Hidden cancer cures

Hidden cancer cures

Daaaaaaaa, hii sasa hatari sana. Nina mgonjwa wa kansa ya ini, huu uzi umeniliza sana. Nimelia kwa uchungu mno. Siwezi kufuta machozi kuanzia mwanzo naanza kuusoma hadi mwisho

Ameandikiwa chemo wiki ijayo. Naomba mkuu Deception na Napoteza munisaidie sana kwa hii kadhia. Jamaa bado yupo fresh anatembea ila amedhofu kidogo ila bado yupo strong. My contacts 0652989109/0684043500
Mkuu Danga habari ya siku,,vp maendeleo ya ndg.yetu uliyesema anasumbuliwa na cancer,,kama hutojali tupe feedback.!
 
Mr Deception ningependa kujifunza zaidi, kuna aina tofauti za Saratani, possibly, njia ya utokeaji au ukuaji wa hizo cancerous cells ni tofauti ikitegemea sehemu ambayo saratani hiyo itatokea, hapa chini na "paste" aina hizo za Saratani. Je zote hizo zitatibiwa au (kukingwa) na aina 21+ ya vyakula/items ulizoziorodhesha? Pia kuna watu ambao huweza kuwa katika stage 3 au 4 ya ugonjwa, wengine wakiwa "malformed" kabisa, mechanism ipi ya hizi food au treatment items ulizoorodhesha itasababisha kwa mfano mtu ambaye seli za saratani iliyokula matiti yake ziweze kuondoka na yeye kupona (simaanishi matiti kurejea kwa yule ambaye yameliwa kabisa, bali kupona tu vidonda).


  • Adrenal Cancer
  • Anal Cancer
  • Bile Duct Cancer
  • Bladder Cancer
  • Bone Cancer
  • Brain/CNS Tumors In Adults
  • Brain/CNS Tumors In Children
  • Breast Cancer
  • Breast Cancer In Men
  • Cancer in Adolescents
  • Cancer in Children
  • Cancer in Young Adults
  • Cancer of Unknown Primary
  • Castleman Disease
  • Cervical Cancer
  • Colon/Rectum Cancer
  • Endometrial Cancer
  • Esophagus Cancer
  • Ewing Family Of Tumors
  • Eye Cancer
  • Gallbladder Cancer
  • Gastrointestinal Carcinoid Tumors
  • Gastrointestinal Stromal Tumor (GIST)
  • Gestational Trophoblastic Disease
  • Hodgkin Disease
  • Kaposi Sarcoma
  • Kidney Cancer
  • Laryngeal and Hypopharyngeal Cancer
  • Leukemia
  • Leukemia - Acute Lymphocytic (ALL) in Adults
  • Leukemia - Acute Myeloid (AML)
  • Leukemia - Chronic Lymphocytic (CLL)
  • Leukemia - Chronic Myeloid (CML)
  • Leukemia - Chronic Myelomonocytic (CMML)
  • Leukemia in Children
  • Liver Cancer
  • Lung Cancer
  • Lung Cancer - Non-Small Cell

  • Lung Cancer - Small Cell
  • Lung Carcinoid Tumor
  • Lymphoma
  • Lymphoma of the Skin
  • Malignant Mesothelioma
  • Multiple Myeloma
  • Myelodysplastic Syndrome
  • Nasal Cavity and Paranasal Sinus Cancer
  • Nasopharyngeal Cancer
  • Neuroblastoma
  • Non-Hodgkin Lymphoma
  • Non-Hodgkin Lymphoma In Children
  • Oral Cavity and Oropharyngeal Cancer
  • Osteosarcoma
  • Ovarian Cancer
  • Pancreatic Cancer
  • Penile Cancer
  • Pituitary Tumors
  • Prostate Cancer
  • Retinoblastoma
  • Rhabdomyosarcoma
  • Salivary Gland Cancer
  • Sarcoma - Adult Soft Tissue Cancer
  • Skin Cancer
  • Skin Cancer - Basal and Squamous Cell
  • Skin Cancer - Melanoma
  • Skin Cancer - Merkel Cell
  • Small Intestine Cancer
  • Stomach Cancer
  • Testicular Cancer
  • Thymus Cancer
  • Thyroid Cancer
  • Uterine Sarcoma
  • Vaginal Cancer
  • Vulvar Cancer
Daah magonjwa yote haya? Tutapona kweli?
 
