Magufuli anatekeleza sera za Chadema .....huyu hafai hela zote anapeleka kwenye miradi, miradi yenyewe hasara tupu! Sasa ndege nani atapanda! Alafu analipa cash, si angekopa tu! Stendi ya mbezi ni ovyo italeta foleni kubwa! Magufuli ni dikteta amekataza siasa! Flyovers zipo Kenya zile za Magufuli hamna kitu!
Haya mzee wa watu kapumzika, shangwe likaibuka, kwisha Mataga, Sukuma gang watakoma! Mama achana na miradi ya Magufuli haina maana! Mama anaupiga mwingi! Mama anafungua uchumi! Sasa nchi inapumua, tuko huru kukosoa na kufanya siasa.
Sasa hivi, tuone mataga na sukuma gang wakisema Mama anaupiga mwingi ni block tu, Mama ni dikteta wa kike! Hata Magufuli hakuwahi kutufungulia mashtaka ya ugaidi! Huyu Mama ndio atakuwa the worst President ever!
Dah! Haya maneno yote yanasemwa na watu wale wale!