Hii gari niliyonunua sijapigwa hapa?

Hii gari niliyonunua sijapigwa hapa?

Mimi sijui nikoje ila kiukwl nkiwaga na hela huwa sipendi kuzungushwa huwa nazama zangu yard navuta chombo chap!! Hayo mambo ya kusubiri siwezagi kwakwl
Mimi kuna siku nilinunua gari saa kumi kamili jioni hapa hapa bongo saa kumi na moja na nusu niko nalo bar napiga kilaji. Siwezi subiri gari wiki zote hizo....
 
Mimi niliagiza Suzuki Jimny 2000
Mwezi wa saba mpaka nimesahau waliniambia mpaka mwishoni mwa huu mwezi.mpaka nilishasahau kama nime order gari
IMG-20210721-WA0025.jpg
 
Sina haja ya kueleza mengi. Mtakumbuka mwanzoni mwa mwezi huu nilikuja hapa kueleza kuwa nina nia ya kununua gari kutoka kampuni ya wauzaji SBT japani. Ni mara ya kwanza kuagiza ktk kampuno hii. Nimezoea Beforward.

Baada ya kufanya process zote za malipo na gari yangu kuaninishwa kama tayari imeshauzwa sasa nikabaki kusubir kile wanaita CAP yani Car at progress. Huu ni mfululizo wa taarifa na habari mteja hujuliwa ni lini gari inafanyiwa booking ya safari, lini itaondoka japani kuja mahali mteja alipo, meli itakayo beba na makadirio ya muda gari itawasili kwa mteja.

Baada ya kukaa siku 10 huki nikiona kimya nikawafata Sales personel huko huko. Nilichojibiwa nimeshangaa.Eti Booking inafanyika ila inakadiriwa kuanza kusafirishwa tar 29 mwezi wa tisa. Hii imenishtua. Au nililipa pesa kwa wajanja?

Kwa Beforward mamvo hayakuwa hivi. Ilichukua wiki sita tu gari zangu mbili zikanifikia. Hii ya sasa sbt wiki sita zinakatika bado haijaanza safari
heeeee mkuu wahi polisi, Tena kimbia saaaana
 
Kilichonitia woga ni huo muda mrefu. Ukiangakia from now tar 29 ni mwezi mzima na wiki moja. Hapo bado safari ya kuja huku na kushuka itachukua miezi miwili mingine.
Mkuu,
Nakuhakikishia hujapigwa. Binafsi ilinitokea Be Forward nilinunua gari tarehe 19 May 2021 nimepokea gari August 21, 2021.
Tatizo corona imeleta shida biashara na usafiri wa meli. Nilipata gari bora kabisa.
Uwe mvumilivu hizo ni kampuni kubwa huwezi kudanganywa.
 
Mkuu,
Nakuhakikishia hujapigwa. Binafsi ilinitokea Be Forward nilinunua gari tarehe 19 May 2021 nimepokea gari August 21, 2021.
Tatizo corona imeleta shida biashara na usafiri wa meli. Nilipata gari bora kabisa.
Uwe mvumilivu hizo ni kampuni kubwa huwezi kudanganywa.
Kweli aisee. Unajua nilikuwa sijazoea kupigwa doro kama hivi. Nilileta mada hapa kupata ushauri na kutiwa moyo.

Mpaka saaa hivi wameshaisafirisha iko njiani inafika tar 3 October. Nilifurahi sana.

wana Jfs walinutuliza moyo.
 
Wanajidunduliza na kujichanga kama kununua kitu kingine chochote.

Wewe una kipato gani kwa mfano nikuulize?!

Kama hauna kipato achana na magari utakuja ona kumiliki magari ni anasa.
Kumiliki gari hutokana na kipato sio kudunduliza. Acha kabisa.
 
We mwenyewe unaliona vizuri hapo ndugu au basi tu unataka kugombana na watu wakikujibu oil chafu hapa?! [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hahahaa jamaa anazingua huyu.
 
Kweli aisee. Unajua nilikuwa sijazoea kupigwa doro kama hivi. Nilileta mada hapa kupata ushauri na kutiwa moyo.

Mpaka saaa hivi wameshaisafirisha iko njiani inafika tar 3 October. Nilifurahi sana.

wana Jfs walinutuliza moyo.
Bila shaka chuma imefika bandarini leo[emoji23][emoji23]

Ikitoka, twende tukaipime mapafu bagamoyo[emoji119]
 
Bila shaka chuma imefika bandarini leo[emoji23][emoji23]

Ikitoka, twende tukaipime mapafu bagamoyo[emoji119]
Aisee nashukuru Mungu wamenitumia Emila Diamond Shipping Agency kuwa itawasili tar 5. Kwa mujibu wa B/L inatakiwa kufika Leo.

Nimeshapokea Documents zote kutoka DHL nasubiri chuma tu hapa.
 
Back
Top Bottom