Mkuu hapo kwenye maandishi mekundu nisaidie dawa za asili zinazoweza kumaliza hilo tatizo sababu Uric Acid imekuwa tatizo kwangu kwa muda mrefu

Sent from my SM-G903F using JamiiForums mobile app
Pole sana ndugu. Ntapenda kujibu au kuchangia kwenye hilo though ulimuuliza mdau mwingine. Pia nijibu kwa uelewa wa tatizo nnalolijua mm yaani kuwa na acid nyingi tumboni naamini hili ndio tatizo lako. Kwa kifupi tatizo hilo hutibiwa na kumalizwa kabisa na limao.

Tumia dozi ya limao moja kila siku asubuh kabla ya kula kitu chochote itasaidia kubalance PH ya mwil wako kwa kuongeza alkaline. Hii pia itakusaidia kupunguza uwezekana wa kushambuliwa na cancer kwani cancer inakaa kwenye mwil wenye acid nyingi.
 
Cancer is a condition/disease characterized by abnormal uncontrolled cell growth in the body. Most cancer related deaths are due to metastasis, malignant cells penetrates through circulatory system and establish colonies/tumor in other parts of the body. If abnormal cells grow in a limited area, are called benign tumors, if abnormal cells spread to other parts of the body, they constitute a malignant tumor one that is cancerous...
Namba 12 inatumikaje kama tiba? Msaada tafadhali wadau wasaidie wagonjwa lakini pia waongeze kipato.
 
Kumbuka kwamba mbegu yake ndio tiba yenyewe angalau tunda lenyewe ni muhimu pia.Wenzako wakitupa mbegu,wewe waelimishe kwamba mbegu ni muhimu,wakidharau,wewe zikusanye mbegu hizo kwa matumizi yako.
Mbegu zake ni ngumu balaa
Unazipasuaje
 
Wakuu huu uzi ni mtamu sana

Watu wa medicine wana kazi ya kufanya mapinduzi kwenye industry yao
 
Mambo ya msingi yanayoweza kusababisha cancer mwilini:

Kwanza kabisa inabidi watu wafahamu kwamba,kila mtu mwili wake unajiponya cancer kila siku katika maisha yake,yaani namaanisha kwamba kila mtu hupata cancer kila siku lakini mwili wake hujiponya kila siku.Hii inatokana na uimara wa kinga ya mtu.

Hivyo basi,ukiona mtu amepata cancer inabidi ufahamu kwanza kabisa kwamba kinga ya mtu huyo ina matatizo,halafu pili ndio unatakiwa kuanza kudadisi mambo yaliyoingia ndani ya mwili wake ambayo kinga yake imeshindwa kuyazuia na hatimaye kumsababishia cancer.

Hivyo basi,mpaka hapo tunaweza kutenga sababu zinazosababisha cancer kwenye makundi mawili ili kurahisisha kuelewa vizuri.Kwanza ni kinga ya ndani ya mwili,na pili ni sababu zitokazo nje ya mwili ambazo huingia ndani ya mwili na kushindwa kuzuiwa na kinga ya mwili na hatimaye kusababisha cancer.

