Hii kasi ya Marekani kujisogeza kwetu baada ya kifo cha Rais Magufuli inatia shaka

Hii kasi ya Marekani kujisogeza kwetu baada ya kifo cha Rais Magufuli inatia shaka

Kama nimekosea nisahihisheni. Serikali ya Marekani haijatoa rambirambi rasmi kwetu kufuatia kifo Cha Rais Magufuli.

Lakini Marekani inajisogeza Sana kwa mama wakidai kutaka kutupa 'misaada' ya kupambanana korona. Tusiwaonee aibu! Tuwaambie hatuhitaji msaada wa kupambana na korona! Kama Wana Nia ya kutupa msaada watupe pesa zitusaidie kumalizia SGR na mradi wa Stigler's George.

Wakapambane na korona huko kwao maana wao tatizo Ni kubwa kuliko kwetu! Hawa mabeberu hawana aibu!
Makamu alitoa Salam za rambi rambi naamini aliwakilisha vyema
Au ulitaka rambi rambi individually?
 
Kama nimekosea nisahihisheni. Serikali ya Marekani haijatoa rambirambi rasmi kwetu kufuatia kifo Cha Rais Magufuli.

Lakini Marekani inajisogeza Sana kwa mama wakidai kutaka kutupa 'misaada' ya kupambanana korona. Tusiwaonee aibu! Tuwaambie hatuhitaji msaada wa kupambana na korona! Kama Wana Nia ya kutupa msaada watupe pesa zitusaidie kumalizia SGR na mradi wa Stigler's George.

Wakapambane na korona huko kwao maana wao tatizo Ni kubwa kuliko kwetu! Hawa mabeberu hawana aibu!
Yaani kweli unataka kupewa msaada halafu unataka ujipangie!? Kweli?
 
Marekani akikusaidia sio lazima awe amekuona masikini kuliko wengine. Anatoa msaada sana kwa Israel, Kenya, Misri n.k. ambako hali sio mbaya. Kimsingi husaidia wale wanaoendana na mtazamo wao duniani. Mtazamo wao hauna ubaya kwetu.

Watu mnalia mitaani hakuna fedha. Mnadhani zitakujaje huko bila FDI na misaada kama hii ya WB, IMF na Marekani? Kwani wametupa CONDITIONS mbaya ili tupate hiyo misaada?

Msaada wowote wa fedha ambao conditions zake zinakubalika kwetu ni vizuri sana kuupokea.
Kwahiyo muhimu zaidi hapa ni kuendana na mitazamo yake anayoitaka ndipo atakupa fedha zake na sio kwamba anatoa tu msaada kwa sababu ya upendo aliyonao au kwa sababu huyo anayemsaidia ni muhitaji sana wa msaada kuliko wengine kama nilivyokuwa nafikiri mimi?
 
Ujinga wetu na kuaminiswa na baadhi kwamba kuna kuna mabeberu na tunatakiwa tuwe wana ‘Umajumuhi wa Kiafrika’ bila kuangalia hali halisi ya dunia ya kisasa ni shida

Huyo Mwendazake alitumia mbinu za zamani na kutengeneza maadui wa kufikirika tu ( Mabeberu) ili apate umaarufu wa kisiasa na yake mengine yaende kwa mkono wa chuma

Dunia yetu toka zama ni ya ushindani na ukiwa weak utapelekwa tu kuanzia ngazi ya mtu mmoja mpaka Taifa na kama tunataka tuwaepuke hawa so called mabeberu ni mkakati wa muda mrefu sana na labda hata uwe wa siri ( mpaka tuwe imara kusimamia kuanzia mifumo yetu ya siasa, uchumi, tamaduni nk )

