Hii ndio (CV) Wasifu ya Nape Moses Nnauye

Hii ndio (CV) Wasifu ya Nape Moses Nnauye

Du!!! Kumbe Nape alipata F Civics ndio maana uwezo na upeo wake katika siasa za ushindani wa vyama vingi ni mdogo sana.
 
.........Huyu Nepi Nnauye elimu yake ina bandage na welding nyingi lol!! Jamaa ameunga unga sana, hata uwezo wake wa kuchambua vitu unadhihirisha kuwa alikuwa 'empty' amesaidiwa na jina la Baba ake kupenya penya kwenye hivyo vyuo na vikozi vya ajabu ajabu.
 
NAPE NNAUYE
DIV IV-29
KISW D, HIST D, GEOG D, ENG F, B/MATH F, BIOL D, CHEM D, PHY D, CIV F

hahahahahaaaaaaaaaaaa ndio kwa usomi huu watoto wetu watafaulu kwel??????????????
 
Mkuu ile post ya Mnyika uliipitia? Nadhani aliweka wazi kutomaliza chuo kwa sababu za hapa na
Pale sasa sielewi matokeo gani tena ya chuo kikuu.... Na huyu Nape did he step to university by any chance?? Sijasikia as nimeona ni diploma mbili tatu..... Hivi Watanzania tumelogwa au? Tunaacha kujadili mambo ya maana ya maemdeleo eti tunajikita na mara elimu ya Nape, Mnyika, mama baba wa Nape, baba wa Slaa..... Mkuu hebu saidia mie kichwa kinauma kwa hili.... Matokeo ya form four tatizo, hospitali zetu tatizo,

Hizi thread nyingine ni burudani tu mkuu. Usizichukulie serious sana. Hatuwezi muda wote kuwa tunaongea mambo serious tu, lazima wakati mwingine tunapiga stroy za kijiweni kama hizi...
 
MMh, Butimba TTC ilikuwa na high school? Hakikuwa chuo cha ualimu kile??
Anyway, hata uwe na Phd kama hamnazo za maisha hazimo tu.

Siku moja nikiwa JKT pale Mafinga kwa mujibu wa sheria tulipanga kuwahadaa Maafande Kuruta Mwenzetu akasimama pembeni wakati wa kupakuliwa ugali kuna Afande mmoja alikuwa akiitwa Afande Mwakyosi akamuuliza yule Kuruta kwanini hataki kula, Kuruta akamjibu afande kuwa hana APATITE, Afande akasema nenda kwa Kota Masta wenzio wamepewa mbilimbili leo we ulikuwa wapi?? Butimba TTC High School.
 
When the going gets tough the tough gets going
 
Kutokana na mabishano ya mda mrefu kwenye mitandao kuhusiana na uwezo wa kielimu juu ya hawa wana siasa wetu,nashauri utungwe mtihani kisha hawa jamaa wafanye tuone nani kilaza.wahusika kwakuwa wote wapo humu naomba mthibitishe utayari wenu wa kushiriki mtihani
 
Hizi thread nyingine ni burudani tu mkuu. Usizichukulie serious sana. Hatuwezi muda wote kuwa tunaongea mambo serious tu, lazima wakati mwingine tunapiga stroy za kijiweni kama hizi...
Hii ni serious kuliko unavyodhani.

Ukosefu wa maelezo ya namna Nape alivyovuka kikwazo cha kutokuwa na credit za kufanya mtihani wa Form VI unampa doa Nape. Vile vile kukosekana maelezo ya kuridhisha ya elimu yake ya Form VI ni fumbo jingine kubwa. Tunapata hisia za uwezekano wa kughushi vyeti au udanganyifu mwingine. Integrity ya Nape inahojiwa hapa.

Ni serious kuliko unavyodhani, na haitaishia hapa JF, mpaka habari za uhakika zimepatikana
 
Siasa za nani alipata degree or not ,hazina mantiki kwa sasa kwani iko wazi CCM ina wasomi wengi na wenye uwezo mkubwa kuliko CHADEMA.
Upeo wa kisiasa na kitaaluma ni vitu viwili tofauti,mfano mzuri ni Dr.Kawambwa ni mtekelezaji wa objectives,hajui porojo za kisiasa ,hana sababu za kutafuta umaarufu kwenye media kama J.Mnyika na ZZK.
Miradi mingi katika wizara zote alizowahi kuongoza ameacha matunda mazuri .