1. Kinga ya mwili:

Mwili unapopata cancer hujiponya wenyewe kwa kutumia kimengenyo cha protini kinachotolewa na kongosho/pancreas kiitwacho trypsin kikishirikiana na chembe nyeupe za damu kufanya kazi hiyo.Chembe nyeupe za damu hazina uwezo zenyewe kushambulia chembe za cancer kwa kuwa zenyewe ni chaji hasi(-ve) pia chembe za cancer ni chaji hasi(-ve) hivyo hukwepana,sasa basi, kazi ya kimeng'enyo cha trypsin ni kumeng'enya ukuta wa nje wa chembe za cancer ambao ni wa protini na una chaji hasi(-ve) na baada ya chembe za cancer kumengenywa huwa zinaachwa uchi na kushambuliwa kwa urahisi na chembe nyeupe za damu.Hivi ndivyo mwili unavyojiponya cancer kila siku.

Kwa watu ambao kongosho zao hazifanyi kazi sawasawa na wanaishi maisha hatarishi huweza kupata cancer kwa urahisi sana.

2.Sababu zitokazo nje ya mwili:

Pamoja na kinga ya mwili kufanya kazi kama nilivyoeleza hapo juu,lakini pia si njia pekee ya kuzuia cancer,hii ni kwa sababu kuna mambo mengi mwilini ambayo yanatakiwa yawe kwenye mlinganyo unaotakiwa kiasilia ili mwili wote uweze kufanya kazi kwa kutegemeana.

Mambo haya ni kama vile;

i/. Kiwango cha tindikali/nyongo(alkali) kwenye damu(blood alkalinity level) ambayo inatakiwa iwe 7.365,
ii/. Mwili unatakiwa uwe na kiwango thabiti cha methly group/HCL tumboni,yaani kiwango kizuri cha tindikali ya HCL kwenye tumbo.Methyl groups husaidia kushikilia maji kwenye utumbo nk,inabidi watu wafahamu kwamba zaidi ya 90% ya afya ya mwili huanzia kwenye utumbo,
iii/. Mwili unatakiwa uwe na vitamini zote muhimu,
iv/. Mwili unatakiwa uwe na madini yote muhimu,
na mambo mengine machache.

Hutakiwi kuogopa kwa kuona kwamba unatakiwa ufanye mambo mengi sana,la hasha,bali mambo yote hayo unaweza kuyakamilisha kwa kufanya vitu vichache sana.

Sasa basi mwili unaweza kuwa na mapungufu katika mambo hayo i-iv kutokana na utaratibu mbovu wa maisha na hasa ule wa kula vitu visivyofaa.Ukila vyakula BORA vya ASILI kwenye mlinganyo unaotakiwa,mwili wako utaondokana na mapungufu ya vitu hivyo nilivyovitaja.

Ulaji wa vyakula vya viwandani/processed foods/enriched foods kama vile white sugar,white flour/sembe,white rice,white salt/chumvi ile ya unga,cornfalkes,KFC foods,vinywaji kama vile soda na juisi zilizosindikwa.Pia ulaji wa mara kwa mara wa vyakula kama vile nyama nyekundu,vyakula visivyooshwa vizuri kutoa sumu za mashambani(pesticides) na pombe kali/zisizo na viwango mara kwa mara,madawa ya hospitali mara kwa mara na mambo mengine kama hayo yanayokiuka asili ya mwanadamu yanaweza kutoa mchango mkubwa sana kusababisha cancer.

Ulaji wa vitu hivyo unaweza kukufanya uwe na tindikali nyingi kwenye damu kitu ambacho ni hatari sana.Uwiano mzuri wa tindikali/nyongo kwenye damu ndio kitu cha msingi sana kukiangalia,wagonjwa wote wa cancer ukiwapima damu zao utaona kwamba damu zao zina tindikali nyingi kuliko kiwango cha kawaida.Hivyo basi,ukiwa na tindikali nyigi kuliko kawaida kwenye damu utapoteza madini mengi muhimu kama vile calcium,magnesium na madini mengine muhimu madogo madogo ambayo yote hayo yana umuhimu mkubwa wa kupigana na cancer,pia ini haliwezi kufanya kazi yake vizuri katika hali ya tindikali nyingi,hali hii pia huweza kuathiri kongosho kushindwa kufanya kazi yake ipasavyo.Hivyo ulaji huu mbovu utakufanya uangukie kwenye matatizo namba i hadi namba iv hapo juu.
Hivyo basi,kama una cancer,huwezi kupona daima kama damu yako ina tindikali.Ili upone kwanza rekebisha kiwango cha tindikali/nyongo(alkali) kwenye damu halafu ndio uendelee na mambo mengine muhimu.

Sasa basi,ili uwe na afya njema na upone cancer kama unayo,inabidi mwili wako uupe virutubisho vyote muhimu ili kuipa nguvu kinga ifanye kazi kwa urahisi.Virutubisho hivi utavipata kwa kula vyakula vya asili vya aina mbalimbali ambavyo vina kazi tofauti mwilini;

1.Ule vyakula vyenye uwezo wa kufanya damu yako iwe na kiwango kizuri cha alkali;
Baadhi ya vyakula hivyo ni juisi ya mboga mbichi za majani kama vile spinach,celery,matembele,broccoli,juisi ya maji ya limao/ndimu nk.

2.Ule vyakula vyenye uwezo wa kuondoa sumu mwilini;
Baadhi ya vyakula hivyo ni tumeric/bizari mbichi,tangawizi,parachichi na mbegu yake,juisi ya maji ya limao/ndimu,juisi ya ubuyu/ukwaju,black seed oil/mafuta ya habbat sauda,kitunguu saumu,juisi ya apple/tufaa,aloevera/shubiri nk.

3.Ule vyakula vyenye uwezo wa kutibu tatizo husika,ambapo kwa maana hii tunazungumzia cancer;
Baadhi ya vyakula hivyo ni mbegu za apricot,mbegu za peach,mbegu za almond,mtama,ulezi,mbegu za maboga,ufuta,juisi/mafuta ya jani kibichi ya bangi,backing soda,juisi ya karoti,juisi ya stafeli nk.

MUHIMU:

1.Huwezi kupona cancer kama damu yako ni acidic,yaani ina tindikali.Inabidi damu iwe alkaline/nyongo kwa kiwango kinachotakiwa ndio uweze kupona.

2.Huwezi kupona cancer kama mwili/damu yako ina sumu.Inabidi uondoe sumu ndio uweze kupona.

3.Ukifanya namba 1 na namba 2 hapo juu ndio hatua namba 3 itafanikiwa kwa urahisi sana.Hapa kwenye hatua hii ni kula vyakula vyenye uwezo wa kuua moja kwa moja chembe hai za cancer.Chembe hizi zikifa hazirudi tena kwa kuwa tayari damu iko safi na mwili/damu haina sumu tena hivyo madini muhimu hayawezi kupotea mwilini.

Hii ndio sayansi ya cancer kwa lugha ya ki laymen/rahisi kabisa.

Baadaye nitaenda specific kwenye tiba mojawapo niliyoizoea na kuwapa specifications zake jinsi ya kumtibu mgonjwa ambaye tayari ana cancer na mmepoteza matumaini kabisa.

Shukrani kwa elimu.
 
Unabisha bila point, c ajabu ndo maana mwapasua watu vichwa badala ya tumbo???? Hata kama anadanganya toa point Za kumkanusha sio kupiga kelele hapa.
Hizo point za kukanusha anazo basi.
 
Unajua chochote kuhusu tumour microenvironment

Dysplastic changes znavyotokea unafahamu

Interactions zake na body immunity

Kweli kitunguu ki interfere na NF-kb hebu njoo hapa tudiscuss hiili mkuu

Nmekua interested ghafla
 
Sasa tuzungumzie cannabis/bangi;

Kama kawaida inabidi mkumbuke kwamba ili uwe na uhakika wa kupona cancer lazima upitie hatua zote tatu,yaani,kuweka damu ya mgonjwa iwe alkaline,kuondoa sumu mwilini na ya tatu kuua chembe za cancer.Kwenye hatua zote mbili nina uhakika wote mnazijua vyema.Sasa kwenye hatua hii ya tatu tayari tumeshazungumzia Vitamin B17/Laetrile/Amygdalin,leo nitazungumzia cannabis/bangi.

