Heroin na cocaine zapanda bei

Heroin na cocaine zapanda bei

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,325
Bei ya heroin na cocaine imeogezeka baada vita dhidi ya biashara ya madawa ya kulevya kusababisha upungufu wa madawa hayo. Kwa mujibu wa msaidizi mkuu wa kitengo cha polisi cha kupambana na madawa ya kulevya Godfrey Nzowa, uchunguzi uliowahusisha watumiaji wa madawa hayo umebainisha kuwepo kwa upungufu mkubwa wa heroin na cocaine.

Kilo moja ya cocaine kwa bei ya mtaani imepanda kutoka Sh. milioni 50 hadi milioni 55. Pia bei ya heroin imepanda kutoka Sh. milioni 45 had milioni 50 kwa kilo. Kamanda Nzowa amedai kuwa polisi wako makini zaidi sasa. Hata hivyo, amekiri kuwa kadri vita ya madawa ya kulevya inavyoongezeka, drug dealers nao wanagundua njia mpya za kuendelea kufanya biashara hiyo.

Kamanda Nzowa amesema drug dealers wanatumia makonteina yenye lebo kama "Original Coffee" na "Sugar" na wakati mwingine hata chupa zilizoandikwa pure water. Amesema kwa sasa madawa mengi ya heroin na cocaine yanasafirishwa kwa njia ya maji, na kudai polisi watageuza kila jiwe. Aidha kamanda Nzowa amesema kuwa kuanzia Januari 2013 jumla ya kilo 32 za heroin zimekamatwa, huku watu 44 wakihusishwa na biashara ya madawa hayo. Pia polisi ilifanikiwa kukamata kilo 4 za cocaine na kumatata jumla ya watuhumiwa 18.

Kamanda Nzowa ameongeza kuwa polisi imemwita na kuhoji mbunge wa Kinondoni Mh. Idd Azan kuhusiana tuhuma zinazoendelea kuwa amekuwa akijihusisha na biashara ya madawa ya kulevya. Amesema uchunguzi wa tuhuma hizo bado unaendelea.

Ziara ya ghafla ya Dkt. Mwakyembe

Wakati huo huo, Waziri wa uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe jana alifanya ziara ya ghafla katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kunako mida ya saa kumi za alfajiri. Katika ziara hiyo, alitembelea vitengo mbalimbali kikiwemo cha ukaguzi wa mizigo na abiria na kitengo cha kamera, ambako hivi karibuni kulipitia dawa za kulevya za mabilioni na kukamatwa Afrika ya Kusini.

Dkt Mwakyembe aliona hali ya ukaguzi katika eneo hilo ilivyokuwa na kubaini kuwa dawa hizo zilionekana katika mzigo lakini kulikuwa na uzembe au njama zilizotokana na maafisa waliokuwa wakikagua. Dkt Mwakyembe alipita katika eneo hilo, ambalo lilikuwa na afisa wa polisi, ambapo alielezwa kuwa siku hiyo mbwa wanaotumika kubaini dawa hizo, walicheleweshwa kufika. Kwa mujibu wa IGP Said Mwema, polisi inamshikilia mtuhumiwa mmoja kuhusiana upitishwaji wa madawa hayo.

Awali wiki hii akitoa ahadi ya kukabilina na biashara ya madawa ya kulevya, Dkt. Mwakyembe amesema kuwa atapambamba kufa na kupona dhidi ya uingizaji wa madawa hayo kupitia kiwanja hapo. "Najitoa mhanga dhidi ya biashara hivyo na siogopi vitisho vya watu, maana nilishakufa siku nyingi, hatuwezi kudhalilisha nchi yetu kiasi hicho," alisema Dkt Mwakyembe.

"Dawa za kulevya sasa zinasafirishwa kupitia kiwanja cha ndege, ambacho kimepewa jina la mtu muhimu katika nchi yetu, Mwalimu Nyerere, ni aibu kwa nchi yetu na Taifa letu, kuona uwanja huo unatumika kwa biashara hiyo, nipeni muda, mimi ndiye Waziri wa Uchukuzi, hatutakubali hali hii," alisema na kuongeza: "Pale uwanjani kuna ofisi nne, Polisi, Uhamiaji, Usalama wa Taifa na watu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, wote nimewaagiza wanipe taarifa, walikuwa wanafanya nini hadi dawa hizo zinapita uwanjani hapo?"