Unamchukia beberu hata kusoma mikataba haujui, na bado unaona ufahari kula pesa za umma kama madawa,madawati , mradi wa maji, umeme , bila kusahau unapanda vipandio vyao, unatumia simu zao na unajinasibisha hata kutumia lugha yao achia mbali ujinga wetu wa kujaza watu wa kabila, ndugu na dini tunazotoka eti ndo tunaweza pambana na Beberu na tunataka mpaka tumpangie nini cha kutupa kama msaada

Tuamke wa Afrika tunatakiwa mikakati imara na tuache ubinafsi ndo tunaweza pambana na hawa sijui mabeberu (USA na nchi za magharibi) sio ‘one man show’ ili kupata umaarufu wa kisiasa na kuendeleza ukandamizaji wa raia na kuwa na uhakika wa kula mali zao (wananchi)

Sorry nimejikita zaidi kwenye term ‘Beberu’ kama ulivyo ainisha hayo ya misaada ya korona na sijui SGR wataona wao inavyofaa
Wewe ni mpumba . vu huna lolote

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kama nimekosea nisahihisheni. Serikali ya Marekani haijatoa rambirambi rasmi kwetu kufuatia kifo Cha Rais Magufuli.

Lakini Marekani inajisogeza Sana kwa mama wakidai kutaka kutupa 'misaada' ya kupambanana korona. Tusiwaonee aibu! Tuwaambie hatuhitaji msaada wa kupambana na korona! Kama Wana Nia ya kutupa msaada watupe pesa zitusaidie kumalizia SGR na mradi wa Stigler's George.

Wakapambane na korona huko kwao maana wao tatizo Ni kubwa kuliko kwetu! Hawa mabeberu hawana aibu!
Inabidi tuendelee na msimamo wetu, kwani hawa jamaa sio wazuri kabisa. Hapo watakuwa wananyemelea Helium, na mama nae amekamia kuwa ichimbwe tu!!
 
Yaani kweli unataka kupewa msaada halafu unataka ujipangie!? Kweli?
Lakini mie naona si mbaya hivyo kama ingewezekana kuchagua ni kipi unachohitaji usaidiwe au usaidiwe kwa namna gani, kwa sababu huyo mtoaji hatoi tu huo tunaoita msaada kwa sababu tu wewe unashida au unahuitaji bali ana malengo yake anataka yatekelezeke ndipo atoe atoe hizo fedha kukupa bila ya hivyo hata kama unashida na uhitaji kiasi gani hatoi fedha zake. Kwahiyo utaona kwa aina ya huu msaada wenyewe ulivyo si ajabu kwa anayesaidiwa kuchagua huo msaada uelekwezwe wapi.
 
Kama nimekosea nisahihisheni. Serikali ya Marekani haijatoa rambirambi rasmi kwetu kufuatia kifo Cha Rais Magufuli.

Lakini Marekani inajisogeza Sana kwa mama wakidai kutaka kutupa 'misaada' ya kupambanana korona. Tusiwaonee aibu! Tuwaambie hatuhitaji msaada wa kupambana na korona! Kama Wana Nia ya kutupa msaada watupe pesa zitusaidie kumalizia SGR na mradi wa Stigler's George.

Wakapambane na korona huko kwao maana wao tatizo Ni kubwa kuliko kwetu! Hawa mabeberu hawana aibu!
Asiye na aibu ni asiyeukubali ukweli .
 
Kama nimekosea nisahihisheni. Serikali ya Marekani haijatoa rambirambi rasmi kwetu kufuatia kifo Cha Rais Magufuli.

Lakini Marekani inajisogeza Sana kwa mama wakidai kutaka kutupa 'misaada' ya kupambanana korona. Tusiwaonee aibu! Tuwaambie hatuhitaji msaada wa kupambana na korona! Kama Wana Nia ya kutupa msaada watupe pesa zitusaidie kumalizia SGR na mradi wa Stigler's George.

