Hii haina tofauti na anaetumia "mkorogo" au "karolaiti"!!

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,891
Najua ukikutana na wanawake 10 barabarani kati yao 9 au wote kumi wametengeneza nywele,yaani wameziondoa kwenye uhalisi wake na wanataka zifanane na za wazungu,waarabu wachina n.k,ukiwauliza sababu hasa ya kufanya hivyo watakuambia "ili wapendeze" kwao kua na nyele ndefu ndo kupendeza!Hili ni tatizo na pia ni maradhi,ni tatizo la kujikataa.Unafikia mahali unadhani hukustahili kuwa na nywele hizo,hili nalo halina tofauti na wale wanaojichubua ngozi zao ili wawe weupe,wanaona weusi ni ubaya,wanajikataa!Watu weusi tumekua na maradhi haya kwa muda sasa,tunaona tumekosewa kuumbwa what a shame!!Hebu fikiria unafikia mahali unabadili ngozi na nywele za asili ukidai eti unataka "kupendeza"!Shame on us black people!Nani kakuambia kua na rangi nyeupe na nywele ndefu ndo kupendeza?Hii ni kwa jinsia zote.Cha kushangaza utamkuta mdada kaenda saloon "kutengeneza" nywele halafu anamzodoa na kumkejeli mwenzie aliechubua ngozi utadhani wanatofauti!WATU WEUSI,TUJITAMBUE NA KUIONA THAMANI YETU!
 
Mkuu hiyo mada ni pana sana.

Vipi wewe nywele zikiwa ndefu huwa unanyoa? Mbona unakosoa kazi ya Mungu? Makucha je?

Nadhani kwa kutengeneza nywele kwa kina dada si sawa na kujichubua, sijui lakini mawazo yangu tu
 
Wanawake wengi hawajikubali.
Kila kitu alichonacho ni cha kubandika.
 
Kutengeneza nywele hakuwezi kufanana na kujichubua hata siku moja.

Sababu ya kwanza ni kwamba nywele zilizotengenezwa zinaweza kurudishwa katika hali yake ya asili wakati ngozi haiwezi.

Pili nia ya kutengeneza nywele sio kupoteza asili bali ni kurahisisha utunzaji pia kumpa mwenye nywele fursa ya kua na muonekano tofauti pale anapopenda kufanya hivyo.Ni sawa na style ya nguo, tunabadili mitindo ili leo iwe tofauti na jana, kuendana na mazingira pia kwa kuzingatia urahisi wa kumove about ndani ya hizo nguo...na sio tunabadili ili tupoteze asili yetu.

Hivyo sioni ubaya mtu kusuka, kunyoosha au hata kulainisha tu nywele zake.
 
unafanya mchezo na kipilipili kichaa, ukimaliza kuchana lazima kichwa kiwe chamotooo! Acha watie nywele kalikiti

Paka mafuta yako na uzipunguze,utapendeza kuliko unavyofikiri!
 
Sokwe mjanja unapozikata unakua umezibadili kutoka uhalisia wake?
 
Lizzy,unapoenda salun unakua umezibadili kutoka uhalisia kwenda kua kitu kingine kabisa,wala hazifanani na zile za asili.Hapa sizungumzii uwezekano wa kuzirudisha au kutozirudisha kwenye uhalisi wake,suala hapa ni sababu ya kufanya hayo.Usilinganishe maradhi ya kubadili nywele na mitindo ya mavazi japokua hata hapa pana ufafanuzi wake na hii ni mada nyingine!Sio kweli kuwa mweny nywele ndefu anazitunza kwa urahisi zaidi ya fupi hili unalijua hata wewe,kwa mtu makini na anaejitambua hakuna sababu yoyote yenye mashiko hapa!
 
Mi ninaowajua wanajikubali ile mbaya!!

Hujui hata maana ya kujikubali ni nini!Huwezi kujikubali halafu ukaanza kubadili baadhi ya maungo na ngozi yako!
 
Hapa ngoja nipite tu. Kuna mtu namsaka kaondoka na bhange yangu,sijaskia harufu humu...
 
Mi wingi ndo silipendi kbs.Utakuta mengine ya blue.
Kuna siku niliona sababuni imeandikwa "sabuni ya wanawake",,nilipouliza ni kwa matumizi gani,,,nilichoka kabisa.
Kucha feki
Nyusi feki
meno feki.
Sauti feki
Poda feki
Macho feki
Kope feki

Mwanamke original ni yule wa miaka 12 tu (baadhi).
 
Lol... Nimecheka sana hapo kwenye sauti feki...ila kweli wadada tumezidi kujikataa, mie kuna siku nilikutana na mdada kashonea nywele kama rangi 3 au 4 kichwani...blue, njano, kijani, na nyekundu alikuwa kama kichekesho flani hivi... Inabidi ifike mahali watu wajikubali...
 

Ni vizuri tukaanza na wewe!
 
mi nimeweka dawa ili ziweze kuchanika kwa urahisi zaidi.
 
Paka mafuta yako na uzipunguze,utapendeza kuliko unavyofikiri!

hivi unakijua kipilipili kichaa wewe? Ukikichana kinajishika kwenye ncha ukitaka kuchana ukakojoe kabisa unaweza chafua mazingira
 
Mada kama hii kuhusu nywele imeanzishwa na Mzee Mwanakijiji kwanini zisiunganishwe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…