Uchaguzi 2020 Hedaru: Dkt. Magufuli amuagiza katibu mkuu TAMISEMI apeleke milioni 100 kukarabati kituo cha afya

Uchaguzi 2020 Hedaru: Dkt. Magufuli amuagiza katibu mkuu TAMISEMI apeleke milioni 100 kukarabati kituo cha afya

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Leo Dkt Magufuli alimtafuta waziri Jaffo kwenye simu lakini hakupatikana na kuamua kumtafuta katibu mkuu na mazungumzo yao yalikuwa hivi.

MAGUFULI: Katibu mkuu hujambo?

NYAMHANGA: Sijambo, shikamoo mheshimiwa Rais

MAGUFULI: Marahaba, habari yako injinia Nyamhanga

NYAMHANGA: Salama mheshimiwa Rais, hongera kwa kampeni

MAGUFULI: Nilikuwa namtafuta waziri wako, waziri Jaffo naona hapatikani kwenye simu.

NYAMHANGA: Atakuwa kwenye kampeni huko Kisarawe.

MAGUFULI: Sasa natoa maagizo hapa, leo niko Hedaru, nimekuta kuna kituo cha afya hapa kina wodi ya kulaza wakinamama na akina baba, hakina wodi ya kufanyia operesheni, hakuna maeneo ya kuhifadhi maiti lakini hakuna X-Ray na vitu vingine.

Nimetoa maagizo mlete Tshs milioni 100(Wananchi shangwe). Na hiyo mjulishe huyo waziri wako, milioni 100 zije hapa Hedaru mfanye ukarabati na kuongeza majengo yote ya wodi ili wana Hedaru operesheni ziwe zinafanyika hapa.

NYAMHANGA: Sawa mheshimiwa Rais

MAGUFULI: Umenielewa katibu mkuu

NYAMHANGA:
Nimekuelewa mheshimiwa Rais

MWISHO WA MAONGEZI

============

MAGUFULULI: Ndugu zangu mimi nimemaliza ahadi niliyoitoa, nimeitoa jua linawaka na hii hospitali itakapokamilika nitakuja kushughulikia lakini sera nyingine ya maji na nini nayo tunaendelea kuyashughulikia, nawashukuru sana Mungu awajaalie. Wangapi mtanipa kura lakini?
 
Magufuli asingelazimisha kununua midege isiyokuwa na faida yoyote kwetu malalamiko haya yasingekuwepo.h

Katika miaka mitano ijayo Magufuli amepanga kutumia billion 490 kununua ndege mpya toka kwa mabeberu.

Sasa hebu jiulize billion 490 zinaweza kukamilisha miradi mingapi ya maendeleo hapa nchini? kwanini wanalazimisha kununua ndege kama hakuna upigaji?
 
Siyo hivyo, sisi watumiaji wa ndege zinaturahisishia sanq
Naona hapo mkiijaza mafuta V8 ya Polepole.
EkkQq3-XgAAaO8n.jpg
 
Hii ni rushwa ya wazi wazi lakini NEC hawalioni hili, ukiangalia suala la Kituo cha Afya Hedaru ni la muda mrefu idadi ya watu iliyopo na uwezo kituo haviendani, inatakiwa pajengwe kituo kingine cha afya viwe viwili kuhusu mochwari ni lazima watu wanapeleka maiti Same bonde lote la Hedaru na viunga vyake.

Pamoja na changamoto zilizopo Hedaru haihalalishi dhambi ya kutoa hii rushwa ili apewe kura tena, Changamoto za Hedaru ni za miaka yote alikuwa wapi huyu mzee.

Alikuwepo mwenyekiti wa kijiji kupitia CHADEMA alifanya makubwa sana mkuu wa wilaya na viongozi wa CCM wakafanya figisu wakamtoa kwa nguvu.

Anachodhihirisha Magufuli kwa watu ni mzembe wa kuona matatizo ya jamii, mtoa rushwa mkubwa na mwenye uchu wa madaraka hafai tena
 
..Magufuli asingelazimisha kununua midege isiyokuwa na faida yoyote kwetu malalamiko haya yasingekuwepo.
Kwa kweli miluzi mingi humpoteza mbwa ,kwa hiyo sekta ya utalii inachochewa na miundo mbinu ipi?

Ndege ni uwekezaji wa kibiashara kama zilivyo biashara zingine ambazo hata wewe ungefanya mfano kuliko kupokea mshahara wa mwezi kununua chakula na malazi ukautumia kuwekeza kununua shamba hivi kweli shamba linaweza kuwa halina faida kwa familia yako iwe sasa au baadae? JPM ilani imemtaka kuboresha shirika la ndege unadhani angeboreshaje na alikuta ndege 1 mbovu.

Hivi unataka kusema viwanda vya Dar vinatunufaisha vipi sisi tuliopo Chongoleani Tanga na Dhahabu iliyo Geita ina manufaa gani kwa watu ,jibu nijepesi miradi yote ya Serikali sio mali ya mtu binafsi bali ni ya Umma hizo pesa zote zinaenda kwenye kapu moja ndilo ambalo linasaidia miradi ya ujenzi Zahati na barabara.

Hivi hujui mradi wa Ziwa victoria kwenda Tabora umefikia wapi,na ule mradi wa Arusha mabilioni unayajua ni mangapi na huku Miradi mingi ya Dar ikiwa ni Trillion of money leo unapiga kelele ndege ambazo ni uhuduma ya kuchochea sekta zingine kukua pia kama Utalii na Usafirishaji.

Nahisi wewe utakuwa umekula age haya sio mawazo ya kijana wa kisasa maana teknolojia inaenda kasi sana sio vibaya na sisi kwenda kama dunia inavyoenda kuwa Bullet train ,Ndege majengo ya kisasa kwenhe miji yetu n.k ,nadhani umeona kwa wenzetu train zao zinavyowakera kwa sababu ya mawazo machache ya washamba kama wewe kwa dunia ya sasa huwezi kuponda ununuaji wa Ndege.

Nchi za wenzetu umeme sio tatizo lakini utakuta mtu yupo village ana mashamba yake kapiga Panel za solar hakuna shida kabisa ila hapa ni malalamiko mnawekewa Bwawa la umeme mnarudisha kelele za tungeanza gesi .

Nimenyoosha mikono Tanzania bila Magufuli tukapata wanaoyumbishwa maendeleo tutayasikia kwingine.
*Magufuli 5 tena*
 
Back
Top Bottom