Wakati huo huo na kufuatia ziara ya ghafla ya Dtk. Mwakyembe kiwanjani hapo, Mkurugenzi wa kiwanja hicho, Ndugu Moses Mlaki amesema kuwa kumekuwa na ushirikiano kati ya waendeshaji wa mashine za uwanjani hapo na baadhi ya maafisa wa usalama wa taifa na hivyo kuwezesha madawa ya kulevya kupitishwa kwa urahisi kiwanjani hapo.

Habari kwa mujibu wa Daily News na Habari Leo.
 
hongera Mwakyembe kwa kuthubutu sababu ata mkuu wako wa kazi aliishia kusema tu anawajua vigogo wa dawa za kulevya!
 
I say .... huyo ni BEST SALESMAN of the year. !!
bonge ya ADV wanafagilia biashara.!!
 
Hata sijakuelewa.
Huyo jamaa ni mbunifu kweli (kwa wafanyabiashara wanaojua) kwa kuwa ipo STOCK zaidi nchini wamekwama kuisafirisha nje sasa wanawalenga watumiaji wajiwahi eti kabla haijawa adimu "yaani imepanda bei na kwa baadaye haitopatikana kabisa" So njooni mujilumbukize TIME IS RUNNING OUT unaona hiyo ? hapo maAdicts ndiyo kifo sasa.
Mungu awasidie na awaponye/awaondolee na msiba huu.AMIN
 
Bei ya heroin na cocaine imeogezeka baada vita dhidi ya biashara ya madawa ya kulevya kusababisha upungufu wa madawa hayo. Kwa mujibu wa msaidizi mkuu wa kitengo cha polisi cha kupambana na madawa ya kulevya Godfrey Nzowa, uchunguzi uliowahusisha watumiaji wa madawa hayo umebainisha kuwepo kwa upungufu mkubwa wa heroin na cocaine.

Kilo moja ya cocaine kwa bei ya mtaani imepanda kutoka Sh. milioni 50 hadi milioni 55. Pia bei ya heroin imepanda kutoka Sh. milioni 45 had milioni 50 kwa kilo. Kamanda Nzowa amedai kuwa polisi wako makini zaidi sasa. Hata hivyo, amekiri kuwa kadri vita ya madawa ya kulevya inavyoongezeka, drug dealers nao wanagundua njia mpya za kuendelea kufanya biashara hiyo.

Kamanda Nzowa amesema drug dealers wanatumia makonteina yenye lebo kama "Original Coffee" na "Sugar" na wakati mwingine hata chupa zilizoandikwa pure water. Amesema kwa sasa madawa mengi ya heroin na cocaine yanasafirishwa kwa njia ya maji, na kudai polisi watageuza kila jiwe. Aidha kamanda Nzowa amesema kuwa kuanzia Januari 2013 jumla ya kilo 32 za heroin zimekamatwa, huku watu 44 wakihusishwa na biashara ya madawa hayo. Pia polisi ilifanikiwa kukamata kilo 4 za cocaine na kumatata jumla ya watuhumiwa 18.

Kamanda Nzowa ameongeza kuwa polisi imemwita na kuhoji mbunge wa Kinondoni Mh. Idd Azan kuhusiana tuhuma zinazoendelea kuwa amekuwa akijihusisha na biashara ya madawa ya kulevya. Amesema uchunguzi wa tuhuma hizo bado unaendelea.

Ziara ya ghafla ya Dkt. Mwakyembe

Wakati huo huo, Waziri wa uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe jana alifanya ziara ya ghafla katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kunako mida ya saa kumi za alfajiri. Katika ziara hiyo, alitembelea vitengo mbalimbali kikiwemo cha ukaguzi wa mizigo na abiria na kitengo cha kamera, ambako hivi karibuni kulipitia dawa za kulevya za mabilioni na kukamatwa Afrika ya Kusini.

Dkt Mwakyembe aliona hali ya ukaguzi katika eneo hilo ilivyokuwa na kubaini kuwa dawa hizo zilionekana katika mzigo lakini kulikuwa na uzembe au njama zilizotokana na maafisa waliokuwa wakikagua. Dkt Mwakyembe alipita katika eneo hilo, ambalo lilikuwa na afisa wa polisi, ambapo alielezwa kuwa siku hiyo mbwa wanaotumika kubaini dawa hizo, walicheleweshwa kufika. Kwa mujibu wa IGP Said Mwema, polisi inamshikilia mtuhumiwa mmoja kuhusiana upitishwaji wa madawa hayo.

Awali wiki hii akitoa ahadi ya kukabilina na biashara ya madawa ya kulevya, Dkt. Mwakyembe amesema kuwa atapambamba kufa na kupona dhidi ya uingizaji wa madawa hayo kupitia kiwanja hapo. "Najitoa mhanga dhidi ya biashara hivyo na siogopi vitisho vya watu, maana nilishakufa siku nyingi, hatuwezi kudhalilisha nchi yetu kiasi hicho," alisema Dkt Mwakyembe.

