Hii biashara inanipa stress wallah!

Hii biashara inanipa stress wallah!

Nimekuwa mkulima wa miwa ya kuzalisha sukari katika Bonde la Kilombero kwa miaka kadhaa sasa ila kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita soko limeyumba kupita kiasi. Tatizo kubwa ni mwekezaji(kiwanda Cha sukari) kushindwa kuhimili wingi wa miwa ya wakulima wa nje (autogrowers).

Kwakuwa ni uwekezaji mkubwa na nguvu nyingi nilielekezea huko ilibidi nitafakari njia mbadala ya kuiuza miwa ile (ukizingatia mimi ni ni mkazi wa Dar, so hata usimamizi wa mauzo kule shamba unakuwa mdogo). Mwanzoni mwa mwezi March nikapata wazo la kuileta Dar kuiuza kwa wanaouza juice ya miwa. Nikaanza kufanya upembuzi wa kutafuta soko kwakuwa miwa ile iko tofauti kidogo kulinganisha na miwa iliyozoeleka kukamua juice hapa mjini.

Ilibidi nilete sample ya bidhaa yangu kwa wateja niliowakusudia, walionyesha kuikubali sababu miwa ile ina sukari zaidi ya hii waliyoizoea. Nikatafuta pia mahali pa kuweka mzigo wangu pindi nitakapoianza hiyo biashara. Baada ya kuona kila kitu kimeenda sawa wakati najiandaa kufuata mzigo ndo balaa la Corona likawa limepamba moto then kukawa na mfungo wa Ramadhan so ikabidi nitulie kidogo.

Baada ya hali kutulia na mfungo kuisha nikafanya safari. Kwa kuanzia nilipanga kuanza na angalau tani10, ili kama biashara itaenda vizuri niongeze ukubwa wa mzigo. Nilifanikiwa kukata na kupakia fuso, Jumapili tarehe 21/6 nikaingiza mzigo Dar.

Balaa lilianza kesho yake Jumatatu nilivyoanza ku-suplly mzigo kwa wateja wangu. Biashara haikuwa kama matarajio niliyokuwa nayo. Hadi leo ninandika thread hii mzigo uko zaid ya tani 7. Mbaya zaidi bidhaa hii baada ya siku 10 haifai tena kwa matumizi kwahiyo nikiangalia uchache wa mzigo ninaoupush per day naona kabisa mzigo hautakwisha na nitapata hasara.

Kinachoniumiza kichwa, matumaini yangu kama biashara ingekuwa vizuri hiyo hela ndo ingenisaidia kumsafirisha first born wangu shule this weekend. Kilichonisukuma kuandika uzi huu wakuu, ni imani yangu kwamba jukwaa hili lina aina zote za watu so kwa yeyote anayefahamu maybe mtu mwenye uzalishaji mkubwa wa Cane juice au popote kwenye kiwanda cha kutengeneza ethanol/spirit ili niiuze hii tani 7 kwa pamoja angalau niokoe gharama za msingi nilizoingia especially usafiri, labour charges etc.

Kwa yeyote mwenye kujua ufumbuzi wa hili jambo nahitaj msaada wake
Mwasiliano: 0624406434
Natanguliza shukrani!
Anzisha kijiwe cha kuuza juice ya miwa. Tafuta location nzuri piga kazi.
 
Jaribu kuwasiliana na Wizara ya ajira na vijana(Mavunde) /Wizara ya kilimo na mifugo wanaweza kukusaidia kwa kiwango fulani kukulink na masoko hata kama siyo to the fullest.
 
Ingekuwa ni miwa ya kienyeji hakuna tatizo la kuharibika, lakini umefanya kosa ndogo, wakati mwingine unavyoleta bidhaa yako kwa mara ya kwanza kwenye soko jitahidi ulete kiasi kidogo hata tani 3, ungeleta na gari canter wala usingelia lia. Soko unatakiwa ujaribu likisoma positive unaongeza kidogo kidogo.
USHAURI:
  1. Kama unaweza kukamu juice na kutunza kwenye freezer alafu unawauzia wauzaji wa juice kwa bei ya jumla
  2. Jaribu kuhifadhi kwenye sehemu ya baridi ukinyweshea maji lakini hiii inategemea jinsi ulivyokata shambani
  3. Watafute waaminifu uwakopeshe lakini hii ni risk pia
Best wishes!
 
Viwanda vitano nchi nzima havina uwezo wa kuhimili miwa ya wakulima nchi nzima kwa sababu viwanda hivi pia vina mashamba yake ya miwa.Mimi ninachoona hapa ni kwamba kuna sera mbovu kwa sababu kama viwanda hivi vina mashamba yake ya miwa je wakulima watauza miwa yao wapi?!

