Hekaheka Uzeeni

Hekaheka Uzeeni

INAENDELEA…

“Well, its okay, lets share the room and I promise will not swallow you…” tukawa tunacheka huku tukielekea chumba husika maana mwenzangu pale inaonekana ni mwenyeji.


2. Sehemu ya pili – KISOMO CHA WATU WAZIMA

Tahadhari zote nilikuwa nazo, za kiusalama wangu na mali zangu pamoja na kifaragha maana matukio ya kusikitisha hutokeaga kama hivi. Hoteli ilikuwa ni ghorofa, sisi tulipata’ first floor’ na chumba kilikuwa kikubwa kiasi cha kusema kwa hela ile ni halali tu.

Nilikagua kila chumba kama kuna kamera-fiche, nikaona pako salama, nikawa nimekaa kwenye kochi na mwenyeji wangu wakati huo alikuwa kwenye kitanda. Mara simu ya mezani pale chumbani ikaita, Janeth akaipokea , kumbe aliweka oda tayari ya chakula kwa ajili ya watu wawili. Mlango ukabishwa na akaingia mhudumu kuleta chips kuku mbili na kuondoka.

“Tule kwanza kisha ndio tuangalie utaratibu wa kulala…” nilipendekeza na ikapita bila kupingwa.

Nilipendekeza pia tuanze sahani moja kwanza wote kwa pamoja na kama hatujashiba basi tuhamie sahani nyingine. Hii ilikuwa mbinu ya kujihami na madhara ya kwenye vyakula, kama yapo basi yatupate sote na wakati wa kula nilihakikisha nasoma lugha ya uso wake ili kujiridhisha.

Maskini binti wa watu wala hakuwa na makuu bali ni ukarimu tu wa kawaida na kama alikuwa na agenda ya siri basi sikuiona haraka ukiachilia mbali na suala la kushiriki tendo la ndoa.

Mfukoni kweli sikuwa na hela za kutosha kwa mambo ya ziada, zaidi ya yale niliyo jipangia hadi kufika Congo, hivyo sikuwa na mzuka maana boom la kustaafu lilikuwa bado kutoka na tayari nilishasota mtaani miezi kadhaa hivyo vihela vyangu vilikuwa vya kuunga unga. Nikatuma ‘txt msg’ kwa Jason Jr ili aniazime dola mia tano atume kwenye account yangu ya benki just incase. Kabla sijalala muamala ulisoma kwenye akaunti yangu.

Janeth alikuwa huru tu, akaingia bafuni na kibegi kidogo na alipotoka alikuja amevaa kaptura na juu alikuwa amevaa fulana nyepesi (haikuwa night dress hizi tunazozijua)

“I am in my period so don’t try anything nasty…!” aliniambia huku akiingia kwenye blanket tayari kuutafuta usingizi.

Moyoni nikajisemea afadhali maana umenirahisishia mambo mengi ambayo tayari nilikuwa nawaza kichwani. Sikuwa na soksi wa vipimo vya kupimia tanesco kama ipo. Nikaingia bafuni na kuanza kuoga, wala sikutumia muda mrefu nikatoka kuja kuungana na Janeth ndani ya blanket na kuanza kuzungumza mengi katika kutaka kufahamiana zaidi.

Saa sita kasoro hivi usiku, Janeth alipitiwa na usingizi akiwa bado amelalia mgongo, nilijuwa baada ya kumuuliza swali fulani ili niendeleze stori niliyokuwa namsimulia lakini hakujibu, kugeuka ndio nikaona amelala hana habari. Nikamfunika blanket vizuri nami nikavuta upande wangu nikawa kama nimelala lakini nipo hadhiri masikio waruuu!

Saa tisa na nusu hivi usiku aliamka kwenda maliwatoni , nilikuwa macho bado maana sikutaka usingizi unipitie hata chembe ingawaje nilifunga macho.

Huwa nina kawaida ya kuamka asubuhi saa kumi na robo kwa ajili ya maandalizi ya siku pamoja na ibada za asubuhi lakini siku hiyo sikusikia alarm hadi saa kumi na moja haja ndogo iliponibana nikaamka na kuangaliaa saa! Nilishangaa sana. Janeth bado alikuwa amelala. Nikaenda maliwatoni na kujimwagia maji safi ya moto tayari kwa maandalizi ya kuendelea na safari. Nilivyotoka bafuni nilimkuta Janeth naye ameamka amekaa kitandani.

“Goodmonring Jane! Leo nimechelewa kuamka na wala sikusikia alarm ya simu…” Nilimsalimia na akajibu…

“Goodmornind Dad, pole kwa uchovu…”

Nje pilika za bodaboda zilikuwa zinazidi kuongezeka, bajaji na magari madogo maana tulikuwa kando kando tu ya barabara ielekeayo stendi.

“Kumekucha, kajiandae tusije tukachelewa…” nilimwambia.

“Bado kuondoka, saa kumi na mbili ndio basi litaondoka, muda bado hata hivyo ngoja nijiandae haraka haraka…” alisema.

Kama nilivyoeleza awali kuwa katika kuandika najaribu kunyoosha maneno yake angalau wewe unayesoma uelewe, lakini ilikuwa ni lugha gongana kwenda mbele ingawaje tulielewana kwa kuchanganya lugha zote mbili Kiswahili na Kiingereza.

Awali nilimuona Janeth kama ni aina ya wale wanawake wafanya biashara ambao wapo tayari ku ‘risk’ chochote ili mradi aingize hela hivyo nami nika ‘adopt’ uelewa ule ndio maana nikaomba nitumiwe hela ambayo hata haikuwa kwenye bajeti ya safari yangu. Uchumi wangu ulikuwa ni wa kawaida tu wa kujikimu ndio maana fursa hii ya kufanya kazi siku 90 DRC niliichangamkia.

“Uko mubaba muzuri, hujanisumbua…” alisema Janeth wakati akimalizia kujipamba.

“My period ended the day before yesterday but I’m not that clean for the game ndio maana nilikuambia nipo kwenye siku zangu…” Aliendelea kujisemesha.

“it’s okay Janeth, mimi wala sikuwa na mpango wowote na nilidhani ningelala kwenye basi, ahsante kwa ushauri wa kupumzika lodge…” nami nilijiongelesha.

Tulitoka pale huku akikataa mimi kuchangia gharama za lodge na chakula, lakini nikawahi kulipia bodaboda mbili ambazo zilitufikisha stendi saa kumi na mbili kasoro dakika kumi.
===

Kifungua kinywa tulipata Ushirombo ambapo pia walitumia nafasi hiyo kujaza mafuta kwenye basi, baada ya hapo moja kwa moja hadi Nyakanazi tulipoacha lami na kuanza njia ya vumbi na mashimo kuelekea Rusumo. Ni kilomita chache tu lakini tulitumia muda mwingi sana kufika border ya Rwanda na Tanzania.

Baada ya kukamilisha taratibu za border na kuvuka, nikaenda kwenye ‘restaurant’ upande wa Rwanda sasa ili nipate chakula, wakati huo Janeth yeye na wafanyabiashara wengine walikuwa wakikaguliwa mizigo yao hapo border ya ajili ya mambo ya ushuru nk. Alinirusuhu nikale maana huenda yeye angechukuwa muda mrefu kukamilisha zoezi. Ni kwamba hapo mpakani kwenye basi hushuka abiria wote na mizigo yote hushushwa ya kwenye buti na ndani ya basi na kila mmoja kupitia ukaguzi kulingana na mzigo wake kisha kwenda uhamiaji kama taratibu za kuvuka boda zilivyo.

“Nipatie mashilingi hayo nikupe faranga, ‘rate’ nzuri kabisa nakupatia…” alisikia ‘husler’ mmoja hapo nje ya restaurant.

Nilibadili dola mia kwake na nikamwomba anipatie kijana anayesajili line ya mtandao wa MTN ili nipate simcard ya Rwanda.

Zoezi la kuvuka hadi basi kuwa tayari kuondoka lilichukuwa zaidi ya saa tatu na kufanya tuwe nyuma ya ratiba ya kawaida ya basi. Abiria wengi walikuwa na mizigo ambayo ilikuwa na utata katika kuvusha lakini hatimaye wote tulifanikiwa kuvuka.

Baada ya kuvuka, dereva tuliyetoka naye Dar alipumzika kwenye siti namba moja na yule dereva wa pili, Mnyarwanda alichukuwa nafasi.

Sasa sijui kwa kuwa tulikuwa nyuma ya ratiba ama ndio uendeshaji wake, ee bwana ee, mwendo ulikuwa si wa kitoto, kuna wakati kwenye gps yangu speed ilisoma hadi 160kph ikabidi niinuke niangalie dashboard ya basi. Njia ilikuwa ya lami lakini nyembamba halafu basi lilikuwa linatembea upande wa kulia, kila mara nikajikuta nabana breki mimi ilhali siye ninaye endesha maana si kwa kuhisi hatari zile! Tena mpambe nilimsikia akisema amsha amsha!

Kabla ya kufika Rusumo, njiani kuna baadhi ya abiria washuka, mmoja tulimwacha pale kizuiani maana watu wa uhamiaji walimtuhumu ame ‘overstay’, wengine walishukia Lusahunga, Benaco na Mizani. Hivyo basi ilipata nafasi kiasi cha kupakia abiria wengine pale boda baada ya kuvuka. Mmoja wa hao abiria nadhani alikuwa wakala wapo ndiye alikuwa akihamasisha sana kuwa gari imechelewa.

Nilikuwa nadhani Rwanda mabasi hayakimbii kama nilivyosikia awali lakini ilikuwa kinyume chake hadi tuliposogea mbele mbele sana na giza likaanza kuingia ndip mwendo ukawa wa kawaida. Ni wastani wa kilomita 160 hivi kutoka Rusumo border hadi Kigali, lakini huwezi kuamini, tulifika saa tatu hivi usiku iwakuwa wakati tunakaribia mjini Kigali tukakuta foleni ndefu sana iliyotulazimu kutembea ‘jino moja moja’.

Safari ilichosa sana kipande cha Nyakanazi hadi Rusumo, tulitembea taratibu mno kwakuwa njia ilikuwa na mashimo na rasta baadhi ya sehemu, haikuwa njia rafiki kwa kweli licha ya umuhimu wake njia kuu hiyo. Nadhani sikuhizi pako vizuri, sijapita tena kwa barabara.

Janeth alinipa ofa ya kwenda kufikia kwao, ingawaje niliikataa na kumweleza kuwa mimi ni mpita njia tu naelekea Rubavu (nilimdanganya). Rubavu ni moja ya majimbo ya Rwanda jirani na Congo huko. Akaniambia basi kesho yake nisiondoke ili anitembeze Kigali kwenye ‘sabasaba’ yao. Focus yangu haikuwa kwenye kutalii bali kibarua kinachonisubiri huko Goma. Lakini nikaangalia kalenda nikaona bado nipo mbele ya muda na nina siku 4 mbele kabla ya kuripoti nikamkubalia ombi la kunitembeza Kigali.

Haikuwa mara yangu ya kwanza kuwepo Kigali lakini nilitaka nipate ‘experience’ nyingine kupitia huyu Janeth ambaye naona kama anataka kunizibia kufurahi na watoto wengine wa Kinyarwanda. Alikuwa anakaba sana kana kwamba tumekubaliana chochote.

Wajihi wangu ni bonge la mtu, mrefu futi sita hivi, maji ya kunde, heavy weight 105Kgs, ndevu zote mvi kichwani nimenyoa unga kuficha wingi wa mvi, nilivalia kawaida tu suruali ‘cadet’ na shati ‘cadet’ la mikono mirefu nililovaa Kahama maana kutoka Dar nilivaa ‘tshirt simple’. Sura yangu haijazeeka ingawaje ukiniangalia kwa makini ndio utaona kilomita zimeenda, hivyo nadhani nilikuwa naonekana bonge la Bwana. Yeye Janeth alibadili nguo zote pale Kahama, mimi suruali sikubadilisha. Alivaa gauni refu na mapambio yake.

Tulibadilishana namba za whatsapp na nikampa namba yangu ya MTN. wote tulishuka Nyabugogo bus terminal. Yeye Janeth alichukuliwa na pickup townhiace ambayo pia ilipakia na mizigo yake, mimi nikachukuwa TOYO (bodaboda) na kunipeleaka Kaizen Hotel ambayo haikuwa mbali na stendi.

Pamoja na mambo mengine, chumbani nilipokelewa na kitanda chenye godoro lenye ‘finishing’ ya material yasiyopitisha maji. Mawazo yakarudi kwa Janeth.

“Hawa si ndio mabingwa wa kurusha maji katika harakati za kilimo ya umwagiliaji!, kwanini nisitumie fursa hii kupata elimu ya watu wazima…” niliwaza. Nikaanza kuona saa haziendi. Kabla ya saa tano usiku kwa saa za Bongo nilikuwa nimeshaegesha, na usingizi haukuchukua muda kunipata kwa kuwa nilikuwa na uchovu uliotokana na usingizi wa mang’amng’am wa Kahama na uchovu wa safari. Nikakumbuka maneno ya Janeth kuwa nisilale kwenye basi nitachoka sana, nikaona kumbe alinishauri vyema ingawaje uchovu mwingi ulitokana na mimi kutolala vema kule Kahama.

Saa kumi na robo simu iliniamsha, nikachungulia nje bado giza sana, ikabidi nirekebishe saa yangu iendane na majira ya kule, hivyo nikarudisha dakika sitini nyuma. Nikaendelea kuegesha huku nikitafakari baadhi ya mambo. Usingizi ukanichukuwa tena hadi nilipostuka saa moja asubuhi kwa saa za Rwanda. Nikaamka na kujiandaa kwa ajili ya kupata kifungua kinywa.

Restaurant wageni wenzangu walikuwepo wengi wakijihudumia kupata breakfast, nami nikaungana nao, wengi wao walikuwa wakiongea kinfaransa na baadhi Kinyarwanda. Wahudumu wa kike wa hoteli walikuwa kama wale tunaowaona kwenye mitandao lakini huko mitaani wanawake wengi sana ni wa kawaida tu tena wengine wala si warefu ama warembo kivile ama wenye maumbile hamasishi. Nikakumbuka ule usemi, ukitaka kuifaidi Kigali, fikia hotel zenye hadhi ya juu ama tembelea kwenye ma-‘shopping mall’ na sehemu kama hizo huko ndiko kuna vile vitu wabongo wengi tunababaikaGa navyo.

Wakati nikiendelea kupata staftahi nilipokea simu ya kwanza kwenye line ya MTN kutoka kwa Janeth, nilijuwa tu ni yeye maana namba bado sikuwa nimeigawa kwa watu wengine.

“…I will be at Nyabugogo terminal at ten thirty, lets meet at Trinity Bus office…” aliniambia.

Ilipofika saa nne kasoro kidogo nami nikakabidhi mzigo wangu mapokezi na kushuka chini kuchukuwa toyo ili inifikishe jirani hapo stendi. Saa nne na dakika chache nikaona nafwatwa kwa ishara ya kukumbatiwa, alikuwa na tabasamu na mwenye uso uliokunjuka.

