Hii Kodi ya Majengo mbona ni utata? Ninawaza tofauti

Hii Kodi ya Majengo mbona ni utata? Ninawaza tofauti

Prof Koboko

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2020
Posts
350
Reaction score
2,550
Ninajiuliza, kama mwanzo kodi hizi zilikua zinalipwa na wamiliki wa majengo, imekuaje mzigo huu utupiwe kwa wapangaji? Hii ni haki siyo uonevu?

Kwanini nisifikiri kuwa viongozi wetu huko juu ndio wengi wao wanamiliki majumba mengi kama miradi yao wanataka kukwepesha mzigo huu kwao? Kwanini umrundikie mzigo mnyonge huyu huyu ambaye mfumoko wa bei tu umemwandama alichilia mbali tozo zingine?

Kuna kila sababu ya kulifuatilia vizuri hili jambo kujua ni kwanini serikali imeamua kuwabebesha mzigo huu watu wa chini badala ya wamiliki, liko tatizo na nitabakia kuwaza kua ni mradi wa watu.

Magufuli asingeweza kuwabebesha mzigo huu raia wake, maumivu tunayaona baada ya yeye kuondoka. Yaani watu wanaamka tu na kumrundikia mzigo wa Tozo raia ambaye pesa ya kula tu bado shida.
 
Kimsingi wanataka wasihangaike kuipata pesa , Yani wapate pesa wakiwa mezani wametulia wakila kuku kwa mrija na kutembelea ma V8...!! Anyway watanzania wote ni ndugu , tuongezeni juhudi kwenye kilimo
 
Kimsingi wanataka wasihangaike kuipata pesa , Yani wapate pesa wakiwa mezani wametulia wakila kuku kwa mrija na kutembelea ma V8...!! Anyway watanzania wote ni ndugu , tuongezeni juhudi kwenye kilimo
Hapa Mwigulu na watu wake wamechemka sana. Hivi kazi ya TRA ni nini?
 
Wchaga na nyumba zao za kufikia december ndio wataisoma vizuri hii.
 
Kimsingi wanataka wasihangaike kuipata pesa , Yani wapate pesa wakiwa mezani wametulia wakila kuku kwa mrija na kutembelea ma V8...!! Anyway watanzania wote ni ndugu , tuongezeni juhudi kwenye kilimo
Hapa tumepigwa balaa
 
Nyumba yangu ni mbavu za mbwa, ina umeme, nilipe kodi ya nyumba?
 
Mkataba wa upangaji unatamka wazi kuwa umeme juu yako mpangaji ina maana ni pamoja na vikorokoro vyote

Mbona umekuwa ukilipa vitu kibao na hulalamiki ukinunua umeme husemi ni juu ya mwenye nyumba mimi nanunua umeme tu

Mfano ukinunua umeme kuna vitu vuatavyo

Kuna kulipa REA
kuna Kulipa EWURA
Na umeme wenyewe ulionunua

Mbona hujawahi sema ohh REA na EWURA alipe mwenye nyumba mwenyewe?

Nikikupa gari nikikwambia mafuta juu yako maana yake ni kila kitu utakachokuta ukinunua mafuta juu yako
 
Uzi huu hauna tofauti na wa tarehe 10 Julai 2021 unaosema WENYE NYUMBA WALIPE KODI YA NYUMBA ZAO.
 
Lakini angebambikizia watu kesi na kuwafunga bila mwisho. Lakini angepeleka TISS kuuwa watu wenye mawazo tofauti na yake. Lakini angechapisha makaratasi ya kura na kujipigia kura yeye mwenyewe. Ni bora alikufa. Nk Nk

Siungi mkono hizi tozo lakini kumlilia Magufuli ni kulilia uovu na mateso kwa watu wengine. Akae huko huko na asirudi tena.
Magufuli asingeweza kuwabebesha mzigo huu raia wake, maumivu tunayaona baada ya yeye kuondoka. Yaani watu wanaamka tu na kumrundikia mzigo wa Tozo raia ambaye pesa ya kula tu bado shida.
 
Ninajiuliza, kama mwanzo kodi hizi zilikua zinalipwa na wamiliki wa majengo, imekuaje mzigo huu utupiwe kwa wapangaji? Hii ni haki siyo uonevu?

Kwanini nisifikiri kua viongozi wetu huko juu ndio wengi wao wanamiliki majumba mengi kama miradi yao wanataka kukwepesha mzigo huu kwao? Kwanini umrundikie mzigo mnyonge huyu huyu ambaye mfumoko wa bei tu umemwandama alichilia mbali tozo zingine?