"Dawa za kulevya sasa zinasafirishwa kupitia kiwanja cha ndege, ambacho kimepewa jina la mtu muhimu katika nchi yetu, Mwalimu Nyerere, ni aibu kwa nchi yetu na Taifa letu, kuona uwanja huo unatumika kwa biashara hiyo, nipeni muda, mimi ndiye Waziri wa Uchukuzi, hatutakubali hali hii," alisema na kuongeza: "Pale uwanjani kuna ofisi nne, Polisi, Uhamiaji, Usalama wa Taifa na watu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, wote nimewaagiza wanipe taarifa, walikuwa wanafanya nini hadi dawa hizo zinapita uwanjani hapo?"

Wakati huo huo na kufuatia ziara ya ghafla ya Dtk. Mwakyembe kiwanjani hapo, Mkurugenzi wa kiwanja hicho, Ndugu Moses Mlaki amesema kuwa kumekuwa na ushirikiano kati ya waendeshaji wa mashine za uwanjani hapo na baadhi ya maafisa wa usalama wa taifa na hivyo kuwezesha madawa ya kulevya kupitishwa kwa urahisi kiwanjani hapo.

Habari kwa mujibu wa Daily News na Habari Leo.

.....Kilo moja ya cocaine kwa bei ya mtaani imepanda kutoka Sh. milioni 50 hadi milioni 55. Pia bei ya heroin imepanda kutoka Sh. milioni 45 had milioni 50 kwa kilo.....???????????????????
Hii biashara mbona inaonekana very lucrative hivi
 
Bei ya heroin na cocaine imeogezeka baada vita dhidi ya biashara ya madawa ya kulevya kusababisha upungufu wa madawa hayo. Kwa mujibu wa msaidizi mkuu wa kitengo cha polisi cha kupambana na madawa ya kulevya Godfrey Nzowa, uchunguzi uliowahusisha watumiaji wa madawa hayo umebainisha kuwepo kwa upungufu mkubwa wa heroin na cocaine.

Kilo moja ya cocaine kwa bei ya mtaani imepanda kutoka Sh. milioni 50 hadi milioni 55. Pia bei ya heroin imepanda kutoka Sh. milioni 45 had milioni 50 kwa kilo. Kamanda Nzowa amedai kuwa polisi wako makini zaidi sasa. Hata hivyo, amekiri kuwa kadri vita ya madawa ya kulevya inavyoongezeka, drug dealers nao wanagundua njia mpya za kuendelea kufanya biashara hiyo.

Kamanda Nzowa amesema drug dealers wanatumia makonteina yenye lebo kama “Original Coffee" na “Sugar” na wakati mwingine hata chupa zilizoandikwa pure water. Amesema kwa sasa madawa mengi ya heroin na cocaine yanasafirishwa kwa njia ya maji, na kudai polisi watageuza kila jiwe. Aidha kamanda Nzowa amesema kuwa kuanzia Januari 2013 jumla ya kilo 32 za heroin zimekamatwa, huku watu 44 wakihusishwa na biashara ya madawa hayo. Pia polisi ilifanikiwa kukamata kilo 4 za cocaine na kumatata jumla ya watuhumiwa 18.

Kamanda Nzowa ameongeza kuwa polisi imemwita na kuhoji mbunge wa Kinondoni Mh. Idd Azan kuhusiana tuhuma zinazoendelea kuwa amekuwa akijihusisha na biashara ya madawa ya kulevya. Amesema uchunguzi wa tuhuma hizo bado unaendelea.

Ziara ya ghafla ya Dkt. Mwakyembe

Wakati huo huo, Waziri wa uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe jana alifanya ziara ya ghafla katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kunako mida ya saa kumi za alfajiri. Katika ziara hiyo, alitembelea vitengo mbalimbali kikiwemo cha ukaguzi wa mizigo na abiria na kitengo cha kamera, ambako hivi karibuni kulipitia dawa za kulevya za mabilioni na kukamatwa Afrika ya Kusini.

Dkt Mwakyembe aliona hali ya ukaguzi katika eneo hilo ilivyokuwa na kubaini kuwa dawa hizo zilionekana katika mzigo lakini kulikuwa na uzembe au njama zilizotokana na maafisa waliokuwa wakikagua. Dkt Mwakyembe alipita katika eneo hilo, ambalo lilikuwa na afisa wa polisi, ambapo alielezwa kuwa siku hiyo mbwa wanaotumika kubaini dawa hizo, walicheleweshwa kufika. Kwa mujibu wa IGP Said Mwema, polisi inamshikilia mtuhumiwa mmoja kuhusiana upitishwaji wa madawa hayo.

Awali wiki hii akitoa ahadi ya kukabilina na biashara ya madawa ya kulevya, Dkt. Mwakyembe amesema kuwa atapambamba kufa na kupona dhidi ya uingizaji wa madawa hayo kupitia kiwanja hapo. “Najitoa mhanga dhidi ya biashara hivyo na siogopi vitisho vya watu, maana nilishakufa siku nyingi, hatuwezi kudhalilisha nchi yetu kiasi hicho,” alisema Dkt Mwakyembe.

“Dawa za kulevya sasa zinasafirishwa kupitia kiwanja cha ndege, ambacho kimepewa jina la mtu muhimu katika nchi yetu, Mwalimu Nyerere, ni aibu kwa nchi yetu na Taifa letu, kuona uwanja huo unatumika kwa biashara hiyo, nipeni muda, mimi ndiye Waziri wa Uchukuzi, hatutakubali hali hii,” alisema na kuongeza: “Pale uwanjani kuna ofisi nne, Polisi, Uhamiaji, Usalama wa Taifa na watu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, wote nimewaagiza wanipe taarifa, walikuwa wanafanya nini hadi dawa hizo zinapita uwanjani hapo?”

Wakati huo huo na kufuatia ziara ya ghafla ya Dtk. Mwakyembe kiwanjani hapo, Mkurugenzi wa kiwanja hicho, Ndugu Moses Mlaki amesema kuwa kumekuwa na ushirikiano kati ya waendeshaji wa mashine za uwanjani hapo na baadhi ya maafisa wa usalama wa taifa na hivyo kuwezesha madawa ya kulevya kupitishwa kwa urahisi kiwanjani hapo.

Habari kwa mujibu wa Daily News na Habari Leo.
Hapo kwenye Red nazidi kupata wasiwasi ha hawa tuliowapa dhamana ya kutusaidia kupambana na biashara hii haramu wanajua hadi bei imepanda lakini hatujasikia ni nani waliyemkamata ambaye kwa sasa anauza hiyo Cocain kwa bei hiyo inamaanisha wanawajua wauzaji na wanunuzi pia lakini kuwakamata ndio imekuwa ngumu kwao.

Na kuhusu ule mzigo wa Kg 150 naona wanazidi kutuonyesha usanii unaofanyika hadi sasa naona wamekamatwa watu watatu yaani wale PUNDA 2 na mtumishi 1 wa pale uwanja wa ndege, tunabaki na maswali mengi ya kujiuliza mbona wanakuwa wagumu sana kututajia ule mzigo ulikuwa wa nani wanabaki kudeal na wahusika wadogo huku hao wakubwa ikiwa ni siri kubwa.
 
Dah kumbe ma agent ni mapolisi hawa hawa! Na wanafurahia kupanda bei sasa. Haya bana dawa yenu ni 2015 tu kusanyeni kilichochenu mapema.
 
Serikari ianzishe chombo cha kusimamia bei kama ilivyo kwa mafuta na mazao ya biashara.
 
Huyo jamaa ni mbunifu kweli (kwa wafanyabiashara wanaojua) kwa kuwa ipo STOCK zaidi nchini wamekwama kuisafirisha nje sasa wanawalenga watumiaji wajiwahi eti kabla haijawa adimu "yaani imepanda bei na kwa baadaye haitopatikana kabisa" So njooni mujilumbukize TIME IS RUNNING OUT unaona hiyo ? hapo maAdicts ndiyo kifo sasa.
Mungu awasidie na awaponye/awaondolee na msiba huu.AMIN
u seem to know a lot of insight bout how this dirty busness is oparated in tz...hebu funguka zaidi mkuu.
 
Aiseee....kama kilo ni mil 55...........mtu anatumia kiasi gani na bei ikoje.......? Au gram 1 ni sh ngapi.......?
 
Nililoliwaza na kulisema sasa limethibitika nilisema maneno haya ktk mchango wangu kwenye mada zilizopita.huenda viongozi wetu wakuu tuliowapa dhamana ya kuongoza vita dhidi ya dawa hizi huenda wameishiwa MBINU AU HAWAJUI WANAPAMBANA NA NINI sasa kwa majibu yao haya mbele ya waandishi wa habari naridhika kabisa kuwa WAMESHINDWA wapishe mawazo mapya na timu mpya hata mhMwakyembe namshauri kwenye mamlaka yake aunde timu mpya huku akishauri idara zingine nazo ziunde timu mpya jibu la kupanda bei kwa bidhaa hizo hapa nchini si udhibiti uliofanywa bali ni NCHI IMEGEUKA GULIO la madawa ya kule vya wafanyabiashara toka mataifa mbalimbali wanafuata bidhaa hiyo hapa kwetu kuipeleka ktk mataifa yao na kwingineko hivyo soko la ndani kupungukiwa bidhaa hiyo. Hivyo kitendo cha wageni kufuata madawa hapa ni kuonyesha kuwa yamejaa.
 
Nguvu kazi ya taifa inapotea kwa ubinafsi na tamaa ya pesa kwa ajiri ya watu wachache wenye pesa. Madawa ya kulevya vita yake ni dhaidi ya tuifikiriavyo, maan ahapo kuna upotezaji wa maisha ya wale watao kua against na hii biashara.
 
Bei ya heroin na cocaine imeogezeka baada vita dhidi ya biashara ya madawa ya kulevya kusababisha upungufu wa madawa hayo. Kwa mujibu wa msaidizi mkuu wa kitengo cha polisi cha kupambana na madawa ya kulevya Godfrey Nzowa, uchunguzi uliowahusisha watumiaji wa madawa hayo umebainisha kuwepo kwa upungufu mkubwa wa heroin na cocaine.

Kilo moja ya cocaine kwa bei ya mtaani imepanda kutoka Sh. milioni 50 hadi milioni 55. Pia bei ya heroin imepanda kutoka Sh. milioni 45 had milioni 50 kwa kilo. Kamanda Nzowa amedai kuwa polisi wako makini zaidi sasa. Hata hivyo, amekiri kuwa kadri vita ya madawa ya kulevya inavyoongezeka, drug dealers nao wanagundua njia mpya za kuendelea kufanya biashara hiyo.

Kamanda Nzowa amesema drug dealers wanatumia makonteina yenye lebo kama “Original Coffee" na “Sugar” na wakati mwingine hata chupa zilizoandikwa pure water. Amesema kwa sasa madawa mengi ya heroin na cocaine yanasafirishwa kwa njia ya maji, na kudai polisi watageuza kila jiwe. Aidha kamanda Nzowa amesema kuwa kuanzia Januari 2013 jumla ya kilo 32 za heroin zimekamatwa, huku watu 44 wakihusishwa na biashara ya madawa hayo. Pia polisi ilifanikiwa kukamata kilo 4 za cocaine na kumatata jumla ya watuhumiwa 18.

Kamanda Nzowa ameongeza kuwa polisi imemwita na kuhoji mbunge wa Kinondoni Mh. Idd Azan kuhusiana tuhuma zinazoendelea kuwa amekuwa akijihusisha na biashara ya madawa ya kulevya. Amesema uchunguzi wa tuhuma hizo bado unaendelea.

Ziara ya ghafla ya Dkt. Mwakyembe

Wakati huo huo, Waziri wa uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe jana alifanya ziara ya ghafla katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kunako mida ya saa kumi za alfajiri. Katika ziara hiyo, alitembelea vitengo mbalimbali kikiwemo cha ukaguzi wa mizigo na abiria na kitengo cha kamera, ambako hivi karibuni kulipitia dawa za kulevya za mabilioni na kukamatwa Afrika ya Kusini.

Dkt Mwakyembe aliona hali ya ukaguzi katika eneo hilo ilivyokuwa na kubaini kuwa dawa hizo zilionekana katika mzigo lakini kulikuwa na uzembe au njama zilizotokana na maafisa waliokuwa wakikagua. Dkt Mwakyembe alipita katika eneo hilo, ambalo lilikuwa na afisa wa polisi, ambapo alielezwa kuwa siku hiyo mbwa wanaotumika kubaini dawa hizo, walicheleweshwa kufika. Kwa mujibu wa IGP Said Mwema, polisi inamshikilia mtuhumiwa mmoja kuhusiana upitishwaji wa madawa hayo.

Awali wiki hii akitoa ahadi ya kukabilina na biashara ya madawa ya kulevya, Dkt. Mwakyembe amesema kuwa atapambamba kufa na kupona dhidi ya uingizaji wa madawa hayo kupitia kiwanja hapo. “Najitoa mhanga dhidi ya biashara hivyo na siogopi vitisho vya watu, maana nilishakufa siku nyingi, hatuwezi kudhalilisha nchi yetu kiasi hicho,” alisema Dkt Mwakyembe.

“Dawa za kulevya sasa zinasafirishwa kupitia kiwanja cha ndege, ambacho kimepewa jina la mtu muhimu katika nchi yetu, Mwalimu Nyerere, ni aibu kwa nchi yetu na Taifa letu, kuona uwanja huo unatumika kwa biashara hiyo, nipeni muda, mimi ndiye Waziri wa Uchukuzi, hatutakubali hali hii,” alisema na kuongeza: “Pale uwanjani kuna ofisi nne, Polisi, Uhamiaji, Usalama wa Taifa na watu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, wote nimewaagiza wanipe taarifa, walikuwa wanafanya nini hadi dawa hizo zinapita uwanjani hapo?”

Wakati huo huo na kufuatia ziara ya ghafla ya Dtk. Mwakyembe kiwanjani hapo, Mkurugenzi wa kiwanja hicho, Ndugu Moses Mlaki amesema kuwa kumekuwa na ushirikiano kati ya waendeshaji wa mashine za uwanjani hapo na baadhi ya maafisa wa usalama wa taifa na hivyo kuwezesha madawa ya kulevya kupitishwa kwa urahisi kiwanjani hapo.

Habari kwa mujibu wa Daily News na Habari Leo.

Hii ni NGUVU YA Soko-Punguza upatikanaji (wakati mahitaji hayajabadilika)=kupanda kwa bei! Vita hii ya madawa ya kulevya pamoja na kutafuta wauzaji wakubwa, ni muhimu kubadili mtazamo wa Mateja na wanaotaka kujiunga!

Kamwe hakuna kiuzikacho kama HAKINA Sokp
 
Dk Mwakyembe Ni Wa Tofauti Na Mungu Amsaidie Sana Mana Kina Amna Chifupa Walifyekwa Hata Kabla Hawajatoa Ukweli, Tanzania Mpya Inakuja,Tuiombee.
 
kilo moja milioni 55!
ENH!

Biashara inalipa sana hiyo. Chezea mpaka mama ntilie nao wamejiingiza kwenye hiyo biashara. Chezea mpaka mama ntilie anaweza kujenga nyumba imara na safi kabisa kwa kuuza wali nyama. Shauri yako wewe na "home chocolate" zako.

Biashara ya dawa za kulevya nchini inazidi kuchukua sura mpya ambapo mama ntilie nao hutumika kusambaza dawa hizo kwa wateja. Uchunguzi uliofanywa na gazeti la Mwananchi kwa muda mrefu katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam unaonyesha kuwa biashara hiyo inafanyika katika maeneo ya Tandika, Manzese, Vingunguti, Temeke, Tandale, Mtongani na Keko.

Wanawake hao wamekuwa wakitumia mwanya wa kuuza chakula kama kinga yao, huku biashara yao kubwa ikiwa ni kuuza dawa za kulevya aina ya heroin, bangi na aina nyingine. Mbinu hii mpya ya usambazaji wa dawa za kulevya kwa kutumia wanawake wanaouza vyakula imeelezwa kuwa inawasaidia wahusika wakuu, kuendesha biashara yao kwa ufanisi zaidi.

Uchunguzi umeonyesha kuwa wafanyabiashara wa dawa hizo wameamua kuwatumia mamalishe kutokana na kuwa waaminifu na kuhudumia wateja wengi, hivyo ni vigumu watu kuwashtukia wakiwamo askari polisi. Imebainika kuwa dawa hizo huuzwa kulingana na maeneo, wakati maeneo ya watu wasiokuwa wa uwezo hupimwa kwa kutumia kipimo kidogo zaidi kwa bei ya chini ambayo watumiaji husika huweza kuimudu.

Aidha dawa hizo hufungwa katika mitindo miwili tofauti, ukiwa katika unga wa vidonge na wa kawaida ingawa bei zake hazitofautiani sana. Uchunguzi unaonyesha kuwa vidoge huuzwa vikiwa vizima au vipande, huku unga wa kawaida ukiuzwa kwa kipimo maalumu. Kwa kawaida ‘unga' huo huuzwa kwa Sh 1,000 kwa pointi huku kete moja ikiuzwa kwa Sh 2,000, wakati vidonge, kizima huuzwa kwa Sh 2,000, huku kipande huuzwa kwa Sh 1,000 zikitofautiana kulingana na maeneo.

Gazeti la Mwananchi lilifanikiwa kuongea na baadhi ya wanawake wanaojihusisha na uuzaji wa dawa hizo. Dada mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Asha (28) ambaye siyo jina lake halisi ni muuzaji mkubwa wa dawa hizo. Awali alikuwa akifanya shughuli zake hizo za uuzaji katika maeneo ya Yombo Kilakala, ingawaje hivi sasa amehamia Temeke. "Unajua siku zote dhumuni la kufanya biashara ni kupata faida, hivyo naweza kusema niliingia kwenye biashara hii kwa sababu tu ina faida zaidi kuliko biashara nyingine," anasema.

