakika angekuwa habari nyingine

Hayati Magufuli angejaliwa subira hakika angekuwa habari nyingine

Suzy Elias

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2021
Posts
1,067
Reaction score
6,200
Pamoja na kupungukiwa subira hakika JPM alikuwa na tamaa ya dhati kabisa kuisaidia Nchi yetu iweze kufikia maendeleo ya kweli.

JPM hakuwa na subira ya hata chembe kitu ambacho kiliwaumiza na wasio husika.

Mfano mzuri ni suala la vyeti fake JPM alitakiwa angalau wale ambao walikuwa na uzoefu wa fani husika na walitumika/hudumu aghalabu zaidi ya muongo mmoja angewasamehe na wangetakiwa wapewe japo muda wa mpito ili waweze kujiendeleza kielimu kwa kuzingatia tasnia waliyokuwapo.

Pia suala la kuvunja nyumba za watu pale Kimara Hayati Magufuli alipaswa kutoa japo fidia kiasi bila kujali mambo ya sheria. Ni wazi JPM hakuwapenda wana kata ya Kimara kwa sababu ya itikadi zao za kisiasa lakini hakupaswa kuwahukumu kwa namna ile aliyoifanya.

Katika yote, JPM alikuwa Rais mzalendo wa kweli ndani ya Nchi yake!

Tuendelee kumsamehe Rais Magufuli na pia tuendelee kumuombea pumziko la milele.

RiP JPM!
 
Hakika Taifa, Afrika na Dunia nzima itamkumbuka huyu mzalendo wa kweli na shujaa wa Afrika.Ilikuwa zawadi ya pekee kutoka kwa Mungu.
... ushujaa wake kwa Afrika ni upi? Elaborate maeneo matatu tu.
 
Uzalendo unatoka wapi kwenye hayo mapungufy uliyoyaainisha?
JPM kama binadamu ilimpasa awiwe mapungufu ambayo kwayo hayawezi kuondoka nia na dhamira njema hasa ihusuyo maendeleo aliyopata kuwa nayo kwa Taifa letu.
 
Pamoja na kupungukiwa subira hakika JPM alikuwa na tamaa ya dhati kabisa kuisaidia Nchi yetu iweze kufikia maendeleo ya kweli.

JPM hakuwa na subira ya hata chembe kitu ambacho kiliwaumiza na wasio husika
hivi wasukuma nchi hii tumewakosea nini? inamaana kweli wote akili zenu mnafanana namna hiyo? how can you preach uzalendo na maendeleo wakati umejifungia kwenye nchi yako na unapunguza ushirikiano kwenye ulimwengu wasasahivi? (I am not being tribalist, hao wafuga ng'ombe ni watani zangu).
 
Hakuna sehemu Dar es Salaam inaitwa " Kimala" ni Kimara! Nyie Wasukuma mmetuchosha sana na lugha zenu mbovumbovu! Rais mnamuita "Laisi", Miradi mnaita "miladi'!
 
Kiburi cha mwanadamu kimapofikia kiwango cha juu, Ndipo Mungu hujitokeza na kuonyesha ukuu wake kwa mwanadamu huyo, Jamaa alikuwa na kibuli sana na kutamani abudiwe hivyo Mungu asingemuacha aendelea kuminya uhuru na haki ya watu wake wa thamani hapa duniani.
 
JPM kama binadamu ilimpasa awiwe mapungufu ambayo kwayo hayawezi kuondoka nia na dhamira njema hasa ihusuyo maendeleo aliyopata kuwa nayo kwa Taifa letu.

Kila mtu ana mapungufu lakini pia mambo mazuri. Dhamira na nia njema hazisimami zenyewe bila matendo. Unajua habari ya “….. imani bila matendo ni kazi bure …..”

Je kulikuwa na haja ya kuumizwa ili maendeleo yapatikane?? Hivi ni sahihi kuwa malipo ya maendeleo kwa mkoja ni maumivu kwa mwingine?

Dhana ya “results justify the means” sio sahihi!
 
Hakika Taifa, Afrika na Dunia nzima itamkumbuka huyu mzalendo wa kweli na shujaa wa Afrika.Ilikuwa zawadi ya pekee kutoka kwa Mungu.

Nadhani una tabia ya kusifiasifia tu! Hata huyu wa sasa utamsifia hivi siku za usoni!

Badala ya kubwatuka kutwa kucha, toa reference. Hao waafrika na dunia wamemsikia wapi akiongea kama hakuwa akienda kwenye mikutano ya EAC, African Union, SADC wala UN. Watakumbuka nini walichosikia kutoka kwake??

SSH ni mtu ambaye dunia imemsikia zaidi kuliko JPM. Katika mashujaa wa Afrika JPM hatapata kuwemo, unless unabadilisha maana ya ushujaa. Uzalendo ni jambo domestic sana, na haliwezi kupimwa kwa kudhulumu watu mali na uhai wao, kukandamiza haki za watu. Uonevu na matumizi ya nguvu. Na utakubaliana nami kuwa sasa raia wengi wanapumua - jiulize kwanini!! Jiulize kwanini wengine sasa wanaanza kupata maumivu!! Haki ni jambo la wakati wote!!
 
Mungu ni mwenye wivu .....ilipitiliza binadamu wakawa wanaabdudu binafamu mwenzake ukuu wa Mungu lazima ujionyeshe ........eti mh mungu wewe dgihaka kubwa hiyo...
 
Pamoja na kupungukiwa subira hakika JPM alikuwa na tamaa ya dhati kabisa kuisaidia Nchi yetu iweze kufikia maendeleo ya kweli.

JPM hakuwa na subira ya hata chembe kitu ambacho kiliwaumiza na wasio husika.

Mfano mzuri ni suala la vyeti fake JPM alitakiwa angalau wale ambao walikuwa na uzoefu wa fani husika na walitumika/hudumu aghalabu zaidi ya muongo mmoja angewasamehe na wangetakiwa wapewe japo muda wa mpito ili waweze kujiendeleza kielimu kwa kuzingatia tasnia waliyokuwapo.

Pia suala la kuvunja nyumba za watu pale Kimala Hayati Magufuli alipaswa kutoa japo fidia kiasi bila kujali mambo ya sheria. Ni wazi JPM hakuwapenda wana kata ya Kimala kwa sababu ya itikadi zao za kisiasa lakini hakupaswa kuwahukumu kwa namna ile aliyoifanya.

Katika yote, JPM alikuwa Rais mzalendo wa kweli ndani ya Nchi yake!

Tuendelee kumsamehe Rais Magufuli na pia tuendelee kumuombea pumziko la milele.

RiP JPM!
Katika mapungufu yake yote kuna mawili ambayo yalimvua credibility zote moja ni kutokutaka kusikiliza ushauri na maoni ya watu kuendesha nchi ya watu over 61M kama unaenda familia yako ni kosa kubwa
Cha pili ni ukabila tukiwa wa kweli hatujawai pata raisi mkabila kama yeye ilifika mda mpaka ukanda wake watu wakajihisi ni special kwenye ili taifa mpaka mtaani wengine wakaanza kujiita wasukuma mbeli ya jamii.

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom