Hii imetokea katika Ziwa Tanganyika Mkoani Kigoma. Mliosoma Geography, hii inamaana gani?

Hii imetokea katika Ziwa Tanganyika Mkoani Kigoma. Mliosoma Geography, hii inamaana gani?

Huwa inatokea kwenye Maziwa, Mito Mikubwa na Bahati...!

Mimi ninazo sababu nyingine ambazo sio za Geography Wala za Ki Sayansi...!

Ila Kwa vile unataka Sababu za Ki Geography, basi Wacha tusibiri.
Na hatapata majibu sahihi huko anakoyatafuta zaidi ya kujazwa uongo was maabara.
 
Wazee, hiyo kitu ni noma sana.

Mimi sijui inaitwaje na hata visababishi vyake sivijui. Ila hiyo kitu ina balaa kubwa.

Niliwahi kuishuhudia nilipoenda Wilayani BUNDA, Mkoa wa MARA, sehemu moja inaitwa BULAMBA. Kuna Kambi ya JKT pale. Tulianza kusikia upepo mkali sana unavuma kutoka Ziwani Victoria, wavuvi walikuwa wameshastukia zali mapema wakatoka majini kwa kasi kubwa, wenyewe walisema machale ya kijadi yaliwacheza.

Kuna mstari ulijichora kutoka mbinguni au tuseme angani kwa kasi sana kuja majini. (Kama mnavyoona kwenye hiyo picha). Ghafla kukawa na upepo mkali na mawimbi makubwa Ziwani. Upepo ulifika hadi nchi kavu mbali sana. Nyumba nyingi ziliezuliwa mabati, vumbi zito mtaani na miti kuvunjika kwa sana maeneo ya BUlamba, Nyatwali, Kasuguti, Mahyolo na kuendelea huko (waliofika Bunda wanayaelewa haya maeneo). Wenyeji walisema hii kitu ikukukuta uko majini ndo tumekupoteza hivyo, "Wafa wagenda! ".
 
Hii imetokea katika Ziwa Tanganyika Mkoani Kigoma

Mliosoma Geography 🗺️🌏📗 hii inamaana Gani?

View attachment 3159312i?
Hicho ni kinyamkera, yaani ni mzungruko wa upepo kwa kasi kubwa yenye uwezo wa kuinua maji au mchanga jicho lake likiwa chini. Hivi karibuni ulitokea Manyara ukainua tanki tupu la maji la lita elfu mbili.
 
Itakuwa inahusiana na huu uzi 👇
Huu uzi umejaa upumbavu achana nao!

Hao wazee wa zamani wengi ni wajinga watupu na wachawi.
 
Huwa inatokea kwenye Maziwa, Mito Mikubwa na Bahati...!

Mimi ninazo sababu nyingine ambazo sio za Geography Wala za Ki Sayansi...!

Ila Kwa vile unataka Sababu za Ki Geography, basi Wacha tusibiri.
Bora uache tu mkuu kwa sababu mambo ya adakadabra yamekua mengi kwa sasa🤔
 
Nafikiri hii ni (splashes) kwa sababu ya shinikizo kubwa na mabadiliko ya msukumo wa maji kwa haraka, husababisha maji kuruka juu🤔🤔🤔🤔
 
Hilo ni joka kubwa (anaconda) anachukuliwa na sir God kwamaana majoka hayo hayawezi kuuawa na binadamu
 
Zamani walikuwa wanasema joka la kwenye maji linaenda mbinguni...
 
Eti Rabbon wewe unasemaje? Dalili ya nini hiyo? 😆
Hiyo ni dhoruba/ tornado, ni kimbunga Cha baharini.

Na upepo unatokana na neno Pepo. Wapo Malaika wanaohusika kuendesha majira na Pepo kuu nne duniani.

Wapo pia miungu wafanyao uharibifu kutumia Pepo hizo hizo maana wameruhusiwa Kwa kiwango Fulani japo Wana limits.

Twende na huku.

(Ufunuo wa Yohana 7:1-4)

1: Baada ya hayo nikaona Malaika wanne wamesimama katika pembe nne za nchi, wakizizuia PEPO NNE ZA NCHI , upepo usivume juu ya nchi, Wala juu ya bahari Wala juu ya mti wowote.

2: Nikaona Malaika mwingine, akipanda Kutoka maawio ya jua, mwenye muhuri ya Mungu aliye hai, akawapigia kelele Kwa sauti kuu wale Malaika wanne waliopewa kuidhuru Nchi na bahari,

3: Akisema, msiidhuru Nchi wala bahari Wala miti, hata tutakapokwisha kuwatia muhuri watumwa wa Mungu wetu juu ya VIPAJI VYA NYUSO ZAO.

......END.....


Pia ujue, mvua ya mawe theluji na tufani ni silaha ambazo Mungu huzitumia kuwaokoa awapendao na kuwaangamiza maadui zake.

(Ayubu 38:22-23)

22: Je ! Umeziingia ghala za theluji, au umeziona ghala za mvua ya mawe,

23: Nilizoziweka akiba Kwa wakati wa misiba,

Kwa siku ya mapigano, Kwa siku ya mapigano na vita?
 
Back
Top Bottom