Hekaya za Abuuwasi na hadithi zingine

Hekaya za Abuuwasi na hadithi zingine

MTEGO WA PANYA HUINGIA WALIOKUWAMO NA WASIOKUWAMO​


Palikuwa mtu na mkewe, Ndani ya nyumba yao walikuwamo panya wengi sana wakiharibu vitu, na kutoboa makanda ya
Mtama. Hata yule bwana wa nyumba akatafuta mtego akaenda ghalani akatega. Hatimye akapita panya akauona ale mtego akatambua kuwa mtego huu ametegewa yeye. Akapita jogoo panya akamwambia jogoo, "Wewe mwenzangu mkubwa kuliko, mimi hufanyi jamala ukaupiga teke huu mtego ufyatuke?"
jogoo akamwambia, "Mtego huu umetegewa wewe, mimi haunihusu kitu."
Panya akanena, "Kweli, lakini nauona umekaa vibaya wasije wakaingia waliomo na wasiokuwamo."
Jogoo akanena, "Najuaje?" akaenda zake.
Mara akapita mbuzi. Panya akamwambia mbuzi, "Bwana mdogo, hufanyi taratibu akaufyatua huu mtego na mimi nikapata riziki?"
Mbuzi akamwambia, "Mimi na mtego tu wapi? Mtego huu umetegewa wewe unayeharibu vitu vya watu, mimi chakula changu majani."
Panya akanena, "Kweli huu ni mtego wa panya, lakini tena ni mtego wa kuingia waliomo na ‘wasiokuwamo."
Mbizi akanena, "Mimi sijui hayo, akaondoka akaenda zake.
Hatimaye akapita ng’ombe. Panya akamwambia, "Ee Bwana mkubwa, tafadhali ufyatue huu mtego, na mimi nikapata riziki, tena nauona umekaa vibaya, wasije wakaingia waliomo na wasiokuwamo."
Ng’ombe akanena, "Hayo ni mambo yako wewe unayetoboa vya watu: mimi nakula majani, na mtama wapendapo kunipa. Sina haja kujishughalisha na mambo yasiyonihusu." Akaondoka akaenda zake. Na panya naye akaenda zake. Akawahubiria wenziwe kuwa ghalani kuna mtego wa kuwanasa.
Mara akapita nyoka naye anawinda panya, akapita njia ya mtego akanaswa. Yule mwenye nyumba aliposikia ukifyatuka akachukua fimbo akaenda ghalani. Mkewe akamwambia, "Bwana, huchukui taa?"
Akanena, "Kuna kuua panya kukahitaji taa?" Alipoufikia mtego kwa ile fimbo yake yule nyoka akamwuma. Yule bwana akasema, "Ah kaniuma ati!" Mkewe akaleta taa kumulika akasema, "si panya, bwana, ni nyoka."
Yule bwana akawa hoi, hoi tena maumivu yamemshika.
Huku na huku wakaitwa jamaa zake, wasidiriki kuja wote, akafa. Basi wakaja watu wachache usiku, ili kuwaliwaza wafiwa. Akachukuliwa jogoo akachinjwa kitoweo cha wale watu waliolala. Siku ya pili wakaja watu wengi kulala matangani. Akachukuliwa mbuzi akachinjwa kitoweo cha watu wa matangani. Hata siku ya kusoma hitma akachukuliwa ng'ombe akachinjwa, maneno ya panya yakatimia, ni mtego wa panya lakini wakaingia waliokuwamo na wasiokuwamo.
 
MGANGA NA MWANAFUNZI BUBU​



Paliondokea mganga stadi mno wa ajabu. Ikawa katika nchi ile hakuwapo mganga kama yeye. Akafanya mali sana. Na watu kadha wa kadha wakataka wajifunze kazi yake, ila huyu mganga hakutaka mwanafunzi anayesema, ila bubu. Maana yake alijua awezi kueleza neno, na ufundi wake hautakwenda mbali, maana hakutaka ufundi wake uenee, wasije wakafaidika watu wengi kwa chumo. Watu walijaribu kumuomba awafundishe hata kwa mali hakutak. Akaondoka mwanamke mmoja aliyekuwa na mtoto wake mmoja tu. Akamwambia, "Mwanangu, wewe ni mwana yatima, baba yako amekufa, na mimi mwanamke siwezi kukufundisha kazi. Nataka usikilize shauri langu. Ipo kazi kwa yule mganga ukiipata utastarehe wewe na mimi. Lakini ina tofauti moja, hatakiwi mtoto ila bubu. Basi mwanangu nataka ujifanye bubu uende kwa fundi ukanyamaze kimya, ukastahimili yote atakayokutenda."
Mtoto akakubali. Mama yake akamchukua akampeleka mpaka kwa mganga akamwambia, "Nimekuletea mwanafunzi."
Akamuuliza, "Huyu mtoto ni bubu?"
Akanena, "Bubu tangu kuzaliwa."
Akamwambia, "Unaona! Hivyo ndivyo nilivyotaka."
Akampokea yule mtoto, mama yake akaenda zake. Yule mganga akamtwaa yule mtoto akamtandika vema kwa bakora, na mtoto kimya. Maana mganga alijua kuwa kama huyu mtoto ni mwongo, akipigwa atalia, "Mama wee! nakufa."
Alipoona hakulia kwa bakora, akatafuta upupu akamtia. Na mtoto akalia kwa kutoa machozi tu, na kujikuna, lakini neno hakutoa. Mganga akaisha mizungu yote ya kutaka kumsemesha. Hakuweza. Hata mganga akayakini kuwa huyu kweli bubu. Akakaa naye.
Akamsabilia kazi zake zote. Kila anapomfanyizia mgonjwa dawa huyu mtoto sharti awepo. Akimtuma hutumika, akimwuliza neno hajibu ila kwa kichwa na mkono.
Wakakaa katika hali hii siku kadha wa kadha.
Siku moja akaja mtu hawezi kichwa, kutaka kuaguliwa.
Mganga akamtazama, akamwambia, Kichwa chako kimepungua, na ukizidi kukaa katika hali hii utafanya wazimu. Na mimi naweza kukufanyizia dawa lakini sharti nitoboe kichwa chako, nitazame yule mgonjwa akakubali. Mganga akatoboa kichwa, akatazama ndani akaona yuko funza mkubwa mweupe kati ya ubongo.
Akafahamu kuwa huyu ndiye anayeharibu ubongo wake, ikawa fundi kutafuta njia ya kumtoa yule funza. Akatufuta kulabu ili aingize katika ubongo ili akamkamate yule funza amtoe. Yule mwanafunzi akatazama akaona ya kuwa Leo mganga anakosea. Ubongo utiwe kulabu mpaka ndani utaharibika. Lakini kusema hapati maana yeye bubu. Lakini tena akawaza kuwa mimi nikinyamaza hata huyu mtu atiwe kulabu atakufa,
Basi akangoja hata mganga alipokuwa karibu kutia kulabu, Akasema, "Fundi unakosea! Huyo funza ukimto kwa namna hiyo, huo ubongo utazidi kuharibika
Twaa moto uweke karibu na kichwa huyo funza atoke mwenyewe kwa joto!"
Yule mganga alipomsikia mwanafunzi wake kusema, alishangaa, "Ah! Kumbe wewe unasema." Akakasirika sana akataka kumfukuza kabisa. Lakini yule mwanafunzi akasema, "tafadhali ufikiri zaidi. Naliweza kukaa kimya kabisa na kukudanganya siku zote ili nipate faida kwa hila, lakini sikupenda mtu huyu afe, wala sikutaka wewe uadhibiwe kwa kosa lako. Kwa hiyo naliacha hila yangu nikasema."
Mganga akasema, "kweli unayosema," Akamsamehe.
Akazidi kumfundisha uganga wake. Wakawa rafiki tokea siku ile wakafanya kazi pamoja wakasaidiana.
 