Baada ya kumbatio motomoto pale na kupeana pole za uchovu akaniambia kuwa yeye hakai mbali sana na hapo, anaishi maeneo ya Kacyiru. Akaniahidi kunipelea kwao. Nikakubali. Lakini akaniambia tuelekee kwenye maonesho kwanza ili tuzunguke humo wee kisha ndio tuende kwao kisha kuzurura jijini Kigali.

Akaniambia tuchukuwe taxi.

“Nyamuneka utujyane i Magerwa…” alisema Janeth akimwambia yule dereva wa teksi atupeleke sehemu iitwayo Magerwa.

Dakika chache tu baadaye tukafika hapo Magerwa, ni kama vile bandari kavu fulani hivi, hatukuingia ndani badala yake akaniambia tutembee kuelekea upande uliouoneshea kidole.

“We are heading to Gikondo area, sio mbali ni paleeee…” alisema.

Kumbe hapo Gikondo ndio kuna sabasaba yao, tukalipa kiingilio na kuingia ndani. Pamoja na mambo mengine ya ki-‘trade fair’, nilikutana na visu hasa, yani Jane wangu nilimuona wa kawaida sana, ingawaje yupo vizuri kisu haswa lakini asikwambie mtu, macho ya wanaume hayachoki kuona vitu vizuri. Tulijifunza mengi humo na baada ya kuchoka tuka kaa sehemu kama mghahawa hivi mumohumo kwenye maonesho na kuanza kuongea mawili matatu huku tukipata viazi mbatata, maharage na samaki kama sato.

Baada ya hapo tulifanya mzungukowa pili ambao sasa huu ulilenga sehemu maalumu tulizoziona kwa ajili ya kununua baadhi ya bidhaa alizotaka nami nikaambulia kununuliwa mkanda wa ngozi pamoja na wallet kutoka kwa wafanyabiashara waliotoka Misri.

“Zawadi yako uwe unanikumbuka…” alisema Janeth.

Baada ya muda kidogo tulitoka tukiwa na mizigo yetu na kuchukuwa Taxi.

“…Kacyiru…” Janeth alimuambia yule dereva na tukaanza kuondoka.

Nilifurahia nidhamu ya barabarani ya madereva wa kule, yani madereva wote wa vyombo vya moto. Sheria za usalama barabarani zilikuwa zinafuatwa vyema.

Baada ya kona mbili tatu nikaona dereva akiuliza maelekezo ya ziada, alipopatiwa nikaona amekuja tena kona kadhaa kisha tukafika eneo tulivu lenye nyumba nzuri yenye ‘umatemate’ fulani hivi.

Nilikaribishwa vizuri na tulikuja kupokelewa na watu wengine mle ndani. Baada ya utambulisho mle ndani mwao kwa waliokuwepo tukaletewa chakula. Kulikuwa na ndizi nyama na vikorobwezo vingine, tukala huku tukiendelea na mazungumzo ya kawaidia.

Baada ya kama saa moja hivi akaniambia twende sasa nikutembeze Kigali. Tukatoka mle ndani, akawasha gari yake vw golf (baby walker) na tukaelekea katikati ya jiji moja kwa moja kwanza kwenye duka lake. Awali nilidhani ni duka dogo tu la wajasiri-amali, lakini kumbe dooo! Ni bonge la duka lililosheheni nguo za wanawake tu.

Alinitembeza kwa gari pale mjini, kisha kwa miguu hadi ilipofika saa moja jioni kwa saa za Rwanda tukarudi dukani kwake ili achukue gari turudi nyumbani kwao. Kwa kweli nilifurahia kubaki Kigali siku hiyo. Tulifika kwao saa mbili kasoro hivi kwa saa za kule na kukaribishwa. Safari hii nilikuta familia imeongezeka, yaani baba yake alikuwepo, mama yake, dada zake na kaka zake. Ilikuwa ni familia yenye furaha. Ilikuwa ni familia ya aina yake ambayo baba ni Mhutu na mama ni Mtutsi, ni familia ambayo imejaribu kuvuja jambo la ukabila katika nchi hiyo na Baba ni afisa wa Polisi katika Serikali ya Rwanda.