Hakuna mtu yeyote duniani aliye na uwezo wa kupinga kwamba cannabis inaua chembe za cancer.Cannabis/bangi ilitumika miaka mingi sana kutibu magonjwa mbalimbali ikiwemo cancer,watu wenye nguvu na ubinafsi wamezuia siri hii kwa manufaa yao binafsi.US government yenyewe inajua kwamba cannabis ina uwezo wa kuua chembe za cancer,Ronald Reagan mwenyewe alijua umuhimu wa cannabis/bangi na ndio maana aliwahi kuilima bangi,lakini yeye mwenyewe aliku mstari wa mbele kupinga matumizi ya bangi baada ya kupata shindikizo kutoka kwa wenzake ambao ni wamiliki wa viwanda vya madawa.

Ili cannabis/cannabinoid iwe na nguvu zaidi,inabidi itumiwe kama extract kwa kutumia solvent extraction.Active ingredient/vimelea vinavyohusika kuua chembe za cancer kutoka kwenye bangi ni CANNABIDIOL(CBD) na TETRAHYDROCANNABINOL(THC).Najua kwa watu wengi hiki ni kitu cha kushangaza sana kwa kuwa wanajua na wamesikia kwamba bangi ni haramu.Lakini inabidi mkumbuke kuwa,hata hao wanaosema bangi ni haramu huwa wanasema ni haramu kuvuta tu,sasa kama mwingine anaitumia kukamulia kwenye sikio kuondoa maumivu,je,uharamu wake uko wapi?Wengine wanakula kama mboga,je,ni haramu?wengine wanaitumia kuondoa kichefuchefu,je,ni haramu?Wengine wanatumia mafuta ya mbegu za bangi kulinda ngozi,je,ni haramu?Hata mahospitalini wanatumia dawa kama vile DRONABINOL na NABILONE ambazo zimethibitishwa na FDA ya Marekani ili kuondoa side effects zilizosababishwa na chemotherapy kwa wagonjwa wa cancer,dawa hizi zimetengenezwa kwa kutumia bangi.

Hawa jamaa wanazuia watu kujua matumizi makubwa sana ya bangi likiwemo lile la kutibu cancer na badala yake wanajifanya kukubali kwamba kweli bangi ina faida lakini wanataja faida ndogondogo tu,kubwa hawazitaji na hata wakizitaja watakwambia bado hazijakuwa proved,sasa tangu miaka 130 ya utafiti wa cancer ipite hadi leo hii wanashindwa vipi kutafuta proof?Kitu kingine ambacho hakiingi akilini ni pale wanaporuhusu bangi itumike baadhi ya states zao kama vile California nk na kuzuia states nyingine wasitumie,mshawahi kujiuliza kwa nini waruhusu sehemu moja lakini wazuie sehemu nyingine ilihali bangi ni haramu?Kama kweli bangi ni haramu kwa nini wasizuie sehemu zote tu?Akili kichwani kwako.

Kati ya mambo rahisi sana kujua ukweli wake,bangi ni mojawapo,ukiamua tu kujua ukweli wa bangi wala haipiti wiki moja utakuwa umejua kila kitu.

Sasa kwenye tafiti nyingi sana imebainika bangi ina uwezo wa kuua chembe za cancer,hata US government yenyewe wanakubali kwamba bangi ina uwezo huo,sasa kwa nini hawaruhusu bangi itumike kwa wagonjwa wa cancer?Wanazuia isitumike active ingredient yenyewe ya bangi kwa kiwango kinachotakiwa na badala yake wanasema eti bangi ikitumika pamoja na chemotherapy au mionzi inaongeza uwezo wa tiba hizo mbili kutibu cancer,yaani huu ni uongo mtupu,wanachanganya tiba sahihi na sumu zao za chemo na mionzi wakati bangi peke yake ina uwezo wa kipekee.Sasa wewe mwenyewe fikiria,kama chemo na mionzi yenyewe husababisha madhara/cancer mwilini ukiachilia mbali ugonjwa wenyewe wa cancer halafu wanasea ukitumia bangi bado unapata nafuu,je,hamuoni kwamba kama mtu atatumia akili atagundua kwamba kweli kumbe bangi ina uwezo mkubwa sana?Kwa maana kwa kesi hii bangi itakuwa inapambana na madhara ya chemo na mionzi na wakati huohuo inapambana na cancer yenyewe.