KIBURI SI MAUNGWANA​


Aliondokea fundi mhunzi nae akawa hodari sana kwa kazi ya uhunzi. Akapata mwanafunzi mmoja naye akaondoka kuwa hodari sana, hata wakamsifu sana huyu mwanafunzi kuliko fundi wake
Hata yule mwanafunzi akafanya kichwa kikubwa akafanya kiwanda chake, na fundi wake asimjue, ila hupata siku kwa nadra kwenda kumtazama fundi wake napo kwa vishindo na makeke. Hata siku moja alipokwenda mtazama fundi wake, akamkuta kazini anafua. Akamwamkia fundi wake kwa hivyo tu, maana sasa anajiona bora yeye. Fundi wake akamwitikia akamwambia, "Je, baba umekuja kututazama." Akamwambia, "Naam." Hata alipokwisha pumzika, fundi akamwambia mwanafunzi wake, "Baba, njoo mara moja utusaidie kufukuta."
Mwanafunzi akashika mifuo kwa ghasia tupu, akafukuta. Na katika kufukuta akailiza ile mifuo kwa mlio huu:
Hapana jingine, fundi.
Hapana jingine, fundi.
Fundi akaona mwanafunzi wake ametakabari sasa, anathubutu kuja mbele yake, na kunena hakuna fundi mwingine. Akaona mwanafunzi wake anakuja kwa meno ya juu. Hatimaye yule fundi akamwambia mwanafunzi wake, "Sasa njoo wewe unipokee, shika nyundo utengeneze hili fuawe." Basi yule mwanafunzi akatwaa nyundo, akashika kufua lile fuawe. Fundi akashika mifuo. Akafukuta kwa taratibu. Naye akailiza mifuo yake hivi:
Jingi liko wee, fundi.
Jingi liko wee, fundi.
Maana yake usiseme hapana fundi jingine, liko fundi jingine.
Wakafanya kazi yao wakaisha. Yule mwanafunzi akaenda zake. Sifa zake yule mwanafunzi zikawa zinavuma kama ngoma, hata zikafika kwa Sultani. Sultani akamwita akamwambia, "Nasikia wewe fundi mkubwa wala hapana kazi inayokushinda katika uhunzi."
Akamwambia, "Naam."
Basi Sultani akamwambia, "Nataka unifulie mtu, umtie na roho Yake, na kama huwezi si fundi kitu, nitakuua."
Yule fundi akashughulika, akili zikamduru. ikatazamwa katika ramli, ikaonekana ya kuwa ametendewa na fundi wake. Yule mwanafunzi akaondoka akaenda kwa fundi wake, akamuangukia. Fundi wake akampokea. Akamweleza ile habari iliyompata. Fundi akamfundisha maarifa mwanafunzi wake. Akamwambia, "Nenda kwa Sultani ukamwambie kazi yake uliyonituma, Maulana, nimesikia, nimeimekubali, lakini nimetindikia kitu kimoja. Haiwi ila unipatie makaa ya mgomba.
Sultani akaagiza watu wakusanye migomba wakaichoma moto wasipate makaa. Sultani akashindwa. Yule fundi akapona asiuawe.
Kisha fundi akamwambia mwanafunzi wake, "Je’ baba fundi jingine lipo halipo?"
Akanena, "Lipo. Akakaa kwa heshima na adabu."
 
