Uchaguzi 2020 Hesabu nzuri inachezwa - Wapinzani kupata zaidi ya 50% ya Wabunge

Uchaguzi 2020 Hesabu nzuri inachezwa - Wapinzani kupata zaidi ya 50% ya Wabunge

Tila-lila2

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2019
Posts
652
Reaction score
1,058
Nimempenda sana Membe. Ukweli nakipenda sana Chama changu cha Mapinduzi yaani CCM. Lakini pia sioni ubaya wa upinzani na zaidi Membe kanibadilisha. Nilikuwa nikimpalilia mno Tundu Lissu lakini kwa sasa ni Benard Membe na Tundu Lisu ndiyo wanashindania kura yangu. Ninajua sana kuwa ni kura moja tu lakini najua ina maana kubwa kwenye Uchaguzi

Ubashiri wangu - mlolongo wa wagombea wa CCM ni lazima utawafikisha kwenye ugomvi na kuna wengine watahama. Ninaomba Act Wazalendo msikatae kuwachukua watakaokosa nafasi CCM wakiamua kuja kwenu. Wapeni nafasi. Hata kama ni mwehu au mwizi akija kwenu ilimradi ana uhakika wa kuongezea kura zenu pls msikatae. Kubalini pls pls. Ninavyoona mwelekeo tayari Act Wazalendo na CHADEMA mnaweza kufikisha idadi ya wabunge kwa asilimia 35 mpaka 50 hivi.

Ukishapata idadi hii ya wabunge basi ujue demokrasia katika nchi hii itakuwa imekuwa kubwa sanaaaaa. Ikitokea hivi kwa kweli Benard Membe atakuwa kailetea sana nchi sifa kuwa kuna demokrasia na yeye atakuwa ni bingwa wa demokrasia. Bila BM kwa kweli upinzani ulikuwa bado unasua sua kwani Tundu Lissu na wengine wanaojulikana ni wapinzani wanajulikana tu kuwa ni wapinzani original na wasingebadili sana matokeo. Ujio wa Bernard Membe kambi ya upinzani una maana kubwa sana sana. Nimekupenda bure Membe!

Kinachotakiwa kufanyika ni kufanya mashambulizi makali sana dhidi ya CCM ambao tayri tamaa yao ya madaraka inaonekana wazi. Mtu alikuwa Mkuu wa Mkoa anataka na ubunge - Puuuuuu! Kule Kigamboni mbona Faustine Ndugulile alikuwa bado anafaa tu sana. Namshauri Ndugulile iwapo CCM wanakukata Kigamboni pls usisite kwenda upinzani. Wewe ni mzuri sana. JIAMINI na Makonda hatakushinda kamwe.

Tena mbaya zaidi kesi dhidi ya Makonda kuhusu vyeti vyake sasa itaiubuka wakati huu itakapotokea kapewa ushindi wa ubunge. Akumbuke kesi ya Kihiyo - linakuja hilo mwaka huu. Makonda anaenda kujiexpose vibaya sana na tena ninafurahia sana nilivyoona kachukua Fomu. Wanasheria wanamsubiria kwa hamu.

Hivyo vivyo hata majimbo mengine wanayoenda kuchukua waliokuwa vigogo wa Serikali kama akina Kabudi, Kitila Mkumbo, Dkt Mpango, Ndalichako, Tulia n.k kuna uwezekano mkubwa sana yatapotelea kwa wapinzani. Kwangu mimi MCCM ninayependa ushindani wa kidemokrasia ambao unaleta maendeleo itakuwa furaha sana sana. Hapo Serikali itakumbuka kupandisha mishahara, kujali uhai wa binadamu, uhuru wa kujieleza na kuacha kuongoza kwa ubabe.

HIMA HIMA WAPINZANI - tupunguzieni makali ya Baba MEKO huyu! Laaahh tumechoka dakeki!
 
Naunga mkono hoja ,CCM wakivurugana huko wakija CHADEMA na ACT wachukuliwe tu lengo ni kuongeza mtaji....Hata Maalim alikuwa CCM , Lema mwenyewe alikuwa TLP kwahiyo tusiwanyanyapae wakija kuongeza nguvu!! Iron Lady Bulaya katoka CCM lakini ana msimamo KONKI.
 