Miwa inayozalishwa na hayo mashamba ya viwanda bado haitoshelezi na ndo mana wanaingiaga mikataba na wakukima wa nje. huu uhaba wa sukari unaotokeaga ni ishara kubwa kwamba miwa inayozalishwa haitoshelezi.
 
Pole but first relax.....halafu mwambie Mungu akusaidie ,nimemuona Mungu akifanya mambo ambayo kwangu ilikuwa ni ngumu,lakini hata kwa yale niliyodhani ningeweza kufanya mwenyewe nilishindwa mpaka nilipomuomba Mungu msaada.
Mfano niliwahi kukosa wapangaji miezi3 mfululizo na nyumba ni classic ila nilipoomba wateja walimiminika from no where.


So muamini na mtegemee Mungu hakuna Neno gumu kwake,Siku moja kwa Mungu ni kama miaka 1000,so anaweza kufanya jambo within a second.....hii dunia tu unayoiona aliiumba kwa siku 5 tu siku ya sita ndo akamuumba mwanadamu,kifupi hashindwi na anatuwazia yaliyo mema.
[emoji106][emoji106][emoji106]
 
Nimekuwa mkulima wa miwa ya kuzalisha sukari katika Bonde la Kilombero kwa miaka kadhaa sasa ila kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita soko limeyumba kupita kiasi. Tatizo kubwa ni mwekezaji(kiwanda Cha sukari) kushindwa kuhimili wingi wa miwa ya wakulima wa nje (autogrowers).

Kwakuwa ni uwekezaji mkubwa na nguvu nyingi nilielekezea huko ilibidi nitafakari njia mbadala ya kuiuza miwa ile (ukizingatia mimi ni ni mkazi wa Dar, so hata usimamizi wa mauzo kule shamba unakuwa mdogo). Mwanzoni mwa mwezi March nikapata wazo la kuileta Dar kuiuza kwa wanaouza juice ya miwa. Nikaanza kufanya upembuzi wa kutafuta soko kwakuwa miwa ile iko tofauti kidogo kulinganisha na miwa iliyozoeleka kukamua juice hapa mjini.

Ilibidi nilete sample ya bidhaa yangu kwa wateja niliowakusudia, walionyesha kuikubali sababu miwa ile ina sukari zaidi ya hii waliyoizoea. Nikatafuta pia mahali pa kuweka mzigo wangu pindi nitakapoianza hiyo biashara. Baada ya kuona kila kitu kimeenda sawa wakati najiandaa kufuata mzigo ndo balaa la Corona likawa limepamba moto then kukawa na mfungo wa Ramadhan so ikabidi nitulie kidogo.

Baada ya hali kutulia na mfungo kuisha nikafanya safari. Kwa kuanzia nilipanga kuanza na angalau tani10, ili kama biashara itaenda vizuri niongeze ukubwa wa mzigo. Nilifanikiwa kukata na kupakia fuso, Jumapili tarehe 21/6 nikaingiza mzigo Dar.

Balaa lilianza kesho yake Jumatatu nilivyoanza ku-suplly mzigo kwa wateja wangu. Biashara haikuwa kama matarajio niliyokuwa nayo. Hadi leo ninandika thread hii mzigo uko zaid ya tani 7. Mbaya zaidi bidhaa hii baada ya siku 10 haifai tena kwa matumizi kwahiyo nikiangalia uchache wa mzigo ninaoupush per day naona kabisa mzigo hautakwisha na nitapata hasara.

Kinachoniumiza kichwa, matumaini yangu kama biashara ingekuwa vizuri hiyo hela ndo ingenisaidia kumsafirisha first born wangu shule this weekend. Kilichonisukuma kuandika uzi huu wakuu, ni imani yangu kwamba jukwaa hili lina aina zote za watu so kwa yeyote anayefahamu maybe mtu mwenye uzalishaji mkubwa wa Cane juice au popote kwenye kiwanda cha kutengeneza ethanol/spirit ili niiuze hii tani 7 kwa pamoja angalau niokoe gharama za msingi nilizoingia especially usafiri, labour charges etc.