Kuna watu walitumia na wanatumia bangi extract na bado hawapitii hatua ya kwanza na ya pili nilizotaja na bado wanapona,hapa ndipo utakapoona kwamba bangi ni suala lingine kabisa.Hawa jamaa kuizuia ili kulinda maslahi yao hawajakosea kabisa.Huko Marekani kuna watu wameshafunguka akili na kujua umuhimu wa bangi na ndio maana maandamano ya kutaka bangi iruhusiwe marekani ni jambo la kawaida sana,lakini kwa nchi zilizo gizani kama zetu hizi huwa wanacheka na kushangaa eti wanaposikia watu wanaandamana kutaka bangi iruhusiwe,ama kweli ujinga ni kitu kibaya sana,wakati tunawacheka wenzetu wakati huohuo wenzetu nao wanatucheka sisi na kweli wao ndio wana haki ya kutucheka.

Ili kujua jinsi ya kupata extract kutoka kwenye bangi na mambo mengine muhimu nitawakea documentary hapo chini kwa kumbukumbuku zenu.Rick Simpson ni mmoja wa watu wanaopigania bangi US Canada,anaelimisha watu bure bila kudai pesa,anafanya hivyo kwa kuwa yeye mwenyewe ndugu zake ni wahanga wa cancer kabla hajajua ukweli huu wa bangi,pia yeye mwenyewe ni shuhuda baada ya kujitibu cancer ya ngozi kwa kutumia bangi.Kama mtu anatoa uelewa huu bure bila kudai fedha,je, watu hawaoni kama kuna ukweli hapo?

Pia wewemwenye unaweza kufuatilia kwenye mitandao mingine kuhusu bangi na cancer,yaani ukweli huu haufichiki,karibu kila site utakayoingia lazima itaonesha kwa namna moja ama nyingine kwamba bangi inaua chembe za cancer.Hata wenyewe wanakubali angalau huwa wanasema kwamba bangi inaua aina fulani ya cancer tu badala ya kusema kwamba inaua chembe za cancer yoyote.Sasa wakati wao wanaendelea kujifanya wanafanya utafiti kuhusu bangi huku wale wanaojua ukweli tayari wanatumia bangi kujitibu.Hawa jamaa hawawezi kumaliza utafiti huu leo wala kesho,miaka 130 sasa imepita bado hawajui.Sasa hata sisi tukijua ukweli huu tutakuwa tunatumia bangi kujitibu cancer wakati wao wanaendelea na utafiti,washenzi sana hawa watu.

Pitia wenyewe kwenye mitandao ujionee,au unaweza kuperuzi hizi baadhi ingawa nazo zimeficha baadhi ya mambo;

Federal Government Finally Admits Cannabis Can Help Kill Cancer Cells

Marijuana can kill cancer cells, says US government-funded research - Americas - World - The Independent

'Major hypocrisy': US govt-funded agency admits marijuana can kill cancer cells ? RT USA

The US Finally Admits Cannabis Kills Cancer Cells | Collective-Evolution

Cannabis kills cancer cells and shrinks brain tumours, report reveals | Daily Mail Online

Cannabis and Cannabinoids - National Cancer Institute


RUN FROM THE CURE/RICK SIMPSON;


Unazjua receptor za tetrahydrocanabinol zpo kwenye ubongo tu na zinaitwa CB-17
itaenda kutibu sehemu zingne za mwili kusiko na receptor unajua kweli how drugs work chief.. I am eager to learn inawezekana una magunduzi ya ajabu hatarii
 
Hapo ndo hua mnakosea! mnadhani kila kitu kwenye science kinafanywa na mzungu! kuna wanasayansi weusi mamilioni, sio kila kitu kinafanywa na mzungu, wapo weusi kwenye cancer research wengi tu zunguka duniani uone...