Awali alikuwa akiuza vyakula huku akifanya biashara hiyo ya kuuza dawa, baadaye akaacha kuuza vyakula akabaki na biashara ya dawa za kulevya. Akielezea namna anavyofanya biashara yake hiyo, Asha anasema kwa kawaida huwa ananunua mkanda ambao unakuwa umefungwa vidoge vidogo vidogo kumi hadi ishirini. Mara nyingi huuza kulingana na mahitaji ya mteja.

"Halafu baada ya kununua hivyo huwa nauza kidogokidogo vidonge hivyo. Kwa kawaida kidoge kimoja huwa nauza kati ya sh 1,000 hadi Sh 2,000. Bei yake hutegemea na mahali unapouzia. Kama unauzia watu waliochoka sana inabidi upaki kidogo kidogo ili kuweza kuliteka soko lao," anasema. "Nimefanya biashara hii kwa muda wa miaka mitatu, lakini ukweli ni kwamba hadi sasa nimefanikiwa kwa kiasi fulani. Nimeweza kujenga nyumba ya kwangu mwenyewe, pia kuhudumia familia yangu. Licha ya kuwa na madhara kwa watu, lakini ukweli ni kuwa biashara ya unga inalipa," anasisitiza.

Abubakari Ismail (33) aliyewahi kutumia dawa za kulevya, ambaye kwa sasa ni kiongozi wa kupambana na dawa hizo kinachofahamika kama Use Ant -Drugs, kilichopo Yombo, wilayani Temeke, anasema kuwa tatizo la wanawake kujihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya linachangia kwa kiasi kikubwa kuzorotesha mapambano dhidi ya dawa hizo hususan kwa vijana.

‘Joseph (17)', siyo jina lake halisi ni kijana aliyekuwa katika matibabu kutokana na matumizi ya dawa za kulevya. Hivi sasa kijana huyu amelazimika kuhama nyumbani kwao kutokana na kumkimbia mama yake mzazi ambaye anajihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya.

Mkurugenzi wa Kituo cha Makangarawe Youth Information Center cha jijini Dar es Salaam, kinachojishughulisha na miradi kadhaa ya vijana ikiwamo mapambano dhidi ya dawa za kulevya kwa vijana, Ismail Mnikite, amesema kitendo cha wanawake kushiriki katika uuzaji wa dawa za kulevya ni tatizo jipya linalochangia kukwamisha juhudi za mapambano hayo.

Chanzo: Mwananchi
 
u seem to know a lot of insight bout how this dirty busness is oparated in tz...hebu funguka zaidi mkuu.
Mkuu Kad' jioni njema, Mpendwa kwa urahisi kabisa nilivyosoma the topic underlines! machale yakani cheza Mmmh, he product siyo common commodity mbona wanaipigia debe? hapo nikajiuliza kweli at this age of mine shida zote tuzipatazo na mifumuko wa bei za maisha hakuna wakutajli. Leo wanakuja wajanja nakujivumishia machafu yao kwetu kwa njia ya Dirty politics. Maana eti kwanza wamedhibiti JNIAirport.. ofcoz hapo tu inaashiria kuwa mizigo imewadodea.... Mkuu hawa jamaa ni hatari sana kwa jamii they don't care... LAKINI mwenyEzzi Mungu ata wa LA'ANI Laana mbaya. AMIN take care and take care for your family members na jirani zako.
 
Biashara inalipa sana hiyo. Chezea mpaka mama ntilie nao wamejiingiza kwenye hiyo biashara. Chezea mpaka mama ntilie anaweza kujenga nyumba imara na safi kabisa kwa kuuza wali nyama. Shauri yako wewe na "home chocolate" zako.

Biashara ya dawa za kulevya nchini inazidi kuchukua sura mpya ambapo mama ntilie nao hutumika kusambaza dawa hizo kwa wateja. Uchunguzi uliofanywa na gazeti la Mwananchi kwa muda mrefu katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam unaonyesha kuwa biashara hiyo inafanyika katika maeneo ya Tandika, Manzese, Vingunguti, Temeke, Tandale, Mtongani na Keko.

Wanawake hao wamekuwa wakitumia mwanya wa kuuza chakula kama kinga yao, huku biashara yao kubwa ikiwa ni kuuza dawa za kulevya aina ya heroin, bangi na aina nyingine. Mbinu hii mpya ya usambazaji wa dawa za kulevya kwa kutumia wanawake wanaouza vyakula imeelezwa kuwa inawasaidia wahusika wakuu, kuendesha biashara yao kwa ufanisi zaidi.