Kwa yeyote mwenye kujua ufumbuzi wa hili jambo nahitaj msaada wake
Mwasiliano: 0624406434
Natanguliza shukrani!
Mkuu pole sana ila ushauri wangu ambao nilishawahi kushuhudia, ni kwamba nunua manual machine ya kukamua miwa 450k uifunge shambani uanze kukamua hiyo miwa kutumia cheap lbr (4) 5000@ kwa siku,

uwanze kuichemsha kwa kutumia hayo magada ya miwa itaganda baada ntakuelekeza chemical( endiony) 50k moja ili isafishe iwenyeupe arafu uisange kuna manual machine vya kusagia inakua sukali nzuri lakini sio high quality

ununue mifiko ya sukali ya kagera suger au mtibwa uchanganye mufuko moja kwenye mifuko 10 ya kwako kisha pakie upeleke sokoni.....unalipwa keshi hela yako hapo hapo inarudi ndoanze paper work ya small scale industry

hiyo ni kazi nzuri ila fitina nyingi kutoka serikalini na wawekezaji kwa kisingizio cha kiwanda bubu, Tbs TRA nk.. ndani ya mwaka unakua mbali sanaaaa
 
miwa inayozalishwa na hayo mashamba ya viwanda bado haitoshelezi na ndo mana wanaingiaga mikataba na wakukima wa nje. huu uhaba wa sukari unaotokeaga ni ishara kubwa kwamba miwa inayozalishwa haitoshelezi.
Ushahidi uliopo sasa hivi wa viwanda kukataa kununua miwa ya wakulima unaonyesha kuwa miwa inayolimwa na viwanda vya sukari huwa inawatosheleza!
 
Ushahidi uliopo sasa hivi wa viwanda kukataa kununua miwa ya wakulima unaonyesha kuwa miwa inayolimwa na viwanda vya sukari huwa inawatosheleza!
viwanda vya sukari vnajitoshelezaje angali kuna malalamiko sukari iliyopo haitoshi? kuna sehemu kuna kauongo.
 
viwanda vya sukari vnajitoshelezaje angali kuna malalamiko sukari iliyopo haitoshi? kuna sehemu kuna kauongo.
Sukari kutokutosha haitokani tu na ishu ya miwa bali kuna sababu nyingine zinazoweza kusababisha tatizo hilo kama vile uwezo wa viwanda kuzalisha sukari,management mbovu,sera mbovu za serekali juu ya usambazaji wa sukari na kadhalika
 
Pole mkuu, juice ya miwa inanyweka sana kufuatana na hali ya hewa, sasa miwa umeitoa kukiwa na hali ya kipupwe, hata biashara zingine za vinywaji kama maji na soda hazitoki sana..

Hope utapata usaidizi...Pole SANA

Everyday is Saturday........................ 😎
 
Pole sana mkuu.
Hiki mi kipindi kibaya sana.
Biashara ya juice ya miwa haitembei kabisa sababu ya baridi.

Hata vijiwe vya juice hiyo vinachelewa kabisa kufunguliwa na mauzo yameshuka.

Kwa sasa hesabu maumivu na ada ya dogo tafuta plan b.

Kuna ushauri hapo umepewa unaweza ifanyia kazi ya kutengeneza sukari.

Komaa hivo hivo kuwa na kakiwanda kako kisirisiri.
 
Sukari kutokutosha haitokani tu na ishu ya miwa bali kuna sababu nyingine zinazoweza kusababisha tatizo hilo kama vile uwezo wa viwanda kuzalisha sukari,management mbovu,sera mbovu za serekali juu ya usambazaji wa sukari na kadhalika
Naona haukosi sababu chief. anyway point yako imeeleweka na point yangu imeeleweka. Amani.
 
Nimekuwa mkulima wa miwa ya kuzalisha sukari katika Bonde la Kilombero kwa miaka kadhaa sasa ila kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita soko limeyumba kupita kiasi. Tatizo kubwa ni mwekezaji(kiwanda Cha sukari) kushindwa kuhimili wingi wa miwa ya wakulima wa nje (autogrowers).

Kwakuwa ni uwekezaji mkubwa na nguvu nyingi nilielekezea huko ilibidi nitafakari njia mbadala ya kuiuza miwa ile (ukizingatia mimi ni ni mkazi wa Dar, so hata usimamizi wa mauzo kule shamba unakuwa mdogo). Mwanzoni mwa mwezi March nikapata wazo la kuileta Dar kuiuza kwa wanaouza juice ya miwa. Nikaanza kufanya upembuzi wa kutafuta soko kwakuwa miwa ile iko tofauti kidogo kulinganisha na miwa iliyozoeleka kukamua juice hapa mjini.

Ilibidi nilete sample ya bidhaa yangu kwa wateja niliowakusudia, walionyesha kuikubali sababu miwa ile ina sukari zaidi ya hii waliyoizoea. Nikatafuta pia mahali pa kuweka mzigo wangu pindi nitakapoianza hiyo biashara. Baada ya kuona kila kitu kimeenda sawa wakati najiandaa kufuata mzigo ndo balaa la Corona likawa limepamba moto then kukawa na mfungo wa Ramadhan so ikabidi nitulie kidogo.