Tulia mkuu hii ngoma bado mbichi!
Tulia ujionee, hata hivyo hata mimi natamani wapinzani wapate angalau viti 10 ili wabunge wa ccm na selikali isilale usingizi

Sent from my SM-T585 using JamiiForums mobile app
Wapinzani wanaviti karibia 130 humo bungeni na bado serikali imekufa hao 10 watakuwa na impact gani kwa serikali mfu?
 
Naunga mkono hoja ,CCM wakivurugana huko wakija CHADEMA na ACT wachukuliwe tu lengo ni kuongeza mtaji....Hata Maalim alikuwa CCM , Lema mwenyewe alikuwa TLP kwahiyo tusiwanyanyapae wakija kuongeza nguvu!! Iron Lady Bulaya katoka CCM lakini ana msimamo KONKI.
Na baadaye wakiunga juhudi msije humu kuwaita wasaliti
 
Meona eee?
Kabisa mkuu hao wachache waliounga mkono juhudi kama wasitutoe kwenye reli ,ujio wa ccm upinzani kipindi cha uchaguzi ni mtaji sana kwenye kampeni na wanaongeza kura sana!! CCM wanalijua hilo na ndio maana wanaeneza propaganda kwamba upinzani hawajajifunza sijui uchaguzi wa 2015 bila kutaja faida waliopata upinzani kujiunga watu waliotoka ccm.
 
Inaonekana hii tabia ya upinzani kupokea watu toka CCM dakika za mwisho na kuwapa nafasi haitakwisha hivi karibuni, ipo kwenye akili za watu na imeshakuwa sehemu ya maisha yao.
 
Inaonekana hii tabia ya upinzani kupokea watu toka CCM dakika za mwisho na kuwapa nafasi haitakwisha hivi karibuni, ipo kwenye akili za watu na imeshakuwa sehemu ya maisha yao.
Sawa tu na CCM. Kwani akina Silinde na Lijualikali si wameenda juzi tu!
 
Huwa najiuliza, hivi Mkwere ameshindwa kumshawishi BM kutulia ama kuomba radhi akarudi CCM? Na urafiki wote ule waliokuwa nao? Mkwere si alikuwa bingwa wa diplomacy yule? Ameshindwa kumshawishi Membe kweli? Kweli kabisaaa????? Wanapanga nini hawa?
 

Attachments

  • 5CBA835E-C7FD-4BF4-8995-1ED82AE9B567.jpeg
    5CBA835E-C7FD-4BF4-8995-1ED82AE9B567.jpeg
    24.8 KB · Views: 1
Huwa najiuliza, hivi Mkwere ameshindwa kumshawishi BM kutulia ama kuomba radhi akarudi CCM? Na urafiki wote ule waliokuwa nao? Mkwere si alikuwa bingwa wa diplomacy yule? Ameshindwa kumshawishi Membe kweli? Kweli kabisaaa????? Wanapanga nini hawa?
Amshauri nini sasa! Mtu wa Pwani hataki kusikia kushindwa na Msukuma kamwe!
 
Inaonekana hii tabia ya upinzani kupokea watu toka CCM dakika za mwisho na kuwapa nafasi haitakwisha hivi karibuni, ipo kwenye akili za watu na imeshakuwa sehemu ya maisha yao.

Bila hivyo unafikiri itakuwaje, kumbuka majimbo kibao tu upinzani wamaekosa watia-nia wenye sifa.... majimbo mengi tu.
 
...Ukweli nakipenda sana Chama changu cha Mapinduzi yaani CCM....Nilikuwa nikimpalilia mno Tundu Lissu lakini kwa sasa ni Benard Membe na Tundu Lisu ndiyo wanashindania kura yangu...
Yaaani "unampalilia mno Lisu" huku unajifanya kujitwika uchama wa CCM. Hata aibu huoni kamanda?
 
Back
Top Bottom