Hesabu ya dereva wa daladala Baada ya nauli kupanda

Tabutupu

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2010
Posts
13,206
Reaction score
18,549
Naomba kujua kama hesabu ya siku ya dereva wa daladala has Dar, inatakiwa ipande kwa kiasi gani ?

Kwa sababu vipuri vimepanda bei sana .

Nina daladala 3 zinatoka buza hadi mnazi mmoja na kwa siku nakusanya 75000 kwa kila daladala, Niongeze kiasi gani kwa haya mabadiriko ya nauli yalitangazwa .
 
Nauli kutoka 500 hadi 700 ni ongezeko la 40%

Kama na wewe unataka kuongeza unaweza kuongeza kwa hizohizo 40% za pato la awali au chini ya hapo kulingana na bei ya za mafuta kupanda

Mfano ongezeko la nauli kwa %
(new value − original value) ÷ original value × 100 = Percentage increase

(700-500)
°°°°°°°°°°°° × 100 = 40%
500

Mfano ongezeko la mapato kwa 40%
75,000 + (75,000 ×40%)
75,000 + 30,000
105,000 pato jipya baada ya kuongeza 40%

Niwewe tu Unaweza kuongeza 20% au 30% kwa kuzingatia gharama za mafuta au 40% ambayo ni sawa na ongezeko la nauli bila kuzingatia Gharama za mafuta

Nimejaribu kwa elimu yangu ya QT
 
700-550=150

150/550 x 100%= 27%

Ongezeko la asilimia 27 %
27% ya 75000 ni 20000

So 75000+20000=95,000/-

Makadirio ni 95,000/-

Mbona hujaweka (hujatoa) fuel inflation au mwenye gari ndiye anaweka mafuta?
Kwa kipindi kifupi tu nimeona mafuta yakipanda bei karibia kila mwezi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…