Huyu sio kwamba sijamsikiliza, nimesoma kila kitu alichoandika na hakuna evidence yoyote ile, uliza mtu yeyote anayehusika na research kwenye cancer, fuatilia publications mbalimbali zinazotolewa na wanasayansi wanaohusika na cancer wote wanasema kitu flani, huwezi nambia kampuni baadhi zinaficha dawa ya cancer, hadi leo hii ingekua ishajulikana, hivi unadhani kuna siri ya watu zaidi ya laki?? its impossible. Angekuja na evidence yoyote ile huyu jamaa ningekua wa kwanza kumpongeza ila sio speculations tupu..

Soma anything science related utaona jinsi gani science haina utani, ni years of research, fixing errors, finding solutions, hakuna speculations huku ni real facts.
Dunia ya wanasayansi inahangaika sana na kitu kinaitwa tumour immunology aisee jamaa angejua watu wasivyo lala huko soon na mimi naenda ku join kwenye hizo research i don't know what this man ana try kusema
 
Unajua chochote kuhusu tumour microenvironment

Dysplastic changes znavyotokea unafahamu

Interactions zake na body immunity

Kweli kitunguu ki interfere na NF-kb hebu njoo hapa tudiscuss hiili mkuu

Nmekua interested ghafla
Mkuu hili suala limeshakuwa discussed sana hapa na huyu jamaa,hivyo kumuita tena mjadili wakati walishajadili naona kama kurudisha mjadala nyuma

Hivyo nadhani wewe ungekanusha hoja zake alizozitoa huko juu katika comment mbalimbali kuliko kuanza tena upya wakati yeye alishamaliza kazi ya kujadiliana na watu humu.

Lakini pia naomba mjadili kwa lengo la sisi malayman kuelewa zaidi na kujua yupi anazo hoja sio kujadili kwa lengo la kuonesha umwamba
 
Mkuu hili suala limeshakuwa discussed sana hapa na huyu jamaa,hivyo kumuita tena mjadili wakati walishajadili naona kama kurudisha mjadala nyuma

Hivyo nadhani wewe ungekanusha hoja zake alizozitoa huko juu katika comment mbalimbali kuliko kuanza tena upya wakati yeye alishamaliza kazi ya kujadiliana na watu humu.

Lakini pia naomba mjadili kwa lengo la sisi malayman kuelewa zaidi na kujua yupi anazo hoja sio kujadili kwa lengo la kuonesha umwamba
Wewe ni nani kunipangia muda wa kujibu?.

Kama ndo naiona mada leo

We jamaa vipi ebu niache aisee
 
Mtu akishasema "NADHANI" maana yake hajalazimisha yaani kama anashauri tu,na mimi nimesema nadhani kwa maana ni kama ushauri,sijakupangia muda.

Kama mada umeiona leo na comment zake zipo pia ni uongo kusema hujaziona,labda usitake kuzisoma.

Sio ugomvi ni ushauri wa nia njema tu.
Achana na mimi

Hujaja kiheshima kabsa like unanipangia rubbish stupid kabsa
Nmemind

Kama kuna sehemu hujaelewa si ungeuliza... Nmesoma comment zote naweka vitu right unaleta upumbavu wako hapa
 
Achana na mimi

Hujaja kiheshima kabsa like unanipangia rubbish stupid kabsa
Nmemind

Kama kuna sehemu hujaelewa si ungeuliza... Nmesoma comment zote naweka vitu right unaleta upumbavu wako hapa
Ok sawa pole sana daktari.
 
Back
Top Bottom