Jambo la msingi,turudi kwenye maadili ya mtanzania,tuwaepushe watoto na starehe za mapema ili wawe makini ktk elimu.
Wanafunzi wengi wanatumia muda mwingi ktk starehe ndiyo maana wamefeli.
Mimi nimesoma chuo ambacho kiliweka sheria kali yakutotumia simu uwapo darasani,ukibainika ilikuwa unanyang'anywa nakupelekwa kwa Principal,wengi tulitii sheria hiyo na kuwa makini darasani.

Hiyo ni university level,lakini tulipokuwa Advance Level tulikuwa huru tukionyeshana umaarufu wa kuvaa nguo(pamba) na kuwa na mademu wengi,hakika matokeo yalikuwa ni mabaya sana licha ya wanafunzi wengi kuwa na uwezo mzuri darasani kwani nilibaini majority tuliingia tukiwa na Division One na Two lakini mambo yalikuwa kinyume kwenye Final(Wengi walipata Zero).

Facebook,Twitter,SMS kwenye SIMU na NGONO za utoto zimewafelisha watoto wetu,BUNGE liunde kamati na kuwasilisha muswaada utakao nasua akili za watoto wa kitanzania.

hakuna hata sababu moja uliyotoa yenye mashiko juu ya kufeli kwa watoto hawa
-umezungumzia fb,twiter,sms na ngono kama sababu,lakini ukweli hii inachangia kwa 0.000001 percent.kwani huko shule za vijini ambako hawjapata ufahamu wa kutumia hizi social network wamefaulu?...
UKWELI NI KUWA
.MFUMO MBOVU WA ELIMU(HASA KUBADILI MITAALA KILA MWAKA) NDO VIMECHANGIA
.BUDGET NDOGO YA ELIMU NI TATIZO KATIKA KUDEVELOP UFANIS I WA ELIMU,..Tanzania ndio inayoongoza kwa budget ndogo kwa elimu compared to EA Countries
.Siasa na sera mbovu,usimamizi mbovu,walimu wasio na uwezo pia imechangia
.Crash program iliyoanzisha na Serikali haya ndio matunda yake sasa
.Migomo ya walimu etc...
KAWAMBA JIUZULU ULINDE HESHIMA YAKO,HAYA MATOKEO NI AIBU KUBWA
 
2pe matokeo yake ya olev na a level ili cv ikamilike

kama umeangalia vizuri ni kuwa alipomaliza A-level alienda diploma.hapo anaweza kuwa alifeli A-level and still akatumia cheti cha form four kuingia diploma.inawezekana
 
kutokana na mabishano ya mda mrefu kwenye mitandao kuhusiana na uwezo wa kielimu juu ya hawa wana siasa wetu,nashauri utungwe mtihani kisha hawa jamaa wafanye tuone nani kilaza.wahusika kwakuwa wote wapo humu naomba mthibitishe utayari wenu wa kushiriki mtihani
nawe utakuwa mtahiniwa wa tatu
 
Hamna haja ya kupoteza muda mtihani wa form four una tosha kujua nani kilaza
 
Hii ni serious kuliko unavyodhani.

Ukosefu wa maelezo ya namna Nape alivyovuka kikwazo cha kutokuwa na credit za kufanya mtihani wa Form VI unampa doa Nape. Vile vile kukosekana maelezo ya kuridhisha ya elimu yake ya Form VI ni fumbo jingine kubwa. Tunapata hisia za uwezekano wa kughushi vyeti au udanganyifu mwingine. Integrity ya Nape inahojiwa hapa.

Ni serious kuliko unavyodhani, na haitaishia hapa JF, mpaka habari za uhakika zimepatikana

Swala la kufoji vyeti kama lipo ni swala nyeti, lakini unaposema tufananishe matokeo ya Nape na Mnyika ya form four wakati ni miaka 16 tangu wamalize form four ni story za kijiweni.
 
Kumbe ni Mbwa wa kuhangaika tu? kimtu kama hichi ana uwezo wa kumtukana Lowassa na Slaa? kijibwa dhidi ya Wafalme?
 
Back
Top Bottom