Baada ya hali kutulia na mfungo kuisha nikafanya safari. Kwa kuanzia nilipanga kuanza na angalau tani10, ili kama biashara itaenda vizuri niongeze ukubwa wa mzigo. Nilifanikiwa kukata na kupakia fuso, Jumapili tarehe 21/6 nikaingiza mzigo Dar.

Balaa lilianza kesho yake Jumatatu nilivyoanza ku-suplly mzigo kwa wateja wangu. Biashara haikuwa kama matarajio niliyokuwa nayo. Hadi leo ninandika thread hii mzigo uko zaid ya tani 7. Mbaya zaidi bidhaa hii baada ya siku 10 haifai tena kwa matumizi kwahiyo nikiangalia uchache wa mzigo ninaoupush per day naona kabisa mzigo hautakwisha na nitapata hasara.

Kinachoniumiza kichwa, matumaini yangu kama biashara ingekuwa vizuri hiyo hela ndo ingenisaidia kumsafirisha first born wangu shule this weekend. Kilichonisukuma kuandika uzi huu wakuu, ni imani yangu kwamba jukwaa hili lina aina zote za watu so kwa yeyote anayefahamu maybe mtu mwenye uzalishaji mkubwa wa Cane juice au popote kwenye kiwanda cha kutengeneza ethanol/spirit ili niiuze hii tani 7 kwa pamoja angalau niokoe gharama za msingi nilizoingia especially usafiri, labour charges etc.

Kwa yeyote mwenye kujua ufumbuzi wa hili jambo nahitaj msaada wake
Mwasiliano: 0624406434
Natanguliza shukrani!
Nenda soko la Tandale
 
Yaani boss hapo ilibdi utafute wewe kijishehemu chako Cha kuuzia hii juice Hasa kariakoo pale hata ungepata vimkokoteni vya kusukuma vya kisasa ingekuwa poa sana

Tuwe tunawaza Mambo mbadala aisee sio kuahikira Jambo moja tu

Don't put all your eggs in one bucket .think aloud

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona Dar kubwa sana?,tembelea vijiwe vya hiyo juice,,naamini kwa dar yote wanaweza kuwa na zaidi ya vijiwe 10,wape sample kisha waachie namba na uwape bei ya chini kidogo
 
Sukari kutokutosha haitokani tu na ishu ya miwa bali kuna sababu nyingine zinazoweza kusababisha tatizo hilo kama vile uwezo wa viwanda kuzalisha sukari,management mbovu,sera mbovu za serekali juu ya usambazaji wa sukari na kadhalika
Hata kampuni nayo inaweza kutoa false information kuhusu scarcity ya bidhaa zake ili ipandishe bei makusudi pale wanapotaka wafikie malengo flani financially.
 
Mkuu pole sana ila ushauri wangu ambao nilishawahi kushuhudia, ni kwamba nunua manual machine ya kukamua miwa 450k uifunge shambani uanze kukamua hiyo miwa kutumia cheap lbr (4) 5000@ kwa siku,

uwanze kuichemsha kwa kutumia hayo magada ya miwa itaganda baada ntakuelekeza chemical( endiony) 50k moja ili isafishe iwenyeupe arafu uisange kuna manual machine vya kusagia inakua sukali nzuri lakini sio high quality

ununue mifiko ya sukali ya kagera suger au mtibwa uchanganye mufuko moja kwenye mifuko 10 ya kwako kisha pakie upeleke sokoni.....unalipwa keshi hela yako hapo hapo inarudi ndoanze paper work ya small scale industry

hiyo ni kazi nzuri ila fitina nyingi kutoka serikalini na wawekezaji kwa kisingizio cha kiwanda bubu, Tbs TRA nk.. ndani ya mwaka unakua mbali sanaaaa
Hebu boss njoo utueleze hiyo chemical mbona juu juu tu umeeleza
 
Mkuu DSM kuna wauza juice wengi sana kama umemaliza tani 3 kwa watu hao hizo 7 zinaisha.

Anza kuwafata Kariakoo pale ndio wengi, makumbusho, mwenge, tandika, temeke, mbagala, mbezi mwisho, gongo la mboto na maeneo mengine ya balabala...kwa idadi wako wengi hizo tank zako 7 zinaenda siku moja tu then tuna Push na zile tani 100 za shambani kwanini mzigo uoze Cheaf.

Nenda na Sample akielewa muuzie kwa Affordable price na asiye na pesa mkopeshe mzigo.

Weka mzigo mezani tufunge Deal hilo chapuuu kijana wa Sales nipo hapaa.
 
Back
Top Bottom