Hii maana yake nini?

KIDUDU

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2012
Posts
2,557
Reaction score
1,927
Jamani nimepita mbeya jana nikakuta kuna jengo limeandikwa SHREE HINDU MANDAL lakini kilichonistua ni alama ambayo imechorwa kabla na baada ya hilo andiko.

Kuna alama ambayo ni sawa na ile iliyokuwa ikitumiwa na watu wa Adolph Hitler ya NAZI.

Naomba kuelewa yafuatayo kwa mwenye mwanga.

1. Chama kile cha wa Nazi kilikuwa na temple yake ya kuabudu? Na kama ni kweli, Je, hawa wahindi na NAZI wana uhusiano gani?.

2. Kisiasa hii ina ishara gani? Yawezekana NAZI party wameamua kujiimarisha kutokea tanzania kwa staili ya dini?

3. Kwa kuwa kila kanisa au taasisi ya dini kwa ujumla husajiliwa kwa mujibu wa sheria za nchi, Je, Tanzania wanajua uwepo wa hili dhehebu nchini?

Kama wanajua, ni nini maana ya alama hii ambayo kisiasa ilikuwa na impact kubwa duniani?

Naomba kujuzwa.
Rejea picha hapa chini.
 

Attachments

  • WP_20160621_17_21_32_Pro.jpg
    82.3 KB · Views: 280
mshana jr alishawahi kuzungumzia hiyo alama maana ake

Kuna Swastika mbili ambazo zinachanganya sana watu ila moja ndio halisi huku nyingine ikiwa imefanyiwa editing kukidhi matakwa ya mtu mmoja
Karibu dini zote zinatumia hiyo alama hebu ona hapahii ndio swastika asili
Halafu hii ni swastika ya hitler, hii imepinduliwa na iko kinyume kwa maana ya Hitler swastika hii maana yake ni socialism, lakini ukija kuangalia ni alama iliyotumika na majeshi ya Nazi yaliyokuwa na ukatili mkubwa akiwemo Hitler mwenyewe
Kwa muktadha wa Buddhism hii ndio maana ya Swastika ona tofauti zake
 
Aisee nadh Nadhan ulijiunga jf kwa sababu maalumu. Sijawahi kujuta kukufahamu. Asante sana na Mungu akubariki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…