Hii maalum kwa walaji wa mishikaki ovyo, barabarani!

Ukienda pupa umekula nyama ya mbwa, akiwekwa kitunguu swaumu, tangawizi, ndimu, pilipili, chumvi kidogo, na chachandu, na uwe ushalewa unaleta uchu wako...umekwisha ndugu yangu!
Kwani ukila unakufa? Katika vitu ambavyo wewe huli, umepokea tu na wala hujui kwa nini huli... UMERITHISHWA KUWA HAVILIWI...

Umeshawahi kujiuliza kwa nini wanyama au wadudu fulani wanaliwa maeneo fulani, lakini maeneo mengine hawaliwi? MAPOKEO
 
Kama Ntwara wanakula Panya, Singida wanateremsha punda, Songea wanakula kumbikumbi, Bukoba wanaondosha senene... wewe una sababu yoyote kwanini huli kimojawapo? Wamsai wao samaki ni ishu...
kumbikumbi nakula! Senene sili! Cha muhimu kuhusu hiyo mishikaki wanapouza wawe wazi! Waseme nauza mishikaki ya mbwa, nyani, mamba, nguruwe,punda n.k.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…