Niliwaza hapa nikijichanganya tu napata ndoa ya uzeeni, maana si kwa ukarimu ule sijui hata Janeth aliwaambia nini. Janeth alikuwa mtoto wa tatu kuzaliwa akitanguliwa na dada zake wawili kisha kufuatiwa na kaka zake wawili. Dada zake wote walikuwa wameshaolewa, lakini yeye na kaka zake walikuwa bado hawajapata ndoa. Baada ya chakula cha jioni, niliaga ili niwahi kupumzika maana asubuhi nilitaka nianze safari kwenda Gisenyi -Rubavu Province kama nilivyomuambia Janeth. Sikutaka ajuwe kama nitavuka mpaka na kuingia Congo kwa wakati huo.

Tulitumia gari ya Janeth hadi aliponifikisha Hotelini kwangu na nikamkaribisha hadi chumbani.

Dhambi iliyofuata nilishaitubu na ugomvi wake na Hamida ulishaisha maana hata yeye alifurahia elimu ya watu wazima niliyoipata huko Kigali niliporudi. Nilikuwa najuwa ‘katerero’ lakini hapa nilipata elimu ya ‘kuyanza’, sijui hata kama nimepatia inavyoandikwa. Ni hatari sana.

Katika kuitumia elimu hii ni muhimu wote muwe na afya njema vinginevyo mtaambukizana maradhi yatokanayo na kujamiiana (ngono). Ni kama vile katerero lakini hii tuseme ni katerero promax. Mtanisamehe, siwezi kuielezea hii hapa kwa sababu ya kuepuka matumizi mabaya ya hii kitu kwa wasiokuwa na ndoa.

“Usiondoke na basi za asubuhi, ondoka saa nne ili upate kupumzika vizuri…” yalikuwa maneno ya Janeth baada ya kumuomba anifundishe kilimo cha umwagiliaji kama kifanywavyo na wanyarwanda.

Nilipata elimu murua, na hakika wana haki ya kuweka sheria ya kila nyumba ya kulala wageni kuwekwe zile foronya zisizopitisha maji. Ewe kijana unayefikiria kuoa Mhaya ama Mnyarwanda, hakikisha unajifunza kilimo cha umwagiliaji maana kwao ni muhimu na haki ya msingi vinginevyo tarajia kutembelewa na kutambulishwa ndugu zake wa kiume usiowajuwa ama kuombwa safari ya kurudi kusalimia mara kwa mara alipotoka ili mradi tu kilimo cha umwagiliaji kifanyike.

Nilikubaliana na wazo lake la mimi kuondoka saa nne asubuhi, hivyo sehemu kubwa ya usiku nilikuwa darasani hadi maji yalipoamua kukatika kabisa, tukalala.

Saa nne na nusu tayari nilikuwa stendi kuu, pale kulikuwa na basi ziendazo Gisenyi, kila baada ya dakika kadhaa basi moja hutoka. Nilipanda RITCO, kampuni yenye huduma bora kabisa Rwanda ambayo baadaye nikaja kujuwa ni mpango mzuri wa viongozi wa Jeshi lao kubuni mradi huo. Safari ilikuwa nzuri na mwendo mzuri kwa sheria za kwao lakini nilikerwa na waendesha baiskeli ambao hushikilia malori kwa nyuma na kupata lifti hatarishi isiyo rasmi.

Kuna sehemu nimeshapasahu, tulipumzika kupata chakula kisha tukaendelea na safari. Yes panaitwa Nyirangarama, nimeona kwenye picha niliyopiga. Njia ni ya milima na mabonde, dereva huko inabidi awe timamu kuweza kuendesha bila kusababisha ajali. Takribani kilomita 150 kutoka Kigali nikaanza kuona ziwa upande wa kushoto, nilipouliza nikaambiwa ni ziwa Kivu, basi lilikuwa linashuka mlima taratibu maana kona ni kali mlima una mwinamo mkali lakini hatimaye tukafika Stendi kuu ya Gisenyi mpakani kabisa na mji wa Goma – Congo, Kivu Kaskazini.