Kuna kila sababu ya kulifuatilia vizuri hili jambo kujua ni kwanini serikali imeamua kuwabebesha mzigo huu watu wa chini badala ya wamiliki, liko tatizo na nitabakia kuwaza kua ni mradi wa watu.

Magufuli asingeweza kuwabebesha mzigo huu raia wake, maumivu tunayaona baada ya yeye kuondoka. Yaani watu wanaamka tu na kumrundikia mzigo wa Tozo raia ambaye pesa ya kula tu bado shida.
Labda kwa mtu ambaye sio mfanya biashara ndio ataliona hili ni geni, lakini hawa TRA, hawajaanza leo kumtwisha zigo mpangaji badala ya mwenye nyumba, mfano withholding tax, hiyo asilimia 10, miaka yote wanamkata mpangaji, kwenye kodi ya pango halafu wanakwambia nenda ukaelewane na mwenye nyumba!!wao wanaposhindwa kumbana mhusika wanamdaka yoyote tu anayetaka kufanana na huyo wanaomshindwa, kwao ni pesa ilipwe tu!!!
 
Tuliambiwa kuwa wamiliki wa nyumba za makazi wakishafikisha miaka 60 hawalipi kodi za majengo bali kulipia kodi za ardhi basi sasa mchezo umegeuka hewani.
 
Huo ni mwendelezo wa tozo ya uzalendo lipa bila shurti, ukiona unamfaidisha mwenye jengo jenga yako ukate mzizi wa fitna......
 
Ninajiuliza, kama mwanzo kodi hizi zilikua zinalipwa na wamiliki wa majengo, imekuaje mzigo huu utupiwe kwa wapangaji? Hii ni haki siyo uonevu?

Kwanini nisifikiri kuwa viongozi wetu huko juu ndio wengi wao wanamiliki majumba mengi kama miradi yao wanataka kukwepesha mzigo huu kwao? Kwanini umrundikie mzigo mnyonge huyu huyu ambaye mfumoko wa bei tu umemwandama alichilia mbali tozo zingine?

Kuna kila sababu ya kulifuatilia vizuri hili jambo kujua ni kwanini serikali imeamua kuwabebesha mzigo huu watu wa chini badala ya wamiliki, liko tatizo na nitabakia kuwaza kua ni mradi wa watu.

Magufuli asingeweza kuwabebesha mzigo huu raia wake, maumivu tunayaona baada ya yeye kuondoka. Yaani watu wanaamka tu na kumrundikia mzigo wa Tozo raia ambaye pesa ya kula tu bado shida.
Mwenye kuielewa hii Kodi naomba atuelimishe na wengine tusioelewa. Kwangu ina mwelekeo wa kubagua Watanzania. Najiuliza Kama hii no kodi ya majengo je inawahusu wenye umeme tu? Wale ambao Nyumba zao hazina umeme ama wanatumia nishati mbadala Kama vile solar ama generator hawahusiki nayo? Pia haizingatii uwezo wa mtu. Bibi wa kijijini mwenye nyumba ya chumba kimoja na sebule na taa mbili nae alipe sawa na mwenye nyumba ya vyumba vitano na kuendelea? Kabla ya utaratibu huu wazee walikuwa wamesamehewa kodi ya majengo. Sasa je msamaha huu umefutwa?
Mwenye uelewa mzuri naomba anielimishe kwa hili?
 
Mwenye kuielewa hii Kodi naomba atuelimishe na wengine tusioelewa. Kwangu ina mwelekeo wa kubagua Watanzania. Najiuliza Kama hii no kodi ya majengo je inawahusu wenye umeme tu? Wale ambao Nyumba zao hazina umeme ama wanatumia nishati mbadala Kama vile solar ama generator hawahusiki nayo? Pia haizingatii uwezo wa mtu. Bibi wa kijijini mwenye nyumba ya chumba kimoja na sebule na taa mbili nae alipe sawa na mwenye nyumba ya vyumba vitano na kuendelea? Kabla ya utaratibu huu wazee walikuwa wamesamehewa kodi ya majengo. Sasa je msamaha huu umefutwa?
Mwenye uelewa mzuri naomba anielimishe kwa hili?
Huyo Bibi Hana uwezo hata wa kununua umeme, Kuna watoto na wajukuu wanaomnunulia huo umeme ndo watamlipia na hiyo Kodi.
 
Back
Top Bottom