Wakapambane na korona huko kwao maana wao tatizo Ni kubwa kuliko kwetu! Hawa mabeberu hawana aibu!
Huna akili
 
Yaani kweli unataka kupewa msaada halafu unataka ujipangie!? Kweli?
Kujipendekeza kunakoitwa uzalendo hakuachi mtu salama. Bado kiwewe cha mwendazake. Mara hawajatoa rambirambi. Kuna rambirambi kubwa zaidi ya msaada? Hata aliyeleta vifuu vya nazi tunywee uji ametufaa. Vitendo kuliko maneno tu ya rambirambi. Hata na maneno yalitangulia. Tunatafuta nongwa bure. Tutengeneze marafiki, maadui wajiunde wenyewe!

Tusisahau kuwa balozi wa sasa wa Marekani ni daktari wa binadamu. Siku si nyingi alikuwa tayari kutumia muda wake kusaidia katika vita dhidi ya uviko-19. Hajaacha kujitoa na kusaidia ikibidi. Daktari wa siku nyingi hapa nchini. Eneo lake hasa la kujidai ni hapo.

Tumeamua kwenda na dunia kuhusu uviko-19. Tume inaundwa. Hakuna kasma ya hilo suala. Kajitokeza mtu kupiga jeki. Tukatae? Msaada haukataliwi. Masharti mabaya yakataliwe. Hiyo ndio sifa yetu kuu ya kujua vigezo na masharti ya hovyo. Tunakataa.

Vile Prof. Beno Ndullo na Mo Dewji kutoka Tz kuwa washauri wa Rais Ramaphosa wa RSA ni kwa sababu Tz ni dona kantri? Hiiiiii!!!!!!
 
Kuna ubaya gani kuwa marafiki na Marekani? Ni vizuri sana tupate misaada ya kuinua hali ya maisha ya watu wetu. Umeshasafiri sehemu za Tanzania ambako hadi sasa watu wanahangaika maji ya kunywa? Ni nyingi.

Asante Marekani kwa misaada yenu. Zingatieni maji, elimu, afya na barabara tafadhali.
Pesa ya msaada wa corona haina impact kwetu, wakishakupa wanakwambia ununue chanjo kwao na mahitaji mengine sasa itaongeza mzunguko gani wakati wanaichukua tena?

Kitakachoonekana ni kwamba wamekusaidia lakini ni njia ya kulet vitu ambavyo ni malengo yao.

Kama wanatupenda walete pesa tuafanyie mahitajibyetu myhimu kama afya miundo mbinu na viwanda.
 
Ila misaada ya vyandarua itarejea tena.
 
Pesa ya msaada wa corona haina impact kwetu, wakishakupa wanakwambia ununue chanjo kwao na mahitaji mengine sasa itaongeza mzunguko gani wakati wanaichukua tena?

Kitakachoonekana ni kwamba wamekusaidia lakini ni njia ya kulet vitu ambavyo ni malengo yao.

Kama wanatupenda walete pesa tuafanyie mahitajibyetu myhimu kama afya miundo mbinu na viwanda.
Sio urafiki wa korona peke yake. Na shughuli za korona zinahusisha watu wengi watakaolipwa, sio ununuzi wa chanjo peke yake. Na hata chanjo kuna wakuzisafirisha kwenda mikoani, wakuchanja watu, etc watakaolipwa.
 
Kwahiyo muhimu zaidi hapa ni kuendana na mitazamo yake anayoitaka ndipo atakupa fedha zake na sio kwamba anatoa tu msaada kwa sababu ya upendo aliyonao au kwa sababu huyo anayemsaidia ni muhitaji sana wa msaada kuliko wengine kama nilivyokuwa nafikiri mimi?
Interest zinapofanana ndiyo misaada inakuwepo. Kwa mfano sisi tunadhibiti majambazi yaliyoko Msumbiji. Hapa ni vita dhidi ya Alkaeda ya Afrika. Marekani watatupa silaha. Kuna mbaya gani hapo?
 
Mleta mada tuliza MANANILIU WEWE, TULIZA MANANILIU HAYOO. TULIZA.
 
Back
Top Bottom