Hii kauli inamaanisha nini wadau?

Hii kauli inamaanisha nini wadau?

Hahaha
Fungua ubongo huo ng'amua mambo hiyo case ndogo sana.
Asante. Ndio maana nimeleta humu kwenye mawazo muyatoe. Msije sikia mtu kafanya maamuzi magumu mkaishia kulaumu shetani .
 
Hata mimi huo ujinga wa mtu alitoa tung'ombe tuwili ammiliki mwanangu akiwa hai na akiwa amekufa siuungi mkono.

Mama aliyezaa kwa uchungu eti hawezi kuamua mwanae azikwe wapi ila hayo mamlaka kanapewa kahuni fulani tu eti kwasababu kametoa tung'ombe tutatu.

Nimke wako akiwa hai, akifa akazikwe kwao ili angalau watoto wako wakienda kutembelea kabuli la mama yao wanapata fursa ya kujuana na ndugu zao upande wa mama.
 
Na haujasema chanzo cha yeye kusema hivyo, watu wanaopendana na kuishi kwa amani katika ndoa zao hawawezi kutoleana maneno kama hayo, ila navojua kuna hasira anayo iliyomjengea chuki ndani ya moyo wake hatamani hata siku akifa umzike wewe, ila ndugu zake akiwemo baba yake
 
Na haujasema chanzo cha yeye kusema hivyo, watu wanaopendana na kuishi kwa amani katika ndoa zao hawawezi kutoleana maneno kama hayo, ila navojua kuna hasira anayo iliyomjengea chuki ndani ya moyo wake hatamani hata siku akifa umzike wewe, ila ndugu zake akiwemo baba yake
Hata kama ni hasira ndio atoe maneno ya hivyo wakati Mimi ni mtu ninayeingilika kimazungumzo vizuri tu. Namhudumia vizuri.
 
Usipate shida, ukikaa nae kwa kutumia mpe peni na karatasi mwambia aandike yale aliyoyasema kwa herufi kubwa sana na aandike pia jina la baba yake na mawasiliano yake. Kama atakubali kuyaandika basi chukua gundi yabandike chumbani kwenu akiuliza mwambie kichwa changu kina mambo mengi nisije nikasahau ukifa
 
Unaumizwa kichwa na kauli ya maiti mtarajiwa. Kwani wewe uli plan kumzikia wapi?
 
Kuhusu kifo chake, Huna haki.. hiyo kazi ya ukoo wake..
 
"Ndoa si kwa ajili yako ni kwa ajili ya watoto"

"Ndoa si pete zinazonga mikono, ndoa ni upendo unabakia baada ya kuchoka kingono"

"Ndoa ni kukumbatia kaa la Moto"

"Ndoa ni Jua Kali"

"Ndoa ni joto"

"Ndoa si drama mbele ya watu nyomi, ndoa ya kweli huanzia Moyoni"

"Ndoa ni fumbo"

Dizasta vina: Ndoano🎶
 
Wakati mwingine unakua mbabe kidogo na ujiweke kama baba.Wanawake huwa na maneno mengi sana wakipewa muda waongee watakacho.Hawana kikomo wala kiwango kwenye kuongea.
 
"Ndoa si kwa ajili yako ni kwa ajili ya watoto"

"Ndoa si pete zinazonga mikono, ndoa ni upendo unabakia baada ya kuchoka kingono"

"Ndoa ni kukumbatia kaa la Moto"

"Ndoa ni Jua Kali"

"Ndoa ni joto"

"Ndoa si drama mbele ya watu nyomi, ndoa ya kweli huanzia Moyoni"

"Ndoa ni fumbo"

Dizasta vina: Ndoano🎶
Ndoa ni ngumu jamani 🎵

Au mpaka mume alete ukimwi nyumbani 🎵
 
A
Mwanandani wangu wa kike amekuwa na tabia kuvutia mambo kwao mathalani kuwafundisha watoto tamaduni za kwao ikiwemo lugha na kusifia mambo mengi ya kwao. (kabila lake).

Sasa Jana ghafla akaanza kumuongelea baba yake mzazi kiufupi siye aliyemlea alimzaa tu wakalea wengine hata MAHARI hakupokea yeye Wala kwenye harusi hakuja japo alikuwepo na alikuwa ni mwenye afya tu.

Mwandani akatamka NENO hili na kuliwekea msisitizo ambao sikumjibu lakini limenikaa kichwani nikaona nishirikishe jukwaa ambalo najua Kuna wenye msaada na hekima na wapumbavu pia. Kuwa siku "akitangulia mbele ya haki kabla ya baba yake mzazi, baba yake ndio atoe maamuzi ya yeye kwenda kuzikwa akasisitiza tena kuwa ikiwa maneno yake ie. mke hayatatekelezwa basi nitajilaumu sana maishani ni kana kwamba nitapata matatizo" kwa kwenda kinyume na matakwa ya marehemu.

Sasa wadau naombeni ushauri hapa Ina maana mimi Sina maamuzi juu yake pamoja na kumlisha na kumtunza kote?. Au ni mtunzaji akiwa hai akifa Sina langu?. Vipi Mimi nikitangulia atawapoteza wanangu wasijue kabisa asili ya baba Yao Wala shangazi, baba wakubwa na wadogo upande wangu?. Anamaanisha Nini?. Au INAMAANISHA Nini hii?.

Naombeni mawazo wadau.

Mara nyingi wanawake ambao walikosa mapenzi ya baba, huwa wanakuja kuwa wasumbufu sana kwa waume zao. Tatizo nikuwa anatamani wewe uwe kama baba yake na pia uplay part ya mumewe pia, ambayo inataka mwanaume strong kitabia na kiuchumi. Sasa kama umelega lega hapo ujue ni dharau ya hali ya juu. Pambana sana mkuu. Ndio maana wazee wetu walishauri tuoe kwenye familia nzuri, ilikuwa ni katika kuangalia hayo.
 
Back
Top Bottom