Kwakuwa ilikuwa jioni, sikupenda kuvuka mpaka siku hiyo, bado nilikuwa nina siku mbili za ziada kabla muda wa kuripoti kibaruani. Hivyo niliamua kutafuta sehemu nzuri ya kupumzika. Baada ya kuuliza wenyeji sehemu ya bei nafuu lakini patulivu na usalama mkubwa ndio nikaaelekezwa sehemu Fulani wanapaitwa kwa Mapadri. Nikachukuwa bodaboda hadi huko. Ile sehemu ni kama Msimbazi centre ya Dar es Salaam. Wana rest house nzuri na tulivu sana. Hapo ndipo akili ya kazi ikaanza kurudi upya maana nilitulia na kuanza kutafakari kibarua ninachokiendea.

Ilikuwa siku ya Ijumaa jioni nikiwa hapo kwa Mapadri, nikapata wasaa wa kutembea kwa miguu hadi ufukweni mwa ziwa Kivu sehemu ambapo watu hupenda kutembelea jioni kama vile Coco beach ya Dar. Hapo uzalendo ukanishinda ikabidi niingie kuogelea na kuchanganyika na wenyeji lakini sehemu ya upande wa watu wazima maana kama vile watu walijigawa, hapo nikakutana na visu vingine hatari. Pia kulikuwa na boti kadhaa za wajasiri-amali ambao walikuwa wanapiga debe ili wapate wateja wa kuwatembeza ziwani kwa ujira wa fulani (dola 10).

Siku yangu iliisha vizuri na giza lilipoingia nilitembea kurudi kiotani kwangu hapo kwa Mapadri. Baada ya chakula cha jioni ambacho nilikipata jirani na hapo kwa Mampadri nilirudi chumbani na kuendelea kuandika simulizi ya Hamida nikisogeza ‘episode’ kuwapunguzia arosto wafuatiliaji wa kila siku mwaka huo. Baadaye nikaanza kupitia yanayohusu kinachonipeleka Goma kwa kuhakikisha nimehabarika ipasavyo kufikia tarehe ya siku hiyo.


INAENDELEA…
Simulizi murua hasa..
Big up mleta mada
 
Nimemaliza kusoma yote mkuu, hakika story ni tamu sana, hua napenda sana vituko vya wakongo...
Kuna safari Moja nilienda Kahama kutoka Dar na kwenye siti nilikaa na Mama wa Kikongo aisee nilijifunza vingi sana...
 
Ushawahi kuwaza kurudi kwenye Ukristo?
Hapana

Watawala za zamani kwa ulafi wa madaraka wametugawa pasipo sababu

Mwenyezi Mungu ni mmoja,
Mitume na manabii wake ni walewale

(Siongelei hawa wa mwendo kasi)

Muhimu ni kumcha Mungu katika ukweli wa kumcha.

Migawanyiko iliyotokea haikupeleki popote kama siyo mcha Mungu.
 
Picha ni kwa hisani ya google, hazina uhusiano wa moja kwa moja na simulizi wala majina katika hizo picha si yenyewe.
Ni bora umesema ukweli,sio Mzee wa Khumbu konda Msafi alivyotupiga kamba ila wabongo wakamuumbua mapema sana kabla jogoo hajawika
 
Lima kwa kumwagilia, hakikisha tu Shamba ama bustani ni yako.
 

Attachments

  • watering3.jpg
    watering3.jpg
    62.6 KB · Views: 51
  • watering2.jpeg
    watering2.jpeg
    13.8 KB · Views: 52
Back
Top Bottom