Uchunguzi umeonyesha kuwa wafanyabiashara wa dawa hizo wameamua kuwatumia mamalishe kutokana na kuwa waaminifu na kuhudumia wateja wengi, hivyo ni vigumu watu kuwashtukia wakiwamo askari polisi. Imebainika kuwa dawa hizo huuzwa kulingana na maeneo, wakati maeneo ya watu wasiokuwa wa uwezo hupimwa kwa kutumia kipimo kidogo zaidi kwa bei ya chini ambayo watumiaji husika huweza kuimudu.

Aidha dawa hizo hufungwa katika mitindo miwili tofauti, ukiwa katika unga wa vidonge na wa kawaida ingawa bei zake hazitofautiani sana. Uchunguzi unaonyesha kuwa vidoge huuzwa vikiwa vizima au vipande, huku unga wa kawaida ukiuzwa kwa kipimo maalumu. Kwa kawaida ‘unga' huo huuzwa kwa Sh 1,000 kwa pointi huku kete moja ikiuzwa kwa Sh 2,000, wakati vidonge, kizima huuzwa kwa Sh 2,000, huku kipande huuzwa kwa Sh 1,000 zikitofautiana kulingana na maeneo.

Gazeti la Mwananchi lilifanikiwa kuongea na baadhi ya wanawake wanaojihusisha na uuzaji wa dawa hizo. Dada mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Asha (28) ambaye siyo jina lake halisi ni muuzaji mkubwa wa dawa hizo. Awali alikuwa akifanya shughuli zake hizo za uuzaji katika maeneo ya Yombo Kilakala, ingawaje hivi sasa amehamia Temeke. "Unajua siku zote dhumuni la kufanya biashara ni kupata faida, hivyo naweza kusema niliingia kwenye biashara hii kwa sababu tu ina faida zaidi kuliko biashara nyingine," anasema.

Awali alikuwa akiuza vyakula huku akifanya biashara hiyo ya kuuza dawa, baadaye akaacha kuuza vyakula akabaki na biashara ya dawa za kulevya. Akielezea namna anavyofanya biashara yake hiyo, Asha anasema kwa kawaida huwa ananunua mkanda ambao unakuwa umefungwa vidoge vidogo vidogo kumi hadi ishirini. Mara nyingi huuza kulingana na mahitaji ya mteja.

"Halafu baada ya kununua hivyo huwa nauza kidogokidogo vidonge hivyo. Kwa kawaida kidoge kimoja huwa nauza kati ya sh 1,000 hadi Sh 2,000. Bei yake hutegemea na mahali unapouzia. Kama unauzia watu waliochoka sana inabidi upaki kidogo kidogo ili kuweza kuliteka soko lao," anasema. "Nimefanya biashara hii kwa muda wa miaka mitatu, lakini ukweli ni kwamba hadi sasa nimefanikiwa kwa kiasi fulani. Nimeweza kujenga nyumba ya kwangu mwenyewe, pia kuhudumia familia yangu. Licha ya kuwa na madhara kwa watu, lakini ukweli ni kuwa biashara ya unga inalipa," anasisitiza.

Abubakari Ismail (33) aliyewahi kutumia dawa za kulevya, ambaye kwa sasa ni kiongozi wa kupambana na dawa hizo kinachofahamika kama Use Ant -Drugs, kilichopo Yombo, wilayani Temeke, anasema kuwa tatizo la wanawake kujihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya linachangia kwa kiasi kikubwa kuzorotesha mapambano dhidi ya dawa hizo hususan kwa vijana.

‘Joseph (17)', siyo jina lake halisi ni kijana aliyekuwa katika matibabu kutokana na matumizi ya dawa za kulevya. Hivi sasa kijana huyu amelazimika kuhama nyumbani kwao kutokana na kumkimbia mama yake mzazi ambaye anajihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya.

Mkurugenzi wa Kituo cha Makangarawe Youth Information Center cha jijini Dar es Salaam, kinachojishughulisha na miradi kadhaa ya vijana ikiwamo mapambano dhidi ya dawa za kulevya kwa vijana, Ismail Mnikite, amesema kitendo cha wanawake kushiriki katika uuzaji wa dawa za kulevya ni tatizo jipya linalochangia kukwamisha juhudi za mapambano hayo.

Chanzo: Mwananchi

kwa mtaji huu home made chocolates zangu hazina issue!mwe!
mpk mama ntiz'
 
Back
Top Bottom