KIBURI SI MAUNGWANA​


Aliondokea fundi mhunzi nae akawa hodari sana kwa kazi ya uhunzi. Akapata mwanafunzi mmoja naye akaondoka kuwa hodari sana, hata wakamsifu sana huyu mwanafunzi kuliko fundi wake
Hata yule mwanafunzi akafanya kichwa kikubwa akafanya kiwanda chake, na fundi wake asimjue, ila hupata siku kwa nadra kwenda kumtazama fundi wake napo kwa vishindo na makeke. Hata siku moja alipokwenda mtazama fundi wake, akamkuta kazini anafua. Akamwamkia fundi wake kwa hivyo tu, maana sasa anajiona bora yeye. Fundi wake akamwitikia akamwambia, "Je, baba umekuja kututazama." Akamwambia, "Naam." Hata alipokwisha pumzika, fundi akamwambia mwanafunzi wake, "Baba, njoo mara moja utusaidie kufukuta."
Mwanafunzi akashika mifuo kwa ghasia tupu, akafukuta. Na katika kufukuta akailiza ile mifuo kwa mlio huu:
Hapana jingine, fundi.
Hapana jingine, fundi.
Fundi akaona mwanafunzi wake ametakabari sasa, anathubutu kuja mbele yake, na kunena hakuna fundi mwingine. Akaona mwanafunzi wake anakuja kwa meno ya juu. Hatimaye yule fundi akamwambia mwanafunzi wake, "Sasa njoo wewe unipokee, shika nyundo utengeneze hili fuawe." Basi yule mwanafunzi akatwaa nyundo, akashika kufua lile fuawe. Fundi akashika mifuo. Akafukuta kwa taratibu. Naye akailiza mifuo yake hivi:
Jingi liko wee, fundi.
Jingi liko wee, fundi.
Maana yake usiseme hapana fundi jingine, liko fundi jingine.
Wakafanya kazi yao wakaisha. Yule mwanafunzi akaenda zake. Sifa zake yule mwanafunzi zikawa zinavuma kama ngoma, hata zikafika kwa Sultani. Sultani akamwita akamwambia, "Nasikia wewe fundi mkubwa wala hapana kazi inayokushinda katika uhunzi."
Akamwambia, "Naam."
Basi Sultani akamwambia, "Nataka unifulie mtu, umtie na roho Yake, na kama huwezi si fundi kitu, nitakuua."
Yule fundi akashughulika, akili zikamduru. ikatazamwa katika ramli, ikaonekana ya kuwa ametendewa na fundi wake. Yule mwanafunzi akaondoka akaenda kwa fundi wake, akamuangukia. Fundi wake akampokea. Akamweleza ile habari iliyompata. Fundi akamfundisha maarifa mwanafunzi wake. Akamwambia, "Nenda kwa Sultani ukamwambie kazi yake uliyonituma, Maulana, nimesikia, nimeimekubali, lakini nimetindikia kitu kimoja. Haiwi ila unipatie makaa ya mgomba.
Sultani akaagiza watu wakusanye migomba wakaichoma moto wasipate makaa. Sultani akashindwa. Yule fundi akapona asiuawe.
Kisha fundi akamwambia mwanafunzi wake, "Je’ baba fundi jingine lipo halipo?"
Akanena, "Lipo. Akakaa kwa heshima na adabu."
Hiki kitabu ninacho hakichoshi kusoma
 
Hizi hadithi za kizazi chetu........the golden age
Hawa vijana wa siku hizi wanataka kusoma hadithi za ujinga ujinga wa kula tunda mara kula bata huku wakipiga miayo ya njaa kali hata asubuhi hajaiona anaanza kuota tunda na bata....
 
Wengi walisoma hizi hadithi zamani. Ngoja tujikumbushe humu. Pia unaweza kusioma ndani ya maktaba app na vingine zaidi ya 60. Tupm au namba 0715278384 ukitaka kuungwa.


HEKAYA ZA ABUNUWASI NA HADITHI ZINGINE

Bombay; London: Macmillan,1942.
pictuspublishers@gmail.com
Pictuss, 2021





YALIYOMO



kisa cha kwanza
Kisa cha pili
Kisa cha tatu
Kisa cha nne
Kisa cha tano
Kisa cha sita
Kisa cha saba
Kisa cha nane
Kisa cha tisa
Kisa cha kumi
Kisa cha kumi na moja
Kisa cha kumi na mbili
Sultani na mvuvi
Sultani na mkwewe
Mvuvi na jin
Kisa cha majuha wawili wanawake
Jogoo na sungura
Kisa cha paka kupenda mekoni
Kisa cha kuku na mwewe
Kisa cha majuha watatu
Simba na sungura
Fikirini na Hemedi
Kisa cha Wadigo
Kisa cha mtu na wanawe
Hadithi ya mtoto wa sultani na wa tajiri
Wezi stadi
Mtego wa panya huingia waliomo na wasiokuwamo
Mganga na mwanafunzi bubu
Kiburi si maungwan
Kisa cha maskini
Hadithi ya bibi mg'indo
Kwanini watu weupe huitwa wazungu
Kisa cha Ali na watoto wa nduguye
Kisa cha sungura na cheche
Wajinga ndiyo waliwao
Mbwa na paka
Njia ya kuvukia mwenye deni
Nyoka na jongoo
Kweli tatu
Ndoto
Mvivu kupita wote ndiye atakayekuwa mfalme
Kisa cha binti Matlai Shems
Muamini Mungu si mtovu
Kasa na kitatange
Hadithi ya chewa
Kisa cha kuku na kanga
Mtoto wa maskini
Mtu aliyesikia lugha za wanyama
Binti Hamadi
Nzuri
 
Back
Top Bottom