Hii Dharau ni mwisho, Sidhani kama kuna ya juu yake

Hii Dharau ni mwisho, Sidhani kama kuna ya juu yake

BM X6

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2020
Posts
1,376
Reaction score
4,222
Asee kuna watu wanajeuri na madharau katika hii Dunia sijawahi ona, Leo ilikuwa ni safari ya kurudi home baada ya kukamilisha kilichonileta huku, nimetoka sehemu niliyofikia (Donholm) fresh sihisi njaa nimepanga nifike Border ndio nipige msosi wa Nguvu (Supu chapoo ya kibongo) Supu za huku sizielewi Sasa sijafika hata mbali njaa ikaanza kuita saa hio Niko Mlolongo nikaona kutoka Mlolongo Hadi border ni parefu sana sitaweza vumilia njaa, nikasogea sogea hadi Athi River nimepitia tu Roundabout ya Athi river mbele kidogo nikaona Hotel nikachoma ndani

Nikapiga hesabu pale kabla ya ku order nikaona nipige tu msosi kabisa niachane na Chai, nikaitisha Ugali Matumbo na Greens, nikaletewa bill ni Ksh 350/= Nikatoa Soo 4 nikampatia yule muhudumu akaenda kwa Cashier akaniletea balance yangu Ksh 50 mm sijaipokea nikamuambia utakunywa soda hiyo, yule mhudumu kwani alinijibu nilimuona tu karudi kwa Cashier tena, alivyorudi kwangu sasa

Akanambia "I have nothing to do with 50 bob, I can see ww ndio unafaa kukunywa soda na si mimi" kumbuka Ile shilingi 50 niliyompatia aliicha pale kwenye meza akatoa mia tano (Ksh 500) "utakunywa soda na food imejisort kwa hiyo pesa balance utatumia kupanda matatu urudi mahali umetoka" halafu akasepa, Asee nilibaki nimeduwaa

Yani Pesa yangu mwenyewe hata kama ni ndogo ndio inanifedhehesha kiasi hiki? kusema ukweli na Mimi sijajivunga nikabeba Ile mia tano, ila na mm nilitaka kumuoneshea dharau yule mkikuyu sijui ni mkikuyu yule, ikabidi tu niwe mpole kwasababu nipo Nchi ya watu ila ingekuwa Bongo haki ya nani nisingekuwa mpole hivyo

Uzuri hajajua kama mm ni Mbongo maana angejua pengine ningehisi kubaguliwa, kwasababu Wakati natoka pale hotelini nikamsikia anamuongelesha mwenzake "Hawa watu wa Mombasa 'Chuani' kwao wanaona ni kama Thao" asee Dada aliniamulia yule sijui alitumwa, sijawahi kukutana na dharau kama hii maisha mwangu


Tafuteni Pesa wadau tena sio Pesa tu, Tafuta Utajiri kwa namna yoyote ile ili ukitoa tip utoe inayoeleweka, Mimi hiyo dharau imenipata katika pilikapilika za kutafuta Utajiri so imeniongezea kasi/speed zaidi, Kasi ilikuwa inasoma 3G baada ya hilo tukio imepanda hadi 4G
Screenshot_20220626-142111.jpg
 
Mimi nilifika hapo Kitengela kwenye kibanda cha Gidheri ilikuwa majira ya saa mbili usiku vijana wawili wakatoka baruti nikashangaa sana

Yule Mhudumu akanishukuru sana akaniambia walikuwa ni Wakora wanataka kupora na wamekufikiria kuwa wewe ni Flying Squad.

Nikamwambia yule Mama kuwa mimi ni Dereva wa Roli kutoka Arusha akasema basi wamekufananisha nikajisemea moyoni Alhamdulilaah..
 
Mimi nilifika hapo Kitengela kwenye kibanda cha Gidheri ilikuwa majira ya saa mbili usiku vijana wawili wakatoka baruti nikashangaa sana

Yule Mhudumu akanishukuru sana akaniambia walikuwa ni Wakora wanataka kupora na wamekufikiria kuwa wewe ni Flying Squad.

Nikamwambia yule Mama kuwa mimi ni Dereva wa Roli kutoka Arusha akasema basi wamekufananisha nikajisemea moyoni Alhamdulilaah..
Huyo flying squad ndio Nan?
 
Pole mkuu ila nahisi hukua na nia mbaya wala dharau juu yake ila yeye ndo kafikilia tofauti japo imekusaidia kidogo 😀.
 
Back
Top Bottom